MGOGORO WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI
Sehemu ya kwanza
Tunaelewa jumuiya ilianza kama pendekezo la shirikisho la kisiasa la Afrika mashariki wazo la Nyerere lililosababisha hata kuchelewesha uhuru wa Tanganyika.Kwa bahati mbaya wazo lilipingwa na Kenya na katika wabunge waliolikataa mmoja wao ni Mwai Kibaki mbunge wa Mkadara wakati huo ambaye alikuja kuwa Rais.
EA community ikaundwa mwaka 1967 ikiwa na nchi tatu. Kenya kama colon ilikuwa mbele kiuchumi na viwanda. Shughuli nyingi za kiuchumi zilikuwa nchini Kenya, washirika wengine wakiwa na sehemu tu ya shughuli hizo. Kupinduliwa kwa Obote na mzozo wa Tanzania na Uganda mwaka 1973 bado hakukutetesha jumuiya.
Aliyekuwa waziri wa sheria na mwanasheria bwana Charles Njonjo, tajiri na mtu mwenye ushaiwshi mkubwa alimshauri Kenyatta kuua jumuiya kwa hoja ya Kenya kuwa mbali kiuchumi na wengine kuwa tegemezi. Mwaka 1977 Kenya ikazuia kila kitu na kupeleka jumuiya kufa
Wakati huo uchumi wa Uganda chini ya Amin ulikuwa katika hali mbaya sana.Tanzania hali haikuwa mbaya kiasi hicho na niwakumbushe wana duru kuwa katika miaka hiyo noti ya sh 20 iliyojulikana kama pound sawa na pound 1 ya UK.Chimbuko la jina la dala dala ni kutokana na magari kufanya trip za mjini kwa kuiba iba wapiga debe wakisema safari ni dollar dollar ndipo neno dala dala likatokea. sh 5 ilikuwa sawa na dollar moja ya Marekani.
Baada ya kuvunjika kwa jumuiya Tanzania ilianza upya kwa kila kitu. Ununuzi wa mabehewa na Injini za treni, mawasiliano ya satellite posta na simu na ilibidi tuazime ndege kutoka msumbiji.Uchumi ulianza kuvurugiga kwasababu ya mikopo na ujenzi mpya wa miundo mbinu.Nchi marafiki zetu kama China, Hungary zilitusaidia kuanza upya ujenzi wa uchumi
Kwa bahati mbaya mwaka mmoja tu uliofuata tukajikuta katika vita na Uganda jambo lililodidimiza kabisa uchumi wa nchi. Baada ya vita miundo mbinu ilikuwa katika hali mbaya na uzalishaji wa kilimo ulipata mtikisiko kwa kuzingatia kuanguka kwa bei katika masoko ya dunia kwa Pamba, Korosho na Katani.
Kuvunjika kwa jumuiya kulilazimu kufunga mipaka na Kenya.Kenya ikatumia fursa ya (black market) ikichukua 'advantage' ya uchumi mbaya wa Tanzania.
Hata hivyo kifo cha EAC kilikuwa na matokeo mazuri kwa upande mwingine. Tuliweza kuwa na viwanda vya bidhaa zetu wenyewe kama za nguo, mafuta ya kula, katani, vifaa na bidhaa (betri, viberiti, zana za kilimo,sabuni) , Mang'ula, Tancut Almas, Mufindi saw mill, Saruji, viwabda vya nguo n.k. Ilituchukua muda mfupi kuanza kujijenga bila kutegemea uagizaji wa bidhaa kutoka nchi za jirani ingawa hatukuweza kujitosheleza jambo lililozua ulanguzi wa bidhaa.
Rais Mwinyi alianzisha sera ya soko huria ikiwa na kufungua mpaka. Kenya ilipata soko kubwa la bidhaa zake Tanzania na kujifunza kuwa haiwezi kuwa na uchumi hutegemeana.
Makubaliano ya Rais Moi, Mwinyi na Museveni yalilenga kuijenga EAC kwa masilahi ya wananchi na si ya kisiasa, ushirika wa kisiasa ufuate baadaye. Ikaamuliwa kuwe na hatua za kufuata kuepuka matatizo ya awali
Viongozi walikubaliana kuwa kwanza taasisi za kiuchumi ziiimarishwe kama soko la pamoja la bidhaa, kuweka uwiano wa viwango vya ushuru, kuwepo kwa taasisi za elimu na afya katika miundo inayofanana na kuwa na benki kuu zinazowasiliana.
Nchi zilikubaliana kuwa makao makuu yawe Arusha yalipokuwa makao makuu ya jumiya ya kwanza.
Rais Museveni akaja na wazo la kuwa na jumiya kubwa kwa kushirikisha Rwanda na Burundi.
Wazo hilo lilileta mgongano kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe kwa hofu ya instability ndani ya jumuiya.
Ikumbukwe kuwa wakati marais wakiwa Moi, Mkapa, Museveni na hata waliokuwa Kibaki, Kikwete, Museveni hali ya jumuiya ilikuwa tulivu sana na mipango ilikuwa inakwenda vema bila mitafaruku.
Tanzania ikaamua kuwa na maoni ya wananchi kupitia naibu wa waziri wa EAC Deod Kamala wakati huo. Wananchi wakaonyesha wasi wasi hasa kwa Rwanda baada ya kuhisi matatizo kuletwa na mataifa hayo mawili.
Ikaamuliwa Rwanda na Burundi ziwe washiriki wa mazungumzo. Wakati huo huo jitihada za kusuluhisha Burundi zikiwa zinaendelea Tanzania ikichukua usukani na Rwanda ikiwa inajikusanya kutoka mauaji ya Kimbari.
Ni rais JK aliyekubali nchi hizo zipewe uanachama akisema hilo ni jambo zuri hata pale wananchi.
Museveni akaitumia karata ya kuingia Rwanda na Burundi ili kupunguza ushawishi katika kupiga kura.
Ghafla Museveni akataka liundwe shirikisho la EA na yeye awe Rais wa Kwanza kwa kuzingatia ukongwe.
Wazo lilileta sintofahamu na kumalizwa kidiplomasia.Ni Tanzania iliyoonyesha shaka mataifa mengine yakiwa kimya.
Inaendelea shemu ya Pili...................................