Duru za Siasa: Matokeo ya Uchaguzi Marekani

Mkuu Nguruvi3 na Mag3 asanteni kwa kutuleteeni updates hapa. Ila week iliyopita nilileta hoja zangu hapa kuwa Trump atashinda mkaniona kuwa mimi sijui lolote.
HC alikuwa anabebwa na media na nyie mkawa mnaziokota habari zake hivyo hivyo bila kuzipima.

[emoji12] Poleni sana team HC, maana naona mmevyata kimya, hamna ule msisimko wa mwanzoni
 
..Duh!!

..kwa kweli haya ni maajabu.

..katika kufuatilia kwangu chaguzi za Marekani, huu ni uchaguzi wa kipekee wa aina yake.

..Sasa ni kazi iko kwa Raisi Donald Trump to deliver on his campaign promises.

..Kwa sisi tulioko dunia ya tatu nadhani tukae chonjo.
 
Mkuu JokaKuu wengine tulikuwa tukisema hapa tunabezwa. Ukweli HC alikuwa hatakiwi ndo maana ukiangalia ametumia nguvu kubwa sana kwenye kampeni. Waafrika wengi walimezeshwa na taarifa za Mainstream media za ndani na nje ya marekani. Hata polls zilikuwa za kulaghai watu. Mainstream media zilikuwa haziandiki habari zozote nzuri kumhusu Trump. Leo wakati akihojiwa na bbc Professor fulbert namwamba alikiri kuwa polls za uchaguzi zilikuwa za kutengeneza ndo maana matokeo hayajaenda sawa na zilivyoonyesha.

Kwa kawaida kura za maoni huwa haziendi tofauti na matokeo. Km trump angesaidiwa km HC huu uchaguzi usingekuwa hivi.
 

..polls hazikuwa za kutengeneza.

..ila kilichotokea ni kitu kipya ktk mchakato mzima wa uchaguzi wa Marekani.

..kwasababu ni jambo jipya ndiyo maana halikuweza kutabiriwa kupitia polls.

.. kundi lililowezesha Trump kuchaguliwa linajumuisha wapiga kura wapya ambao maoni yao hayakuweza kuwa captured na njia na taratibu zilizozoeleka za kukusanya kura za maoni.

..Trump went into this election believing in MIRACLE. And, yes, a miracle happened.

..Hilary Clinton ameshindwa lakini hajashindwa vibaya kuasi cha kusema alikuwa hatakiwi. This election was very close.

..Hakuna tofauti kubwa ktk idadi ya POPULAR VOTES pamoja na ELECTORAL VOTES baina ya
wagombea hawa wawili.

..Habari hii imekuwa kubwa kwasababu wachambuzi wengi walitegemea Hillary Clinton atashinda.
 
Mkuu sijui kama unaelewa maana ya kuchambua. Halikuwa suala la kuandika nani atashinda nani atashindwa, bali kujadili mchakato mzima.

Hili tuliandika wiki iliyopita, angalia tofauti ya kusema atashinda au atashindwa na tulivyoandika. Hata unaposema anabebwa bado upo wrong kwasababu hujatueleza ni kwa namna gani.

Kwa taarifa yako Putin akampongeza Trump na kusema Russia ita restore full relationship
Unajua maana yake? Kuna factors nyingi za kuangalia kutoka diffent angle na ndicho tunafanya.

Tulichosema ni kuwa ushabiki wa simba na yanga hautusaidii.

Hivi unataka kusema hukujifunza kitu?
Na kama ingalikuwa Fulani atashinda Fulani atashindwa hiyo ingetusaidi?
Soma tena Halafu tukaendelea hapa
Mkuu hapa ina maana hukuona kitu au kupata hata moja linalofanana au kutoa picha ya matokeo?
 
Hapana polls zinaweza kuwa zipo sahihi.

Mfano waliposema Michigan ni battleground baada ya ku lean Dem, huoni kuna ukweli?
Fuatilia polls utaona nyingi zilikuwa na usahihi wa aina Fulani

Kilichotokea ni factors ambazo wakati mwingine hazina control.

Kwa mfano sampling ya polls inaweza kuwa sahihi, kikatokea kitu kingine nje ya hapo na kuharibu kila kitu

Ukifuatilia polls nyingi zilionyesha tight race mwishoni, hakuna aliyejua Wisconsin na Michigan zinaweza kuwa katika play.

