gfsonwin
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 18,272
- 20,692
Mkuu gfsonwin,nimefurahi kukusoma kwa mara nyingine tena,nafarijika sana...
Unajua kwa nchi za wenzetu,hizi tunazoziita dunia ya kwanza huwa wanavipaombele vya taifa ambavyo huwa haviyumbishwi na siasa zao,
Kwa mfano Bill clinton(Democrat) alipoiacha nchi ile kwa George Bush(Republican) na kisha G Bush kuondoka na kuiacha nchi hiyo hiyo tena Barack Obama wa Democrat hawatofautiani katika kusimamia vipaombele vya taifa lao,
Ima iwe ni uchumi,usalama na kadhalika,
Huku kwetu inashangaza sana,kila anaekuja huwa anakuja na sera zake na ajenda zake na kuacha kuangalia lipi ni la msingi na la kitaifa la kuliendeleza na lipi la kulipa muda,suala la Mtwara Corridor JK kalipuuza ili hali suala hili lilikuwa na umuhimu kitaifa na si kikanda,mwezangu yeye nadhan kaja kulichukulia kuwa sual hili chinga Mkapa alifanya katika kutafuta kujikomba na kuwasaidia wamachinga wenzake na sio taifa na ndio kwa maana hatushangai kwa yeye kulipuuza na kuhamishia akili yake kwao bagamoyo kwa kipindi hiki cha miaka miwili ilyobakia,najiuilza sana huyo rais ajaye atakuwa na misimamo ipi??sijajua kama atatokea CCM au la,
Ila kikubwa kinachonishangaza ni kwamba wenzetu hawa nchi zao hizi huwa wanabadilishana badilishana,
Msimu huu chama hiki,msimu ujao chama kingine,lakini linapokuja suala la national interests siasa na ubabaisha huwekwa kando na kufanya kazi,sasa hawa jamaa hupokezana vijiti wenyewe kwa wenywe,sasa najiuliza tatizo linatokea wapi??
Kwanini huyu anakuja kulipindisha la yule hali ya kuwa wote ni wamoja??na huwa wote kwenye meza moja za maamuz kichama na kiserikali??
Inashangaza sana kwa kweli...
Karibu sana kaka yangu THE BIG SHOW.
Naomba sasa nijibu hoja yako na ya ndugu yangu , kaka yangu Zinedine kama ifuatavyo;
Nimeona hoja iliyoibuka katika mabandiko yenu #278 na #280 ni kwamba HATUNA NATIONAL PRIORITIES ambazo zinatakiwa ziwe AMONG THE FIRST PRIORITIES kwa pesident candidate. na baraza lake la mawaziri.
Kwangu mimi naona sasa umefika wakati wananchi tuamue kwenye katiba hii mpya of which sijui kama itakuwepo kweli ama la kwamba among other things, ni kwamba rais anayechaguliwa lazima ahakikishe kwamba anafwata national interest na hizi zinatakiwa zipangwe na Katibu mkuu Kiongozi akishirikiana na watu wa sera na mipango ya ofisi yake.
hapa nina assume kwamba huyu CHIEF PERMANENT SECRETARY sio mwanachama wa chama chochote cha siasa na huyu tunaweza kumfkukuza na kumshtaki iwapo atakwenda kinyume na matakwa ya katiba yetu.
Binafsi kuna siku nilishiriki kwenye mjadala wa rasimu mpya ya katiba, nilishangazwa sana kuona pale hatukujadili mambo kama haya ila tulijadili sijui eti katiba iwe inasema mwanaume/mwanamke badala ya mwananchi...........ghhhhhhhhhhhhh nilikasirika sana, yaani sijui na wale waliokuja walitudororesha na nini......................
mara tunajadili ooh! kwenye katiba tuondoe ulazima wa mtu kuimba wimbo wa taifa, kwasabbau uko biased kwa mtu asiye mwamini Mungu.............. mimi niliboreka sana nikajiondokea manake niliona sina cha kuongea. Kumbe kuna mambo ya msingi kama haya ambayo tunatakiwa tuyajadili kwa kina kabisa.
napenda sana niwashukuru Zinedine, THE BIG SHOW Nguruvi3 na Mchambuzi kwa kunishirikisha katika mjadala huu na kujibu hoja zangu. Lakini pia napenda niwasisitize kwamba we are the voices of soo many people tusikae kimya lets talk am sure ipo siku tutasikika tu.
Binafsi sijapata muda mzuri wa kujadili rasimu ya katiba ila when given chance ningependa sana nishiriki mjadala wenu wa aina hii.
once again thanks.
Last edited by a moderator: