Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #161
LWAKATARE
MASHARIKI YA KATI SYRIA
Kama tulivyowahi kueleza hapo nyuma, suala la mkanda wa video linalomhusu Lwakatare baso limechukua nafasi kubwa nchini. Tulisema kuwa suala lile limeshupaliwa na Polisi kwasababu kubwa moja ambayo ni kuzima kabisa mjadala unaomhusu Kibanda.
Hakika wamefanikiwa sana kwasababu hakuna anayeongelea tena kuhusu Kibanda.
Tulisema Lwakatare amekamatwa bila maandalizi na ndivyo ilivyotokea. Amechiwa na kukamatwa tena ili kuzima hoja ya yeye kuwekwa rumande bila mashtaka. Hatutaweza kuliongelea kwa undani tukijua lipo mahakamani.
Hata hivyo kisiasa suala hili linachukua sura isiyotarajiwa.
Inaonekana kana kwamba limehusishwa sana na Chadema na hiyo ndiyo kete inayotaka kutumiwa kuwamaliza.
Kuna tatizo moja linaloikabili CDM kwasasa.
Kwanza haijulikani mkanda huo ni wa kweli au la kwa kuzingatia kuwa Ludovic na Lwakatare wameonyesha kwa kiasi fulani kufahamu baadhi ya maudhui. Kisichojulikana ni je, hii ilikuwa ni set up''mtego'' au ni hujuma ?
Swali la kujiuliza ni kuwa endapo mkanda huo utathibitika kuwa ni wa kweli, je CDM inawezaje kujiondoa katika kashfa hiyo? Tunadhani viongozi wa CDM lazima wawe makini sana, na kwavile wana wanasheria wanaoweza kufanya analysis ni muhimu sana kuwatumia ili kupata ukweli wa suala zima.
Ni kwa njia hiyo CDM wataweza kuwa salama kama hawapo salama au wanaweza kuitumia hiyo kete vizuri sana kama wapo salama.
Jambo lililowazi ni kuwa suala la Kibanda linaonekana kuzibwa na kitu kisichohusiana nalo kabisa.
Hili linaacha maswali mengi kuhusu mateso ya Kibanda.
Polisi wanatakiwa waje na jibu na si vitambaa vya kuzuia uchunguzi halali na wakina kama suala la Lwakatare.
MASHARIKI YA KATI SYRIA
Hali imekuwa ni tete sana na kuna tuhuma kuwa Asad ametumia silaha za sumu (Chemical weapon) dhidi ya wananchi wake.
Bashir Al Asad ni mtoto wa Rais Hafidh Al Asad. kiti cha urais katika nchi hiyo kimekuwa kama cha kurithi.
Ikumbukwe kuwa chama kinachotawala kinajulikana kama Ba'ath kama kile cha Saddam Hussein.
Chama hicho kimekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 41 sasa. Ingawa serikali ya Asad inaonekana kupoteza uungwaji mkono na sehemu kubwa ya wananchi, kuna makundi yanayo muunga mkono.
Vyombo vya usalama zaidi ya 10 vinamuunga mkono ikiwa ni pamoja na kundi dogo la Alawai ambalo linaundwa na wakristo wengi.
Tofauti na watu wanavyodhani, nchi za kiarabu zina dini zote kwasababu ya historia ya dunia ilivyo.
Kule Iran jews wana viti maalum katika bunge la nchi hiuo, kama alivyokuwa Tareq Azizi makamu wa rais wa Saadam Hussein n.k. Kwahiyo siasa za mashariki ya kati si za ujumla wa Waislam bali kuna michanganyiko mingi ikiwemo Orthodox kama wale wa Misri.
Makundi mengine yanayomuunga mkono Alsaad ni pamoja na wafanyabiashara na daraja la juu.
Nchi za magharibi zimewaunga wapinzani wa Asaad mkono kwa kuwapa silaha wamuondoe madarakani.
Ziara ya Obama nchini Jordan ina maana zaidi kwa kuzingatia kuwa Jordan ni sehemu muhimu sana ya kupitishia silaha kwenda kwa wapinzani.
Katika vita ya Lebanon kati ya Hezboullaha na Israel silaha nyingi za Hezbollah zilitoka Syria.
Kwa wakati huu silaha za wapinzani wa Asaad nyigni zinatoka Lebanon isyokuwa ya Hezboullah.
Inatosha kusema Lebanon na Jordan ni mikondo muhimu ya kupitishia silaha ili kuwafikia wapinzani wa Alsaad.
Pamoja na hayo Al Asaad anapokea misaada kutoka kwa Brotherhood ambao sasa wana shina la kudumu nchini Misri.
Kwahiyo suala zima la Syria ni mchanganyiko wa makundi, na kana kwamba hiyo haitoshi kuna nyongeza ifuatayo.
Kundi la Alqaeda linampiga vita Al Asaad na kiongozi wake Dr Ayaman Al Zawahir ametangaza vita rasmi dhidi ya Syria.
Kwanini Alqaeda wampige vita Asaad inaonekana kama kituko '' Bizzare'' kwasababu wengi walitegemea kumuunga mkono dhidi ya nchi za magahribi.
Sababu kubwa ni kuwa utawala wa baba yake (Hafidh Al Asaad) uliua Brotherhood katika miaka ya 1980 wapatao 10,000 katika mji wa Hama. Waliotekeleza jukumu hilo ni Alawi ambao wengi wao ni kutoka dini ya wakristo.
Na tunafahamu kuwa AlZawahir alikuwa mfungwa kwa nyakati fulani na yeye ni zao la Brotherhood.
Inawezekana kuwa miongoni mwa waliouawa ni wenzake katika harakati.
Lakini pia Syria inalaumiwa kwa kuwasaliti Wapalestina kuhusu vita yao dhidi ya Israel.
Tunakumbuka kuwa katika miaka ya '81 Israel ilichukua kwa nguvu milima ya Golan (Golan height) na kuikalia tokea wakati huo.
Milima ya Golan inatoa sehemu kubwa sana ya maji yanayotumika Israel na milima hiyo ipo katika maeneo muhimu ''strategy position'' iwe Israel kushambulia au kushambuliwa.
Kuanzia wakati huo Syria imekuwa kama imeachia eneo hilo na hili linawaudhi sana waarab wakiwemo Alqaeda.
Kw mtazamo huo ugomvi wa Syria ni faraja kwa Israel na pengine inapunguza pressure ya suala la Wapalestina kwani macho ya dunia yanaelekea Syria zaidi.
Pengine nchi za magharibi zingeweza kuitumia sana Ufaransa kupitia koloni lake la Lebanon.
Tatizo ni kuwa Syria nayo inadai Lebanon ni sehemu yake kihistoria.
Hilo linakuwa ni mwiba mkubwa kwasababu kadri nchi hizo zinavyojizatiti kukabiliana na Asad yapo mengine yanazuka.
Hofu inayofuata ni ya kuingilia kati kwa kundi la Hezboullah chini ya Imam Hassan Nasrallah.
Israel inakumbuka machungu ya vita iliyopita na hivyo isingependa kuvutika katika mzozo huo.
Wakati huo huo, Iran imekuwa inaisadia Syria kwa silaha kukabiliana na wapinzani.
Tunafahamu mtafaruku uliopo kati ya nchi za Magharibi na Iran.
Ni majuzi tu kiongozi wa kiroho Imam Ayatollah Khamenei amesema iwapo Israel itashambulia Iran basi miji ya Haifa na Tel Avivu itateketea. Hilo limekuwa linaitia hofu Israel kwa sababu ni tishio la kweli na linaweza kutokea.
Juzi Obama alikuwa Israel na katika mambo aliyofanikiwa ni kuilazimisha Israel kuomba radhi kwa Turkey kutokana na shambulio la Flotilla lililolaaniwa na jumuiya ya kimataifa.
Israel chini ya Benjamin iliwahi kukataa kata kata kuomba radhi.
Kugeuga kwa msimamo huo ni kutaka Turkey irudi kuwa mshirika wa Israel kwa hofu kuwa kadri siku zinavyosonga mbele vita eneo la mashariki ya kati litakuwa maafa kwa Israel.
Mathalan, Iran inaweza kuitumia Turkey ambayo kijeshi inasimama kidole kwa kidole na Israel (toe to toe).
Wakati huo huo kuna Hezboullah na Brotherhood achilia mbali Tunisia na majirani wengine.
Kwa maneno mengine mizozo inayoendelea mashariki ya kati inaihusu sana Israel kiusalama.
Kwa kumalizia tunasema kuwa hali ya mashariki ya kati inaingiliana sana kisiasa, kiuchumi na kijamii kwahivyo mzozo wa eneo moja ni mzozo wa eneo lote na wala haitegemewi kuwa kundi fulani linaweza kuunga mkono upande mwingine, la hasha! tumeona ya Al qaeda n.k.
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana na zinaathiri sana usalama wa eneo lote na dunia kwa ujumla.
Tusemezane.
MASHARIKI YA KATI SYRIA
Kama tulivyowahi kueleza hapo nyuma, suala la mkanda wa video linalomhusu Lwakatare baso limechukua nafasi kubwa nchini. Tulisema kuwa suala lile limeshupaliwa na Polisi kwasababu kubwa moja ambayo ni kuzima kabisa mjadala unaomhusu Kibanda.
Hakika wamefanikiwa sana kwasababu hakuna anayeongelea tena kuhusu Kibanda.
Tulisema Lwakatare amekamatwa bila maandalizi na ndivyo ilivyotokea. Amechiwa na kukamatwa tena ili kuzima hoja ya yeye kuwekwa rumande bila mashtaka. Hatutaweza kuliongelea kwa undani tukijua lipo mahakamani.
Hata hivyo kisiasa suala hili linachukua sura isiyotarajiwa.
Inaonekana kana kwamba limehusishwa sana na Chadema na hiyo ndiyo kete inayotaka kutumiwa kuwamaliza.
Kuna tatizo moja linaloikabili CDM kwasasa.
Kwanza haijulikani mkanda huo ni wa kweli au la kwa kuzingatia kuwa Ludovic na Lwakatare wameonyesha kwa kiasi fulani kufahamu baadhi ya maudhui. Kisichojulikana ni je, hii ilikuwa ni set up''mtego'' au ni hujuma ?
Swali la kujiuliza ni kuwa endapo mkanda huo utathibitika kuwa ni wa kweli, je CDM inawezaje kujiondoa katika kashfa hiyo? Tunadhani viongozi wa CDM lazima wawe makini sana, na kwavile wana wanasheria wanaoweza kufanya analysis ni muhimu sana kuwatumia ili kupata ukweli wa suala zima.
Ni kwa njia hiyo CDM wataweza kuwa salama kama hawapo salama au wanaweza kuitumia hiyo kete vizuri sana kama wapo salama.
Jambo lililowazi ni kuwa suala la Kibanda linaonekana kuzibwa na kitu kisichohusiana nalo kabisa.
Hili linaacha maswali mengi kuhusu mateso ya Kibanda.
Polisi wanatakiwa waje na jibu na si vitambaa vya kuzuia uchunguzi halali na wakina kama suala la Lwakatare.
MASHARIKI YA KATI SYRIA
Hali imekuwa ni tete sana na kuna tuhuma kuwa Asad ametumia silaha za sumu (Chemical weapon) dhidi ya wananchi wake.
Bashir Al Asad ni mtoto wa Rais Hafidh Al Asad. kiti cha urais katika nchi hiyo kimekuwa kama cha kurithi.
Ikumbukwe kuwa chama kinachotawala kinajulikana kama Ba'ath kama kile cha Saddam Hussein.
Chama hicho kimekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka 41 sasa. Ingawa serikali ya Asad inaonekana kupoteza uungwaji mkono na sehemu kubwa ya wananchi, kuna makundi yanayo muunga mkono.
Vyombo vya usalama zaidi ya 10 vinamuunga mkono ikiwa ni pamoja na kundi dogo la Alawai ambalo linaundwa na wakristo wengi.
Tofauti na watu wanavyodhani, nchi za kiarabu zina dini zote kwasababu ya historia ya dunia ilivyo.
Kule Iran jews wana viti maalum katika bunge la nchi hiuo, kama alivyokuwa Tareq Azizi makamu wa rais wa Saadam Hussein n.k. Kwahiyo siasa za mashariki ya kati si za ujumla wa Waislam bali kuna michanganyiko mingi ikiwemo Orthodox kama wale wa Misri.
Makundi mengine yanayomuunga mkono Alsaad ni pamoja na wafanyabiashara na daraja la juu.
Nchi za magharibi zimewaunga wapinzani wa Asaad mkono kwa kuwapa silaha wamuondoe madarakani.
Ziara ya Obama nchini Jordan ina maana zaidi kwa kuzingatia kuwa Jordan ni sehemu muhimu sana ya kupitishia silaha kwenda kwa wapinzani.
Katika vita ya Lebanon kati ya Hezboullaha na Israel silaha nyingi za Hezbollah zilitoka Syria.
Kwa wakati huu silaha za wapinzani wa Asaad nyigni zinatoka Lebanon isyokuwa ya Hezboullah.
Inatosha kusema Lebanon na Jordan ni mikondo muhimu ya kupitishia silaha ili kuwafikia wapinzani wa Alsaad.
Pamoja na hayo Al Asaad anapokea misaada kutoka kwa Brotherhood ambao sasa wana shina la kudumu nchini Misri.
Kwahiyo suala zima la Syria ni mchanganyiko wa makundi, na kana kwamba hiyo haitoshi kuna nyongeza ifuatayo.
Kundi la Alqaeda linampiga vita Al Asaad na kiongozi wake Dr Ayaman Al Zawahir ametangaza vita rasmi dhidi ya Syria.
Kwanini Alqaeda wampige vita Asaad inaonekana kama kituko '' Bizzare'' kwasababu wengi walitegemea kumuunga mkono dhidi ya nchi za magahribi.
Sababu kubwa ni kuwa utawala wa baba yake (Hafidh Al Asaad) uliua Brotherhood katika miaka ya 1980 wapatao 10,000 katika mji wa Hama. Waliotekeleza jukumu hilo ni Alawi ambao wengi wao ni kutoka dini ya wakristo.
Na tunafahamu kuwa AlZawahir alikuwa mfungwa kwa nyakati fulani na yeye ni zao la Brotherhood.
Inawezekana kuwa miongoni mwa waliouawa ni wenzake katika harakati.
Lakini pia Syria inalaumiwa kwa kuwasaliti Wapalestina kuhusu vita yao dhidi ya Israel.
Tunakumbuka kuwa katika miaka ya '81 Israel ilichukua kwa nguvu milima ya Golan (Golan height) na kuikalia tokea wakati huo.
Milima ya Golan inatoa sehemu kubwa sana ya maji yanayotumika Israel na milima hiyo ipo katika maeneo muhimu ''strategy position'' iwe Israel kushambulia au kushambuliwa.
Kuanzia wakati huo Syria imekuwa kama imeachia eneo hilo na hili linawaudhi sana waarab wakiwemo Alqaeda.
Kw mtazamo huo ugomvi wa Syria ni faraja kwa Israel na pengine inapunguza pressure ya suala la Wapalestina kwani macho ya dunia yanaelekea Syria zaidi.
Pengine nchi za magharibi zingeweza kuitumia sana Ufaransa kupitia koloni lake la Lebanon.
Tatizo ni kuwa Syria nayo inadai Lebanon ni sehemu yake kihistoria.
Hilo linakuwa ni mwiba mkubwa kwasababu kadri nchi hizo zinavyojizatiti kukabiliana na Asad yapo mengine yanazuka.
Hofu inayofuata ni ya kuingilia kati kwa kundi la Hezboullah chini ya Imam Hassan Nasrallah.
Israel inakumbuka machungu ya vita iliyopita na hivyo isingependa kuvutika katika mzozo huo.
Wakati huo huo, Iran imekuwa inaisadia Syria kwa silaha kukabiliana na wapinzani.
Tunafahamu mtafaruku uliopo kati ya nchi za Magharibi na Iran.
Ni majuzi tu kiongozi wa kiroho Imam Ayatollah Khamenei amesema iwapo Israel itashambulia Iran basi miji ya Haifa na Tel Avivu itateketea. Hilo limekuwa linaitia hofu Israel kwa sababu ni tishio la kweli na linaweza kutokea.
Juzi Obama alikuwa Israel na katika mambo aliyofanikiwa ni kuilazimisha Israel kuomba radhi kwa Turkey kutokana na shambulio la Flotilla lililolaaniwa na jumuiya ya kimataifa.
Israel chini ya Benjamin iliwahi kukataa kata kata kuomba radhi.
Kugeuga kwa msimamo huo ni kutaka Turkey irudi kuwa mshirika wa Israel kwa hofu kuwa kadri siku zinavyosonga mbele vita eneo la mashariki ya kati litakuwa maafa kwa Israel.
Mathalan, Iran inaweza kuitumia Turkey ambayo kijeshi inasimama kidole kwa kidole na Israel (toe to toe).
Wakati huo huo kuna Hezboullah na Brotherhood achilia mbali Tunisia na majirani wengine.
Kwa maneno mengine mizozo inayoendelea mashariki ya kati inaihusu sana Israel kiusalama.
Kwa kumalizia tunasema kuwa hali ya mashariki ya kati inaingiliana sana kisiasa, kiuchumi na kijamii kwahivyo mzozo wa eneo moja ni mzozo wa eneo lote na wala haitegemewi kuwa kundi fulani linaweza kuunga mkono upande mwingine, la hasha! tumeona ya Al qaeda n.k.
Siasa za mashariki ya kati ni ngumu sana na zinaathiri sana usalama wa eneo lote na dunia kwa ujumla.
Tusemezane.