Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
-
- #221
Inaendelea.....
Tanzania: Ujio wa Obama Tanzania ni wa kiuchumi zaidi.
Tukumbuke kuwa Rais wa China mara baada ya kuapishwa alikuja Tanzania.
China ina miradi mingi sana Afrika hata kufikia kujenga makao makuu ya AU kwa gharama zao. Imejiingiza katika kila nchi kutoa misaada ya ujenzi, ufundi n.k.
Interest za China kwa Tanzania ni zaidi ya sehemu nyingine za Afrika kwasababu, kwanza, Tanzania ilisimama kidete wakati wa suala la China kuwa katika UN.
Ni kwa kutazama hilo China inaona Tanzania ni muhimu na ni rafiki anayeaminika.
Kwa kulipa fadhila hizo China walijenga Tazara, mradi mkubwa waliowahi kuufanya barani Afrika.
Lakini pia kimkakati Tanzania ipo mahali pazuri. Sasa hivi China imejiingiza sana maeneo kama Congo na Zambia, na Tanzania ni eneo muhimu la kuingiza na kutoa bidhaa zao.
Tanzania inaonekana kuwa ni uchumi unaokua, kwamba hilo lina ukweli inabaki kujadiliwa.
Kilicho na ukweli ni kuhusu maliasili kama madini na gesi ambazo ni muhimu sana kwa matumizi ya nishati ambayo China inayahitaji kukuza uchumi wake.
Ukuaji wa uchumi wa china ni kiwango cha asilimia 8-9 kwa mwaka, na wachumi wanatabiri kuwa kama hali itabaki kama ilivyo China itakuwa na uchumi nambari 1 baada ya miaka 10-15 ijayo
China na Marekani zinatambua kuwa uchumi wa Afrika unakua kwa kasi na ni moja ya chumi 10 zinazokua kwa kasi duniani(namba 6)
Wachumi wanatabiri kuwa katika miaka ijayo Afrika utakuwa uwanja wa vita ya kiuchumi kati ya Mashariki na Magharibi,Kwahiyo ziara ya rais wa China ilikuwa kuweka mambo sawa kabla ya wapinzani hawajatia timu(U.S.A)
Ujio wa obama umelenga kiuchumi zaidi na kwa kiasi fulani kiusalama.
Kiusalama ni kuzingatia kudorora kwa hali ya pembe ya Afrika (Somalia) ambako ni kiota cha kuzalisha magaidi wa siku za baadaye, na pia usalama wa maziwa makuu
Tanzania ina moja ya balozi kubwa za Marekani katika sub sahara.
Balozi za Marekani ni za kiusalama na kiuchumi na uwepo wake una sababu.
Hivyo Tanzania kama ilivyo Senegal ipo katika eneo la mkakati kiusalama
Ziara ya Obama itamchukua hadi kuzindua mradi wa umeme unaosimamiwa na GE Co.
Hii ni kampuni kubwa sana Duniani kiasi cha kujiuliza kuna nini hadi iwekeze Tanzania katika nishati?
Jibu hapa ni geresha tu kuwa Wamarekani wana interest ya kusaidia katika nishati .
Nyuma yake kuna suala la gesi na madini kama vile Uranium.
Mkakati ni kuhakikisha kuwa maliasili hizo hazitumiki au kutumiwa ''vibaya'' na wapinzani wa Marekani kiuchumi.
Siku zijazo watakuwa na sababu za kusema wao walianza kuwekeza katika nishati miaka mingi iliyopita
Na katika kuficha lengo la ziara hiyo Rais wa zamani G.Bush amekuja kusimamia ujenzi wa Clinic ya Kansa. Ni Bush huyu huyu aliyesaini Millenium Challenge na ni Bush huyo huyo aliyegawa vyandarau kuzuia Malaria. Rais wa Marekani agawe vyandarau???
Bush atakuwepo katika round table na CEOs na wafanyabiashara. Leo tunaonyeshwa picha akipaka rangi clinic. Hapo hapo kuna Clinton foundation ambayo nayo kama zingine inashughulikia mambo ya afya!!!
Haya yote ni kuhakikisha kuwa lengo la ziara ambalo ni kiuchumi linafunikwa ili kuepuka vita isiyo ya lazima ya kiuchumi na China au nchi za BRICS
Inaweza kuchukua miaka 10 kabla ya rais wa Marekani hajaietembelea Tanzania tena.
Kazi kubwa imeshafanywa na akina Clinton na Bush na Obama anamalizia tu.
Shughuli nyingine zitaendelea kufanywa na balozi na maafisa wa serikali ya Marekani
Tunasisitiza kuwa kazi za balozi za wenzetu si kutoa visa na kupokea wageni.
Ni pamoja na ulinzi na usalama ambavyo haviachani na uchumi.
Ni wakati sasa tujifunze kuwa balozi zetu si vituo vya visa au mapunziko kwa viongozi wastaafu, ni sehemu muhimu sana za usalama na uchumi wa nchi.
Sina hakika kama balozi zetu zilizopo Kigali, Kampala au Nairobi zinaweza kutueleza kwa ukamilifu nini kilichopo nyuma ya mkutano wa Kagame, Uhuru na Museveni.
Hiyo ndiyo sehemu ya kazi za ubalozi na lazima tubadilike na kuelewa kuwa usalama wa taifa au nchi si bunduki au kung'oana kucha ni pamoja na uchumi kwa dunia tuliyo nayo
Tusemezane
Tanzania: Ujio wa Obama Tanzania ni wa kiuchumi zaidi.
