Nguruvi3,
Karibu sana katika mjadala;Kimsingi, naunga mkono hoja zako zote katika bandiko namba 34, lakini nikienda mbali zaidi, inaamsha mawazo mengine ambayo nadhani ni muhimu kwa huu mjadala kama nitakavyo fafanua;
Kwanza - hoja zako zinatulazimisha pengine tuangalie kwa undani the socio-economic profile ya eneo husika (Mtwara) kisha tuoanishe na thamani ya gesi asilia from the business and economic point of view, hasa nini kinaweza kupatikana kama benefits kwa wananchi wa eneo husika - both directly and indirectly;
Kama nilivyokwisha jadili, future value ya gesi asilia ni kwenye suala la nishati ambalo demand yake itazidi kukua siku hadi siku, huku projections zikiweka wazi kwamba mahitaji ya umeme wa gesi will outstrip umeme wa makaa ya mawe, nuclear na hydro duniani in the next 30 years;kuna sababu nyingi kwanini ni hivi, na partially Waziri Muhongo alielezea jana katika kuhitimisha hoja yake kwamba ukiondoa umeme wa hydro, umeme wa gesi ni bei nafuu per unit, huku akijadili kwamba pamoja na umeme wa maji kuwa nafuu, gharama zake za uwekezaji na uendeshaji, ni kubwa kuliko gesi; hivyo ndivyo nilivyomuelewa; Kwa maana hii, nishati ya gesi ndio where the future of this resource holds, hivyo uwekezaji wetu pamoja na faida kwa maeneo husika ujikite zaidi huko.
Lakini haina maana kwamba uwekezaji kwenye LNG plants hauna maana, kwani maana ipo, lakini cha msingi hapa ni kwamba matumizi haya yatazidi kupotea with stages of economic development yani matumizi ya gesi kwa ajili ya residential, commercial, industrial, na world energy outlook wanaweka wazi jinsi gani demand ya gesi kwa ajili ya matumizi haya inafikia saturation point marekani na sehemu mbalimbali za EU; Point yangu ya msingi hapa ni kwamba tuendelee to take advantage ya demand ya gesi kwa ajili ya residential, commercial and industrial wakati bado tupo kwenye take off stage of economic development ili tuvuke low levels of development ya sasa; Lakini kwa manufaa ya vizazi vijavyo, mbali ya kuwekeza ipasavyo na kupata short term and medium term gains ambazo zitatunyayua pia, tusijisahau kujipanga kisera tukapitwa na suala la gesi as the major source of energy for the future relative to thermal, hydro and nuclear;
Pengine hoja yangu hapo juu itaeleweka zaidi nikifafanua kama ifuatavyo:
Energy/Nishati ni basic input ambayo inahitajika kukidhi mahitaji mbalimbali ya binadamu kama vile heating, motive power (e.g water pumps, transportation etc) and lighting; businesses, industry na public services za kisasa kama vile afya, elimu, mawasiliano vyote hivi vinategemea sana access to energy services;as a matter of fact, ukosefu wa huduma za nishati upo directly linked na matatizo ya umaskini kama vile high mortality rates, low life expectancy, illiteracy and many other poverty indicators; katika nchi nyingi maskini, ukosefu wa huduma ya nishati pia huchangia sana tatizo la rural - urban migration; Kwetu Tanzania, Nishati ya gesi ni fursa muhimu sana ya kutusaidia kutatua matatizo yote haya, sio tu kwa mtwara bali nchi nzima; Ni katika muktadha huu, Waziri Muhongo alijeng hoja wakati wa hitimisho la bajeti ya wizara yake kwa kusema kwamba gesi ni mwokovu wa maskini wa Tanzania na serikali yake imejipanga kuitumia rasilimali hii kuiandaa Tanzania sio tu ipande na kuwa nchi ya uchumi wa kati ifikapo 2025 lakini pia itatuandaa kuingia karne ya ishirini na mbili kama taifa imara na bora kabisa socially, economically n.k; Naungana na hoja hii ya Muhongo lakini only if we manage to invest vizuri on where the future holds when it comes to suala zima la matumizi ya gesi baina na energy na Matumizi mengine;
Nikiwa bado katika hoja hii kuhusiana na faida za gesi asilia kwa uchumi, nadhani ni muhimu tukafanya profiling ya mkoa wa mtwara ili tupate fursa ya kuelewa jinsi gani viongozi wetu wanaweza kukaa nao na kukubaliana katika mambo ya msingi kuliokoa taifa letu; kwa maana nyingine, wengi tunasahau kufanya a profile analysis na ndio maana we fall short of understanding jinsi gani tulimalize tatizo la mtwara na kurudisha taifa letu katika hali yake ya amani, umoja, upendo, mshikamano na utulivu tuliyoizoea;Nitagusia machache kwa haraka haraka ili hata huko mbeleni, yakitokea matatizo kama haya mikoa mingine basi tutazame masuala kama haya:
1. At the turn of the new millennium (the year 2000) mtwara ilikuwa ni the second smallest region in Tanzania after Kilimanjaro; Sasa kwa wale wenye hoja kwamba gawio la bajeti lazima liendane na ukubwa wa eneo husika, suala la kilimanjaro kuwa top ten consistently na mtwara kuwa bottom five in terms of mgawanyo wa keki ya taifa, katika hili hoja zao zinakosa mashiko;
2. Mgawanyiko wa eneo per square kilometa, masasi ina cover 53% ya mkoa mzima huku newala, mtwara vijijini na tandahimba iki share the remaining area; implicationa zake hapa ni nyingi na tutazijadili baadae;
3. About 85% ya ardhi mkoani mtwara ni arable land, huku chini ya 25% of the 85% ikiwa katika matumizi ya kilimo; zao kuu la kilimo cha biashara ni korosho lakini pia wanalima karanga, sorghum,mihogo, paddy, mahindi, millet na simsim; Tukumbuke pia kwamba mtwara wana historia kubwa sana ya baa ya njaa na ni moja ya mikoa ambayo bado haijitoshelezi kwa chakula pamoja na ukweli kwamba sehemu kubwa ya uchumi wake ni subsistence based;
4. Mtwara unapakana na mikoa minne ya Tanzania - Morogoro, DSM, Ruvuma na Lindi; ni muhimu kuangalia economic linkages kati ya mtwara na mikoa hii kwa undani ili kubaini kwamba wapi kuna inputs muhimu kwa wanamtwara in the context of natural resource base yao, hivyo kuwekeza huko accordingly badala ya kuamua tu kwamba DSM is the only choice;
5.Mtwara ni moja ya mikoa iliyoathirika sana na net migration - net lifetime migration ni moja ya the highest in the country; Hii ni kwasababu mkoa huu umekuwa very unattractive kwa vijana lakini pia vizazi vipya, kwahiyo wanaenda kwingineko for greener pasture and by coincidence, vivutio vikubwa kwa wanamtwara ni ile mikoa niliyojadili kwamba throughout history imekuwa inapewa kipaumbele when it comes to keki ya taifa (bajeti); ni kwa mantiki hii, hata tume ya mipango katika taarifa yake ya mkoa wa mtwara inawaita vijana wa mtwara wanaohamia miji mingine kwamba ni "ECONOMIC REFUGEES"; kumbuka, hii ni serikali; Katika hili, tume ya mipango inajadili kwa uwazi kabisa kwamba ili kutatua tatizo husika, ni muhimu kwa serikali kuwekeza ili kuvutia nguvu kazi ya mtwara ibakie mtwara; Tume ya mipango inaenda mbali zaidi na kutaja maeneo muhimu ya kufanya ili kuinua mkoa huu kwamba ni pamoja na development of infrastructure, viwanda based on "local available resources", n.k, huku ikijadili kwamba - "this will make mtwara attractive to youths so that they don't need to go beyond its borders to seek a secure economic future";
6. Mtwara wakati wa mwalimu nyerere ulikuwa na viwanda - agro based industries, vitano vya kubangua korosho, viwili vya mkonge ambavyo vilikuwa vinatoa ajira na kuleta economic benefits mbalimbali kwa mkoa; leo katika hili, hali ni mbaya;
Tume ya mipango katika ripoti zake miaka nenda miaka rudi imekuwa very optimistic na maendeleo ya mtwara and mentions potential areas kuwa ni pamoja na maendeleo ya tourism industry, kilimo, forestry, ufugaji nyuki, uvuvi na VIWANDA; Sasa kama haya yamekuwa yakiwekwa bayana na tume ya mipango (serikali), basi ujio wa gesi ni fursa muhimu ya kutekeleza kwa vitendo;
Nguruvi3, maeneo mengine uliyojadili ni suala la quality na ajira kwa mtwara; naunga mkono hoja, na kwa kuongezea, ni muhimu kwa taifa sasa kuanza kuwa serious na national innovation systems ambayo itajenga skills, capabilities and entreprenuership drive kwa wanamtwara na watanzania kwa ujumla katika maeneo ya gesi na mafuta; na kwa mtwara, seriousness ni muhimu ianze kwa serikali kujenga chuo kitakachotoa mafunzo ya gesi na ambacho wawekezaji watalazimika kukichangia na pia kukishirikisha katika shughuli zao; kwa kifupi - faida ya gesi kwa wanamtwara itakuwa na manufaa tu iwapo itajitokeza katika economic output ya mkoa na employment na haya yalenge katika value chain ya sekta ya gesi - exploration, extraction, production, transportation, storage, distribution, servicing, maintenance, legal services, well services, construction, power generation, engineering services etc;inawezekana kwa leo hakuna such skills lakini tukiwekeza sasa, mtwara can become the centre of excellence afrika mashariki na kati katika utaalam wa gesi within the next 25 years;"