Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #181
TUMEFIKAJE HAPA HADI KUALIKA FBI (Sehemu ya pili)
Inaendelea.......
Katika mazingira ya kawaida, wataalamu wa Tanzania wanaoifahamu kijiografia, kisiasa, kikabila, dini n.k. ndio walipaswa waongoze uchunguzi. Endapo tungekuwa na vyombo vya usalama vya miaka ya 70 na 80 nina hakika tungekuwa tunafahamu mengi zaidi ya tuyajuayo leo.
Ninashangaa eti serikali ya mapinduzi Znz impeiga maruku CD, DVD na kila kinachohusu uchochezi.
Huku bara nako kumekuwa na kamati za usuluhishi kana kwamba tatizo ni la waumini na si watu wachache.
Mbinu zote hizo ni dhaifu sana na zinaonyesha kiwango gani usalama wa taifa ulivyo njia panda.
Ningedhani uchunguzi ungefanywa na wataalam katika fani mbali mbali kuja na suluhu na si masuala ya kisiasa.
Kuzuia CD na DVD bila kuwashughulikia wanatoa maudhui, wanaotengeneza na kusambaza hizo DVC na CD ni kazi bure na ya kiwango hafifu sana.
Tatizo si DVD au CD, tatizo ni wale wanaotengeneza vitu hivyo kwa kushirikiana na wale wenye maudhui ndani ya vitu hivyo.
Kuwaita viongozi wa dini wazungumze ni njia nyingine dhaifu na ya ajabu sana ya kukabiliana na tatizo.
Viongozi wa dini hawana matatizo na wala waumini wao hawana matatizo.
Matatizo yapo kwa vikundi vya watu wachache ambavyo vimeteka ajenda ya dini na kuingizia hisia zao kwa ajili ya masilahi yao.
Sidhani kuwa kadinali Pengo anaweza kuzuia wendawazimu wachache wanaotaka kufanya uhalifu.
Sidhani kuwa sheikh mkuu anaweza kuzuia wendawazimu wachache wanaotaka kufanya uhalaifu.
Na wala sidhani kuwa kadinali na sheikh mkuu wametoa amri za vikundi hivyo kuendeleza chuki na fitna katika jamii.
Sasa kama hilo siyo, kwanini basi wao wabebeshwe mzigo wasiojua unatoka wapi na kwanani na unaelekea wapi?
Kuwaita wajadiliane ni upotezaji wa muda, ukosefu wa maarifa na umbumbu wa hali ya juu sana the least to say.
Nilidhani hili lilikuwa jukumu la idara ya usalama wa taifa siku nyingi sana.
leo wangeshakuwa na orodha ya watu wenye kunuia au wanaojipanga kufanya uhalifu.
Kazi yao ingekuwa kuchuja na kubaki na mashudu.
Eti hawajui na wanawaita FBI? Real! kwamba FBI wanawajua wadogo zetu zaidi ya sisi wenyewe.
Vyombo vya usalama vinahitaji modernity. Hizi si zama za kubeba bunduki au kufuatilia wanasiasa majukwaani.
Hizi si zama za kung'oa watu kucha au kutuma watu wakamtoe mtu jicho.
Kweli ndio usalama wa taifa? I mean serious!
Nabaki kusema vyombo vya usalama ndio tatizo, mabomu na risasi, mauaji, mateso na kiwacho ni matokeo ya ulegevu wa vyombo hivyo. Ni matokeo ya vyombo hivyo kuwa sehemu za ajira tu kwa watu kwavile wazazi au ndugu zao wanalindana na wala hakuna suala la utaalamu
Lingekuwepo basi wataalamu hao wangeshaiona hatari tuliyo nayo mapema sana na wala tusingefika hapa tulipo.
Lakini inatosha kuvilaumu vyombo hivyo?
Jibu ni ndio kwa vile vimebeba dhamana, na ni hapana kwasababu vinafanyakazi chini ya maelekezo ya serikali.
Ni kwa msingi huo viongozi wake ni wateule wa Rais na wanawajibika kwakwe.
Sasa vyombo hivyo vikishindwa kazi maana yake si kuwa vimeshindwa bali serikali imeshindwa kuvisimamia vifanye kazi tarajiwa.
Kwa msomaji wangu wa duru nadhani utakuwa umeelewa japo kwa uchache maana na dhana nzima ya kile ninachokiongelea
Tusemezane
Inaendelea.......
Katika mazingira ya kawaida, wataalamu wa Tanzania wanaoifahamu kijiografia, kisiasa, kikabila, dini n.k. ndio walipaswa waongoze uchunguzi. Endapo tungekuwa na vyombo vya usalama vya miaka ya 70 na 80 nina hakika tungekuwa tunafahamu mengi zaidi ya tuyajuayo leo.
Ninashangaa eti serikali ya mapinduzi Znz impeiga maruku CD, DVD na kila kinachohusu uchochezi.
Huku bara nako kumekuwa na kamati za usuluhishi kana kwamba tatizo ni la waumini na si watu wachache.
Mbinu zote hizo ni dhaifu sana na zinaonyesha kiwango gani usalama wa taifa ulivyo njia panda.
Ningedhani uchunguzi ungefanywa na wataalam katika fani mbali mbali kuja na suluhu na si masuala ya kisiasa.
Kuzuia CD na DVD bila kuwashughulikia wanatoa maudhui, wanaotengeneza na kusambaza hizo DVC na CD ni kazi bure na ya kiwango hafifu sana.
Tatizo si DVD au CD, tatizo ni wale wanaotengeneza vitu hivyo kwa kushirikiana na wale wenye maudhui ndani ya vitu hivyo.
Kuwaita viongozi wa dini wazungumze ni njia nyingine dhaifu na ya ajabu sana ya kukabiliana na tatizo.
Viongozi wa dini hawana matatizo na wala waumini wao hawana matatizo.
Matatizo yapo kwa vikundi vya watu wachache ambavyo vimeteka ajenda ya dini na kuingizia hisia zao kwa ajili ya masilahi yao.
Sidhani kuwa kadinali Pengo anaweza kuzuia wendawazimu wachache wanaotaka kufanya uhalifu.
Sidhani kuwa sheikh mkuu anaweza kuzuia wendawazimu wachache wanaotaka kufanya uhalaifu.
Na wala sidhani kuwa kadinali na sheikh mkuu wametoa amri za vikundi hivyo kuendeleza chuki na fitna katika jamii.
Sasa kama hilo siyo, kwanini basi wao wabebeshwe mzigo wasiojua unatoka wapi na kwanani na unaelekea wapi?
Kuwaita wajadiliane ni upotezaji wa muda, ukosefu wa maarifa na umbumbu wa hali ya juu sana the least to say.
Nilidhani hili lilikuwa jukumu la idara ya usalama wa taifa siku nyingi sana.
leo wangeshakuwa na orodha ya watu wenye kunuia au wanaojipanga kufanya uhalifu.
Kazi yao ingekuwa kuchuja na kubaki na mashudu.
Eti hawajui na wanawaita FBI? Real! kwamba FBI wanawajua wadogo zetu zaidi ya sisi wenyewe.
Vyombo vya usalama vinahitaji modernity. Hizi si zama za kubeba bunduki au kufuatilia wanasiasa majukwaani.
Hizi si zama za kung'oa watu kucha au kutuma watu wakamtoe mtu jicho.
Kweli ndio usalama wa taifa? I mean serious!
Nabaki kusema vyombo vya usalama ndio tatizo, mabomu na risasi, mauaji, mateso na kiwacho ni matokeo ya ulegevu wa vyombo hivyo. Ni matokeo ya vyombo hivyo kuwa sehemu za ajira tu kwa watu kwavile wazazi au ndugu zao wanalindana na wala hakuna suala la utaalamu
Lingekuwepo basi wataalamu hao wangeshaiona hatari tuliyo nayo mapema sana na wala tusingefika hapa tulipo.
Lakini inatosha kuvilaumu vyombo hivyo?
Jibu ni ndio kwa vile vimebeba dhamana, na ni hapana kwasababu vinafanyakazi chini ya maelekezo ya serikali.
Ni kwa msingi huo viongozi wake ni wateule wa Rais na wanawajibika kwakwe.
Sasa vyombo hivyo vikishindwa kazi maana yake si kuwa vimeshindwa bali serikali imeshindwa kuvisimamia vifanye kazi tarajiwa.
Kwa msomaji wangu wa duru nadhani utakuwa umeelewa japo kwa uchache maana na dhana nzima ya kile ninachokiongelea
Tusemezane