Duru za siasa - Mgongano wa mawazo

Duru za siasa - Mgongano wa mawazo

Mkuu Mkandara hili jambo la kuhusu wawekezaji linanitatiza kidogo.Wamarekani wenyewe walitaka uhuru kwasababu sheria ilikuwa ikiwataka wapeleke mapato mengi in forms of taxes nk,back to the "mother land" yani kwa malkia uingereza.Walipokwa wakipinga,makampuni ya marekani yakawekewa vikwazo.Wakati ule biashara kubwa ikiwa ni chai.

Kampuni ya uingereza ambayo haikuwekewa vikwazo,ilikuwa na mzigo ya chai kwenye bandari ya Boston,wafanyakazi wakamwaga chai yote kwenye maji na ndipo ikaanza ile kauli ya "Taxed enough already" aka tea party...Haya ni baadhi ya matukio tu yaliyo highlight path waliyoichukuwa wamarekani ili kupambana na mwekezaji beberu wa uingereza ambaye aliwacolonise.Baadae wamarekani walipata uhuru baada ya kumwaga damu dhidi ya mwingereza.Na pia mmarekani aliyegombea uhuru ni mwingereza pia aliyehama kutoka uingereza akitafuta uhuru wa kujiamulia mambo na kuwa na mawazo ya tofauti.Lakini cha kushangaza kwasasa,ni kama the same thing is going on,especially dhidi ya Africa,bado tusitegemee eti kuwa wawekezaji wataleta maendeleo kama hawatabanwa.Na hakuna kampuni ya nje ambayo hailinufaishi taifa ilikotoka,ndo ubepari huo,yale mambo ya "mother land" yapo lakini kwa namna ya tofauti.Kwa wenzetu,kampuni hizo hata kama zinakwenda kuwekeza nje,bado zina majukumu kwa motherland kwasababu ndo wenye kuzilinda na kuzipatia ile "superiority" ndo ubepari huo.
Hapo sasa ni lini Simba akaacha asili yake?.. utamfuga na hata kumchezesha sarakasi lakini siku akirudi nyikani ule Usimba wake hurudi palepale..

Tunachotakiwa sisi ni kujihadhari kama tuwajuavyo Simba au nyoka, nasi kama Ngo'mbe nadhani tuna experience kubwa kuliko mataifa mengi lakini ajabu ni kwamba tumekuwa kama mbwa na chatu. na huwezi kuwalaumu Marekani kwa Ubeberu wao maana ndio uzawa wao ambao halikuwa na rasimali nyingi isipokuwa kipaji cha uwindaji kuwa na na kucha na meno K9 nasi kama ngo'mbe tuna kwato, maziwa, nyama na hata ngozi yetu ni chakula kwao, kwa nini tunashangaa Simba kuendelea kuwinda ng'ombe! - kazi kwetu.
 
Pamoja sana wakuu wangu:
Nadhani wote sasa tunakubaliana kwamba, Ujamaa na Ubepari sio mwisho, Tunaweza kujiundia mifumo yetu binafsi Kutuongoza, TUNAHITAJI KUKAA CHINI NA KUUMIZA VICHWA KISAWASAWA IKIWEZEKANA HADI VIPASUKE TUFE, kwani si kazi rahisi, tufanye UBUNIFU zao la Tafakari zetu!
Maswali muhimu wakati wa Tafakari:
1. Ni lazima tubainishe kwanza, "NI WAPI HASA TUNAPOTAKA KUFIKA"
2. Upi ni Msingi mkuu au Dira kuu ya kutuongoza kufika tunapotaka? Yaani kipi kiwe kioo chetu kujitazama ili kutotoka nje ya malengo?
Hayo ni muhimu sana kwangu. Nawasilisha!
Mungu wetu yu hai, tayari kutushindia vitani!
Anaita sasa!
 
Pamoja sana wakuu wangu:
Nadhani wote sasa tunakubaliana kwamba, Ujamaa na Ubepari sio mwisho, Tunaweza kujiundia mifumo yetu binafsi Kutuongoza, TUNAHITAJI KUKAA CHINI NA KUUMIZA VICHWA KISAWASAWA IKIWEZEKANA HADI VIPASUKE TUFE, kwani si kazi rahisi, tufanye UBUNIFU zao la Tafakari zetu!
Maswali muhimu wakati wa Tafakari:
1. Ni lazima tubainishe kwanza, "NI WAPI HASA TUNAPOTAKA KUFIKA"
2. Upi ni Msingi mkuu au Dira kuu ya kutuongoza kufika tunapotaka? Yaani kipi kiwe kioo chetu kujitazama ili kutotoka nje ya malengo?
Hayo ni muhimu sana kwangu. Nawasilisha!
Mungu wetu yu hai, tayari kutushindia vitani!
Anaita sasa!

-Vision
-Core Values
Hivi vitu vikisimama vema haitajalisha ni chama gani kimeshika madaraka ya nchi...vitu hivi vitabaki vimesimama imara!
 
-Vision
-Core Values
Hivi vitu vikisimama vema haitajalisha ni chama gani kimeshika madaraka ya nchi...vitu hivi vitabaki vimesimama imara!

Tupo pamoja mkuu wangu:
CORE VALUES:-
Kwangu mimi "Core Value" yetu si nyingine ila "UTU"- yaani KUFIKIRIANA, UWIANO SAHIHI-MANTIKI!
Lakini tusiseme tena Chama, kwani Ubunifu wetu haujafanyika bado, na hatujui kama utaruhusu uwepo wa vyama ama laa, mambo mengi yanaweza kubadilika au kuzaliwa mapya kabisa, hata hivyo yapo machache yaliyopo sasa yanayoweza kuchukuliwa yakidhihirika kukidhi vigezo, yaani yawe na MANTIKI, nayo ni UTU!
MTU MWEUSI ANA AKILI NYINGI SANA, NI ZAIDI YA TUJUAVYO. Tumetengenezwa kujidunisha, lakini kikitokea kikundi kidogo tu cha wanaojitambua, na wakathubutu, basi NURU ya fanaka itakuwa imeanza kutuwakia!
Mungu wetu anaita sasa!
 
Tupo pamoja mkuu wangu:
CORE VALUES:-
Kwangu mimi "Core Value" yetu si nyingine ila "UTU"- yaani KUFIKIRIANA, UWIANO SAHIHI-MANTIKI!
Lakini tusiseme tena Chama, kwani Ubunifu wetu haujafanyika bado, na hatujui kama utaruhusu uwepo wa vyama ama laa, mambo mengi yanaweza kubadilika au kuzaliwa mapya kabisa, hata hivyo yapo machache yaliyopo sasa yanayoweza kuchukuliwa yakidhihirika kukidhi vigezo, yaani yawe na MANTIKI, nayo ni UTU!
MTU MWEUSI ANA AKILI NYINGI SANA, NI ZAIDI YA TUJUAVYO. Tumetengenezwa kujidunisha, lakini kikitokea kikundi kidogo tu cha wanaojitambua, na wakathubutu, basi NURU ya fanaka itakuwa imeanza kutuwakia!
Mungu wetu anaita sasa!

Na huu ndio msingi hasa unaopaswa kuwekwa sawa tunapotengeneza katiba mpya... Tuzaliwe upya!!
 
Tupo pamoja mkuu wangu:
CORE VALUES:-
Kwangu mimi "Core Value" yetu si nyingine ila "UTU"- yaani KUFIKIRIANA, UWIANO SAHIHI-MANTIKI!
Lakini tusiseme tena Chama, kwani Ubunifu wetu haujafanyika bado, na hatujui kama utaruhusu uwepo wa vyama ama laa, mambo mengi yanaweza kubadilika au kuzaliwa mapya kabisa, hata hivyo yapo machache yaliyopo sasa yanayoweza kuchukuliwa yakidhihirika kukidhi vigezo, yaani yawe na MANTIKI, nayo ni UTU!
MTU MWEUSI ANA AKILI NYINGI SANA, NI ZAIDI YA TUJUAVYO. Tumetengenezwa kujidunisha, lakini kikitokea kikundi kidogo tu cha wanaojitambua, na wakathubutu, basi NURU ya fanaka itakuwa imeanza kutuwakia!
Mungu wetu anaita sasa!
Jingalafalsafa mkuu wangu hii tafsiri ya UTU kusema kweli naona imepooza sana na inaweza kupotrosha hasa unapotumia neno UUWIANO..Hili neno uuwiano lsilipendi kabisa na ndilo lilopelekea hizi fikra za Ujamaa wa Kikomunist.. Binafsi naamini Mungu katuumba sote na tofauti zetu, vijapi vyetu, uwezo tofauti na hulka tofauti. Kila mmoja wenu ni unique kwa umbo lake hivyo hawezi kuweka uuwiano kwa lolote zaidi ya kuwepo nafasi na fursa sawa kwa wote kushiriki badala ya kutazama uuwiano. Leo hii kuna wanawake wengi kuliko wanaume nasikia mara 5, sasa kwa kuleta uuwiano ndio tunasikia haya ya kuzuia wake zetu kutozaa watoto wa kike... Yameanza huko India na China ili kuleta uuwiano..

Haya ya Uuwiano ndio yanapelekea leo tuwe na viti maalum Bungeni, haya ya Uuwiano ndio yanapelekea sisi kuwa na viongozi kadhaa kutoka bara na kadhaa kutoka visiwani tukisahau kwamba ni wananchi wanatakiwa kuhudumiwa sio viongozi na vyeo maofisini. Fikra za kutazama watu na vyama kwa makabila na imani za dini za viongozi na wanachanma wake. Yote haya yanatokana na elimu dhaifu ya ukomunist ktk uuwiano tulojazwa vichwani toka enzi za mwalimu..

UTU kwangu utabakia kuwa ni ile hali ya kuthamini na kujali Uhuru (Freedom), HAKI (Justice) na Usawa (Equal opportunity) wa binadamu wengine (The quality of compassion or consideration for others) maana Humanity ni pamoja na Unyama wetu, hivyo nguzo hizi zinapambana na hasi ya ule Unyama wa binadamu - Siamini ktk uuwiano ambao unamkandamiza mmoja ili mwingine apande..
 
Mkuu wangu Mkandara,

1. Kwanza nimesema UTU ni MANTIKI KUU, yaani UUWIANO SAHIHI (si uuwiano tu), yaani KUFIKIRIANA, ndicho pia ulichogusia "The quality of Compassion or Consideration for Others (one another)" niseme kuwa, hakuna KUFIKIIRIANA kama hakuna UUWIANO SAHIHI. Tafsiri ya UWIANO SAHIHI ni "KUTOKINZANA"

Ninaamini Gender balance si Uwiano Sahihi, huwezi kumlinganisha mwanamke na mwanaume kwa chochote! Ila kuna neno HAKI-UHURU-UHALALI, hayo ndiyo yapindishayo dhana ya "UTU-MANTIKI-UUWIANO SAHIHI-KUTOKINZANA-KUFIKIRIANA" hata kwenye kuandika huwa tunaambiwa kupanga hoja zetu kiwantiki, yaani ziwe na mtiririko sahii, zisikinzane!

2. Ni sahihi kabisa kuwa tumeumbwa tofautitofauti sana, na tofauti hizi ndizo ziletazo machafuko baina yetu, sasa ili tofauti hizi zetu zisituingize matatizoni, ni lazima kuwepo kwa UWIANO SAHIHI-KUTOKINZANA (mizani sawa na si Haki)! Yaani hakuna tofauti kati ya MANTIKI, UUWIANO SAHIHI, KUFIKIRIANA, KUTOKINZANA, UTU. Usiseme tu UUWIANO bali UUWIANO SAHIHI.

3. Hakika kabisa UTU si kuthamini HAKI, UHURU na USAWA! Kwani mambo hayo matatu yanakinzana kwa kiasi kikubwa, kwenye HAKI kuna UHURU lakini si USAWA, sawa na kwenye UHURU Haki inapatikana lakini si USAWA, lakini katika Usawa kuna Haki na Uhuru, lakini si haki na uhuru huu mnaoutaka na kuuishi kwa sasa. Pigania Usawa, kwani ndani yake kuna Haki laki usipiganie Haki kwani ndani yake kuna Ubinafsi. Haki ijengwayo na Usawa, ni zao la UTU.

Mungu wetu anaita sasa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JingalaFalsafa,

Kwanza niwanukuu wachangiaji kwa michango ya karibuni ili nieleweke.

Mkandara anasema hata sisi tulikuwa na mifumo ya ubepari na ujamaa. Kilichotuzidi ni wenzetu kuirasimisha na hasa kuiandika pengine kwa mantiki tunayoona mifumo yetu haikuwa kama iliyoandikwa na intellectuals wa magharibi.

Kasema tuwe na kitu chetu kitakachotuwezesha kupambana na maadui wa nje na ndani. Hawa wa ndani ni umasikini,maradhi na ujinga. Ili tupambane nao lazima tuwe na miiko na maadili. Hapa anaungana na hoja yangu kuwa tuwe na kitu chetu kilichojengwa kwa misingi ya sheria, kanuni na taartibu. Unapokuwa na sheria, kanuni na taratibu basi hapo utaupata UTU unaoongelea.

jmushi1 anasema kwanini tusiwe na mfumo 'mixed' unachagua mazuri na kuacha mabaya kwasababu hakuna mfumo tunaoweza kusema unasimama wenyewe au ni timilifu. Naye pia anaoongelea ili kuwa na kitu chetu ni tutengeneza kinacholingana na mazingira yetu kama alivyosema Mkandara. Sina shaka hata yeye anaunga mkono Sheria, taratibu na maadili.

Mwalimu hapo juu anasema tumeaminishwa kuwa ni lazima tuwe bawa la kulia au kushoto, tufuate weupe, njano n.k. Tumefungwa na hatuna chaguo.

Nakubaliana naye kuwa hayo ndiyo mawazo yaliyopo na nadhani hata viongozi wetu wanafikiri hivyo. Ninapotofautiana naye ni pale nikizikumbuka nchi za Scanadinavia na Asian Tiger. Najiuliza zenyewe zimewezaje kujitikomboa kutoka makucha makali hata kama bado zinafungwa na vikamba vidogo miguuni? Kwanini sisi tuwe completely paralyzed kiasi hatuwezi kuamka tulipo?

JingalaFalsafa anasema vyovyote iwavyo ni lazima kuwa na UTU wa KUFIKIRIANA. Kwa muda nimekuwa nangojea kusikia ni jinsi gani utu na kufikiriana tunaweza kuviingiza katika akili za kibinadamu.

Nijuavyo mimi binadamu kama walivyo wanyama wengine ana matamanio na hulka kama zao. Tofauti ni kujitambua na kutambua, kupanga na kuchagua.

Naomba ufunguke kuwa tunawezaje ku-instill utu na kufikiriana ikiwa hatuwezi kutafakari kuwa ni dhambi kutumia kodi ya mtu kununua VX na kumwacha akifa kwa kukosa Aspirini!

Hoja yangu ni wewe ufunguke na utuambie, sisi kama nchi tufanye nini ili kutanguliza utu na kufikiriana kabla hatujafikiria mifumo ya kutuongoza?

Endapo masheikh, maaskofu na Maolegwanan wanahubiri kila uchao dhidi ya ukatili na bado tunasikia ukatili mpya kila siku , ni kitu gani au tufanye nini ili basi tuhakikishe kuwa kwanza tuna utu na kufikiriana katika vichwa vyetu?
 
Mkuu wangu Nguruvi3, swali lako ni zito mno, nakiri mimi sitoshelezi kusema tufanye lipi na lipi, lakini nitatoa maoni yangu ambayo nanyi mnapaswa kuyameng'enya, na kutoa kwa hoja kama tuendeleavyo. NASHUKURU!

1. Natofautiana nawe hapa unaposema Kanuni, Taratibu, Maadili na Sheria hujenga UTU, si kweli.

UTU ni mantiki iliyomo nafsini mwa kila mtu, "inborn (innate) quality", hakukuwa na mtu auae pasi kujihisi Hatia (you must feel guilty) hufundishwi hilo, wala kupandikizwa (tusichanganye na wale wanaopandikiziwa ukatili). Hakuna mtu atendaye ovu pasi kujihisi hatia! Labda awe kichaa! Atumiaye kodi yangu kununua vx, si kwamba hajui ni kosa, ila mazingira yameruhusu yeye kutekeleza tamaa na hulka zake! Sheria, maadili, kanuni na taratibu unazosema zipo, lakini bado hayo yapo. Hapa ndipo tunapohitaji mipaka isiyokinzana! UTU haujengwi, ila unapaswa kuwekwa kwenye vitendo vyetu, hivyo UTU ndio ujengao SHERIA, KANUNI, MAADILI na TARATIBU. Kitu ambacho hakipo kwa sasa, sheria, kanuni, na taratibu zetu zimejengwa na UBINAFSI, zao la kumuacha binadamu huru kufuata matamanio na hulka zake!

2. Kuwepo kwa mfumo-mixed, sikatai. Ila tu uzaliwe kutokana na tafakari zetu huru! Si kukaa chini na kuanza kuchambua mazuri ya ujamaa na ubepari na kuyaweka pamoja - HAPANA! Tukae chini, tutafakari tutakacho kuishi, ubunifu wetu waweza kuangukia kwenye mfumo ambao una elements za ubepari na ujamaa, au ujamaa tu, au ubepari tu, au mambo mapya kabisa, hiyo si hoja, bali tunachotaka ni UBUNIFU WETU UWE UMETOKANA NA TAFAKARI HURU zisizofungwa na upande wowote si ubepari wala ujamaa, si uislamu au ukristo, si upagani au uyahudi, si demokrasia wa haki, si Biblia wala Kuruan, bali ni MANTIKI tu, nayo ni UTU.

3. Hapa ni mwiko kusema mbona wenzetu wamefanya hivi, vile na vile. Ni kujifunga! Kwanini tujifananishe na watu ambao hatufanani nao kimazingira wala kinyakati? Ukiona wazungu wameungana ujue ni kuunganisha nguvu kumnyonya mtu mweusi! Nilishazungumzia dhana ya Internal na External Capitalism.

4. Suala si kusimika dhana ya KUFIKIRIANA kwani imo ndani yetu tayari. Kazi ni kuifanya hai dhana hii kwenye matendo yetu ya kila siku. Mantiki ya UTU i nafsini mwake mtu, kutoiishi ni sawa na kujinafiki na kujisaliti mwenyewe. Sasa kwakuwa wote tunakubali kwamba binadamu ameumbwa na Hulka na Matamanio, japo utu upo ndani yake, tamaa zake hukiukisha mantiki katika matendo yake, kwani hulka na tamaa kuu ya mwanadamu ni KUJIKWEZA-Ubinafsi. Hapo ndipo tunapohitaji UTU kuzaa sheria, kanuni, taratibu, maadili, mienendo, falsafa, itikadi, mila, desturi, mitazamo, imani, n.k hapo ndipo dhana ya KUFIKIRIANA inapoweza kutekelezwa katika Vitendo. Kwa sasa haipo, kwani HAKI zilizopo humpa mtu uhalali wa kuwa huru kufuata hulka na tamaa zake! Na matokeo yake ni unyama tunaouona sasa. Gari 10 uwani, jirani yake anakufa njaa na watoto wake chini ya maboksi juu ya mkeka chakavu, nasi tunasema HAKI - UHURU, TUMEROGWA.

5. Haya hatuwezi kuyasimika kwenye katiba yetu kwa sasa japo yalipaswa kuwemo, kwani mfumo hauruhusu-hatutaeleweka. Lakini tukitaka, mimi na wewe tukathubutu, basi wajukuu wetu watayashuhudia haya!

Mungu wetu anaita sasa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu JingalaFalsafa,kuhusiana na utu,ni kwamba huwezi kuutenganisha na maadili na sheria.Hivi vinategemeana kabisa.Vitendo ambavyo viko classified as "utu",vingi vinasimamiwa na sheria za nchihusika na hata za kimataifa ama hata moral obligations,rules and regulations za any given society and so forth.Hizo zote ni kuhakikisha kwamba matendo hayo ambayo yanareflect utu,yanasimamiwa na sheria na kuwa promoted.

Ni kweli you feel guilty unapofanya kosa ama kuvunja sheria,lakini kama punishment na accountability hakuna,basi inakuwa more disasterous.Kwa mfano ni ukweli kuna makosa ambayo yanastahili adhabu ya kifo kwa mujibu wa sheria za nchi,lakini bado watu wanauwa nk.Hayo yakufanye utambue kuwa kuna matatizo ya kisaikolojia vile vile kwa binadamu.

Nakubali pia kuwa utu ni mantiki,lakini mantiki husimamiwa na sheria,yes you feel guilty,lakini how does it help kama hakuna consequences zinazofuatia?Kama vitendo vya kutokuwa na huruma ambavyo ni kinyume na utu ie missusing of public funds etc haviwi punished,then kuwa na huruma hakuna mantiki.

Hata hao wenye kununua mashangingi na wakati hospitali hazina madawa wala vifaa,bado wanaweza kuwa punished kwasababu vitendo ambavyo vina personal rewards lakini ni vibaya kwa jamii mfano ufisadi,must receive maximum punishment,ni juu yetu sisi wananchi kuweka sheria zinazoendana na matendo ya kwenye jamii yetu.

Tunaweza tukawa na sheria na katiba nzuri tu kwenye makaratasi lakini si nzuri kwetu kama Taifa.Ndo maana kuna wanaowashangaa wachina.Ni kwamba waliona tatizo kuu kwao ambalo linawarudisha nyuma ni rushwa,na wakaipatia possible maximum sentence that is death.Yote hayo ni kuhakikisha matendo yenye utu yanasimamiwa na kuwa promoted by any means neccessary for the benefit of the community at large.

Kuhusiana na mixed economy,unayosema ni kweli kwa kiasi kikubwa kama alivyosema Mkandara.Isipokuwa ni ukweli mtupu kuwa chumi za dunia sasa ziko very intertwined,na ndiyo maana matatizo ya uchumi sehemu moja huwa yana affect sehemu karibia zote duniani kiuchumi.Kwa hiyo hatuwezi tu kuja na a "foreign" plan no matter what,lazima mfumo tutakaochaguwa utakuwa na elements za mifumo iliyopo duniani.
 
Mkuu jmushi1, nilichosema ni kuwa Sheria na Maadili (pamoja na itikadi, falsafa, imani, kanuni, taratibu, mitazamo, n.k.) vinapaswa kuzaliwa na UTU, yaani UTU ni mama, na Sheria na Maadili vinapaswa kuwa watoto wake UTU! Sasa labda nikuulize, ni sheria na maadili yepi kwa sasa yanayozingatia dhana hii ya UTU? Je, ni sheria na maadili ya kikristo au kiislamu au kipagani, je ni sheria na maadili ya demokrasia au mziitazo za kidikteta, je ni sheria na maadili ya kijamaa au kibepari? Sheria ni zao la akili ya binadamu, lakini UTU ni thamani azaliwayo nayo mtu! UTU upo hata sheria zisipokuwepo, lakini ili sheria iwe na mantiki, ni lazima itegemee UTU katika kuundwa kwake!
Ndio maana nasema, tusifungwe na chochote kilichopo kwa sasa, TUFANYE UBUNIFU, tuongozwe na UTU! Lengo la kutaka UTU uzingatiwe katika uundaji wa sheria na maadili, ni kutaka UTU uwe katika vitendo, si nafsini mwetu tu!
Pia kumbuka kwamba, HATUTOCHAGUA MFUMO, BALI TUTAFANYA UBUNIFU KUUPATA! Hata ukiwa na elements za mifumo iliyopo, muhimu iwe imekidhi haja yetu, UTU, kama msingi mkuu! Liwe zao la Fikra zetu HURU!
Mungu wetu anaita!
 
Mkuu JingalaFalsafa,kuhusiana na utu,ni kwamba huwezi kuutenganisha na maadili na sheria. Hivi vinategemeana kabisa. Vitendo ambavyo viko classified as "utu", vingi vinasimamiwa na sheria za nchihusika na hata za kimataifa ama hata moral obligations, rules and regulations za any given society and so forth.Hizo zote ni kuhakikisha kwamba matendo hayo ambayo yanareflect utu, yanasimamiwa na sheria na kuwa promoted
Thank you so much!

Bandiko la #300 JingalaFalsafa anakubaliana kuwa utu ni 'in born (innate) quality'' .

Anakubaliana kabisa kuwa sote tumezaliwa tukiwa na element za utu na huo ndio unatufanya ubinadamu wetu.

Nitoe mfano, wanasaikolojia wanasema 'Every human is a psychiatry case, the only differece is on degree from one person to another'' kwamba sote tumezaliwa tukiwa na element za maradhi ya akili, lakini tunatofautiana kwa viwango, na ndio maana wenye viwango fulani tunawaita wagonjwa. Hii haina maana wengine wapo salama, yoyote yule anaweza kuwa mgonjwa kiwango kikibadilika. Na wagonjwa tunawapa matibabu ambayo tumeyatengeneza wanadamu kukabiliana na maradhi.
jmushi1 ameeleza vema sana hapo nilipo mnukuu, kwamba uwepo wa sheria, taratibu na kanuni ni sehemu ya kulinda utu.

Kama utu unajitosheleza basi tusingukuwa na sheria, lakini fungamano la viu hivyo linafanya utu utegemee sheria, kanuni na taratibu ili uendelee kuwa thamani kama ilivyokusudiwa.

Bandiko# 302 JingalaFalsafa anasema ili sheria, kanuni na taratibu ziwe na maana lazima itegemee utu. Mimi nasema mantiki ya sheria ni kulinda UTU. Uuundwaji wa sheria, maadili kanuni na taratibu ni lazima uzingatie kulinda UTU.
Na hapo ndipo tunashadidia ukweli kuwa utu upo tu kila mara na kila wakati isipokuwa unahitaji sheria na kanuni za kuulinda (si kusimamia utu) ili usibomolewe na wale ambao UTU wao umeshavuka mipaka ya kawaida.
Mkandara ameeleza mahali kuwa tusidhani kuwa mifumo iliyopo haikuwepo kwetu, kinachotokea ni sisi kusoma ile iliyoandikwa na intellectuals na kudhani tuna kitu tofauti sana. Nakubaliana naye sana.
jmushi1 anasema maingiliano ya dunia ya sasa yanahitaji kitu kinachoingiliana na si dude tofuati kabisa. Tunaweza kuangalia mifumo yetu iliyekuwepo tukachukua hili na lile kwa uzooefu wa kwingine.

JingalaFalsafa, sasa wewe unadhani tunawezaje kuufanya utu kwanza ili sheria zifuate? Kwa maneno mengine ili tuwe na kitu kama wanachosema waungwana hapo juu, tunapaswa tuanzie wapi katika kujenga UTU. Kumbuka utu ni innate quality.

Sheria za fizikia zinasema 'to every action there is an equal and opposite reaction' miaka mingi kama nipo sahihi.
Ukiwa na UTU (Humanity/ moral etc) basi ujue kuna mbadala wa hayo, Inhumane /Immoral etc.

Swali ni je, unawezaje kujenga UTU bila kuwa na vitu vya kuulinda ili usiwe kinyume?
Swali la pili, Tunawezaje kuufanya UTU uwe ndani ya matendo na si nafsi.

Hapa ndipo tunaomba ufunguke
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3,

Si kila sheria inalenga kulinda UTU, kumbuka hata watumwa walitungiwa sheria na mabwana zao, hapo ndipo napotaka nieleweke kuwa, ili sheria iweze kulinda UTU inapaswa kuundwa kwa misingi ya UTU! Naomba nisitafsiriwe vibaya kwamba sioni umuhimu wa sheria na maadili katika kulinda UTU, nachosema si kila sheria zimeundwa kulinda UTU, zipo zilizoundwa kwa lengo la kukiuka MANTIKI, yaani UTU. Mfano wake, ni sheria zote under Capitalism, na chache under Socialism. Sheria chini ya Ubepari zinalenga ku-maintain "individualism" wakati UTU ni KUFIKIRIANA, tunaweza kujionea UKINZANI wa sheria hizo na UTU.

*Ni sahihi kabisa kusema UTU upo kila mahali, na unapaswa kulindwa si tu na sheria na maadili, bali kila kitu chetu; imani, falsafa, itikadi, desturi, mitazamo, nk. Lakini ili falsafa iweze kulinda UTU, ni lazima ijengwe kwenye misingi ya UTU, sawa vile kwa sheria, maadili, itikadi, n.k.

1. Ni lazima kwanza tutambue adui wa UTU, kabla hatujafikia kuamua tuanzie wapi kuulinda UTU. Kwa vile UTU ni innate quality basi kwanza huanza kuzongwa na kukiukishwa na innate quality yenzake, nayo ni Matamanio/Hulka za binadamu, hizi ndizo zimpelekeazo mwanadamu kutumia HISIA zake na si MANTIKI katika kufanya maamuzi! Hisia za binadamu zinazowaka na hulka zake, zilipelekea kuzaliwa kwa dhana za Uhuru na Haki, lengo ni kuhalalisha matamanio yake yakiukayo UTU. Akaweza, ndipo alipojiundia na mifumo-sheria, maadili, kanuni, taratibu n.k ili kulinda Hulka zake! Ndio maana sitaacha kusema "Adui yetu wa kwanza ni nafsi zetu wenye, humo ambamo MANTIKI na HISIA vinapatikana! Embu fikiria, na njaa zetu, utumwa wa fikra wetu, unyonge, physical & pyschological diseases zetu, ujinga wetu...eti tunaachana huru kujifanyia maamuzi, how can we make critical decisions?

2. TUFUNDISHANE KWELI KWANZA, tupindue nafsi zetu ili zifuate Mantiki na si Hisia zetu, tupiganie kusimika dhana hii katika akili za watu, kabla sheria hazijafanya hivyo, imani yetu inapaswa kujengwa kwa mantiki hiyo, falsafa, itikadi, mitazamo, desturi, n.k. Kama mbinu za kukiuka Mantiki ya UTU ilivyokuwa, nasi hiyo hiyo tunapaswa kuitumia kuirudisha, ni KUCHEZA NA AKILI ZA WATU KWA HESABU KUBWA ILIYOTULIA, simika hili katika ya dhana ya uwepo wa Mungu (imani juu ya Mungu-dini), sanaa zetu zishadidie UTU, nyanja ya Habari nayo ishadidie UTU, kubwa zaidi ni Elimu, kuanzia mfumo hadi maudhui yake-hapa ni muhimu sana! Mwishowe dhana hii itajengeka akilini mwetu, na itafanywa kuwa Utamaduni wetu - our total ways of life. Hapa sasa sheria za kulinda UTU zitaundwa, za kisiasa, kiuchumi na kisiasa! Hii ni kusema kwamba, imani, itikadi, falsafa, sheria, maadili, mitazamo, mienendo, desturi ye n.k. zitajengwa kwa misingi ya UTU, na hayo yote yatatufunga na kuuongoza katika Matendo ya UTU...kwani kila kitu chetu kitakuwa kinatufungamanisha na UTU.

Mungu wetu anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
JingalaFalsafa

Nitarudia tena kusema unapotumia neno UBEPARI kuwa unakiuka UTU kusema kweli sikubaliani nawe kabisa ktk hilo maana kiongozi yeyote anaweza kuwa Mjamaa au bepari na akakiuka UTU kwa sababu za Ubinafsi.. Ubianfsi mara zote ni kutojali interest za mwingine isipokuwa zako wewe, UTU kama ulivyosema ni KUFIKIRIANA na ndio aana tumekuwa na sheria z akimataifa zikifuatwa na nchi zote iwe za Kibepari au Kijamaa..

Sheria na kanuni siku zote zimetanguliwa na UTU na ndjio maana zimetungwa kuulinda. Lakini sheria hizo hizo zinapomzuia mtu ama watu kujiendeleza kwa matakwa yao pia ni ukiukaji wa UTU hivyo sheria yenyewe kutengua UTU kwa tafsiri yake. Tulipingana na UTUMWA sii kwa sababu ya malipo duni ya kazi walizofanya isipokuwa ni pamoja na kukosa haki ya umiliki wa mali zile kama walivyokuwa wayahudi Misri au Waafrika huko Marekani. Tulipingana na Utumwa kwa vitendo vya kuwalazimisha kufanya kazi ktk mazingira magumu na mateso wakiadhibiwa kwa kutoweza kuendelea na kazi.. Ule unyama wa manyapala kuwacharaza bakora ilikuwa kinyume cha utu japokuwa kulikuwepo na Ulazima wa kazi ifanyike.

Hivyo hivyo ukitazama ktk Ujamaa na nchi zilizofuata siasa za Ujamaa kulizuka Utumwa wa kulazimisha watu kufanya kazi, kuwaabudu viongozi wao kama wateule na wenye mamlaka juu yao badala ya Ujama wa waafrika ulokuwa sehemu ya maisha yetu nhata kabla ya kukoloniwa..

Ni Ujamaa upi wa Kiafrika ulojali UTU wetu, Huu nadhani unaelezwa vizuri na De Graft Johnson wa Ghana aliposema wazi kwamba " What we have here in our clans or tribes which are in fact extended families. In our society, The collective wealth of the extended family is used for the welfare of the family as a whole. The extended families take on the functions of social insurance, and if a member of the family falls into debt, all the others help him to pay it; if he is ill, they look after him; if there is a bright boy in the family whom the immediate parents cannot afford to educate, the others help in educating him. Property, especially land, often belongs to the whole extended family. There are abuses in the extended family system, but its basic pattern, when enlarged to embrace the state, is virtually what is meant by socialism.

Halafu inaelendela kwamba - Advocates of African socialism claimed that it was not the opposite of capitalism nor a response to it, but something completely different. Na hapa ndipo niliposimama mimi ya kwamba nchi zote za kiafrika kabla na baada ya kupata Uhuru ziliweka lengo moja la Pan Africanism ambalo kwangu ni Ujamaa wa Mwafrika - Pan-Africanism represents the aggregation of the historical, cultural, spiritual, artistic, scientific and philosophical legacies of Africans from past times to the present. Pan-Africanism as an ethical system traces its origins from ancient times, and promotes values that are the product of the African civilization and the struggles against slavery, racism, Colonialism, and neo - colonialism..

Somehow, somewhere nasema tulipoteza dira, tulipoteza itifaki, mila na desturi za WAZUNGU waliotutawala walituacha na aina fulani ni utumwa wa fikra..Pengine sisi Tanzania tulikuwa na bahati sana kuwa na kiongozi kama Nyerere ambaye yeye alikuwa na dira yake lakini haikuwa hivyo Ethiopia, cambodia, Vietman ama nchi nyingine zilizofuata siasa Ujamaa, lakini pia watu walilazimika kuhamishwa, kuimba nyimbo, kujiunga na kwa nguvu pasipo kuwepo hatari ama ulazima wa kuwahamisha. lakini pia sisi wenyewe tulipoteza dira, tukaacha Ujamaa wa mwafrika na kuiga ule wa Ulaya ulotufanya kulaani Ubepoari badala ya kulaani utumwa, ukoloni na ukoloni mamboleo..

Hivyo narudia tena Ujamaa wa mwafrika haukupewa nafasi kabisa na ndio maana leo nchi za kiafrika zinazidi kugawanyika. Tunazidi kuunda utengano zaidi ya UMOJA wetu hivyo haya yote yanaokana na Umaskini wala sii Ubepari. Nchi zote maskini iwe Afrika au Ulaya (former Yugoslavia na Czechoslavakia) adui wao mkubwa ni UMASKINI ambao umevunja kabisa mila na desturi za UTU hasa pale fedha ilipotawala maamuzi yetu.. Utajiri hauna Ubepari wala Ujamaa ni fursa ya mwanadamu kujiendeleza na tamaa ya Utajiri ni ya kila mtu, kila upande isipokuwa kinachotazamwa zaidi ni mgao wa keki ya taifa na sio kugawana umaskini (mbegu)...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mkandara,

Mbona unazungumzia vitu viwili tofauti, tangu post yangu ya kwanza katika thread hii hazijawahi kukinzana, kuna nilishajieleza juu ya hiki uzungumziacho.

Labda nitoe mfano:
Inasemekana Ukristo ni dini ya Upendo. Je, ikitokea mchungaji anachukia na kuwanyanyasa waumini wake, tafsiri yenu kwa ukristo itabadilika na kuwa chuki badala ya upendo? Pia inasemekana kuwa Uislamu ni dini ya Haki, Je, ikitokea shehe amepokea rushwa kutoka kwa muumini wake, itabadili tafsiri na kuwa ufisadi badala ya haki?

*Naposema ubepari ni kinyume na UTU, sizumngumzii Bush au Adolf, wala France wala UK, Kenya wala SA, si mzungu wala mweusi au mchina, hapa ninamaanisha FALSAFA KUU YA UBEPARI-ULE MSINGI MKUU WA UBEPARI NDIO UKIUKAO UTU, KWA MAANA HIYO HATA MAZAO YAKE YOTE YAMEOZA...falsafa hiyo ni "PRIVATE OWNERSHIP". Nikatolea maelezo namna gani huipa nguvu matamanio hasi ya mwanadamu ya kujikweza na umimi, matokeo yake wa juu atamkandamiza wa chini yake kulinda nafasi yake alipo.

Katika Ujamaa, sijasema ule wa China, Russia, Vietnam, Chile, Tanzania wala Cuba, sikumtaja Ho Chi Minh, Mao, Castro wala Nyerere, nilichosema ni juu ya Falsafa kuu ya Ujamaa, nayo ni "From Each According to His Ability. To Each According to His Needs" dhana hiyo ndiyo izaayo "Common Ownership". Sasa kama unapinga, naomba upinge hizo falsafa juu ya UTU kama nimeongea tofauti. Lakini usiseme mbona kiongozi fulani au nchi fulani walijinadi kuishi ujamaa lakini walikuwa hivi na hivi na vile, HAPANA. Ikitokea ustadhi mroho akala nguruwe, haimaanishi uislamu umeruhusu kula nguruwe, HAPANA! Tena, huyo hatokuwa muislamu tena amekiuka sheria za uislamu! Beba dhana hii nzima nzima kwenye ubepari na ujamaa!

Pia, ninategemea kukosolewa kuwa ubepari si kinyume na UTU kwa hoja binafsi za ubepari, si kusema mbona hata kwenye ujamaa kuna a, b, c,...!

*Mkuu wangu Mkandara, kipi kinachokushawishi usema Sheria za Kimataifa zimetungwa kulinda UTU? Ipi, je ni ya uwekezaji? Ubinafsishaji? Demokrasia? Haki za Binadamu? Kuwa mkweli tu katika hilo. Nikutolee mfano mmoja tu katika uwekezaji: Sheria hizi zinawajumuisha watanzania, wamalawi na wamsumbiji kushindania fursa za kuwekeza dhidi ya wachina, wamarekani, wajerumani na wafaransa. Je, hiyo ni Fair/unfair competition? Hatufanani nao kimtaji, kiteknolojia wala chochote kile! Unathubutu vipi kusema ushindani huo UNA MANTIKI-UTU? Usifungwe na kanuni wala sheria zozote, ila Logic. Mugabe alisema...usimuamini mzungu yeyote labda aliyekufa-maiti yake!

*Binafsi naamini sana katika hili...Maisha ni Hatua, kusiwe na 2 kama hakuna 1 na 1, kusiwe na 3 kama hakuna 2 na 2. Ukipiga hatu ya 1, ni jukumu lako kunisaidia nifikie ya 1, tukishafika ya 1 wote, ndio tuitafute ya 2. Iwe hivyo katika ngazi ya mtu na mtu, kikundi na kikundi, kanda na kanda, nchi na nchi-Afrika nzima! Huo ndio Ujamaa kwangu mimi, na huo Ndio UTU!

Adui yetu wa kwanza si Umasikini, ila ni Nafsi zetu wenyewe, kukiuka Mantiki na kufuata Hisia zetu!

Mungu wetu anaita sasa!
 
JingalaFalsafa

Mkuu wangu wala sikuelewi kusema kweli.. Ulipotoa mfano wa mchungaji anayekiuka Ukristu na kufanya yasiyokubaliwa na Ukirstu haiwezi kubadilisha maana ya Ukiristu ama Sheikh kufanya kinyume nilidhani nimekuepata vizuri ktk mfano huo..lakini ajabu ulipokuja kwenye Ubepari unabadilika sasa na kuzungumzia msingi wa Ubepari badala ya kina Bush (mchungaji au Shehe) na mabaya yao hayawezi kubadilisha maana ya Ubepari imekuwa ndio maana ya Ubepari na ndio maana wamefanya hivyo..Hii sii kweli hata kidogo maana kama ingekuwa kweli wazazi wetu wasingekuwa mabepari kabla ya kukoloniwa na walikuwa tofauti na hawa wageni.

Nitakwambia kwa nini, fursa ya PRIVATE OWNERSHIP inabakia palepale hata ktk ujamaa wa Mwafrika maana waliishi hivyo..Na ndio maana hata Pan africanism imesema mtu akiwa na DENI, kijiji kizima kitamsaidia kulipa maana hakuna kitu deni la kijiji kama walovyofanya kina Nyerere ktk kuzuia private ownership. Mtu mmoja mmoja anakuwa na maisha yake ndani ya jamii hasa baada ya kuoa ama kuolewa. walikuwepo matajiri namskini lakini mavuno ya Utajiri wao yaliwafikia wengine pia. Hi ni nature ya mwanadamu mkuu wangu huwezi kuibadilisha hata wanyama na viumbe wengine wote wana asili ya maisha maadam kila mmoja wetu kazaliwa pekee na atakufa pekee, hivyo maisha yake yanatangulia UMOJA wa uzao wao..

Hii dhana ya Common Ownership ndani ya Ujamaa ndiyo makosa makubwa sana yaliyofanyika. Muda wote nimepingana na dhana hii kwa sababu ni falsafa ilotungwa na binadamu kupingana na Ubepari (opposite of capitalism) hivyo huwezi kusema kutowataja Ho Chi Minh, Mao, Castro wala Nyerere utapoteza maana yake ikiwa hawa walikuwa wanafunzi na wafuasi wa falsafa hiyo. Nitarudia kusema makosa yaliyofanyika ktk Ujamaa ni pale walipoutazama Ubepari kama ndiye adui wa wananchi wake kutokana na kwamba Utajiri wa nchi zao ulikamatwa na wageni hivyo wakataifisha mali zao na kuziweka chini ya ulinzi wa serikali. Inafact, they had no choice isipokuwa kufanya hivyo wasingweza kutaifisha mali zile na wakazigawa kwa wananchi wote.. Lakini baada ya kutaifisha waligundua pia wanafanya kinyume cha UTU kutaifisha wageni tu hivyo kuonyesha Ujamaa una UBAGUZI na kinyume cha UTU ndio wakaamua kila mtu hata mwananchi aathirike, mali zote ziwe ya serikali hivyo kuweka usawa ktk sheria ilokusudiwa mwanzo kwa hadi ya kugawana utajiri sawa..

Hitler yeye aliamua kuwaua kabisa Wayahudi waliotawala utajiri wa Ulaya akisema haiwezekani watu hawa ndio watawale Utajiri wote wa Ulaya na waliitwa Mabepari vile vile. Hivyo kitendo cha yeye kuua Wayahudi hakipelekei maana ya ndio tafsiri ya Udikteta..Na naweza sema kutokana na wayahudi kujilinda na Udikteta wa watu kama Hitler wamechukua wao nafasi ya Udikteta kuweka kwa fikra za dawa ya moto ni moto hivyo leo wao wanaogopewa kuliko hata huyo Hitler badala ya kupambana na Wajarumani kutafisri udiketa wa Hitler. Infact hakuna Wajamaa kama wao na hakuna mabepari kama wao dunia hii hivyo kufanikiwa kwao sio kwa bahati ama wao ni wateule wa Mungu isipokuwa wanafuata ethic na principle za uzawa wao. Kila Myahudi ni mjamaa kwa myahudi mwenzake, kila mtu ana own mali zake lakini anachangia ktk mfuko wa maendeleo ya Wayahudi popote duniani na WANAFIKIRIANA siku zote...

UTU ni pamoja na mila na desturi za watu, na unapoukiuka ndipo madhara hutokea. Kushindwa kwa Ujamaa haikuwa bahati mbaya isipokuwa Ujamaa ulikiuka UTU wa walengwa, badala ya kuulinda uliwakwaza kwa kuunda mfumo unaokizana na asili ya mwanadamu wakaongozwa kama wanyama kwa hisia zaidi ya kuenzi akili, uwezo na vipaji vyao.. Hakuna Taifa wala nchi yenye uasili ya watu wake waliwahi kushiriki maisha yao kwa kufuata Common ownership kabla ya kukoloniwa - HAKUNA. na hakuna historia ya uzawa wetu (nature yetu) waliotangulia kuishi in Common owenrship isipokuwa kushirikiana inapopaswa.

Na niseme kwamba Uwekezaji, Ubinafsishaji, Demokrasia hizi sio SHERIA wala KANUNI bali ni mifumo ya MAISHA ambao pia ni tunzi ya hao intellectuals waliokaa na kufikiria njia ama mbinu za kupambana na mfumo hasi ulokuwepo. UTU wetu hauna mwanzo wala ubunifu wa mtu ama mwana falsafa ni nature ya mwandamu, ni asili ya uzawa wa mwanadamu na UTU wake hutambulika tu kwa fikra na matendo yake kwa kuthamini UHURU, HAKI na USAWA baina yao na unatungiwa sheria na kanuni kuhakikisha vitu hivyo vinawafikia walengwa. Haki za binadamu ni sehemu tu na ulinzi wa UTU japokuwa nachopingana nacho ktk kauli yako ni pale mwanandoa anapoona mateso ktk ndoa yake basi anaamua kuacha kabisa ndoa na kuhukumu jinsia nzima ya mwenza na kutowaamini kabisa kama ilivyotumika Ujamaa dhidi ya Ubepari. He/she will end up being a loser..

Hivyo haikuwa mfumo wa maisha yetu isipokuwa common ownership imekuja pinzani ya Ubepari..Huu sii msingi wa maisha ya mwanadamu isipokuwa ni fikra za mtu ama watu waliokaa na kufikiria jinsi gani wataweza kupingana na Ubepari, ni Falsafa ilobuniwa in response to Capitalism, hayakuwa maisha ya mwanadamu kwa asili yake maana tusiseme UTU umeanza baada ya Ujamaa. Na nimeshindwa zaidi kukuelewa pale Makosa yanapofanywa na King George au Malkia Victoria kuitawala Afrika kuwa ndio Ubepari na tuhukumu Ubepari wakati Lengo la King Geroge ni kufisadi maliasili za makoloni yake kuijenga Uingereza yake. Au niseme kina Chenge kununua rada na kuweka vijisenti millioni account za nje iwe sababu ya kimfumo ukalaani utawala wenye mawakili wa serikali ukapiga vita mtanzania yeyote kuwa na account nje..

Labda niseme hivi leo Utajiri wa dunia umekamatwa na watu asilimia 1 tu, hii haitokani na Private ownership maana utajiri sio mbegu ama msingi wa maendeleo bali ni mavuno ya kile ulichopanda. Tanzania ni nchi tajiri sana lakini wananchi wake ni maskini toka wakati wa Nyerere..Russia nadhani ndio nchi yenye Uajiri mkubwa duniani kwa maliasili lakini pia WATU wake walikuwa maskini kuliko nchi zote za Ulaya wakati wa Ujamaa wa common owenership.. China vile vile ilikuwa nchi yenye wasomi wengi kuliko kote duniani lakini wananchi wake walikuwa maskini kuliko nchi za Asia kutokana na common ownership.

Nchi zote za Kijamaa kwa wakati wote waliopambana na Ubepari, wananchi wake walikuwa na dhiki kubwa wakigawana umaskini, wakila hadi mbegu za uchumi wao hivyo kutoweza kupanda zaidi kwa mavuno ya ziada. Na sababu kubwa ilikuwa kupambana na mfumo (Ubepari) badala ya watu wanaokiuka UTU. Sheria siku zote zipo kumlinda mwenye duka hivyo adhabu ni kwa mwizi badala ya kunmlazimisha mwenye duka asiuze mali zake kwa kuogopa wezi..

Mawazo ya kuhofia Ubepari (private ownership) ambao ni sehemu ya maisha ya mwanadamu yalibadilishwa kwa kuhofia mafanikio ya mtu mmoja (choyo, inda na kikorosho). Binadamu hatuwezi kuishi ktk mazingira ya Common ownership kwa sababu tumeumbwa na matamanio tofauti ya maisha, hakutuumbwa kama nyuki ama salmon kufuata nyendo zile zile z auzawa wetu isipokuwa tumeumbwa na vipaji na kila mmoja wetu ni unique hafanani hata na mzazi wake ama pacha wake kifikra. Ni wewe mwenye nguvu na uwezo wa kupiga hatua ya kwanza, ya pili ya tatu na hata ukaanz akukimbia siwezi kukusaidia ktk hatua ya kwanza ama ya pili zaidi ya mimi mwenyewe pia kufikiria kupiga hatua ya kwanza..Waswahili husema hatuwezi kupanda ngazi moja watu wawili kwa pamoja, anapanda mmoja kisha anafuata kmwingine kwa wale walioshindwa kupanda tutawatupia kamba nao watapanda na kujumuika nasi juu ya paa..

EID MUBARAK!...
 
Last edited by a moderator:
Mkandara,ubepari bila restrictions hauna utu...Ndo maana tunarudi kwenye kutizama sheria zenye kuifaa jamii yetu badala ya kuwa na maneno matamu kwenye makaratasi.Ndo hapo umuhimu wa serikali unapokuja,kuleta check and balance otherwise ubepari hauna utu mkuu.
 
Last edited by a moderator:
Mkandara,ubepari bila restrictions hauna utu...Ndo maana tunarudi kwenye kutizama sheria zenye kuifaa jamii yetu badala ya kuwa na maneno matamu kwenye makaratasi.Ndo hapo umuhimu wa serikali unapokuja,kuleta check and balance otherwise ubepari hauna utu mkuu.
Nani kasema Ubepari hauna restriction?.. jamani mbona mnachanganya madawa! Ubepari ni kuachia wananchi (sio wageni) waendeshe njia za uzalishaji uchumi na restrictions zipo pale pale. Ubepari sio mfumo wa siasa kama tulivyofundishwa enzi za vita baridi bali ni aina ya mfumo wa kiuchumi (ecomonic system) unaowapa fursa wananchi kuendesha njia za uchumi - niseme mara ngapi jmushi1...

Wanaokataa regulations (sio restrictions) ni Conservative na wanafanya hivyo kwa sababu UCHUMI wa nchi zao unategemea MATAJIRI wawekezaji wa ndani (sio wa nje) hao wakoloni mamboleo wanaokuja makwetu na kutuibia.. To them the ends justifies the means hivyo morality of their actions foresee the positive outcome.. Hivyo Conservatives hawataki kubadilisha itifaki zilizolizaa Utaifa wao iwe wazungu wa apatheid, Waingereza ama Wamarekani matajiri wezi na walafi waliokuja kwetu kutuibia maliasili zetu na hata kusababisha nchi hizo kuwa na nguvu kubwa ya Kiuchumi. Bare in mind matajiri are the source of their economic sustainability..

Liberal ndio kidogo wako laini kwa fikra za mageuzi kutokana na mfumo hasidi kwa nchi maskini na kusisitiza usawa ktk nafasi na fursa kwa wananchi wake kufaidika na wizi, Ulafi na hasidi zote wanazozifanya nchi za maskini (Ukoloni mamboleo). Hawa wanatazama zaidi mgao wa keki kwa wananchi wake yaani tunaiba nje lakini je wananchi wetu wanafaidika vipi na fedha hizo..Hivyo ukinambia Uhafidhina una tatizo nitakubaliana na wewe kwa sababu unapinga kuwepo regulations ktk makuzi ya Uchumi lakini ktk mazingira yao na Progressive ndio wanasisitiza zaidi regulations ili kuzuia wezi na walafi ambao hawawezi kuishia nje bali tamaa na ulafi wao unaingia hadi nyumbani kwa kukataa kushare kile walichokivuna nje kwa kutumia bendera ya nchi yao. Hivyo pilitics zao It's all about their interest na kwa watu wao sii mimi na wewe.

Sisi watanzania Uhafidhina wetu inabidi unatazame hali yetu, UMASIKINI wetu kwanza maana tunataka kuondokaana na umaskini wakati Ulaya wanataka kulinda MATAJIRI wake ambao ndio wakulima wenye mbegu ya kuzalisha uchumi wao.. Sisi hatuna matajiri, ni maskini wa hali na mali, hatuna mbegu wala mtaji utawalinda vipi matajiri wasiokuwepo?.. Hivyo uhafidhina wetu unaanza na kuzalisha matajiri sio kwa wizi bali kwa kuwawezesha wenye uwezo kukamata njia za uzalishaji iwe ukulima, uvuvi ama mifugo maana hii ndio maliasili tulokuwa nayo mkononi na tuna uwezo na ujuzi nayo.

Inatakiwa mtu kutafakari kwa makini falsafa inayolingana na sisi na mazingira yetu, restrictions ni lazima hata Marekani kuna restrictions sana tu kwa wageni. na conservative ni wagumu sana kuruhusu wageni kuingia na kuwekeza Marekani, lakini hawana restrictions nje ya mipaka yao wanakoiba... Liberal wako poa lakini pia wanapima faida kwa nchi yao na sii usawa kweru. Hakuna kitu hiyo hawa ni mabepari mkuu wangu. Uhafidhina kwetu nchini unaweza kufanya kazi kutumia matajiri wachache Watanzania kupitia kilimo, uvuvi, na ufugaji kuzalisha ajira badala ya kuwa against utajirisho.

Tatizo tulokuwa nalo sisi ktk Ubepari ni kubwa zaidi ya kufikiria tu Ubepari, maana ukweli ni kwamba hatuna restrictions wala regulations kwa wageni ama viongozi wetu ilihali wenzatu mabepari wana restrictions na regulations when dealing with foreigners ama viongozi wake na ndiio maana utakuwa wote wana msimamo mmoja kuhusu Iran maana wanatazama interest za Marekani kwanza. haya kina sisi tuna restrictions na regulations kibao kwa wananchi wazawa wenyewe (Ujamaa ulowakandamiza wananchi) kuliko kwa wageni wawekezaji na viongozi..Itazame vizuri picha hii utaona ya kwamba viongozi wetu hawalipi kodi, wanalipwa mishahara mikubwa wakati wanajengewa nyumba wanapewa magari, wanalipiwa usafiri na hata suti wananunuliwa. Hawa hawana miiko wala maadili isipokuwa yale ya chama tawala ambacho leo hii kimejaa MAFISADI lakini waadirifu kwa chama.

Maendeleo yetu yanategemea kiongozi kuweka madeal na nchi za nje kwa 10% kuvuna rasilimali zetu pasipo restrictions japo tunaibiwa. Kifupi siasa zetu hazina Uhafidhina wala Progressive, sii Ubepari wala Ujamaa kutokana na kwamba tuna Wakulima (wazalishaji) lakini hawana mbegu, viongozi mafisadi, hatuna dira wala mitaji hivyo huwezi kusema kuna Ubepari mahala ambapo hakuna mtaji (capital) na tunataka vitu vikubwa kuliko uwezo wetu. Kwa mtu yeyote ama nchi yoyote inayotaka vitu vikubwa kuliko uwezo wake mara nyingi huishia katika Umalaya na Ndivyo Tulivyo..

Tanzania hakuna Ubepari bali kuna Ukoloni mamboleo na ndio maana tuliletewa Demokrasia na utandawazi hii ni siasa ilotungwa makusudi kuwaondoa viongozi walikuwa wagumu kuupitisha Ukoloni mamboleo na ndio maana kila nchi ya kiafrika, Asia na South Amerika kuna mashirika yameingia makusudi kwa kuhamasiha demokrasia ili mtawala kama Mugabe wasipewe muda mrefu wa kuongoza dhidi ya Ukoloni mamboleo.. