Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Nguruvi3, Trump ndiye Rais mteule wa Marekani lakini, pamoja na madoa yanayomkosesha usingizi kama hayo uliyoyataja, hili la popular votes pia linamkera kweli kweli. Angekuwa ameshinda na kwenye hili watu wangemkoma lakini sasa anaanza kuyaona matatizo huko mbele ya safari. Tayari imani kwa wale waliokuwa wakitegemea mabadiliko kama alivyojinadi inaanza kupungua kadiri anavyoendelea kufanya teuzi zake.

Latest Popular votes update...
  • Hillary Clinton: 65,737,041.....48.08%
  • Donald trump: 62,896,704......46.00%
  • The difference: 2,841,337.......2.08%
Hata kama wako wanaopuuzia tofauti hii lakini inampunguzia Trump uhalali wa kudai kapewa mandate na Wamarekani walio wengi. Tayari wapo wanaoanza kuamini tuhuma zinazoelekezwa kwa Urusi kuingilia mchakato wa uchaguzi na pengine kuwa na mkono katika ushindi wa Trump. Trump aliyeapa kwamba akishindwa hatakubali hadi uthibitisho upatikane kwamba hapakuwepo na faulo katika ngazi zote za mchakato.
 
Yaani Urusi iweze ku hack uchaguzi wa Marekani?

Urusi wana uwezo mkubwa kiasi hicho?

Wali hack kivipi na ni kivipi hiyo hacking ilimfanya Trump ashinde?

Na wali hack nini hasa? Mtandao wa tume ya taifa ya uchaguzi? Marekani kuna tume ya taifa ya uchaguzi?

Hao Warusi walipenyeza kura feki kwenye masanduku ya kura?

Na kama waliweza ku hack mambo ya uchaguzi, ina maana Warusi wanawazidi Wamarekani katika maujanja ya mtandao?

Hapa kuna harufu kali ya propaganda inayolenga kum discredit huyo rais mteule.

Si bure.
 
Yaani Urusi iweze ku hack uchaguzi wa Marekani?

Urusi wana uwezo mkubwa kiasi hicho?

Wali hack kivipi na ni kivipi hiyo hacking ilimfanya Trump ashinde?

Na wali hack nini hasa? Mtandao wa tume ya taifa ya uchaguzi? Marekani kuna tume ya taifa ya uchaguzi?

Hao Warusi walipenyeza kura feki kwenye masanduku ya kura?

Na kama waliweza ku hack mambo ya uchaguzi, ina maana Warusi wanawazidi Wamarekani katika maujanja ya mtandao?

Hapa kuna harufu kali ya propaganda inayolenga kum discredit huyo rais mteule.

Si bure.
Mkuu nilikuwa na mtazamo kama huo nikijua uchaguzi wa US siyo centralized na hacking inaweza ku affect pengine county moja isiyo na impact kama ikitokea.

Ni ngumu kufanya hacking ya ujumla,nilizungumzia pia wakati wa madai ya Trump kuhusu rigging

Kinachotokea ni tofauti.
Hacking inayoongelewa si uchaguzi bali ile ya DNC ambayo internal info ziliwekwa hadharani.
Na hilo lilifanyika kipindi chote cha uchaguzi. Initially ilidhaniwa ni Wikileaks na ilitoka kwa jina hilo.

Hata pale internet ilipokuwa disconnected katika ubalozi anaoishi Assange, haikuzuia chochote

Hapo ndipo swali linapokuja, kwamba Wikileaks ilifanya yenyewe au ilikuwa na msaada?

Intelligence community ikapewa jukumu la kuangalia ilikuwaje,majuzi wakasema Russia ina mkono. Hawajatoa evidence lakini IC zina namna zao za kufanya kazi.

Maseneta wanne akiwemo McCain, Lindsey Graham na Chuck Schumer wameandika barua wakitaka uchunguzi zaidi ili kujiridhisha hakuna taifa la nje linalo influence uchaguzi wa Marekani

McCain(Rep) ameongelea kwa uhakika kuwa Russia wali ingilia akiwa ni senior senator

Hadi hapo hoja si matokeo, wala hacking iliyoathiri matokeo bali alleged external influence

Na wala hakujatolewa uthibitisho, kinachotaki ni investigation itakayohusisha IC na kamati za Bunge

Kinachoshangaza ni kuwa investigation haiwezi kutoa matokeo nje ya yale yaliyopatikana kwa uchunguzi wa vyombo husika. Hivyo kwanini Trump anakataa hilo ilihali Urais wake upo pale pale?

Hapa kuna hoja ya kuharamisha urais wake, lakini pia kwa ushindi alioupata itaondoa shaka kwa wenye mashaka na kumpa mandate zaidi kuliko ilivyo sasa anapojaribu kuzima suala hilo

Trump amehoji credibility ya security apparatus zake kama CIA.

Ni Trump aliyemsifia James Comey na kutumia taarifa tu za kufungua uchunguzi kuhusu email.
Leo inakuwaje ni jambo asiloamini vyombo ambavyo sasa vitakuwa chini yake?
 
McCain(Rep) ameongelea kwa uhakika kuwa Russia wali ingilia akiwa ni senior senator

Hivi huyo babu ana credibility gani?

Ulimsikia kipindi kile cha kabla ya uvamizi wa Iraq?

Babu hana credibility kabisa huyo.

Jionee mwenyewe hapo....





Sasa hapo vipi baada ya kuziangalia hizo video? Babu alikuwa sahihi? Au hakuwa anaongea kwa kujiamini?

Hadi hapo hoja si matokeo, wala hacking iliyoathiri matokeo bali alleged external influence

Na wala hakujatolewa uthibitisho, kinachotaki ni investigation itakayohusisha IC na kamati za Bunge

Ndo maana nasema kuna kila harufu ya propaganda za kisiasa tu. Election cycle ya Marekani huwa haina mwisho. Ni endelevu.

Ukidhani hakuna nia za kisiasa hapo basi lazima utakuwa naive sana.

Kinachoshangaza ni kuwa investigation haiwezi kutoa matokeo nje ya yale yaliyopatikana kwa uchunguzi wa vyombo husika. Hivyo kwanini Trump anakataa hilo ilihali Urais wake upo pale pale?

Mimi naamini there is no there there.

Hivi unadhani roles zingebadilishwa na tuseme Dems ndo wangekuwa beneficiaries wa hiyo alleged hacking ya Russia wasinge react kama anavyo react Trump?

Kilichopo hapo ni siasa tu.

Trump amehoji credibility ya security apparatus zake kama CIA.

Na ana hoja ya msingi kabisa.

Kwani uongo kwamba CIA huwa hawadanganyi? Ni uongo kwamba CIA huwa hawakosei?

Kabisa unadhani kuwa huko CIA kila mtumishi ni apolitical?

Ni Trump aliyemsifia James Comey na kutumia taarifa tu za kufungua uchunguzi kuhusu email.
Leo inakuwaje ni jambo asiloamini vyombo ambavyo sasa vitakuwa chini yake?

Hahaaaa mimi ni bonge la political junkie. Nasikiliza talk radio za pande zote [left and right] kila siku. Naangalia politcal shows kwenye cable networks.

Kwa hiyo, kuhusu hilo la Trump kumsifia Comey halafu baadae kuonekana kana kwamba haamini [baadhi ya] kazi zinazofanywa na hivyo vyombo ambavyo vitakuja kuwa chini yake, mimi nakwambia hapo ni siasa tu.

Kama huamini hebu cheki hizo video hapo chini uone jinsi ambavyo Democrats walivyokuwa wanamwagia masifa kemkem huyo huyo James Comey pale aliposema FBI haitapendekeza mashitaka dhidi ya Bi. Clinton halafu baadae walipokuja kumgeuka aliposema FBI wanafufua tena uchunguzi dhidi yake.

Republicans nao walimlaani Comey aliposema Hillary hatafunguliwa mashitaka halafu alipokuja kusema kuwa wanafufua tena uchunguzi wakaanza kumsifia.





Hivyo mimi nakuhakikishia kuwa hapo kuna malengo ya kisiasa tu kwa sababu kwenye siasa perception ndo reality.

Ukifanikiwa kumjengea mpinzani wako taswira flani...haijalishi kama ni ya kweli au la...halafu hiyo taswira imgande, basi huo ni ushindi kwa kiasi flani.

Ndo maana sishangai kuona Dems wamekomalia huo uchunguzi na hizo habari za Russia kuingilia uchaguzi wao kwa sababu hilo linahusiana na 'bromance' kati ya Putin na Trump.
 
Nyani Ngabu nimemtaja McMcaina makusudi nikijua alikuwa na sijui kama bado yup katika kamati ya foreign affairs. Nadhani kuna jambo analoliona ingawa hakusema, na alisema kwa uhakika.
Hiyo tu ndiyo ilikuwa hoja

Pili, Trump anapoanza kusigishana na security apparatus zake si jambo jema.
Hao CIA wanakosea, ndiyo maana kunatakiwa kuwe na congressional investigations kama ile ya Republican iliyomchunguza Clinton na kutoa matokeo yake

Tatu, kama kuna nia ya kisiasa na Trump kashinda decisively kuna tatizo gani investigation kufanyika?
Kumbuka haitaathiri urais wake kwa namna yoyote ile

Nne, je nani ali hack DNC na je hilo halihitaji uchunguzi kama sehemu ya security?

Jambo zuri kwa USA inapotokea tatizo lazima watafute nini chanzo hata kama ni miaka 50
Je kuna tatizo kuangalia retrospectively na kujiridhisha tu kuwa si Russia ni michezo ya ndani?

Tano, sijui una maoni yapi kuhusu Trump kuwa nervous, nini hasa kinachoweza kutokea ambacho yeye asingependa au anaona kita athiri presidency yake?
 
Nyani Ngabu nimemtaja McMcaina makusudi nikijua alikuwa na sijui kama bado yup katika kamati ya foreign affairs. Nadhani kuna jambo analoliona ingawa hakusema, na alisema kwa uhakika.
Hiyo tu ndiyo ilikuwa hoja

Kwangu McCain hana credibility yoyote ile hivyo huwa sichukulii maanani mengi ayasemayo.

Pili, Trump anapoanza kusigishana na security apparatus zake si jambo jema.

Hilo ni kweli.

Hao CIA wanakosea, ndiyo maana kunatakiwa kuwe na congressional investigations kama ile ya Republican iliyomchunguza Clinton na kutoa matokeo yake

Hizo congressional investigations nazo zimejaa unafiki wa kisiasa tu maana kila upande utavutia kwake.

Tatu, kama kuna nia ya kisiasa na Trump kashinda decisively kuna tatizo gani investigation kufanyika?
Kumbuka haitaathiri urais wake kwa namna yoyote ile

Hapo ndo nadhani hujaelewa.

Ni hivi, kwenye siasa za Marekani na pengine hata kwingineko ukiweza kum define mpinzani wako kuwa yuko hivi na vile na hiyo taswira ika stick, basi huo nao ni ushindi.

Tatizo lilipo hapo ni kum discredit na kum delegitimize Trump hususan kwenye court ya public opinion. Kwamba ni rais ambaye si chaguzi la Wamarekani bali ni kibaraka wa Russia kwa sababu Russia ilimsaidia kuingia madarakani.

Mambo ya perception vs reality.

Ni rais gani au ni kiongozi gani kwenye nchi zenye demokrasia anapenda kufanya kazi under a cloud kwamba alisaidiwa kuingia madarakani na wadukuzi wa nchi hasimu?

Nne, je nani ali hack DNC na je hilo halihitaji uchunguzi kama sehemu ya security?

Kwa nini iwe ku hack-iwa tu? Vipi kama huko DNC kulikuwa na wasaliti waliovujisha hizo nyeti?

DNC wafaye uchunguzi wao wenyewe.

Tano, sijui una maoni yapi kuhusu Trump kuwa nervous,

Kwamba Trump yuko nervous...huo u-nervousness ni suala la tafsiri tu. Naamini wapo ambao hawatafsiri hivyo, kwamba Trump yuko nervous. Mim sioni kama yuko nervous. Nachoona ni natural reaction tu. If the shoe was on the other foot I can almost guarantee you the reaction would've been similar if not the same.

nini hasa kinachoweza kutokea ambacho yeye asingependa au anaona kita athiri presidency yake?

Hapo naamini anachoona kitaweza kuathiri urais wake ni hiyo cloud of suspicion kwamba Russia ndo walisababisha akashinda.

Na kama nilivosema hapo juu kwamba kwenye siasa perception is king.

Ni rais gani anapenda kuwa na hiyo cloud of suspicion akiwa madarakani?
 
"Nyani Ngabu, post: 18837889, member: 188"]Hizo congressional investigations nazo zimejaa unafiki wa kisiasa tu maana kila upande utavutia kwake.
Iliyomchunguza Hillary ilikuwa ni ya Republican na ikam clear kuwa hakuwa na tatizo.
Ni hivi, kwenye siasa za Marekani na pengine hata kwingineko ukiweza kum define mpinzani wako kuwa yuko hivi na vile na hiyo taswira ika stick, basi huo nao ni ushindi. Tatizo lilipo hapo ni kum discredit na kum delegitimize Trump hususan kwenye court ya public opinion. Kwamba ni rais ambaye si chaguzi la Wamarekani bali ni kibaraka wa Russia kwa sababu Russia ilimsaidia kuingia madarakani.
NN hii ni investigation tu haina conclusion, inaweza kufikia tamati na matokeo mengine kabisa.
Fikiria kama ni Democrat waliofanya hivyo! Huoni hapo itaondoa wingi la utata?
Ni rais gani au ni kiongozi gani kwenye nchi zenye demokrasia anapenda kufanya kazi under a cloud kwamba alisaidiwa kuingia madarakani na wadukuzi wa nchi hasimu?
Jibu ni hakuna, je huoni ni muhimu kuondoa hiyo cloud kwa kuruhusu investigation? Hapa investigation si facts ni process ya kupata facts na nadhani ingemsaidia yeye kuliko kuacha hili jambo libaki hewani maana kila mara litarudi. Akifanya deal na Russia hata yenye manufaa tayari ana strings attached, hivi si vema akaachana na hilo kwa kukubali uchunguzi ufanyike?
Kwa nini iwe ku hack-iwa tu? Vipi kama huko DNC kulikuwa na wasaliti waliovujisha hizo nyeti?DNC wafaye uchunguzi wao wenyewe.
Very possible, sasa tutajue ni Russia au DNC kama hakuna investigations.
Nadhani hapa umuhimu wa investigation unaonekana kuliko kuishi kwa hisia hisia
Hapo naamini anachoona kitaweza kuathiri urais wake ni hiyo cloud of suspicion kwamba Russia ndo walisababisha akashinda.
Anawezaje ku get rid of suspicion bila uchunguzi?
Huoji kukataa itakuwa ku prolong suspicion na mbele ya safari anything can be linked with.
Ni rais gani anapenda kuwa na hiyo cloud of suspicion akiwa madarakani?
Hakuna, Obama alijaribu kukaa kimya na suala la' Birth cet' ilimsumbua sana na aliyemsumbua ni huyu Trump.

Obama akatoa hoja ikafikia mwisho. Hakupenda kuishi katika cloud of suspicion.
Why not Turmp? Just investigation
 
Iliyomchunguza Hillary ilikuwa ni ya Republican na ikam clear kuwa hakuwa na tatizo. NN hii ni investigation tu haina conclusion, inaweza kufikia tamati na matokeo mengine kabisa.
Fikiria kama ni Democrat waliofanya hivyo! Huoni hapo itaondoa wingi la utata?Jibu ni hakuna, je huoni ni muhimu kuondoa hiyo cloud kwa kuruhusu investigation? Hapa investigation si facts ni process ya kupata facts na nadhani ingemsaidia yeye kuliko kuacha hili jambo libaki hewani maana kila mara litarudi. Akifanya deal na Russia hata yenye manufaa tayari ana strings attached, hivi si vema akaachana na hilo kwa kukubali uchunguzi ufanyike? Very possible, sasa tutajue ni Russia au DNC kama hakuna investigations.
Nadhani hapa umuhimu wa investigation unaonekana kuliko kuishi kwa hisia hisia
Anawezaje ku get rid of suspicion bila uchunguzi?
Huoji kukataa itakuwa ku prolong suspicion na mbele ya safari anything can be linked with. Hakuna, Obama alijaribu kukaa kimya na suala la' Birth cet' ilimsumbua sana na aliyemsumbua ni huyu Trump.

Obama akatoa hoja ikafikia mwisho. Hakupenda kuishi katika cloud of suspicion.
Why not Turmp? Just investigation

Hahahaaaa haya sawa.

Acha wafanye huo uchunguzi manake inaonekana wenye hamu na huo uchunguzi wapo 'wengi sana' kama vile ambavyo 'wapo wengi' waliotaka recount ifanyike kwenye yale majimbo matatu tu ambayo Trump alishinda.

Kujificha nyuma ya kuutafuta ukweli ilhali ni dhahiri shahiri kabisa kuna malengo ya kisiasa.

Yaani recount zifanyike kwenye majimbo matatu ambayo Trump alishinda na ambayo Hillary alishinda hakuna recount.

Kwa hiyo, kuna recount, sasa kuna uchunguzi wa hacking za Russia pamoja na lobbying ya wale electors wa electoral college wasimpigie kura Trump.

Hapana aisee. Kutokuona malengo ya kisiasa hapo ni kuwa naive.

Na watu wanaweza kabisa kujificha nyuma ya hoja inayoonekana ina mashiko huku wakiwa na ulterior motive
 
Oh by the way, hivi Marekani yenyewe huwa haijaribu ku influence chaguzi za nchi zingine?

Kabisa yaani Marekani yenyewe iko innocent kabisa kwenye hilo?

Hahahaaaa sitashangaa kabisa kama wapo watu wataodai Marekani huwa haijiingizi kwenye chaguzi za mataifa mengine.

Unafiki. Unafiki. Unafiki.
 
Oh by the way, hivi Marekani yenyewe huwa haijaribu ku influence chaguzi za nchi zingine?

Kabisa yaani Marekani yenyewe iko innocent kabisa kwenye hilo?

Hahahaaaa sitashangaa kabisa kama wapo watu wataodai Marekani huwa haijiingizi kwenye chaguzi za mataifa mengine.

Unafiki. Unafiki. Unafiki.
Mkuu hapa ni sawa na kuhoji mbona US wana Nyuklia halafu wanakataa wenzao wasio nazo. You know better, ni mkubwa that's it
Nchi nyingine kama hzichunguzi ni mapungufu yao

Kuhusu investigations, anayeleta curiosity siyo wanaotaka bali Trump, ni kitu gani anakataa ikiwa ni just investigations and he won decisively?

Pili, huyu ndiye aliyehubiri uwazi katika mchakato, mbona anarudi nyuma katika jambo lisilo na madhara kabisa kwakwe kiasi cha kuanza kutibuana na Intelligence community?

Kitu kizuri kwa US wana long memory na hawataki jambo likaisha tu bila kujua ni kwanini
Nilisoma mahali kuna kitongoji Kentuky, kime vote Democrat miaka 144, this time Trump kashinda.

US wanataka kujua nini kinaendelea na kwasababu gani,wapo ahead of game always

Vinchi masikini uchaguzi ukifanyika, mgombea Urais anapata kura 10,000 halafu mgombea ubunge wa chama hicho hicho anapata 1500 , kura zilizohariabika ni 100. Hakuna anayejiuliza nini imetokea kwa hesabu kama hizo, not in US baby! watachimba wapate ukweli

Ndivyo walivyochimba ushindi wa Obama na millennial na jinsi alivyotumia social media
Sasa hivi kila mmoja anatumia. Hii ni kwasababu watu wanaangalia vitu retrospectively

Endapo wangemtuhumu Trump kwakweli ningeshangaa sana, hakuna tuhuma wala kuhoji ushindi wake.

Wanachotaka ni kuchunguza kama kuna external influence na kwanini.
Hilo tu, ubaya upo wapi mkuu?
 
Mkuu hapa ni sawa na kuhoji mbona US wana Nyuklia halafu wanakataa wenzao wasio nazo. You know better, ni mkubwa that's it
Nchi nyingine kama hzichunguzi ni mapungufu yao

Kuhusu investigations, anayeleta curiosity siyo wanaotaka bali Trump, ni kitu gani anakataa ikiwa ni just investigations and he won decisively?

Pili, huyu ndiye aliyehubiri uwazi katika mchakato, mbona anarudi nyuma katika jambo lisilo na madhara kabisa kwakwe kiasi cha kuanza kutibuana na Intelligence community?

Kitu kizuri kwa US wana long memory na hawataki jambo likaisha tu bila kujua ni kwanini
Nilisoma mahali kuna kitongoji Kentuky, kime vote Democrat miaka 144, this time Trump kashinda.

US wanataka kujua nini kinaendelea na kwasababu gani,wapo ahead of game always

Vinchi masikini uchaguzi ukifanyika, mgombea Urais anapata kura 10,000 halafu mgombea ubunge wa chama hicho hicho anapata 1500 , kura zilizohariabika ni 100. Hakuna anayejiuliza nini imetokea kwa hesabu kama hizo, not in US baby! watachimba wapate ukweli

Ndivyo walivyochimba ushindi wa Obama na millennial na jinsi alivyotumia social media
Sasa hivi kila mmoja anatumia. Hii ni kwasababu watu wanaangalia vitu retrospectively

Endapo wangemtuhumu Trump kwakweli ningeshangaa sana, hakuna tuhuma wala kuhoji ushindi wake.

Wanachotaka ni kuchunguza kama kuna external influence na kwanini.
Hilo tu, ubaya upo wapi mkuu?

Kwani Trump kakataa hiyo investigation isifanyike au katoa tu maoni yake na kui dismiss?

Manake Trump hana mamlaka yoyote yale sasa hivi ya kukataa chochote kile kuhusiana na hiyo investigation.

Katoa tu maoni yake kwamba hiyo investigation iko politically motivated...jambo ambalo hata mimi naliona.

Tena hizo political motivation zimejificha conveniently nyuma ya hoja ya kuutafuta ukweli[emoji23] [emoji23] [emoji23].

Very funny.

Yote hayo ni katika jitihada za kum discredit na kum delegitimize kwenye court of public opinion.

Ni kama tu zile recounts [kwanza zimefikia wapi...manake sizisikii tena].

Eti ooh hazilengi kubadili matokeo bali kujua tu na kubaini dosari zilizojitokeza.....halafu aliyezidai wala hata hakupata asilimia 5 ya kura zilizopigwa lakini yuko mstari wa mbele kudai recount.

Haya mambo yasije kuwa ni mwendelezo wa fake news.

Things that make you go hmmm......
 
Kwani Trump kakataa hiyo investigation isifanyike au katoa tu maoni yake na kui dismiss?

Manake Trump hana mamlaka yoyote yale sasa hivi ya kukataa chochote kile kuhusiana na hiyo investigation.

Katoa tu maoni yake kwamba hiyo investigation iko politically motivated...jambo ambalo hata mimi naliona.

Tena hizo political motivation zimejificha conveniently nyuma ya hoja ya kuutafuta ukweli
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
.

Very funny.

Yote hayo ni katika jitihada za kum discredit na kum delegitimize kwenye court of public opinion.

Ni kama tu zile recounts [kwanza zimefikia wapi...manake sizisikii tena].

Eti ooh hazilengi kubadili matokeo bali kujua tu na kubaini dosari zilizojitokeza.....halafu aliyezidai wala hata hakupata asilimia 5 ya kura zilizopigwa lakini yuko mstari wa mbele kudai recount.

Haya mambo yasije kuwa ni mwendelezo wa fake news.

Things that make you go hmmm......
Kweli mapenzi hupofusha! Just imagine for one moment that the shoe was on the other foot and that it was the GOP that lost the election with all this cloud hanging over the Democrat's win! Just imagine Donald Trump won the popular votes but lost the electoral votes! Just imagine tea-partiers suspected the outcome of the election was influenced by the Soviet action of hacking the Republican party! Just imagine...

Just imagine the the outcry, the hubba-hubba, the uproar, the tumult, the screech, the hullabaloo, the convulsion, the hoo-ha, the protest, the cry...but here is Nyani Ngabu trying to play it all down simply because he'd rather have Trump than Clinton! One thing I can say without any doubt is that what we are seeing and hearing today would be like child's play compared to what Republicans led by Trump would do.

In 2008 if anybody was given the mandate by Americans it was Obama but even with his overwhelming victory, the Republicans never gave him a chance. One notable Republican named Donald Trump never once accepted the legitimacy of Obama's presidency. Not even after a repeat performance in 2012 did it ever sink into their heads that Americans had made their choice...Nyani Ngabu was also one such Republican.
 
Wiki hii imetawaliwa na habari kadha wa kadha. Kwanza, katika transition ya Trump Rudy Gullian na Chris Christie wameondolewa katika nafasi ya SoS.

Wameondolewa?

Rudy alimtaarifu PE Trump kuwa angependa kumsaidia akiwa nje tokea 11/30 na mda wote Trump alikuwa kimya.

Kuna tofauti kati ya kuondolewa na kujitoa.
Ni pigo kwa loyalist wanaoona kusalitiliwa. Giuliani hatakuwa katika cabinet kabisa

Sio lazima watu wa karibu wote wawe kwenye cabinet, kuna nafasi zingine.

Trump alisema, "I will call upon him for advice and can see an IMPORTANT place for him in the Administration at a later date"

Trump anamfikiria CEO wa Exxon Mobil, Rex Tillerson
Tatizo la CEO huyo ni mahusiano yake na Russia na Rais Putin
PE Trump aliweka wazi toka mwanzo nia yake ya kutaka kuelewana na Russia. Hiyo ni significant shift katika foreign policy za US na Wamarekani walimchagua Rais ambaye sio 'aggressive' kwa Russia.

Inafahamika kuwa Tillerson amekuwa akipinga Sanctions alizopigwa Russia na kudai hazina maana.

Ishu hapa ni kuwa na SoS na Rais ambao sio aggressive kwa Russia, ambao wanataka kumchukulia Russia kama 'rafiki' na mwishowe kumuondolea sanctions. Baadhi ya Establishment ndio wana tatizo na hilo.

Lakini mwisho wa siku Trump atamteua Tillerson kuwa SoS na ataidhinishwa.
Ikitokea Mitt kuachwa SoS, Gavana atakuwa amedhalilika sana.

Pengine itakuwa sawa na yeye (Romney) alivyomdhalalilisha sana Trump kipindi cha kampeni.

Hasira hizo zitambana Trump katika seneti ambako the establishment wapo.
Baada ya Senator John McCain, Lindsey Graham (senators ambao hawakufurahishwa na Trump kumsifia Rais Vladimir Putin) na Mitch McConnell kuzungumzia suala la Russia, umepata matumaini kuwa kuna Republicans watawaunga mkono Democrats kupinga teuzi za Trump!! Usijipe matumaini hewa!

Hakuna tatizo kwa Senator wa Republican kusema kwamba anasubiri 'fair' Senate hearing ili aweze kufahamu mambo ya msingi kuhusu mtu alieteuliwa na Trump.
 
Kweli mapenzi hupofusha! Just imagine for one moment that the shoe was on the other foot and that it was the GOP that lost the election with all this cloud hanging over the Democrat's win! Just imagine Donald Trump won the popular votes but lost the electoral votes! Just imagine tea-partiers suspected the outcome of the election was influenced by the Soviet action of hacking the Republican party! Just imagine...

Just imagine the the outcry, the hubba-hubba, the uproar, the tumult, the screech, the hullabaloo, the convulsion, the hoo-ha, the protest, the cry...but here is Nyani Ngabu trying to play it all down simply because he'd rather have Trump than Clinton! One thing I can say without any doubt is that what we are seeing and hearing today would be like child's play compared to what Republicans led by Trump would do.

In 2008 if anybody was given the mandate by Americans it was Obama but even with his overwhelming victory, the Republicans never gave him a chance. One notable Republican named Donald Trump never once accepted the legitimacy of Obama's presidency. Not even after a repeat performance in 2012 did it ever sink into their heads that Americans had made their choice...Nyani Ngabu was also one such Republican.

I am never blinded by party politics. Never.

I call things as I see them and that's why I told Nguruvi3 if the shoe was on the other foot the same thing would be happening.

So what the hell are you talking about, fool?

Read and understand things before you start running your mouth.
 
Republicans never gave him a chance.

Not true.

Democrats passed ObamaCare when they had 60 Senators and a House majority, remember there was like six months in 2009 when they had filibuster proof majority in the Senate?

But when their House majority vanished they didn't wanna use the reconcilliation bill to pass deficit neutral reforms.

The House majority switched to Republicans in Nov 2010 because of Americans' anger with with Pres. Obama, his Affordable Care Act, large budget deficits and the weak economy.

Don't blame Republicans for Pres. Obama's failures, blame Democrats including Pres. Obama for doing nothing in those two years.
 
The whole thing was a sham and it fell flat on its face.

So now on to the next one: Russian hacking.

Indeed Trump is a tricky virus.
Huoni ilivyo nzuri kwake, kwamba no more innuendos!

Nadhani kuna kitu tujifunze hapa, kwamba wenzetu process zako zipo open
Mtu akidai haki inatendeka. From the very beginning nilisema, Trump hakuwa na sababu za ku react, the process ndiyo ina clear doubts

Sasa hili la Russia hacking reaction yake si nzuri. Limeanzishwa na kuendelezwa na Bipartisan. Trump anasema CIA hao ndio waliongopa kuhusu Saddam. Hii maana yake anafanya kazi na security apparatus asizoziamini

He won decisively hana sababu za kujenga mazingira ya kuonyesha ana hofu

Uchunguzi ufanyike na conclusion itolewe.
Na upo uwezekano, haya yametoka Dem au other sources

Now, in order to clear doubt aache kuzozana na security organs au congress

He is pres elect
 
Huoni ilivyo nzuri kwake, kwamba no more innuendos!

Nadhani kuna kitu tujifunze hapa, kwamba wenzetu process zako zipo open
Mtu akidai haki inatendeka. From the very beginning nilisema, Trump hakuwa na sababu za ku react, the process ndiyo ina clear doubts

Sasa hili la Russia hacking reaction yake si nzuri. Limeanzishwa na kuendelezwa na Bipartisan. Trump anasema CIA hao ndio waliongopa kuhusu Saddam. Hii maana yake anafanya kazi na security apparatus asizoziamini

He won decisively hana sababu za kujenga mazingira ya kuonyesha ana hofu

Uchunguzi ufanyike na conclusion itolewe.
Na upo uwezekano, haya yametoka Dem au other sources

Now, in order to clear doubt aache kuzozana na security organs au congress

He is pres elect

Mzee...naona una gloss over political motivation iliyopo.

Hivi kabisa unaamini huyo Jill Stein alitaka hiyo recount kwa nia njema?

Unaamini kabisa kuwa hakuna mkono wa Dems nyuma yake uliokuwa unamsukuma kuomba hizo recounts?

Halafu hujaona kabisa jinsi narrative inavyobadilika? Ilikuwa recounts na sasa imekuwa Russian hacking na tayari baadhi ya Dems wanawaaza wale electoral college electors wasimchague Trump.

Yaani kabisa unataka kunambia hakuna politricks zinazoendelea hapo?

Hebu soma hii....

A Democratic lawmaker is desperately lobbying the Electoral College to shun Donald Trump, and vote for Hillary Clinton — even though he conceded Monday that the Republican won the election “fair and square.”

The plea from Rep. Jim Himes (D-Conn.) comes a week before the Dec. 19 vote, which is expected to affirm the results of the Nov. 8 election, in which Trump beat Clinton with 306 Electoral College votes.
 
HACKING
Habari nyingine ni hacking kutoka Russia. Wiki hii Obama aliagiza vyombo vifanye uchunguzi

Zipo taarifa za intelligence community kuhusisha Russia na interference ya uchaguzi wa Marekani

Maseneta 4, wawili kila chama wametengeneza Bipartisan letter ya uchunguzi wa kina ufanyike
Trump na kampeni yake wanapinga suala wakisema suala halitabadili matokeo ya uchaguzi

Hapa kuna hoja mbili za kuelewa

Trump na transition wanasema hizi ni mbinu za kutaka kuondoa uhalali wa ushindi na Urais wake
Maseneta wanasema ni suala la kuchunguzwa na si kubadili matokeo kwanini nchi za kigeni ziingilie

Utata
Kwavile uchunguzi unataka kubaini kama kuna mataifa ya nje yanayoingilia uchaguzi wa Marekani, na kwavile WH na Maseneta wanasema lengo si kubadilisha matokeo, kwanini Trump hataki lifanyike?

Hebu tujiulize, kwanini Rais Obama anakuja na hili suala ya 'full review' ya Russian hacking mda huu (why now?), kwanini sio kabla ya uchaguzi?

Intelligence agencies zilishadai kabla ya uchaguzi kuwa DNC na baadhi ya Democrats walikuwa hacked na Russia, kwanini Rais Obama hakutaka 'full review' kipindi hicho? Au kwa sababu aliamini hakuna namna Trump atafika 270?

Ili kuiongezea uzito, wanasema hiyo 'full review' itakayoongozwa na DNI itaenda mbali na kuhusisha uchaguzi wa mwaka 2008 ambapo ilisemekana China iliingilia uchaguzi wa US. Kwanini hakuagiza uchunguzi ufanyike mwaka 2009? Au kwa sababu alishinda uchaguzi? Huu ni unafiki mkubwa kutoka kwa Rais anaendoka madarakani na legacy ya kufeli.

Kwanza ieleweke kuwa ni 'full review' ya rumours tu na hamna ushahidi wa wazi. Rep. Davin Nunes (Chair wa House Intelligence Committee) amesema "There is no clear evidence - even now, there's a lot of innuendo, lots of circumstantial evidence, that's it."

CIA wanadai kuna watu wenye 'connections' na serikali ya Russia wali-hack computers za DNC na RNC na kuamua kuwatumia WikiLeaks documents mbaya za DNC na John Podesta et al.. Lakini watu haohao waliamua kutowatumia WikiLeaks documents za RNC. Purely Circumstantial!

RNC wamesema hawakuwa hacked na wana ushahidi, na kwahiyo taarifa ya CIA inakuwa na walakini.

Labda ndio maana FBI wanapishana na CIA kuhusiana na suala la 'Russian hacking'. FBI wamesema hawajaona evidence beyond reasonable doubt kuhusiana na hayo madai.

Rais Obama ameagiza baada ya 'full review' apewe ripoti kabla hajaondoka madarakani!! Kwanini kabla hajaondoka madarakani?

Rais Obama anataka Rais Trump aonekane kama 'puppet' wa Russia na kwamba Russia ndio wamemfanya Trump kuwa Rais na sio wananchi waliochoka wanasiasa na kuamua kumpigia kura Trump kwa wingi na kumpa ushindi katika Swing States 9 kati ya 13 na kushinda States 30. Absurd.

Hizi blah blah za Rais Obama ni katika kutaka kubadilisha msimamo wa Trump kuhusiana na Russia, ili asiwaondolee sanctions + awe aggressive. Ni katika kumzuia Trump kumteua Secretary of State ambae ana maelewano mazuri na Putin. Trump yupo smart sana zaidi ya Rais Obama na anajua mchezo mzima.
 
Back
Top Bottom