Tukumbuke kuwa Rais wa China mara baada ya kuapishwa alikuja Tanzania.
China ina miradi mingi sana Afrika hata kufikia kujenga makao makuu ya AU kwa gharama zao. Imejiingiza katika kila nchi kutoa misaada ya ujenzi, ufundi n.k.
Interest za China kwa Tanzania ni zaidi ya sehemu nyingine za Afrika kwasababu, kwanza, Tanzania ilisimama kidete wakati wa suala la China kuwa katika UN.
Ni kwa kutazama hilo China inaona Tanzania ni muhimu na ni rafiki anayeaminika.
Kwa kulipa fadhila hizo China walijenga Tazara, mradi mkubwa waliowahi kuufanya barani Afrika.
Lakini pia kimkakati Tanzania ipo mahali pazuri. Sasa hivi China imejiingiza sana maeneo kama Congo na Zambia, na Tanzania ni eneo muhimu la kuingiza na kutoa bidhaa zao.
Tanzania inaonekana kuwa ni uchumi unaokua, kwamba hilo lina ukweli inabaki kujadiliwa.
Kilicho na ukweli ni kuhusu maliasili kama madini na gesi ambazo ni muhimu sana kwa matumizi ya nishati ambayo China inayahitaji kukuza uchumi wake.
Ukuaji wa uchumi wa china ni kiwango cha asilimia 8-9 kwa mwaka, na wachumi wanatabiri kuwa kama hali itabaki kama ilivyo China itakuwa na uchumi nambari 1 baada ya miaka 10-15 ijayo
China na Marekani zinatambua kuwa uchumi wa Afrika unakua kwa kasi na ni moja ya chumi 10 zinazokua kwa kasi duniani(namba 6)
Wachumi wanatabiri kuwa katika miaka ijayo Afrika utakuwa uwanja wa vita ya kiuchumi kati ya Mashariki na Magharibi,Kwahiyo ziara ya rais wa China ilikuwa kuweka mambo sawa kabla ya wapinzani hawajatia timu(U.S.A)
Ujio wa obama umelenga kiuchumi zaidi na kwa kiasi fulani kiusalama.
Kiusalama ni kuzingatia kudorora kwa hali ya pembe ya Afrika (Somalia) ambako ni kiota cha kuzalisha magaidi wa siku za baadaye, na pia usalama wa maziwa makuu
Tanzania ina moja ya balozi kubwa za Marekani katika sub sahara.
Balozi za Marekani ni za kiusalama na kiuchumi na uwepo wake una sababu.
Hivyo Tanzania kama ilivyo Senegal ipo katika eneo la mkakati kiusalama
Ziara ya Obama itamchukua hadi kuzindua mradi wa umeme unaosimamiwa na GE Co.
Hii ni kampuni kubwa sana Duniani kiasi cha kujiuliza kuna nini hadi iwekeze Tanzania katika nishati?
Jibu hapa ni geresha tu kuwa Wamarekani wana interest ya kusaidia katika nishati .
Nyuma yake kuna suala la gesi na madini kama vile Uranium.
Mkakati ni kuhakikisha kuwa maliasili hizo hazitumiki au kutumiwa ''vibaya'' na wapinzani wa Marekani kiuchumi.
Siku zijazo watakuwa na sababu za kusema wao walianza kuwekeza katika nishati miaka mingi iliyopita
Na katika kuficha lengo la ziara hiyo Rais wa zamani G.Bush amekuja kusimamia ujenzi wa Clinic ya Kansa. Ni Bush huyu huyu aliyesaini Millenium Challenge na ni Bush huyo huyo aliyegawa vyandarau kuzuia Malaria. Rais wa Marekani agawe vyandarau???
Bush atakuwepo katika round table na CEOs na wafanyabiashara. Leo tunaonyeshwa picha akipaka rangi clinic. Hapo hapo kuna Clinton foundation ambayo nayo kama zingine inashughulikia mambo ya afya!!!
Haya yote ni kuhakikisha kuwa lengo la ziara ambalo ni kiuchumi linafunikwa ili kuepuka vita isiyo ya lazima ya kiuchumi na China au nchi za BRICS
Inaweza kuchukua miaka 10 kabla ya rais wa Marekani hajaietembelea Tanzania tena.
Kazi kubwa imeshafanywa na akina Clinton na Bush na Obama anamalizia tu.
Shughuli nyingine zitaendelea kufanywa na balozi na maafisa wa serikali ya Marekani
Tunasisitiza kuwa kazi za balozi za wenzetu si kutoa visa na kupokea wageni.
Ni pamoja na ulinzi na usalama ambavyo haviachani na uchumi.
Ni wakati sasa tujifunze kuwa balozi zetu si vituo vya visa au mapunziko kwa viongozi wastaafu, ni sehemu muhimu sana za usalama na uchumi wa nchi.
Sina hakika kama balozi zetu zilizopo Kigali, Kampala au Nairobi zinaweza kutueleza kwa ukamilifu nini kilichopo nyuma ya mkutano wa Kagame, Uhuru na Museveni.
Hiyo ndiyo sehemu ya kazi za ubalozi na lazima tubadilike na kuelewa kuwa usalama wa taifa au nchi si bunduki au kung'oana kucha ni pamoja na uchumi kwa dunia tuliyo nayo
Tusemezane