Hakuna aliyejua vijijini kuna watu wengi waliaoshiriki kuliko nyuma

Hakuna aliyejua impact ya Comey au WikiLeaks. Utaona kila kitu kimetokea nje ya normal

Polls nyingi zilinyesha economy ni issue lakini to what extent?

Hakuna anayejua mpact ya WikiLeaks kwa Democrat yenyewe na kwamba kunawezekana ipo disfranchise ya Team Bernie Sanders ambayo ni reservations usioweza kuibani kwani ipo kwa mtu

Hakuna aliyeweza kujua women hawapendani kwani ipo kwa mtu

Hakuna anayeeleza kwanini white wame vote kwa wingi kwasababu hilo lipo ndani ya mioyo ya watu. Kunawezekana wana reservations zao tofauti

Hakuna anayejua impact ya policy zilizopo, zipo ndani ya mioyo ya watu

Tena kuanzia mwanzo tulisema polls zina errors zake

Tofauti pengine iliyopo ni jinsi gani tunaangalia suala na si suala la yule MaU huyu Arsenal

Nina uhakika si suala la kushinda au kushindwa bali wapo waliojifunza mengi ambayo ni kupitia uchaguzi. Kwa mfano, wakati tunaleta update jana tuliongelea America territories na Washington DC kwanini zina mchango tofauti katika election za Marekani na zina impact vipi

Na kadri tunavyosonga mbele tutaendelea na mjadala kunyumbulisha matokeo ili kujifunza

Kitu ambacho wengine hatutafanya n kuleta uzi ' Trump atashinda, no Clinton atashinda' kwasababu kusema hivyo hai add value katika knowledge na understanding na si njia bora ya kujifunza kutoka kwa wengine. Sote tunajifunza na hakika nimejifunza mengi

Lakini pia jiulize kwanini wachambuzi, institutions zote na sehemu kubwa ya dunia imepigwa mshangao kama ule wa Brexit?
 
..sasa wale waliosema uchaguzi wa Marekani unaweza kuwa rigged sijui wana maoni gani.

..Trump anatakiwa ajipange kwelikweli. Hizi kura alizopata zinaonyesha jambo moja, kwamba Wamarekani wana matatizo na wanataka yatatuliwe bila kuchelewa.
 
..sasa wale waliosema uchaguzi wa Marekani unaweza kuwa rigged sijui wana maoni gani.

..Trump anatakiwa ajipange kwelikweli. Hizi kura alizopata zinaonyesha jambo moja, kwamba Wamarekani wana matatizo na wanataka yatatuliwe bila kuchelewa.
Na hapo ndipo anaanza na challenges. Kwa mfano, ikitokea suala la ugaidi hata uwe kidogo kwakwe ni kipimo.
Yale yote aliyosema lazima yahitaji 'delivery' na mengi utayaona katika complicated world yanachangamoto zake.
 
Na hapo ndipo anaanza na challenges. Kwa mfano, ikitokea suala la ugaidi hata uwe kidogo kwakwe ni kipimo.
Yale yote aliyosema lazima yahitaji 'delivery' na mengi utayaona katika complicated world yanachangamoto zake.


..
JokaKuu
Mwanzoni atafanikiwa kwasababu wana control ya Senate na House. Kadri siku zinavyosonga utaona hali itakavyokuwa, akitakiwa ku deliver huku system ikifanya 'check and balance'

..wasiwasi wangu ni kama ataweza ku-deliver kwa Wamarekani walioko rust-belt.

..lingine ni kama ataweza kurekebisha race relations baina ya Wamarekani.

..halafu kuna suala la immigration na UKUTA alioahidi kuujenga. Sijui kama watu wanakumbuka ahadi ya Obama kuhusu kulifunga gereza la Guantanamo.

..kufanya kampeni, na kutawala, ni mambo mawili tofauti.

NB:

..wananchi wanaweza kuchagua democrats kwenye mid term elections na kupelekea Trump kukwama kama ilivyotokea kwa Obama.
 
Tena aliyawekea muda wa siku 100

Kwa mfano kufuta Obamacare kutaleta 'crisis' hilo linaonekana. Inaweza kuwa si perfect lakini 22M utawaeleza nini kama si kuwapa kilicho bora? Na kilicho bora hajasema Zaidi ya kufuta Obamacare

Pili, watu wa rust belt watamwangalia kwa matumaini makubwa hasa katika viwanda
Hapa ataingia katika mambo ya trade. Je, ataweza kufanya trade kama inavyotegemewa?

Ukuta anatakiwa aujenge na Mexico walipe. Ataendaje senate au congress kuwaambia anataka pesa wakati kuna midterm elections. Seneti na Congress wataogopa kupoteza

Nne, gun control ameahidi kila mtu awe nayo. Yakitokea mauaji kama ilivyokuwa atawaambia Wamrekani solution gani? Tayari kaahidi ku keep second amendment 100%

Tano, suala la race halijaisha na wala halitaisha. Ameahidi law and order. Je ni kwa nani?
Polisi au waathirika kama wanavyodai? Na tension itakuwaje kati ya black and white na ana solution gani

Sita, hajaeleza nini atafanya Syria na kwingineko. Kuanzia Tarehe 20 Jan atakuwa Rais wa 'dunia'
Je atakwenda sambamba na Russia?

Saba, nini hatma ya siasa za nje za Marekani kuhusu majeshi na washirika?
 
Trump anayo miaka miwili ya kuonesha uongozi na katika hiyo miaka miwili misingi ya legacy atakayoiacha itaangaliwa, kupimwa na kuhakikiwa kama ni thabiti. Kama Obama, miaka minane iliyopita, kapewa Urais na Congress na hapo ndipo atafuatiliwa kwa makini kafanikisha nini katika hiyo miaka miwili.

Kosa la Obama ilikuwa ni kusita kutekeleza ahadi zake akijikita zaidi kwanza katika kutafuta muafaka na ushirikiano wa Republicans na alipogutuka kwamba si rahisi akawa tayari amechelewa. Wamarekani wanachoangalia ni mafanikio na hawataki kisingizio cha kutopata ushirikiano kutoka upande wa pili.

Hilo ni somo tosha kwa Trump kama anafundishika kwamba pamoja na kufanya jitihada za kuleta muafaka, baada ya miaka miwili watampima kwa matokeo na si jitihada tu. Kapewa congress nzima (house na senate) na kama katika muda huo wa miaka miwili hakufanikisha ahadi zake ajue mwaka 2018 atawajibishwa.
 
Naenda kwenye hoja zako Mwalimu wangu!

1.Poll zilitengenezwa na MSM...na wafuatiliaji wa mambo kuficha ukweli huu MSM hasa cnn.com walikuwa wanaficha picha za rally za 'mama'. Inasemekana wala alikuwa hajazi umati. Pia Democrats walikuwa wanaogopesha watu kuhudhuria kampeini za Trump (wala siyo za Republican maana walimsusia) kwa kuleta vurugu. Ushahidi upo.
2. wapiga kura wapya?Mkuu ebu fafanua.
3.No, mtu wa kuamini kwenye miracle hawezi kutamka kuwa wewe mwenyekiti wa chama endelea na kampeini nyingine mimi niachie kampeni ya Urais (Baada ya mwenyekiti wa Rep kususa); mtegemea miracle hawezi kutamka kuwa sitakubali matokeo kama sitashinda tena nchi yenyewe US. yule ni mfanyabiashara mzoefu, alishapiga hesabu zake vizuri alijua bila rigging anashinda na imekuwa (exposure ya rigging techniques za system za US kwa msaada wa WikiLeaks zimesaidia kuzuia wizi wa kura, kura zililindwa kwa namna hiyo; establishment, soros, wall Street elites et.al they were caught unprepared)
4.'Mama' asingepoteza majimbo ambayo alikuwa anajinasibu kuchukua mfano Penn ,nadhani convention yao ilifanyika huko. 'Mama' alikuwa hatakiwi
5.weka takwimu.
6.Wachambuzi wengi walikuwa 'paid ' for the job Kuhakikisha poll zinapata justification
====
Haya ni maoni yangu ,Nitaendelea kupitia post nyingine
 
1. Baadhi tulijua madhara ya wikileaks, na tukajaribu kuyaeleza hapa, ingawa hatukueleweka!
2.Wanawake wanapendana ila wanachukia ulaghai na kusingiziana. Ile ya Hillary kutumia wale wa mama kumsema vibaya Trump tena bila ushahidi iliwakera wanawake wengi. Mwanzoni Hillary kabla ya kuharibu alikuwa na back up kubwa ya wamama kiasi cha Trump kusema Hillary hana lolote isipokuwa nakuwa protected na 'woman factor '!
3.Ni kweli policy za serikali ya Obama na establishments wao hasa zile za ndani zinazolenga kuwadhibiti middle class na wale wa vipato vya chini zimechangia Trump kushinda.
4. Zimepigwa na butwaa kwani kwa nguvu kubwa iliyotumika kumbeba Hillary kwenye kampeni ingeweza kuwa dissolved na jeshi la 'mtu mmoja, Trump '
 
Mkuu it's too early kujua nini kimesababisha na bandiko langu ulilonukuu sija single out sababu halisi

Nilichosema ni kuorodhesha wachunguzi wanayoyafanyia kazi kwa takwimu
The notion kwamba alibebwa bila kuwa na back up evidence(s) hazileti mantiki

Kwa mfano, kushindwa kwa Clinton katika blue state utakuelezaje kwa hoja hapo juu?
Tayari wachunguzi wanasema Clinton alichukulia Wisconsin for granted.

Tangu primaries hakurudi tena, Trump amekwenda mara kadhaa VP wake na Speaker Ryan wakizunguka, wapiga kura walipiga kwa kusikiliza hoja za Trup pekee

Sasa ukitazama 'facts' zako hakuna inayo fit narrative hata moja.

Pili, wanafuatilia kwanini idadi ya white imeongezeka wakati blacks ikipungua na Latinos wakiwa hawana effect iliyotarajiwa kwa Clinton?conclusion yako hai fit popote

Tatu,wanaangali ni Comey au WikiLeaks ipi ilikuwa na impacts. Kwa mfano, WikiLeaks zilitoa habari za kampeni za primaries, je, wafuasi wa Sanders walio retaliate

Nne, Kampeni ya Clinton kabla ya Comey ilikuwa inafanya mkutano mmoja kwa siku, Trump akifanya mine au mitano. Je, kampeni iliwafikia watu wa vijijini?

Tano, ukiangalia mikutano ya Trump ilikuwa inajaza watu . Hawa walikuwa wapi na wana reservation gani kuhusu system au mgombea?
Ni watu wa Republican? Ni watu wa GOP na Sanders, ni independents au ni kitu gani

Sita, kwanini wanawake waliotegemewa kumuunga mkono hawakufanya hivyo.
Lazima data zipatikane kwa locations n.k. Kama wanawake wamechukizwa na kashfa za wenzao, wanaume wamechukizwa na nini? Kwa analysis yako hakuna jibu

Saba, kunatakiwa takwimu za college educated, non educated na kwanini kuna tofauti

Nane, kunatakiwa analysis kuhusu uchumi na suala zima la jamii kama race

Tisa, kama chuki ni establishment kwanini katika congress na senate wamerudi wengi?

Kumi, yale aliyozua Trump yalipokelewaje na wapiga kura

Kumi na moja, kuna uhusiano gani wa BREXIT na Uchaguzi.
' Is it the new world order politically''

Orodha inaendelea. Ndiyo maana watu wanachanga akili kujua nini kimetokea

Hapa wenzetu wanapotuzidi, kwamba, wanafanya postmortem ya kila jambo kwa kina

Kusema Prof kasema si fact, ni maoni Prof mwingine anaweza kuwa tofauti.

Nimeandika haya kama yupo atakayenielewa.

Watanzania hatuna utamaduni wa kufuatilia mambo.

Nimesoma maoni ya mswada unaopelekwa kuondoa watumishi baadhi kutoka utumishi
Hakuna anayehoji ni kwanini imetokea, huko nyuma ilikuwaje na imelenga nini na impact yake ni kitu gani. Mwisho wa siku watu wanashtukizwa tu na kuanza kulalama

Hili linazidi kueleza hata upande wa siasa. Baada ya uchaguzi hakuna anayefanya analysis kwanini CCM ikiwa imechukiwa na wananchi bado imeshinda.

Je, ni system ilitotumika kuwahujumu? Na kama ni ndiyo ni ipi na kwa njia gani?
Je, ni sera zao zisizokubalika, kama ni hivyo eneo gani hawakugusia
Je, ni wagombea wao na agenda za taifa? Na kama ndivyo nini kinafanyika

Dunia ya sasa is all about how you interpret information etc

Tusemezane
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…