Duru za siasa - Matukio

Duru za siasa - Matukio

MBOWE KUSAKWA NA POLISI USIKU WA MANANE

Tukio la mwenyekiti wa CDM kusakwa saa 7 usiku na polisi wenye silaha kama lilivyothibitishwa na mwenyekiti wa CDM mbowe na msema wa chama Tumaini Makene ni la kushtua na kusikitisha

Kinachoshtua ni kuona matukio ya namna hii yakiendelea bila serikali kuchukua hatua na wala kuona hatari inayolikabili taifa siku za mbeleni.

Mbowe ni mbunge wa Wilaya ya Hai na ni mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani na kiongozi wa upinzani bungeni. Nyadhifa hizi zinaendana na idadi kubwa sana ya wafuasi wake kisiasa na kijamii.

Kama ilivyokuwa kwa mbunge Lema kusakwa usiku hili limekuwa muendelezo wa tabia hii ya hatari sana katika mustakabali wa taifa.

Viongozi ni watu wanaofahamika katika jamii na katika fursa walizo nazo ni pamoja na kuwa 'public figure' na upatikanaji wao ni rahisi sana kuliko mtu mwingine.

Na katika mazingira fulani watu hawa huweza hata kujidhamini kwa baadhi ya tuhuma kwasababu ya nafasi zao katika jamii kwa kuaminika.

Hivi karibuni kulikuwa na mlipuko Arusha ambao Mbowe na Lema walikuwepo.
Katika mlipuko huo hadi sasa hakuna anayejua nani alitupa bomu na kwa madhumuni gani.

Mbowe alitakiwa aripoti kituo cha Polisi na yeye alifanya hivyo bila kushikiwa silaha au kutafutwa na mtu yoyote bali kuitikia wito wa Polisi

Siku za karibuni mwanachama wa Chadema Henry Kileo alitakiwa kufika kituo kikuu cha Polisi.
Alikwenda huko ambako aliishia kukamatwa. Hakufuatwa kwa silaha bali walikwenda mwenyewe kwa kuitikia mwito wa Polisi.

Inapotokea hali ya Mbowe kutafutwa usiku wa maanane tena askari wakuu wakiwa hawana habari kama alivyodai mkuu wa mkoa wa kipolisi wa Kinondoni ni jambo la kusikitisha.

Haieleweki kuwa kweli ni Polisi waliomfuata au ni majambazi.
Lakini ukweli unabaki kuwa Polisi wanatupiana mpira ikiwa ni ushahidi kuwa wanajua nini kilichotokea. Na hata kama ni majambazi tulitaraji Polisi washirikiane na walinzi wa Mbowe kuwatafuta.

Hilo Polisi hawajalifanya ikiwa ni dalili nzuri kuwa hawaguswi na maisha ya kiongozi huyu iwe kwa bahati mbaya au kukukusudia.

Yapo matukio ya watu kuumizwa kama lile la Dr Ulimboka ambalo hadi sasa hakuna anayejua nani alifanya hivyo na kwanini.

Kuna tukio la mwandishi Kibanda na lile la Kanisani Olisati.
Matukio yoye hayo yamehusishwa na vyombo vya dola huko mitaani na kwingineko.

Hatudhani kuwa Polisi walishindwa kumtumia Mbowe ujumbe kama walimuhitaji.
Na hata baada ya kujua yupo safarini Polisi hawajamkamata kwa maana kuwa hawakumuhitaji kama walivyokuwa wanaMtaka usiku wa manane.
Sijui madai ya Polisi kumtaka Mbowe usiku yalihusisha nini na hilo linabaki kuwa Swali.

Hatari inayolinyemelea taifa ni ukweli kuwa matukio haya yanayohusisha Polisi sasa yanaonekana kushamiri na kuwa sehemu ya utawala. Leo kama waliomfuata Mbowe ni majambazi sijui nani angeamini kuwa ni majambazi na si vyombo vya dola.

Kesho vibaka wakimdhuru Mbowe nani ataamini kuwa ni vibaka na si vyombo vya dola.
Keshokutwa Mbowe au kiongozi mwingine akidhurika kwa namna ambayo haitaeleweka kwa jamii nani atakubali kuwa si vyombo vya dola.

Kwa maneno mengine serikali inazidi kujitia katika 'kibano' cha kuhakikisha usalama wa Mbowe na viongozi wengine. Hakuna maelezo yatakayojitosheleza iwe kwa bahati mbaya au makusudi kwa lolote linaloweza kuwasibu viongozi hao kwasababu tayari serikali imeonyesha kuwa sehemu ya mipango michafu kama uvamizi wa saa 7 usiku.

Ni kwasababu hizo duru za siasa zinaiona hatari kubwa sana inayolikabili taifa.
Machafuko hutokea kwa mambo kama haya. Habyarymana wa Rwandara aliuawa jambo lililochochea mauaji ya kimbari. Si kwasababu alikuwa rais bali nyuma yake walikuwepo wafuasi.

Sheikh Abdul Rogo wa Mombasa alipouawa yalitokea machafuko Mombasa, si kwasababu ni kiongozi wa serikali bali kiongozi wa jamii na ana wafuasi.
Na ndivyo mauaji mengine duniani yalivyo, kwamba hutanguliwa na kichocheo 'precusor' kabla hayajotokea.

Katika nchi yetu hali ya kiuchumi, kiusalama na kijamii si nzuri.
Kumekuwa na mivutano ya kidini,kisiasa na kikabila kuliko wakati mwingine wowote wa uhai wa taifa hili.

Haya ni mambo kama tembo aliyelala 'sleeping giant' kama ni sahihi kusema hivyo.
Yanasubiri kichochoe kidogo tu yalipuke.Katika mazingira ya kuhisi, kuona na kuusema uonevu, uvunjwaji wa sheria na utawala usiozingatia haki za watu, hakihitajiki kichocheo kikubwa.

Duru za siasa kama walivyo Watanzania wengine tunatoa thadhari kuwa mchezo huu mchafu ima wa kisiasa au vyovyote iwavyo hasa kwa kutumia vyombo vya dola ni hatari sana kwa taifa hili kwa wakati huu.

Wananchi waliokata tamaa hutafuta mahali pa kumalizia machungu yao,na fursa hiyo ikijitokeza basi wataitumia ipasavyo.

Rais JK, taifa linaingia na kupita katika wakati mgumu sana kiutangamano katika uongozi wako.
Tanzania ni yetu sote na wala hakuna atakayekuwa salama hali ikichafuka.

Rais kama hatachukua hatua za makusudi na za haraka basi historia ya kuvurugika kwa taifa hili pengine na maumivu, machungu au damu hazitakuwa mbali na mikono ya serikali yake.

Tusemezane!


Mgeni wa leo Radhia Sweety


cc. Invisible Dr.W.Slaa Nape Nnauye Zitto
 
UCHAGUZI WA ARUSHA NA YATOKANAYO

Uchaguzi uliokuwa unasubiriwa umemalizika kwa Chadema kushinda kata zote nne.
Ni uchaguzi ulioahirishwa kutokana na mlipuko wa bomu ambao hadi leo hakuna anayejua chanzo chake na sababu zake. Tunachokijua sote ni roho za watu wasio na hatia kupotea wakiwemo akina mama na watoto, kundi ambalo ni adhimu sana kuwa katika migogoro.

Kauli za awali za viongozi ni kukishambulia Chadema kwa kusema kilitafuta kura za huruma hata kama viongozi wake wakuu wa chama walikuwa karibu sana na ajali hiyo.

Duru za siasa zinaamini kuwa tukio hilo linaweza kutokea kona yoyote kwasababu lilitanguliwa na tukio la bomu la nmna hiyo kule kanisani.

Kwa viongozi wa serikali na wabunge wa CCM kutamka maneno bila kuwa na ushahidi inaweza kumaanisha kuwa hata kanisani nao walikuwa wanatafuta huruma, sijui masikini walikuwa wanatafuta huruma ya kitu gani huku wakiwa wamejipinda kwa miaka 5 kujenga jengo la kiroho.

Uchaguzi huo uliambatana na kuvamiwa na kukamatwa kwa viongozi wa Chadema usiku, huku wapiga picha na wenye kamera wakiandamwa pengine watoe mkanda wa ushahidi ambao Chadema wanasema wanao.

Kama busara zingetumika ingeundwa tume ya kimahakama kama walivyoomba CDM ili kutafuta ukweli. Tume hiyo haijaundwa na kwa kuogopa hilo hakuna sababu za msingi za kuwabana CDM watoe ushahidi kwa polisi, chombo kilichopoteza imani, maadili na sifa ya kutumikia jamii yetu.

Polisi wameendelea kuwabana wanachama wa CDM ili kupunguza kasi huku CCM ikiwatuma vijana wake akina Mwigulu, Nape pamoja na Juliana na Mtela kutumia fursa hiyo
Hili lilifanyika makusudi ili kukabiliana na nguvu ya vijana wa CDM.
Lakini pia kisiasa lilikuwa na maana kubwa sana.

Arusha ni mji unaotokea kuwa vuguvugu la mabadiliko nchini. Historia inaonyesha Wapinzani wakwanza kupenya Arusha alikuwa Dr Slaa kule Karatu.
Ni kwa mfano huo moto ukahamia Tarime kwa muda kabla ya kurudi Arusha.

Arusha ndiko anakotoka Lowassa mtu anayeangaliwa kama mgombea urais mwaka 2015.
Ni jimbo muhimu sana katika siasa za nchi kwasababu ya influency yake hasa kwa mikoa ya jirani kama Mwanza, Shinyanga na Singida.

Kilimanjaro CCM wanafahamu kuwa kete yao ipo Mwanga ambako uasi unaendelea na kule Same ambako pia hali si nzuri.

Mtu aliyetarajiwa kuongoza kampeni alikuwa ni Lowasa. Kutokana na matokeo ya Arumeru ingekuwa ni maafa kama Lowasa angepoteza viti 4 vya udiwani akiwa kiongozi.

Ni sababu hizo ndizo zilimweka pembeni huku akialika timu kubwa ya chama chake ifanye kazi anayoikusudia. Kwabahati mbaya ameshindwa mtihani huo tena

Makosa yapi yalifanywa na CCM
Kuwatisha wananchi kwa kutumia askari kunajenga chuki badala ya upendo.
CCM wanadhani kuwa kumtia ndani kijana mmoja wa CDM ni kuidhuru CDM.

Wasichokijua ni kuwa kijana huyo ana ndugu na marafiki pengine ni wanachama wa CCM ambao wangeudhika na hatua hizo.

Kutisha wananchi hakuchagui nani anatishika na ndiyo maana kati ya watu 16,000 waliopiga kura 2,000. Hao 2000 ni wale waliojitolea kwasababu tu ya ujasiri na pengine kura ya chuki.
CCM wametisha wanachama wa CDM na wanachama wao wenyewe, imewaumiza sana.

Mkakati wa kutumia lugha chafu nao umechangia sana. Wananchi wanataraji kusikia mengi kutoka katika chama tawala.Wanaposikia jinsi Juliana Shonzo alivyohama CDM kunakifanya chama kionekane kama hakina sera na hakina la kuwaambia wananchi.
CCM wanasahau kuwa watanzania si wapuuzi kiasi wanachodhani. Tanzani ya leo si ya 1954.

Kitendo cha akina Nape kuwatumia majeruhi kutoka CDM na kuwaacha wenye chama Arusha kimewaudhi sana na hivyo kususiwa kampeni. Hapa ni upungufu wa maono tu na mkakati na hilo lazima wajiulize kama lina tija siku za usoni.

Kwanini Chadema wamefaidika na uchaguzi huu
CDM wametoa ujumbe kwa sehemu nyingine kuwa wakati wa kupigania haki hakuna kuogopa na kwamba si wakati wa kuogopa vitisho vya askari.

Wamedhihirsha kuwa uwepo wa viongozi kama mkuu wa mkoa na wilaya ndio chanzo cha vurugu katika chaguzi nyingi.

Wameweza kutetea viti muhimu ambavyo walivyopoteza kwa maamuzi magumu.
Hili linapeleka ujumbe mkubwa sana kwa wanachama na viongozi wao kuwa wanaweza kupoteza uongozi na CDM ikabaki na nafasi kwasababu wana mbadala.
Kwahiyo sasa nidhamu kwa viongozi itakuwa ya hali ya juu.

Nini kitatokea ndani ya CCM
Kutakuwa na mtifuano kwasababu makundi yanayowania urais yatahisi ugumu.
Makundi hayo yatatuhumiana kwa jinsi kampeni na sera za chama zinavyoelezwa.

Hatutegemei Mwihulu kuongoza kampeni tena kwasababu hili ni anguko lake la pili kubwa.
Lakini pia amehdhirisha uwezo mdogo wa kueteta sera za chama zaidi ya kelele za majukwaani kuzusha uongo na kuwakamia wapinzani badala ya kushinda nyoyo za wapiga kura.

Nguvu kubwa sana ya CCM itaelekezwa mikoa ya Arusha, Mwanza na Mbeya ili kuwadhibiti wapinzani kwa kutambua kuwa mikoa kama Lindi, Mtwara, Singida, Shinyanga, Tanga,Pwani, Dar es Salaam na Ruvuma ni salama kwao.

Tatizo watakalo pambana nalo ni ukosefu wa watu wenye ushawishi.
Kwasasa hivi CCM haina akina Malecela au Kingunge, akina Msuya, Kisumo, Ndejembi n.k. Wapo akina Serukamba, Kibajaji n.k. ambao ni tatizo kwanza kabla ya tatizo.

Chadema Wafanye nini
Kwanza waepuke makosa ya dhahiri ili kuzuia kuzushiwa kesi zisizo na maana.
Utaratibu utakaotumika ni kuwabambikia kesi na kesi hizo zitavuma sana kuelekea uchaguzi ili kuvuruga nguvu na mipango yao

Waendelee na kampeni zao na watarajie kuwa mahudhurio yatakuwa madogo kwa vitisho vilivyojitokeza. Kazi yao kubwa ni kuendelea na mikuatano ili kuwaondoa wananchi hofu.

Chadema wajisafishe kwasababu uwezekano wa kutumika kwa mamluki sasa ni mkubwa sana. Na kama wangelikuwa makini Chadema walitakiwa wafanye uchaguzi mapema ili waweze kujipanga, kujua wasaliti na wachumia tumbo.

Chadema waendelee na kampeni katika mikoa ambayo hawajaingia kwa kasi.
Watumie nafasi zinazojitokeza kujipenyeza huko kwa sera mbadala na si malalamiko.

Wananchi wa Mtwara wangefarijika kusikia Chadema wanasema nini kuhusu kadhia zao na si CDM wanasema nini kuhusu CCM.

Kuelekeza nguvu katika mikoa wasiko na nguvu kutawalazimisha CCM kurudi kujilinda na huo ndio mwanya wa wao kushambulia maeneo hayo kwa sera na siyo CCM wanafanya nini.

Ukweli unabaki kuwa uchaguzi wa Arusha umeacha kovu kubwa sana CCM

Tusemezane

Mgeni wa leo Arushaone
 
Nguruvi3, Mchambuzi,

..sasa ni maeneo mangapi watakuwa na hasira/usongo wa kwenda kupiga kura against CCM au CDM??

..je, kundi gani kati ya vijana, wazee, na wanawake, liko more likely kupiga kura ya hasira dhidi ya CCM,CDM,au chama chochote kile?

..mimi nadhani mwelekeo wa siasa za sasa hivi, kila chama kinajaribu kutafuta kura za hasira dhidi ya mwenzake. CCM wanadai wenzao ni wamwagaji wa damu hivyo wasichaguliwe. CDM nao wanadai wenzao ni mafisadi, na hameshindwa kutatua kero za wananchi.
Mkuu JokaKuu, nianzie kujadili hoja zako kuanzia ulipomalizia.

Hili la kutuhumiana CCM wana wakati mgumu sana. Tuhuma zao kuwa Chadema wanataka kumwaga damu haziingii akilini mwa wananchi. Watu wanajiuliza ni kwa kutumia njia gani hawa watu wanataka kumwaga damu.

Kinyume chake wananchi wanaona wazi jinsi CCM inavyobebwa na Polisi na jinsi Polisi wanavyotumika kuwanyanyasa wapinzani. Nimesema hapo awali kuwa huu mkakati wa CCM kutumia vyombo vya dola ni mbovu sana.
Wapinzania wanaonekana kama mayatima na wanapata sympathy kirahisi sana.

Kuhusu kundi gani litapiga kura ya hasira, nadhani unaona jinsi vijana walivyokumbatia mabadilliko.

Zamani siasa ilikuwa jambo la wazee na akina mama, siku hizi ni suala la vijana na hao wazee hata kushiriki wanaogopa kwasababu wanaona kama wakati umeshawapita.

Kundi hili la vijana ndilo pia kundi linaloathirika sana na mabomu ya machozi, virungu na kutiwa ndani bila sababu.
Mfano, Arusha wamekamata wapiga picha na yoyote mwenye Camera ili mradi tu.
Ukiangalia wapiga kura waliokataa kutishwa 70% ni vijana ambao likely walinyanyaswa na Polisi

Likitokea jambo watu wa mwanzo kuathirika ni kundi la vijana.
Ndilo kundi lenye hasira na mfumo mzima wa siasa, uchumi,uonevu na sasa unyimwaji wa haki za kushiriki katika mambo ya kisiasam,lipo more likely kupiga kura ya hasira kwa CCM ambayo imepoteza sehemu kubwa ya kundi hili.

Kwa upande wa kura ya huruma, CCM wanategemea akina mama watu wazima na si vijana kwa mazoea tu kuwa uwepo wa amani ni matokeo ya utawala na kwamba yanayotokea hayakuwepo siku za nyuma. Ni kundi linaloishi kwa historia na hisia na halipendi mabadiliko.

Kundi la wanaume wenye umri kupindukia ujana linaegemea sana upande wa wapinzani.
Sababu kubwa ni hasira kutokana na mambo yanavyokwenda hasa katika rushwa, ukosefu wa maadili n.k yanayotokana na CCM na serikali yake. Ni kundi la wastaafu au wastaafu watarajiwa ambalo linaona limemenyeka na sasa watu wanakula tena kwa gharama kubwa za vijana wao. Ni kundi linalohisi kuwa uzalendo haukulisaidia kimaisha na hivyo lipo likely kupiga kura against CCM.

Ushahidi kuwa CCM ipo matatani ni kuzingatia kuwa kila chaguzi wana loose ground na wapinzani wana gain ground. Na angalia nani wapo behind the oppositions' success.

Habari za siri kuvuja kutoka ndani ya CCM au serikali ni kutokana na uwepo wa makundi mawili niliyotaja.
Wengi wao ni wanachama wa CCM kwa mafao lakini wana sympathy kubwa sana na opposition kama nilivyoeleza.

Maeneo gani yatakayokuwa na hasira na CCM, hili lipo wazi sasa. Arusha CCM wameshasalim amri na kura za chuki zitaendelea. Kilimanjaro chuki imeshaingia katika wilaya tiifu za Mwanga na Same na CCM ipo neck in neck na wapinzani.

Mwanza kuna kura za chuki, Igunga, Morogoro mjini, Mbeya, Tarime na Bukoba.Hayo ni maeneo ambayo wagombea wa CCM wanaweza kushindwa kwa kura ya chuki bila kujali ni wazuri na weledi kiasi gani.

Utashangaa kama nikikuambia kuwa Mtwara mjini imeshaondoka mikononi mwa CCM na sasa ni swing constituent, Singida ni hotbed kwa CCM na kuna ondoka chini ya umiliki wa CCM.Tukio la Mwangosi linaiweka Njombe kama toss up constituent

Kwa Dar CCM wapo salama Ilala na Kigamboni. Kinondoni sasa ni toss up.
Kwa Tanga jimbo la kwanza kufanya uasi dhidi ya CCM litakuwa Muheza mjini na ushawishi wa Muheza kwa mkoa wa Tanga hasa Tanga mjini ni mkubwa sana.

Uwezekano wa Lushoto kupoteza jimbo moja kati ya mawili ni mkubwa sana kuliko ilivyowahi kuwa huko nyuma
CCM bado ni salama Korogwe na Handeni.

Kwa haraka haraka, Kigoma, Kilimanjaro, Arusha, Mwanza, Mara, Bukoba, Mbeya, Iringa yameshaondoka CCM.
Morogoro, Mtwara mjini na Masasi, Singida, Igunga,Muheza, Lushoto, Same, Mwanga, Kindondoni, Njombe haya ni toss up na likely kutumia kura ya adhabu dhidi ya CCM.

CCM wanabaki salama Ruvuma, Lindi, Dodoma, Pwani, Simiyu, Morogoro vijijini, Katavi, Shinyanga.

Tusemezane

Mgeni wa leo gfsonwin
 
Last edited by a moderator:
TUME NA MABARAZA YA KATA

Mabaraza ya kujadili rasimu ya katiba mpya yanaanza kazi wakati wowote
Hali inaonekana kama kutulia,wasomi wakitafakari kwa undani nini cha kuongeza na nini cha kupunguza.

Ukiangalia rasimu utaona kuwa Tanganyika imetajwa takribani mara 9 na Tanzania bara zaidi ya mara 40. Kama tulivyowahi kujadili huko nyuma serikali ya Tanganyika itajulikana kama Tanzania bara wakati ya Zanzibar itajulikana kama Zanzibar.

Rasimu hapo mwanzo imeeleza kuwa serikali ya muungano ni zao la Tanganyika na Zanzibar kama zilivyokuwa nchi huru mwaka 1964 kabla ya muungano.

Kinachoshangaza! Watanganyika hawajaulizwa serikali yao ijulikane kwa jina gani, tume imekuja na neno Tanzania bara.

Inavyoonekana kulikuwa na hali hizi katika majadiliano
1. Zanzibar haikukubali kuitwa serikali ya Tanzania visiwani na ikataka ibaki kama ilivyo
2. Uwepo wa jina Tanganyika utapunguza nguvu za neno Tanzania

Tatizo ni kuwa inakuwaje Tanganyika isipewe nafasi ya kuamua utambulisho wake na tume imekuja na jina tayari?

Tunaelewa kuwa hiyo ni katika kupunguza uvutano na ushindani lakini lazima tukubali kuwa Tanganyika ina haki ya kupewa nafasi ya kuamua jina la utaifa wao.
Haiwezi kuachwa ili ibebe utaifa wa Tanzania ambao znz haipo tayari kuuafiki.

Mabaraza ya kata lazima yaulize kuhusu suala hili kwasababu utaifa ni utambulisho wa kila mtu na ni haki ya mtu kujinasibisha nao.

Suala lingine ni kuhusu uwepo wa Marais watatu.
Hata kabla ya kuangalia ugumu wa protocol kunatatizo lilijitokeza wakati wa majadiliano ndani ya tume.

Kulikuwa na uwezekano wa kuwa na rais mmoja na mawaziri wakuu 2 kila mmoja akiongoza nchi yake.Tatizo ni kuwa znz hawakubali kuwa na waziri mkuu kwasababu wao wangependa kubaki na wadhifa wa rais.Hili ndilo limelazimisha uwepo wa majina ya marais watatu.

Tatizo linabaki kuwa znz hawapo tayari katika kujadiliana na hilo litaleta tatizo mbele ya safari.
Hoja ya znz ni kuwa mshirika mwenza wa muungano wakiwa na rais kamili.

Kwao neno rais lina maana sana hata kama majukumu yake yatakuwa kama ya waziri mkuu. Lakini wanashau kuwa wakati wa sultan walikuwa na waziri mkuu ambaye ndiye aliunda serikali. Sasa kugomea kuwa lazima kuwe na rais ni hoja inayoonyesha wzn kutokuwa tayari katika compromise. Hili nalo ni tatizo.

Baada ya kikundi cha Uamsho kuzuiliwa kuendesha siasa za chuki, wanachama wa kikundi hicho ambacho kinaungwa mkono na maalim Seif wamekuja na kitu kingine.

Kitu hicho kinaitwa BAKAZA yaani baraza la katiba znz. Lengo lake eti ni kuwaeleimisha wznz kuhusu katiba. Kiongozi wake ni Profesa Abdul Sherrif aliyewahi kuwa prof wa UDSM

Prof Sheriff ni mmoja wa watu wanaopinga muungano lakini si wazi kama ilivyo kwa Seif.
Juzi ameonekana katika mikutano ya BAKAZA akiwa amejificha nyuma ya pazia la BAKAZA ili hali mawazo na maoni yake yaliwakilisha Uamsho.

Katika mambo anayohimiza ni pamoja na kuiangalia znz kama mshirika mwenza SAWA katika muungano (Daily news July 15).

Tunapenda kuwakumbusha Watanganyika kuwa usawa wa ZNZ katika muungano hauna shaka. Lakini usawa huo usiishie katika ajira na kugawana masilahi.

Ni lazima znz kama mbia mwenza aheshimu nafasi yake katika muungano.
Kwa vile ni mbia mwenza hatutegemei liwepo jambo ambalo litaifanya znz ionekane ndogo au isio na uwezo.Ni kwa mantiki hiyo michango ya kuendesha serikali za muungano lazima iwe sawa.

Siku zote wzn wanapoongelea usawa, wao hutanguliza faida kwa upande wao na gharama humuachia Mtanganyika.

Rasimu inapaswa kuliangalia suala hili kwasababu haiwezekani upande mmoja ukawa unapata mafao kwa gharama za upande mwingine.

Tunapenda kumkumbusha prof Sheriff na Maalim Seif kuwa with great power comes responsibilities na hapo suala la gharama halitakwepeka.

Watanganyika wasikubali kujadili nafasi za ajira na uongozi bila kuhoji mchango wa kuendesha nafasi hizo. Haiwezekani Tanganyika iendelee kuwa shamba la bibi kwa kutoa ajira na kugharamia muungano. Ni wakati sasa kila kitu kiwekwe mezani ikiwa ni pamoja na mali, uchangiaji na madeni ili kila mshirika wa muungano ambaye ni mbiya sawa apate shea yake

Kama ikionekana haiwezekani basi wznz wapewe kura ya maoni kama tulivyowahi kushauri ili waamue hatima yao.

Vinginevyo basi tutawasihi tukutane EAC au SADC kwasababu muda wa kubeba gharama sasa umefikia kikomo.

Tusemezane

Mgeni wa leo Pasco
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3, ahasante sana kwa nafasi hii.

Mimi naomba nianze kwa kusema hivi, kwanza kabla ya yote naomba nileweshwe manake yawezekana kabisa nikawa nilipitwa na hoja hii. Juu ya Tanzania tunatumia sera gani kumtanganza mshindi wa kiti cha uraisi??

Je! tnaangalia yule aliyepata kura nyngi katika wote pasi kujali idadi ya kura zilizopigwa??
je! tunaangalia yule ambaye amepata kura nyingi lakini pia ana viti vingi vya uwakilish bungeni.
je tunangaalia yule mwenye kura nyingi lakini zilizo juu ya quoram iliyowekwa??
ama tunaangalia nini ambacho sijaweza kukiweka hapo??

Kwa mtazamo wangu kaka mkubwa ni kwamba, CCM kama chama bado ni maarufu na kinapendwa zaid na watu ambao ama ni wazee/ wastaafu, ambao wao wakikubuka walikotoka basi kuwaambia chochote kinyume na CCM wataona wewe sio mzalendo wala hujui nchi ilitok wapi. Kadhalika ni chama ambacho kina umaarufu sana kwa watumish wa umma hasa wa serkali kuu, na wale wa serikali za mitaa ambao ni seniors. Hawa ni kwasababu wao mpaka sasa anajua wanabefit nini kutokana na mfumo uliopo wa CCM na hawa huwez kuwabadilisha msimamo kabisa manake watakuambia wazi kwamba wapinzani bado hawana ukomavu wa kuweza kuongoza nchi hii.

CDM(nakichukulia kama chama kikuu cha upinzani kwa sasa) kwa upande mwingine hiki kimejizolea umaarufu mkubwa sana kwa vijana toka wale ambao wako jobless na wasio na uhakika wa maisha hadi kwa vijana ambao wanajitambua na wanauwezo wa kuyaendesha maisha kwa namna bora zaid.

nikijadili makundi haya mawili kwa kuyasemea tofauti zao yaani kundi la vijana na kundi la wazee naweza kusema hivi:

Vijana wana nguvu na ari na moyo wa kujitolea zaid wakiamini kwamba saa ya mabadiliko ni sasa. kwao hawaogopi vitisho ama misukosuko wanayoipata kwenye siasa hizi hali wakiamini kwamba mapinduzi lazima yatokee ili hali ibadilike, ili maendeleo yawepo ili siasa za kifisadi zikome. Vijana hawa wanahamasishana na kutiana ari kila uchwao na kwao ni heri kujitoa kuleta mabadiliko ya kisiasa kuliko kuwa mwoga maisha yakazidi kuwa magumu.

Kitendo cha viongozi wa CDM kupita na kukaa na haa vijana wale ambao wanaonekana kama kusahauliwa kimeleta hisia na kimeamsha ari ya kutaka kuona CDM ikiwamadarakani. kwasababu ya uthubutu wao ni wazi kwamba wengi wao lazima wataitokeza kupiga kura na ile hofu ya vijana ya zamani ya kukataa kupiga kura kwasasa imeondoka kwa kiasi fulan.

Kundi la wazee hawa wanaipenda zaid CCM ila wanazidiwa kete na vijana, kiasi kwamba ujasiri wa kutoka kwenda kucompromise nao haupo. na hii ilitokana na ukweli kwamba hili kundi liliachwa nyuma na wazee hawa. wazee hawa ndio waliokuwa wanaongoza kwa kupiga kura, lakn leo hii idadi yao imeanza kupungua kwasababu kuu moja nayo ni hawataki fujo na wanahofia vurugu za vijana.

Lakini swali la msingi la kujiuliza je ni mshindi a kiti cha urais anapatikana vipi baada ya kupiga kura?? tukipata jibu hapo basi kila mtu kwa mrengo wake atakwenda kulifanyia kazi jibu hilo.
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin ahsante kwa mchango wako , na nianze kwa kusema rais wa nchi yetu anaweza kuchaguliwa na idadi yoyote ya wapiga kura. Mwaka 2010 walikuwa milioni 6.

Tukizingatia kuwa karibu asilimia 70 ya watu wapo kati ya 20-40 yrs ambao ndio umri wa kupiga kura namba hazionyeshi dalili nzuri ya demokrasia. Kwamba katika 40M wapiga kura ni 6M!!!

Kwa mfumo wetu wapiga kura wanaweza kuwa milioni 1 na wakamchagua rais.
Hakuna quorum inayohitajika ili rais kupatikana.

Mfumo wetu wa uchaguzi ni wa ‘winner takes all' kwamba mshindi ni kwa idadi yoyote .
Endapo wapiga kura watakuwa milioni 1 na CUF wakapata 5%( 50,000) TLP 15%(150,000) Chadema 35%(300,000), CCM 45%(450,000), Mshindi kiti cha Urais atakuwa wa CCM bila kujali idadi ya wapiga kura au asilimia alizopata

Kwa nchi za wenzetu uchaguzi ungerudiwa kati ya CDM na CCM ili mshindi apatikane kwa asilimia 50+

Kwetu sisi rais anachaguliwa moja kwa moja na watu na wala si idadi ya viti bungeni.
Kwamba, kuna uwezekano wa kuwa na rais wa CCM na Bunge la Chadema.

Pili,Kuhusu uungwaji mkono wa vyama, CCM kimepoteza kada ya kati ambayo yenye weledi wanaotaka mwelekeo mpya w anchi. Kada hiyo kwasasa ni sehemu ya Chadema ambao pia wanaungwa mkono na wale unaosema wa Jobless na wasomi wengi waliochukizwa na taratibu za kiutawala za CCM.

Ngome kubwa ya CCM imebaki kwa akina mama wa umri(siyo vigoli au mabinti).
Wengi wana familia wana hofu tu isiyo na msingi. Ni watu wanaohisi na kuhofu machafuko hata kama hayapo. Hawapendi mabadiliko kama ilivyo kwa UWT na wala hawatamani uwepo wa damu changa katika safu za uongozi(limejaa ukiritimba).

Sehemu niyingne inayowaunga mkono CCM ni vijijini kwasababu tu ya mazoea na kuenea kwa chama tangu zamani. Hata hivyo uasi umeanza na haionekani kama CCM wana njia mbadala za kuzuia.

Kundi la wastaafu unalosema tayari limeshakata tamaa na CCM. Wengi hawaridhishwi lakini hawana jinsi kwasababu wapo nje ya system.Ni kundi lililopoteza nguvu za ushawishi kutokana na CCM 'kutekwa' hivyo uwezo wa kuhimili mikiki ya siasa umekuwa mdogo sana.

Ni kwasababu ya kupoteza uungwaji mkono na sehemu muhimu za jamii, CCM imeamua kuziba pengo kwa kutumia Polisi na vyombo vya usalama, mkakati mbaya sana kwa mtu anayefahamu jamii ya Tanzania.

Kama ungeniuliza wapinzani wafanye nini kwasasa, ningewashauri wavunje nguvu ya kundi la akina mama. Chama kama CDM kinaungwa mkono na mabinti na Vigoli na wala si kundi la akina mama.
Wanachotakiwa ni kushawishi akina mama na kumega sehemu yao katika jamii.

Tazama nguvu za UWT na BAWACHA.
UWT ni kiungo muhimu ndani ya CCM wakati BAWACHA ni alama ya uwepo wa akina mama na ni jumuiya mfu.
Kwa jinsi BAWACHA ilivyokosa ushawishi ndani ya Chama ndivyo ilivyo kwa jamii sijui nani atafanya recruitment ya akina mama wenye hofu tu kwa hisia. Ni lazima uwepo ushawishi wa makusudi ili kupunguza nguvu ya CCM, ni sawa na kuvunja nguzo moja muhimu.

Historia ya nchi yetu inaonyesha sehemu kubwa ya wapiga kura ni akina mama hivyo kuzishinda nyoyo zao ni muhimu sana. Kwa BAWACHA Kama ilivyo sasa Chadema wana wakati mgumu sana eneo hilo.
Hiyo itakuwa ni fimbo ya kuwatandika kila siku kama hawatabadilika.
 
my broda Nguruvi3 ulilolisema juu ya wanawake nakubaliana nalo kwa asilimia 100.

lakini unafikiri kwamba BAVICHA inashindwa kuwin nguvu ya akina mama?? sio kweli ila hawajaamua kabsa. nashindwa kuelewa kwann hasa bavicha wamejiestablish huko juu wakaacha huku chini ambako ndiko wapiga kura walipo.
kwann kila lilipo shina la CDM basi kusiwe na umoja wa akina mama wa CDM?? wanaona ugumu gani kurudi huku chini??ama ni kwasabbau CDM haina akina mama ambao ni watu wazima ambao wanweza kuwashawish wamam wa mitaani??
 
Last edited by a moderator:
Mkuu nguruvi3,

Ningependa kusikia maoni yako juu ya hili:

Kwa mtazamo wangu, Dar-es-salaam is key for any political party to become a major success provided nje ya dar chama hicho kina a decent presense; DSM is the most heterogenous city in the country with dwellers from diverse ethnic groups, different walks of life and economic status; Kwa maana hii, DSM is a good ground kwa chama cha siasa kujipima iwapo kinakubalika au bado kina safari ndefu kuelekea kukubalika juu ya utayari wa kukamata madaraka ya nchi; Kwa maana nyingine, Dar is the last mile in the journey towards ikulu na ndio maana pamoja na ushawishi mkubwa wa mwalimu Nyerere na TANU katika maeneo ya Tanga, Singida, Mwanza na kadhalika wakati wa harakati za ujenzi wa TANU miaka ya 1950s, key determinant ya mafanikio ya Mwalimu na TANU ilikuwa ni the conquest of Dar-es-salaam; Sasa given the success of Chadema katika kushawishi umma kwamba hiki ni chama mbadala wa ccm, given maelezo yangu hapo juu, kwanini Chadema ina wakati mgumu to conquer dsm? Kwani wakikamata tu dar-es-salaam, given mawasiliano na muingiliano wa kila sekunde baina na dsm na mikoa mingine ya nchi kisiasa, kijamii na kiuchumi katika muktadha wa rural - urban linkages, Chadema to conquer Dar-es-salaam itakuwa ni pigo takatifu kwa ccm na a guaranteed strength to finish the last mile; Kwanini Chadema hawafanikiwi kupenya dsm kwa kasi wakati ilitarajiwa chama hiki kiwe na nguvu katika mkoa wa dsm kuliko mikoa mingine given the dynamics ya upinzani africa ambapo urban areas are normally for the opposition and rural areas largely remain pro ruling parties?

Kitendo cha mikoa mingine kuambukiza dsm kisiasa in terms of mabadiliko badala ya the other way round kidogo I find it strange;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Mchambuzi
Ahsante kwa mchango wako. Nikubaliane nawe kuhusu Dar kuwa Cosmopolitan and heterogeneous in all aspect. Na niongezee kuwa Siasa za Dar es Slaam zinazungukwa na factors nyingi sana

Dar imepoteza geographical/dermographical presentation iliyokuwepo miaka ya 1954 kutokana na uwepo wa makundi mawili, kwanza la wenyeji na la pili la wakazi.

CCM inajua vizuri sana jambo hili ndio maana wakati wa uchaguzi serikali hufunga vyuo ili wakazi waondoke wabaki wenyeji ambao ni loyal kwa CCM

CCM wana uhakika wa Ilala na Temeke kwasababu kuna wenyeji.
Ubungo, Kawe, Kinondoni,ukonga ni maeneo ya wakazi yanayohitaji nguvu zaidi ya 'loyality'.

Da es Slaam imepoteza uongozi wa nchi (leadership) ya miaka 30 iliyopita, sasa hivi ni mzalishaji (manufacturer) kutokana na diversity ndio maana ni rahisi kuambukizwa zaidi ya kuambukiza.Ni jambo la kushangaza lakini ndiyo reality

CCM pia ni waathrika wa diversity ingawa hawaonekani kuelewa hilo. hawaelewi hili ndio maana Mbinu za kufunga vyuo ili wapate kura za wenyeji kuna saidia kusambaza siasa za Dar mikoani,na ndicho chanzo cha wapinzani kushinda maeneo wasiotarajiwa

Dar es salaam inabomoka kwasababu leadership sasa ipo Arusha, Mwanza na Mbeya.
Huko ndiko watu wanasikiliza kuna nini.CCM wajilaumu kwasababu wamesaidia ku-suppress opposition Dar na naturally zikamea mikoani.

Chadema inaendelea kukubalika huko dalili ambayo ni njema kwao. Ile rural-urban linkage inakuwa kwa kasi huko mikoani kuliko jambo amblo ni zuri. Nani alitegemea ushindani mkubwa eneo la Makuyuni Arusha.


Chadema kushindwa 'Kuiteka' Dar ni kwasababu za kimkakati na kimazingira ya kisiasa.

1. Chadema hakikuungwa mkono na makundi muhimu ya jamii siku za awali. Mpambano wa kisiasa wa kichichini i.e Mtei Vs Nyerere uli polarize potential political figure kujiunga na ikawa ya nne baada ya CCM, NCCR,CUF. Inferiority complex ikawaingia kwa kasi na wao kukimbilia maeneo waliyodhani wanaweza na si maeneo wanyopaswa kupenya kama Dar.

2. Inferiority complex ilisababisha waogope kuweka wagombea pale wapinzani walipokuwa na fursa. Wakasahau kuwa wanapaswa kuwa aggressive wakiwa Dar.

3.Chadema hawakuwa na mkakati wa kuiteka Dar.kwasababu nilizozitaja hawakuweza kuwashawishi viongozi wao kugombea Dar kwa inferiority . Mkakati ukawa ni kuingiza wabunge wengi bila kujali wanatokea eneo gani la kisiasa.wakasahau kuwa umuhimu wa Dar es Slaama haujafutika.

Kama Mrema alishinda Temeke kwanini Mbowe akimbilie Hai.
Kwanini Zitto afanye tahmini ya kuwa Mbunge Shinyanga na wala si Kinondoni.
Kama Anna Komu alikuwa neck to neck na ccm Kigamboni ingekuwaje kama wangekuwa na wagombea maarufu sehemu nyingine za Dar.

4. CDM wana tatizo katika inner circle. Kuna tension na power struggle zinazozuia kuona mbali. Hivi unawezaje ukashinda ilala na Temeka, Dodoma na Tanga kama huna BAWACHA yenye nguvu?

Kule kwa Halima Mdee na Mnyika kuna wakazi,wabunge wanapimwa kwa hoja na weledi.
Ilala, Temeke,Ubungo na Kigamboni ni kwa wenyeji kunahitaji nguvu zaidi za ushawishi

Nilitegemea Komu aliyeleta upinzani mkubwa kwa CCM angekuwa ndiye BAWACHA Dar akiandaa njia. Leo BAWACHA ipo wapi na ina nguvu gani Dar?
Siasa za Dar ni endelevu na siyo seasonal.JJ.Mnyika alikomaa na Ubungo hata baada ya kushindwa na Keenja. Leo niulize yupo wapi Mpendazoe!

5.Chadema ina ingiwa na woga wa kupambana katika baadhi ya maeneo.
Si Dar es Salaam tu bali ukanda wa pwani.Hawajawa na mkakati wa kuingia maeneo hayo.

Given the dynamics of political trend in Africa ni kosa kwa Chadema kutoingia katika miji mikubwa kama Dar na Tanga. Kwa hali yoyote CDM hawana muda wa kupenya zaidi katika rural areas kwasababu inahitaji miaka mingi wasiyo kuwa nayo.

Pamoja na Dar kupoteza leadership katika political land scape ya nchi, bado umuhimu wake upo pale pale kwa sababu za kisiasa na kijamii.

Chadema wameshindwa kupenya kwasababu ya woga, inferiority complex, lack of aggressiveness. Hawajaweka mkakati wa muda mrefu na kazi hiyo wamewaachia aspirants wa nafasi kuliko jukumu la chama.

Wanachotakiwa kufanya ni kurudi katika drawing board na kuangalia wapi kuna tatizo, kifanyike nini na nani apewe jukumu hilo na kwasababu gani.

Wanatakiwa wafanye dissection ya Dar es Salaam mtaa kwa mtaa na mkakati madhubuti.
Hilo litawezekana kwa urahisi kama wataimarisha BAWACHA na BAVICHA.



Tusemezane


 
my broda Nguruvi3 ulilolisema juu ya wanawake nakubaliana nalo kwa asilimia 100.

lakini unafikiri kwamba BAVICHA inashindwa kuwin nguvu ya akina mama?? sio kweli ila hawajaamua kabsa. nashindwa kuelewa kwann hasa bavicha wamejiestablish huko juu wakaacha huku chini ambako ndiko wapiga kura walipo.
kwann kila lilipo shina la CDM basi kusiwe na umoja wa akina mama wa CDM?? wanaona ugumu gani kurudi huku chini??ama ni kwasabbau CDM haina akina mama ambao ni watu wazima ambao wanweza kuwashawish wamam wa mitaani??
gfsonwin nadhani tatizo lipo katika ngazi ya taifa kwamba jumuiya muhimu kama BAWACHA haina msisimko kama tunaouona UWT. Sina maana waige lakini uwepo wa jumuiya na umuhimu wake upo pale pale.

Suala si kupata viongozi wazee akina mama, suala ni kupata viongozi ambao wataifanya jumuiya yao iwe effective na ichangie katika maendeleo ya chama.Viongozi watakaovutia hata hao wazee kujiunga. Hivyo basi CDM wanapaswa kuanzia sasa waamke.

Nina imani kuna viongozi wazuri tu kutoka katika kundi la akina mama na hao wanaweza kuwa na mchango mzuri sana.

Ningewashauri wavunje uongozi uliopo na waweke uongozi mpya.

Lada niulize hivi hawa wabunge wa viti maalumu wana kazi gani ndani ya chama?
Kwanini wasipewe jukumu la kuendesha jumuiya hata kama si uongozi.
Nina maana wasimamie jumuiya hizo ili ziwe effective.

Kwa upande wa BAVICHA huko nako kuna tatizo kwasababu ni nadra kumsikia kiongozi wa mkoa au wilaya anayesimama na kuzielezea, kuzitetea sera na kuonyesha mwelekeo wa chama.
Zaidi utamsikia John Heche, sasa huyu ataweza kuwepo kila mahali kweli.

Kama CDM hawatajipanga mapema migogoro itawakuta wakati wasioutaka.

 
Last edited by a moderator:
gfsonwin nadhani tatizo lipo katika ngazi ya taifa kwamba jumuiya muhimu kama BAWACHA haina msisimko kama tunaouona UWT. Sina maana waige lakini uwepo wa jumuiya na umuhimu wake upo pale pale.

Suala si kupata viongozi wazee akina mama, suala ni kupata viongozi ambao wataifanya jumuiya yao iwe effective na ichangie katika maendeleo ya chama.Viongozi watakaovutia hata hao wazee kujiunga. Hivyo basi CDM wanapaswa kuanzia sasa waamke.

Nina imani kuna viongozi wazuri tu kutoka katika kundi la akina mama na hao wanaweza kuwa na mchango mzuri sana.

Ningewashauri wavunje uongozi uliopo na waweke uongozi mpya.

Lada niulize hivi hawa wabunge wa viti maalumu wana kazi gani ndani ya chama?
Kwanini wasipewe jukumu la kuendesha jumuiya hata kama si uongozi.
Nina maana wasimamie jumuiya hizo ili ziwe effective.

Kwa upande wa BAVICHA huko nako kuna tatizo kwasababu ni nadra kumsikia kiongozi wa mkoa au wilaya anayesimama na kuzielezea, kuzitetea sera na kuonyesha mwelekeo wa chama.
Zaidi utamsikia John Heche, sasa huyu ataweza kuwepo kila mahali kweli.

Kama CDM hawatajipanga mapema migogoro itawakuta wakati wasioutaka.

Nguruvi3 nakubaliana na wewe sana juu ya BAVICHA kuundwa upya nikiwa namaana kwamba ibadilishwe uongozi.

lakini kuna tatizo ambalo kwangu mimi naliona na hilo liko miongoni mwa akina mama zaid sijui tuna mentality gani lakini mama yyte yule wa makamo ukimweka mahali kumwelezea jambo kama ni binti mdogo watakuskiliza lakini wataona kwamba unapotoka.

binafsi kwa experience niliyonyo na akina mama kwenye vikundi vya kijamii naweza kukwambia kwamba wamama wanapenda zaid vijana wadogo wawaongoze ila sasa uogozi wa vijana hao uwe unakuw amonitored na wamama hawa. jambo hili huwafanya wengi wa wanwake vijana kujichokea na kukata tamaa.

linalotokea kwa bawacha ni ukweli kwamba vijana wanajua complications za akina mama hivyo kila mmoja kuona ya nini mm kwenda kupata tabu na akina mama??

kuhusu BAVICHA naomba hapa nisiseme jambo manake hili ni bomu lilitegwa ndani ya CDM ama kwa kujua ama kwa kutokujua.
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin;6865776]Nguruvi3 nakubaliana na wewe sana juu ya BAVICHA kuundwa upya nikiwa namaana kwamba ibadilishwe uongozi.

lakini kuna tatizo ambalo kwangu mimi naliona na hilo liko miongoni mwa akina mama zaid sijui tuna mentality gani lakini mama yyte yule wa makamo ukimweka mahali kumwelezea jambo kama ni binti mdogo watakuskiliza lakini wataona kwamba unapotoka.

binafsi kwa experience niliyonyo na akina mama kwenye vikundi vya kijamii naweza kukwambia kwamba wamama wanapenda zaid vijana wadogo wawaongoze ila sasa uogozi wa vijana hao uwe unakuw amonitored na wamama hawa. jambo hili huwafanya wengi wa wanwake vijana kujichokea na kukata tamaa.

linalotokea kwa bawacha ni ukweli kwamba vijana wanajua complications za akina mama hivyo kila mmoja kuona ya nini mm kwenda kupata tabu na akina mama??

kuhusu BAVICHA naomba hapa nisiseme jambo manake hili ni bomu lilitegwa ndani ya CDM ama kwa kujua ama kwa kutokujua
gfsonwin nichangie kuhusu hili la akina mama. Heshima ya mtu inatokana na huduma yake kwa jamii kama ilivyoandikwa katika miongozi nadhani wa TANU.

Kwamba ukitoa huduma yako inayotarajiwa na jamii utaheshimika na jamii hiyo bila kujali sifa nyingine zinazoambatana nawe.Kwamba mtoto hadi akina mama watakuheshimu.

Tatizo lipo katika social interaction kati ya akina mama na mabinti.
Kwa vijana wa kiume ni rahisi sana kuishi na wazee wao na kukubalika kwasababu kwanza wanawaheshimu hao wazee kwa nafasi zao. Pili, hawana mambo ya ku-twit na mama zao kwa wazee hao.

Sasa kwa upande wenu, wakina mama si kuwa wanataka ku-monitor utendaji wenu, wanachofanya ni kudhibiti vitabia vyenu hasa mnapokuwa na baba zenu katika safu nzima ya uongozi.

Mnaanza twitter, face book mara invitation whatsup kwenye vikao mnacheka na kulaliasuti zao, mara sharafa zako zinang'aa sasa haya wakiyasikia na kuyaona akina mama wengine wanakuwa na shaka na hivyo kuweka udhibiti.

Utakuwa katibu BAVICHA au UWT lakini with close watch.
Kwahiyo usilaumu kwa kufumba jicho, gfsonwin lazima tuangalie kutoka angle zote.

Akina mama watu wazima wanakuwa defensive in a way, wakiondoka nyumba beki 5 au Mercury(Hg) wanashambulia, kazini kuna 'naomba thoda' wanashambulia, akina mama lazima wawe nervous. Ukikabidhibiwa BAVICHA lazima wahakikishe anacheza FIFA (fairplay) si vikao kunduchi beach kila wa leo.

Ni makosa kusema mnadhabitiwa na hivyo kujichokea. Ni lazima muwe sehemu ya mchakato na mapambano ya kisiasa. Njia rahisi ni kupitia jumuiya zenu na huko ninyi muwe chachu ya mabadiliko na si kuchezea sharafa za watu.

Mkijiheshimu watawaheshimu na mtajikuta siku moja wameacha kuwa monitor.



 
gfsonwin nichangie kuhusu hili la akina mama. Heshima ya mtu inatokana na huduma yake kwa jamii kama ilivyoandikwa katika miongozi nadhani wa TANU.

Kwamba ukitoa huduma yako inayotarajiwa na jamii utaheshimika na jamii hiyo bila kujali sifa nyingine zinazoambatana nawe.Kwamba mtoto hadi akina mama watakuheshimu.

Tatizo lipo katika social interaction kati ya akina mama na mabinti.
Kwa vijana wa kiume ni rahisi sana kuishi na wazee wao na kukubalika kwasababu kwanza wanawaheshimu hao wazee kwa nafasi zao. Pili, hawana mambo ya ku-twit na mama zao kwa wazee hao.

Sasa kwa upande wenu, wakina mama si kuwa wanataka ku-monitor utendaji wenu, wanachofanya ni kudhibiti vitabia vyenu hasa mnapokuwa na baba zenu katika safu nzima ya uongozi.

Mnaanza twitter, face book mara invitation whatsup kwenye vikao mnacheka na kulaliasuti zao, mara sharafa zako zinang'aa sasa haya wakiyasikia na kuyaona akina mama wengine wanakuwa na shaka na hivyo kuweka udhibiti.

Utakuwa katibu BAVICHA au UWT lakini with close watch.
Kwahiyo usilaumu kwa kufumba jicho, gfsonwin lazima tuangalie kutoka angle zote.

Akina mama watu wazima wanakuwa defensive in a way, wakiondoka nyumba beki 5 au Mercury(Hg) wanashambulia, kazini kuna 'naomba thoda' wanashambulia, akina mama lazima wawe nervous. Ukikabidhibiwa BAVICHA lazima wahakikishe anacheza FIFA (fairplay) si vikao kunduchi beach kila wa leo.

Ni makosa kusema mnadhabitiwa na hivyo kujichokea. Ni lazima muwe sehemu ya mchakato na mapambano ya kisiasa. Njia rahisi ni kupitia jumuiya zenu na huko ninyi muwe chachu ya mabadiliko na si kuchezea sharafa za watu.

Mkijiheshimu watawaheshimu na mtajikuta siku moja wameacha kuwa monitor.




dah!!! bestie yaani hii post naisoma nikiwa nimekamatia glas ya safari sasa nimeielewaje???
dahhh!! idumu milele TBL sio siri hii bia ni TAMU sana acha tu.

nirudi kwenye mada.
kaka yangu Nguruvi3 umesema jambo ambalo kila siku huwa nalisemaga kwenye vikao vyetu vya akina mama. Sikufichi na hapa nitaomba akina mama ambao kidogo wana exposure kama yangu na kuendelea waongezee nianze na wale wenye exposure kubwa zaid kuliko mimi kama vile Mwali, AshaDii, MwanajamiiOne, Roulette, Kaunga , King'asti, Kongosho et al.

jamani tunakutana na mengi sana ambayo kimsingi yako nje ya uwezo wetu. Nguruvi3 utakubaliana na mimi kwamba mwanaume ameumbwa kutamani, na haijalish anatamani nani na wakati gani. sasa kwa wale akina mama ambao huwa wanatokaga wanakutana na challenge hizi tena pasi wao kutaka kuzianzisha yaani unakuta nyingine hadi zinaboa kabisa.

unaposema wamama watu wazima wako ili kulinda tusi cheze na ndoa zao nakuelewa kabisa lakin umesahau kwamba huyu binti wala sio yy anayeleta haya ila ni hulka ya baba husika muda mwingine. ninachokiona mimi hapa ni kwamba kama akina mama wanaona sisi wamama vijana ni matatizo basi wanakosea kwasababu tatizo lipo kwao wanatakiwa waweze kuongea na wenzi wao lugha ngumu lkn zinazoeleweka na sio kuja kutuangushia mzigo sisi kwasabbau tu wanyonge.

hakuna binti mwanasiasa anayefurahia kuona anakuwa chumba cha kutongozwa na kila kiongozi ama kila mwanaume mwanasiasa lkn pia ni nje ya uwezo wake kulikataa hili la kutongozwa as utongozaji ni hulka ya kiume, binti kama binti atakachifanya ni kukataa tu na tena mahali pengine huzidiwa jamani akajikuta bad ameanguka dhambini. tena kwa kosa la kusababishiwa.

nafikiri ufike mahali sasa wamama wanasiasa waanze kwanza kusem an waume zao ili japo kuua hulka ya utongozaji ndani ya waume zao( sijui kama hili linawezekana) lkn ndio njia pekee hii. ila kusema tu kwamba binti anakuwa monitored kwasababu mama anaogopa atatempa na mumewe(baba kwa maana ya umri) ni makosa sana.

hii ni kwa mujibu wangu tu. na ndio maana wanawake wengi wamejitoa kwenye siasa hizi. Binafsi nilikuw amwanasiasa mzuri sana wakati nakua na wapo ambao wanashangaa kwann mm niliacha siasa kabisa actually nilichoshwa na niliyoyakuta humo. nilipoondoka wengi waliokuja kunuliza niliwaambia ukweli kabisa kwamba nimeshindwa kwasababu ya mitongozo and walikuwa wanacheka na kusema mbona wewe mwoga lkn huo ndio ukweli ninao wenza kusema kwa uhalisia manake nilijionea ya kutosha na nikasema this is too much.

kimsingi siasa ni mchezo ambao kwa nchi changa kidemokrasia kama Tazania haim-fevi binti na ukitizama kwa makini utagundua once umekuwa mwanasiasa utaandamwa na mengi ikiwemo kuandikwa hata list ya bf zako uliokuwa nao miaka iyo. nafikiri unakumbuka nini kilitokea kwa wanasiasa wamama wengi. but do you want to tell me kwamba kuwa na bf ama kutoka na wewe Nguruvi3 ni kosa la kunifanya mimi nisiwe mwanasiasa?? na kama sio kwann kwangu mimi iwe ni news headlines lakin kwako wewe kutoka na na mimi gfsonwin isimake headlines kwenye news??
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin kabla sijarudi katika mada ya kisiasa ningependa nichukue uwakili wa muda kwa kundi la akina mama. Ninaelewa frustrations kutokana na mapigo wayapatao mahausigeli,maofisini hadi wanaporejea. They are nervous, sure! we need to acknowledge this

Pili, not true kuwa wanaume wanawasumbua mabinti. Of course nature in play role lakini mabinti wamekosa ujasiri wa 'confrontation'. Simama kidete na mwambie wewe mume wa mama madame X tafadhali acha tabia hii la sivyo nitamweleza mama.

Ironically ninyi mabinti mmekuwa mnawafuata nataka Sienna, Hariela, n'nataka 'Lexus ipo chati' ukijua kabisa huyo ni mume wa mtu. Mume anakualika fb kwanini usimwalike mkewe ili kuwe na mawasiliano ya wazi. kwanini unaficha!

Ni kwasababu hizo wakija katika Politics wanashindwa,hawakuwa tayari kukabili challenges.Hawakuwa na :
(a) objective; kuwa kwanini wanaingia katika siasa na kwa impact gani katika jamii.
Mathalan, mwanamke anaweza ingia katika politics kwa malengo tofauti
(i)kutumia Political influence kwa wasichana waliopata mimba kupata second chance ya elimu (ii)kutoa msaada wa kisheria kuwabana wasambaza mbegu na kuacha mzigo kwa mwanadada
(iii)kuhakikishia wasichana waliokosa fursakutokana na majukumu ya kifamilia wanapata fursa hiyo n.k. n.k.

(b)Kukosa political ambitions;
kwamba hawana malengo kufikia viwango vya kisiasa.Ni mara chache sana mabinti watajiuliza kwanini wasiwe kama Dambisa Moyo, Ngozi ikowaje, Cond Rice, Hillary, Margareth thatcher,Mongela, Indira, Benazirh au wataalam katika siasa kama Christian Lagarde.
Kwanini wasing'are kama akina Rosa Park, Matahare Wangare,Linda Choka n.k

Kwasababu wengi hawana courage ya confrontation objective na ambition(malengo na matamanio ya kimaendeleo)wanaishia katika 'politics for convenience' na hapo ndipo quid pro quo inaingia na wao kujikuta vulnerable.

Kukua na kuendelea kwao kisiasa kutategemea quid pro quo(nifae kwa jua nikufae kwa mvua). Wakati wa kutafuta hayo sehemu rahisi kupiga ni familia za akina mama watu wazima.

Na kwasababu akina mama ni victims of circumstance ndio maana huwaweka karibu ili kudhibiti nyendo zenu kijamii na si kisiasa kwa uhalisia.

Kutokana na kutoaminiana siku zote wanaume wanafidika katika siasa kwasababu ya wekaness zenu, kwamba mama mtu mzima atamkubali mwanasiasa mwanaume kuliko kabinti.
Mabinti wanaona watu wazima wataziba rizki zao.

Matokeo ya hayo ni kutegemea viti maalumu ambavyo kutokana na hali ya udhaifu miongoni mwa wanawake hata hizo nafasi za upendeleo zinapatikana kwa quid pro quo na inakuwa vicious circle.

Mimi nakusihi sana gfsonwin urudi katika politics. Tanguliza courage, objective na ambition.
Kitendo cha wewe kukimbia non stop mtongozo ni usaliti kwa daughter wako, causin sister, na wanawake in general.

Kama wewe umekosa courage ya kukabiliana na misuko suko ya kisiasa inayoambatana na 'maombi' kila siku, huyo daughter wako atapata wapi courage? Nani atamkomboa kama wewe mama ni mshindi wa mbio za mita 100

What a message 're you sending across to your daughter! kwamba yeye asifikirie political objective na ambition zake kwasababu mama alifunga mortar miguuni na kutoka mita baada ya incessant mitongozo. gfsonwin on that assertion am' wrong?

Nimalizie kwa kusema ili mabinti mfanikiwe kisiasa kwanza mnahitaji uungwaji mkono na akina mama watu wazima. Ninyi mnawajibu wa kuwa approach hawa watu wazima na kuwahakikishia kuwa mna objective na ambition na wala siyo mission nyingine.

Ni lazima mkubali kuwa ili kujenga confidence kuna wakati mnapaswa kukubali kuwa chini ya uangalizi wao as launching platform.

Ahsante
 
PROFESA LIPUMBA AKUTANA NA RAIS KIKWETE

Katika wiki chache zilizopita kumekuwa na utata kuhusu matamshi ya kiongozi wa CUF profesa Lipumba katika nyumba za ibada na kufuatiwa na msimamo wa CUF kuhusu gesi Mtwara.

Juzi Ikulu imetoa picha za profesa Lipumba alipokutana na Rais.
Umuhimu wa picha hiyo ni wa kisiasa zaidi kwani wangeweza kukutana bila Kuonyesha picha.

Tunakumbuka profesa aliwahi kutoa matamshi ya jinsi CUF kilivyoshirikiana na CCM katika uchaguzi uliopita kwa kile kilichosemwa kuokoa jahazi.

matamshi hayo yameambatana na lawama kuhusu kutelekelekezwa kwa waislam licha ya juhudi hizo kama alivyonukuliwa profesa Lipumba.Tumeshalijadili hili na hakuna sababu ya kulirudia.

Makusudi ya bandiko hili ni kujaribu kuelezea kile ambacho kinaonekana kuleta sintofahamu miongoni mwa jamii kuhusu mkutano huo. Mengi yamesema na tunajaribu kuyaangalia kwa mtazamo mwingine.

Mkutano wa wawili hao unaweza kuwa umechagizwa na mambo makubwa mawili.
(1) Gesi Mtwara
Kwamba CUF inataka kuandamana kupinga ukatili wa majeshi huko mtwara.
Hivi karibuni katika mitandao kumeonekana picha za watu waliolabuliwa kwa mikwaju na zana zingine. CUF bado wanamsimamo wa kuandamana kuhamasisha wananchi wa Mtwara.

Wakati mabomba yanateremshwa Dar na Mtwara kumetokea mashambulio ya magari yaliyobeba mabomba hayo. Hili linaonyesha kuwa hali si shwari na kunahitajika jitihada za makusudi, kwanza kuzima 'uasi' huo usiendelee kwasababu unatishia usalama wa wawekezaji na mradi kwa ujumla na pili kuzuia mambo yanayohusu utesaji kuibuka zaidi ili kuweka taswira ya nchi katika hali nzuri.

Tunafahamu kuwa kumekuwepo na picha zinazosambaa katika vyombo vya habari ikiwa ni pamoja na mitandao ya kijamii ikionyesha uvunjaji wa haki za binadamu wa kiwango cha hali ya juu. Kuendelea kutoa picha zaidi kunaharibu taswira nzima ya serikali ya Kikwete.

2. Kuna uwezekano rais amemwita Lipumba ili kumsihi asiendelee na uchochezi wake katika nyumba za ibada.Inamwia rais vigumu kumtia pingu profesa ambaye ni mwenyekiti wa chama cha upinzani ambaye alishiriki kuokoa jahazi mwaka 2010 kama ambavyo angemtia pingu sheikh Ponda.

Tunadhani rais ameshauriwa kumkanya Profesa kwa njia za kiutu uzima kwani kutofanya hivyo kutazuia vyombo vya dola kuwachukulia hatua dagaa na wakati huo huo kuendelea kuiumbua serikali. Kauli ya kuokoa jahazi hatudhani ilipokelewa vema na kambi ya rais na chama chake.

Kutokana na hali ya misuguano ya kidini ilivyo kuendelea kumwachia profesa kumwaga sumu kunaiweka serikali na watendaji wake katika wakati mgumu na imebidi rais aingilie kati.

Hakuna anayejua kwa uhakika nini wameongelea lakini kwa mujibu wa duru za kisiasa nchini mambo hayo mawili ni sehemu muhimu sana ya maongezi yao.

Tusemezane

Mgeni wa leo THE BIG SHOW
 
Last edited by a moderator:
UZAO WA MTOTO FAMILIA YA KIFALME UINGEREZA

Prince William na mkewa Kate Middleton wanataraji kupata mtoto wa kwanza wakati wowote.
Hadi tunaandika bandiko hilo wawili hao bado wapo Hospitali na hakuna tangazo la uzazi.
Inasemekana tarehe za kuzaliwa mtoto zimepita kwa muda fulani jambo la kawaida katika uzazi

Wanahabari wamepiga kambi kupata habari za uzao wa mtoto huyo ambaye hadi sasa anajulikama kama baby Cambridge. Haijulikani ni wa kiume au wa kike.

Utaratibu wa kufuata katika kutangaza habari za uao ni kwa prince William kumpigia simu malkia kwanza halafu wana familia wa Buckingham kutoa taarifa za ujio wa mtoto katika familia ya malkia. Huyu atakuwa kitukuu cha malkia Elizabeth II

Imefika wakati watu kuhoji jina la mtoto huyo litakuwa ni nani huku kukiwa na orodha ndefu ya mapendekezo.

Swali kubwa linaloulizwa ni hili, kwanini mtoto huyo apewe 'attention' ili hali kuna mamia ya watoto wanazaliwa kila siku tena wengine katika hali ngumu zaidi?

Kuna majibu mengi juu ya hili.
1. Jambo linalohusu familia ya kifalme Uingereza hufungamanishwa sana na biashara.
Inasemwa kuwa ndoa ya Kate na William iliingiza mabilioni ya dola kupitia bidhaa, matangazo, utalii n.k.

Na hili halionekani kwenda mbali na ukweli huo. Bidhaa zinauzwa kuhusiana na mtoto huyo mtarajiwa na vyombo vya habari vikitoa makala na habari za kibiashara.

2. Waingereza ni wazuri wa kupiga debe katika mambo yao.
Wanapoamua kulifanya jambo dogo kuwa kubwa wanauwezo huo.
Hili linagusa sana tamaduni zao na ni moja ya mambo yanayowaunganisha waingereza.

3. Mtoto mtarajiwa ana uhusiano na siasa za nchi yake na za kimataifa.
Hapa ndipo tuanzie kwasababu ni sehemu muhimu sana ya uzao huu.

Kwanza, tuangalie kwa uchache kuhusu familia ya kifalme. Familia hii ndio inayotoa mkuu wa nchi ya falme za uingereza (United Kingdom).
kuna tofauti ya united kingdom na England na ni rahisi sana kuchanganya mambo hayo.

Waziri mkuu wa Uingereza ni mkuu wa serikali na siyo mkuu wa nchi. Yeye hupata ridhaa ya kutawala kutoka Buckingham Palace ndipo anaelekea number 10 Downing street.

Familia ya kifalme ndio pia wakuu wa kanisa la Uingereza la Church of England.
Kutokana na ukoloni tulikuwa na kanisa la England church ambalo limebadilika kwa jina kutokan sasa hivi linajulikana kama Anglican na sehemu nyingine wanaita African Inland church n.k.

Kwa muda wa miaka 300 taratibu za utawala zilihusisha unasaba wa damu, kwamba kurithi kiti cha enzi wanaume walipewa kipaumbele. Iwapo mfalme au malkia alikuwa na watoto 3 wakwanza wa kike na wa pili wa kiume, kiti cha enzi kilimruka mwanamke na kwenda kwa mwanaume(throne)

Malkia Elizabeth alikuwa mtoto pekee wa King George na hivyo hakukuwa na chaguo bali yeye.
Kuna mambo yasiyosemwa kuhusu yeye kurithi kiti hicho kwani aliyepaswa kwa taratibu alikuwa mwanafamilia wa ndugu ambaye alikuwa ni mwanaume. hilo tutalijadili wakati mwingine.

Katika familia zilizofuata utaratibu wa uzao ni ile ya Diana na Charles ambao walipata watoto wawili Harry na William,William ndiye mrithi wa kiti na Harry ni kama spea.

Kwavile falme ilikuwa inafuta utaratibu wa miaka 300 iliyopita, urithi wa malkia ulikuwa ufuate utaratibu wa Elizabeth II, Prince Charles, William na Harry.

Utaratibu huu uliwaruka watoto wa Elizabeth wasichana kwasababu watoto wa kiume walifuatana na wao ndio warithi.Kwa muktadha huo prince Harry ni mrithi wa tatu(3rd in throne).
Kumbuka hili lina umuhimu katika mjadala.

October 28 2011 ufalme ulibadili taratibu na kuwa urithi wa kiti sasa hautachagua jinsia tena.
Kwa maneno mengine kama mtoto wa kwanza atakuwa mwanake basi atakuwa malkia hata kama wanaomfuata ni wa kiume.

Hii maana yake ni nini?
Maana yake ni kuwa mtoto mtarajiwa wa William na Kate siku moja atakuwa mfalme au malkia wa Uingereza na hivyo kiti cha enzi kitafuta utaratibu ufuatao:
1. Prince Charles
2. Prince William
3. 'Babay Cambridge' ambaye hajazaliwa
4. Prince Harry

Kwamba nafasi ya prince Harry sasa ni namba 4 na si tatu kama tulivyosema hapo awali.
Kwa kuangalia umri wa maisha 'longevity' wa malkia Elizabeth ni wazi prince Harry hatakuwa mfame.

Baba yake ana zaidi ya miaka 60,kaka yake ni mdogo katika miaka 30 na sasa kichanga na kila mmoja atakula shea yake kabla ya Harry ambaye hataonja ufame labda tu litokee janga kubwa sana lisilotarajiwa.

Ni kwa muktadha huo baby cambridge anategemewa kukalia kiti cha enzi kama mfalme au malkia na hapo atakuwa mkuu wa Anglican, mkuu wa nchi na mkuu wa jumuiya ya madola
(commonwealth).

Hivyo msisimko ni wa jumuiya kubwa ya kimataifa ni kwasababu mtarajiwa atakuwa na ushawishi mkubwa katika medani za kiutawala na kiimani ndani na nje ya Uingereza, na hili hasa ndilo linaleta msisimko duniani.

Endapo baby cambridge atakuwa wa kike basi uwezekano wa kuitwa Elizabeth au Victoria ni mkubwa sana. Sababu kubwa ni kuwa Victoria ndiye malkia aliyeongoza Uingereza kwa muda mrefu akifuatiwa na Elizabeth wa sasa ambaye itakapofika september 5 mwaka 2015 ataukuwa ameifikia rekodi ya Victoria.

Kwa uchache mtoto mtarajiwa atakuwa sehemu yetu Watanzania na mataifa ya madola kwasababu ndiye atakayekuwa mkuu wa jumuiya hiyo hata kama ni miaka 100 ijayo.

Haya ndiyo yanajiri na tutaendelea kuwaletea habari zaidi kadri zitakavyopatikana.

Tusemezane

Mgeni wa leo Roulette
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,
Shukran kwa uchambuzi wako wa kina na uliojaa uhalisia wa hali ya juu,

Jambo ambalo namimi naona tuzungumze katika suala hili hususana kadhia ya GESI MTWARA,wanasiasa especially CUF wanalichukua juu juu na kuliwekea ushabiki kana kwamba wao ndio hasa wahanga na waathirika wa jambo hili hali ya kuwa uhalisia ni kwamba wahanga na waathirika wa jambo hili ni wana mtwara na taifa zima kwa ujumla pasi na kuangalia itikadi za kisiasa,kidini na kikabila...

Sote tunafaham ya kwamba miongoni mwa kauli mbiu ambazo watu wa kusini wanazitumia na kuziamiini ni hii inayosema GESI KWANZA SIASA BAADAE,
Waliamua kusema hivi kwa uwazi wa hali ya juu ili wanasiasa wasije wakaipora hoja hii na kuifanya kama ajenda yao ya kupambana na serikali na kujenga umaarufu wao kwa wananchi,kwani mwanasiasa ni mwanasiasa tuh,na siku zote hawa wa nchi zetu hizi wamekuwa ni vigeu geu kwa kias kikubwa sana...

Ni wazi kwamba wana Mtwara hawakuwahitaji wanasiasa ili kuwapa backup ila hawakuwazuia wanasiasa kujiunga katika harakati hizi pale walipoona wao wanafursa hiyo,
Nafas ya wanasiasa ipo sawa kabisa na nafasi ya wanaharakati wa asas za kirai,wanaharakati wa haki za binadamu,jumuiya za kidini za iman zote kuu,na wananchi wa kawaida waishio kanda hii,ambao ni wakazi na wenyeji.

Kuonekana Leo Profesa Lipumba kuichukua hoja hii juu juu kama hoja ya CUF na kwamba waliopigwa ni wanachama wa CUF na viongozi wake kwenda nayo machoni mwa watanzania kama msemaji wa wana mtwara na wanakusini kwa ujumla mpaka kufikia hatua ya kuitisha maandamano ya kwenda ikulu kushitaki kwa kikwete maandamano ambayo yalizuiwa kwa kupisha ziara ya Rais Barack Obama,na kisha hivi majuzi kuonekana kwake akipiga picha na huyo huyo aliedeploy jeshi la wananchi kuja kuwatesa wananchi wa mtwara kwa kicheko kikubwa cha kulewa propaganda na uchumia tumbo ni jambo la kulaaniwa na kupingwa kwa nguvu zote,

1.Lipumba atambue ya kwamba yeye si msemaji wa madhila ya wana mtwara,pindi wana mtwara wanaanza vugu vugu hili atambue ya kwamba hawakushawishiwa na CUF na walaviongoz wake,walishawishiwa na uzalendo wao kwa mkoa huu na taifa kwa ujumla.

2.Lipumba atambue ya kwamba suala la gesi ya mtwara hawez kujipatia nalo umaarufu na kutegemea litamjenga eti kwa kuonekana ni kiongoz barid barid kwa JK,huku wananchi wa mtwara ambao hata hawajamuagiza yeye kwenda kuwasemea wakiendelea kuumia na kudharaulika,hilo akae akilitambua.

3.Lipumba aache kuunasibisha uislam kwa faida zake kisiasa,tunajua madhila yanayotumbuka waislam katika nchi hii,na tunajua solution siyo tu kupata rais muislam au kufanya uislam wa kisiasa kwenye taifa hili,solution katika hili ni sisi wenyewe waislam kujitambua,kujiratibu na kutafuta chombo kitakachouwa free katika kusimamia mambo yetu tofauti ya BAKWATA KINAVYOTUMIKISHWA KISIAISA NA CCM NA MAFISADI KWA UJUMLA..

Lipumba ajipime na ajiangalie mara mbili mbili,kulichukua suala la kisiasa na kuingiza uislam kijanja kijanja,huku akisema waislam ndan ya taifa hili wengi tunaish kama raia daraja la nne ni upotofu wa hali ya juu na kupandikiza chuki zaid,kama yeye anatembea vijijin hata mijini atakuja kuona wapo wanaoish maisha duni hata zaid ya baadhi ya waislam katika taifa hili,je tuseme kwamba hao wameathiriwa na nini??kwaiyo utakuja kuona anatumia ujanjaujanja katika madai yake na kuuweka ukweli nje,aeleze madhila ambayo waislam wameyapata tokea uhuru,aeleze zipi sababu zilizopelekea hivo na yeye anafaham,kisha aeleze sisi kama waislam tufanye nini ili kupambana na hali hiyo,
Asije hapa na conclusion zake za ajabu ajabu eti ya kwamba tukikipa kura CCM ambacho kinaongozwa na muislam au CUF amabcho kinaongozwa na muislam basi hapo tutakuwa tumejikomboa,kwani hao viongoz ambao ni waislam katika ya vyama vyao wanavyovisimamia WANATUMIA QUR AN NA HADITH ZA KIPENZ CHETU MOHAMMAD S.A.W KAMA KATIBA YAO??sasa kwanini asisitize waislam tuweke matumain yetu moja kwa moja kwa wanasiaisa?

Aeleze mambo kisomi yeye kama Profesa,na sio kueleza mambo kwa kukariri na kuigawa jamii ya Watanzania kwa mwamvuli wa uislam...

THANKS NGURUVI3...
 
Mkuu THE BIG SHOW nimesoma bandiko lako mara mbili mbili,lazima nikiri sikutarajia uchambuzi wa hali ya juu toka kwako.Nimebaki na mshangao kama si mshtuko kumbe mkuu wangu una uwezo mkubwa sana sema wakati mwingine sijui unafanya maksudi au ?.

Mkuu THE BIG SHOW ni kweli Prof Lipumba mara kadhaa amenukuliwa akijipachia uwakilishi na utetezi wa Uislam labda baada ya kushindwa katika chaguzi zilizopita kaamua kukimbilia kete ya udini.Ni ajabu msomi wa kiwango cha Lipumba mwenye ufahamu mkubwa wa masuala ya uchumi kaamua kujichimbia katika hoja dhaifu "DINI".

Prof Lipumba kaweka rekodi ya kugombea kiti cha urais mara nyingi kuliko mwanasiasa yoyote hapa Tanzania.Sina sana uhakika labda anaweza kushika nafasi ya juu sana katika level ya dunia.

Nilitarajia Prof Lipumba kwa usomi wake angetoa maoni nini kifanyike ili gesi iliyogunduliwa Mtwara isaidie kuinua kiwango cha maisha bora kupitia miradi ya kiuchumi kama ujenzi wa viwanda vidogo na vikubwa,ujenzi wa miundombinu ya kisasa reli,barabara na bandari itakayotoa huduma kwa wilaya na mikoa inayopakana na Mtwara.Gesi ya Mtwara Ni nyingi sana kuna jarida niliwahi kulisoma wana sema gesi ni nyingi kuliko mahitaji ya Tanzania !.Kama ni kweli basi gesi ya Mtwara ni lazima isafirishwe sehemu mbali mbali za nchi si Dar bali mikoa mingine ya Tanzania ikichagizwa zaidi na sababu za kiuchumi zaidi.Nilitarajia pia angezungumzia uwazi wa mikataba ya gesi,angezungumzia sera ya gesi,angezungumzia uimarishwaji wa TPDC kwa maana ya kujengewa uwezo wa kutafuata na kuchimba mafuta na gesi siku za usoni.Hoja hizi nilitarajia zingetolewa na Prof Lipumba lakini kinyume chake kakimbilia kujivika umiliki wa gesi ya Mtwara na ukombozi wa waislam Tanzania.

Nikushukuru tena na tena umenena jambo jema.


Mkuu Nguruvi3,
Shukran kwa uchambuzi wako wa kina na uliojaa uhalisia wa hali ya juu,

Jambo ambalo namimi naona tuzungumze katika suala hili hususana kadhia ya GESI MTWARA,wanasiasa especially CUF wanalichukua juu juu na kuliwekea ushabiki kana kwamba wao ndio hasa wahanga na waathirika wa jambo hili hali ya kuwa uhalisia ni kwamba wahanga na waathirika wa jambo hili ni wana mtwara na taifa zima kwa ujumla pasi na kuangalia itikadi za kisiasa,kidini na kikabila...

Sote tunafaham ya kwamba miongoni mwa kauli mbiu ambazo watu wa kusini wanazitumia na kuziamiini ni hii inayosema GESI KWANZA SIASA BAADAE,
Waliamua kusema hivi kwa uwazi wa hali ya juu ili wanasiasa wasije wakaipora hoja hii na kuifanya kama ajenda yao ya kupambana na serikali na kujenga umaarufu wao kwa wananchi,kwani mwanasiasa ni mwanasiasa tuh,na siku zote hawa wa nchi zetu hizi wamekuwa ni vigeu geu kwa kias kikubwa sana...

Ni wazi kwamba wana Mtwara hawakuwahitaji wanasiasa ili kuwapa backup ila hawakuwazuia wanasiasa kujiunga katika harakati hizi pale walipoona wao wanafursa hiyo,
Nafas ya wanasiasa ipo sawa kabisa na nafasi ya wanaharakati wa asas za kirai,wanaharakati wa haki za binadamu,jumuiya za kidini za iman zote kuu,na wananchi wa kawaida waishio kanda hii,ambao ni wakazi na wenyeji.

Kuonekana Leo Profesa Lipumba kuichukua hoja hii juu juu kama hoja ya CUF na kwamba waliopigwa ni wanachama wa CUF na viongozi wake kwenda nayo machoni mwa watanzania kama msemaji wa wana mtwara na wanakusini kwa ujumla mpaka kufikia hatua ya kuitisha maandamano ya kwenda ikulu kushitaki kwa kikwete maandamano ambayo yalizuiwa kwa kupisha ziara ya Rais Barack Obama,na kisha hivi majuzi kuonekana kwake akipiga picha na huyo huyo aliedeploy jeshi la wananchi kuja kuwatesa wananchi wa mtwara kwa kicheko kikubwa cha kulewa propaganda na uchumia tumbo ni jambo la kulaaniwa na kupingwa kwa nguvu zote,

1.Lipumba atambue ya kwamba yeye si msemaji wa madhila ya wana mtwara,pindi wana mtwara wanaanza vugu vugu hili atambue ya kwamba hawakushawishiwa na CUF na walaviongoz wake,walishawishiwa na uzalendo wao kwa mkoa huu na taifa kwa ujumla.

2.Lipumba atambue ya kwamba suala la gesi ya mtwara hawez kujipatia nalo umaarufu na kutegemea litamjenga eti kwa kuonekana ni kiongoz barid barid kwa JK,huku wananchi wa mtwara ambao hata hawajamuagiza yeye kwenda kuwasemea wakiendelea kuumia na kudharaulika,hilo akae akilitambua.

3.Lipumba aache kuunasibisha uislam kwa faida zake kisiasa,tunajua madhila yanayotumbuka waislam katika nchi hii,na tunajua solution siyo tu kupata rais muislam au kufanya uislam wa kisiasa kwenye taifa hili,solution katika hili ni sisi wenyewe waislam kujitambua,kujiratibu na kutafuta chombo kitakachouwa free katika kusimamia mambo yetu tofauti ya BAKWATA KINAVYOTUMIKISHWA KISIAISA NA CCM NA MAFISADI KWA UJUMLA..

Lipumba ajipime na ajiangalie mara mbili mbili,kulichukua suala la kisiasa na kuingiza uislam kijanja kijanja,huku akisema waislam ndan ya taifa hili wengi tunaish kama raia daraja la nne ni upotofu wa hali ya juu na kupandikiza chuki zaid,kama yeye anatembea vijijin hata mijini atakuja kuona wapo wanaoish maisha duni hata zaid ya baadhi ya waislam katika taifa hili,je tuseme kwamba hao wameathiriwa na nini??kwaiyo utakuja kuona anatumia ujanjaujanja katika madai yake na kuuweka ukweli nje,aeleze madhila ambayo waislam wameyapata tokea uhuru,aeleze zipi sababu zilizopelekea hivo na yeye anafaham,kisha aeleze sisi kama waislam tufanye nini ili kupambana na hali hiyo,
Asije hapa na conclusion zake za ajabu ajabu eti ya kwamba tukikipa kura CCM ambacho kinaongozwa na muislam au CUF amabcho kinaongozwa na muislam basi hapo tutakuwa tumejikomboa,kwani hao viongoz ambao ni waislam katika ya vyama vyao wanavyovisimamia WANATUMIA QUR AN NA HADITH ZA KIPENZ CHETU MOHAMMAD S.A.W KAMA KATIBA YAO??sasa kwanini asisitize waislam tuweke matumain yetu moja kwa moja kwa wanasiaisa?

Aeleze mambo kisomi yeye kama Profesa,na sio kueleza mambo kwa kukariri na kuigawa jamii ya Watanzania kwa mwamvuli wa uislam...

THANKS NGURUVI3...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ngongo, THE BIG SHOW pale anaposimamia ukweli, huusema ukweli huo kama ulivyo na utajua ni kutoka moyoni mwake, na hili bandiko lake ni mfano mmoja tu. Namshukuru kwa hilo.
Ni mjenga hoja mzuri sana!

Suala la gesi Mtwara mara zote nimekuwa najiuliza, hivi hawa wananchi ni wendawazimu, mahayani, maalun tu kwamba wanaamka asubuhi na kupinga kitu kwa pamoja bila sababu!!!

Najiuliza nani amewahi kuka nao na kuwasikiliza wanasema nini!
Nani ameshawahi kutueleza kwa uhalisia kile wasichokielewa au kinachowachanganya wanamtwara!

Kwanini iundwe tume ya bunge na si kuwatumia wabunge wa Mtwara kueleza tatizo lao?
Na kwanini taarifa ya tume ya bunge ifichwe kama kweli kulikuwa na lengo la kutafuta uwazi na suluhu!

Ni nani mwenye nafasi nzuri ya kuwaongelea wana Mtwara, je ni mbunge wa Katavi, Tarime, Muheza na kondoa kwa kupitia kamati ya bunge! AU ni wabunge wa Mtwara?

Tuliwahi kuwaasa wana Mtwara kuwa suala lao lisifanywe katika misingi ya dini au siasa.
Kwamba majadiliano yasifanywe na baadhi ya watu misikitini na wala wanasiasa uchwara wakija wasiongee na wazee wa dini bali wa Mtwara na kwamba wafikirie mikindani na Ndanda pia.
Wameelewa na hatuoni maandamano ya Ijumaa wala vikundi vya watu bali Wana Mtwara.

Prof Lipumba anachosema ni cha kushangaza. Nilitegemea katika nafasi yake angekuwa na uwezo mkubwa sana wa kulielezea suala la Mtwara kiuchumi kuwaeleza nini kinaendelea iwe kwa kuungana au kutofautiana nao lakini aongozwe na weledi. Masikini hajafanya hivyo.

Prof amechukua suala la gesi tena bila kulieleza zaidi ya hoja dhaifu za mitaani, kalifanya la ukanda wa Pwani, kaliunganisha na Uislam na kamalizia na Uchaguzi.

Prof anaamini kuwa Umasikini wa Mikindani ni mbaya zaidi wa Ndanda, umasikini wa Naliendele ni mbaya zaidi ya Nyangao na umasikini huo umeuma kwa kutumia dini!!

Prof Lipumba anaamini kuwa ukiwa unatoka Kadewele Tunduru na jina la Hussein ukahamia Masasi mission na kubadili jina tu(siyo dini) na kujiita JohnWalker umasikini umekwisha.
Ndivyo anavyoamini prof katika kuungwa mkono kwa karata ya dini. Too low

Kwasasa amelichukua tatizo la Wanamtwara na kulifanya agenda ya kisiasa.
Hili si tatizo la Kanda ni tatizo la wananchi kama ilivyokuwa Nyamongo na mashimo yaliyojaa mercury.
Si tatizo la dini ni tatizo la kutoshirikishwa wananchi katika miradi.

Kitendo cha kuchukua tatizo la Mtwara na kuliita rasilimali za watu wa pwani, kulinasibisha na Uislam na kete za kisiasa ni kutotenda haki wa jamii.

Ni moray decay ya hali ya juu sana.Kinachotia maudhui na prof wetu ni kitendo cha kuchukua ajenda ya Mtwara kushindwa kuieleza kisomi na kuiunganisha ni dini kibubusa tu.

Mara zote tumesema wananchi wa Mtwara wana shea yao ya lawama hasa wasomi waliowatelekeza kwao, lakini hiyo si sababu ya kutosikiliza wale wenye manung'uniko wanalalamikia nini na je tunaweza kuwajibu wakaelewa au tunaweza kuwaelewa na kufanyia kazi concern zao? Hilo ndilo muhimu.

Wananchi wa Mtwara wanachosema si kuwa gesi ibaki tu ardhini au wavune kwa sululu na masufuria, hapana! wanachosema ni kuwa wao kama wadau wa mradi, je wameshirikishwa vipi na nini sehemu yao katika mradi? Iwe katika ulinzi wa rasilimali, mazingira au huduma za jamii.

Uwepo wa mradi una impact kubwa sana katika maisha yao iwe kimazingira, social n.k.
Wao wana fit wapi!

Bomba la gesi likihujumiwa wao ndio wanajua hujuma anaweza kufanya nani.
Bomba likivuja wao ndio waathirika si wachina na je kuna mkakati gani wa kuwasaidi kwa hilo, wahame vijiji au watenge maeneo yaliyo salama katika vijiji hivyo.

Ujio wa mradi unakuja na ongezeko la watu, nini impact yake katika huduma za jamii.
Je, kuna hospitali za kutosha kukabiliana na ongezeko hilo, je kuna shule za kutosha kukabiliana na wimbi la wanafunzi. Je kuna vituo vya kutosha kutoa ulinzi na usalama tukijua uhalifu utaongezeka n.k Je, hizo si genuine concern?

Leo taarifa ya kamati ya bunge imekuwa siri, halafu kuna mashujaa wa kusema Mtwara wamegomea gesi bila sababu.

Kama kamati ya bunge haiwezi kusema tatizo, hivi hapo watu hawaoni kuna tatizo tena kubwa.
Kama wabunge wa Mtwara hawatakiwi kueleza ya wananchi wao hivi watu hawaoni kuna tatizo!
Nani alisema tatizo la watu wa Mtwara ni chuo cha VETA!!!

Narudia hoja zangu za kila siku, wasomi wa Mtwara rudini mkawasaidie wananchi wenu kujenga hoja katika intellectual perspective ili wanafiki kama akina Lipumba wasitumie fursa hiyo kutoa machozi wakiwa Mikindani na tabasamu wakishapewa juisi ya maembe Ikulu.

Kuzuia wanafiki na wachovu wa kisiasa kama Lipumba kuligawa taifa kwa misingi ya udini ilimradi tu wao wapate mradi wao.

Kwa wananchi wa Mtwara, msikubali kugawanywa kwa misingi ya udini.
Ninyi nyote mnatatizo moja la umasikini ambalo halina unafuu wa jina, dini au ukabila.

Katika kutafuta majibu ya tatizo lenu mbegu za udini zinazopandwa na akina Lipumba zitawamaliza kisiasa na kijamii.

Mbegu hizo zitaota na kuwa miti mirefu ambayo wanasiasa wativunja na kuwa bakora za kuwaadhibu. Mtaadhibiwa na hoja dhaifu.

Mwambieni Lipumba kwanza awaeleze kama anajua tatizo lenu, awaambie suluhu ya tatizo lenu hapo hapo Mtwara na si Magogoni.

Akichoimeka mbegu za dini mumzomee kabla hajamiliza sentensi na kumtaka aondoke awaachie Mtwara yenu yeye aendelee na taifa lake la udini analotaka kulijenga.

Serikali elezeni nini wanamtwara wanalalamikia, na je, magrunedi, baruti, magobore ni suluhu ya tatizo? Nigeria walimnyonga Ken Sorowiwa wa Delta province kwasababu ya mafuta, je tatizo la uasi limekwisha?

Mbona kila siku ugomvi tukijua Nigeria walipeleka jeshi tena kufyeka watu na si kulinda amani, je ninyi mtatumia mbinu gani tofauti na za Nigeria ili zilete matunda tofauti?

Tusemezane

Mgeni wa leo Zinedine
 
Nguruvi3
Shukrani kwa mara nyingine tena,nimependa unavojimwaga mwaga na mitaa yangu ya nyumbani huku kama naliendele,nyangao,ndanda etc just to mention a few of them,
Yaonesha unakufaham haaswaana sio juu juu,tupo pamoja sana Mkuu,
Hoja zako zinafariji sana,wewe ni Mkwasi sana wa Fikra Mkuu...
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom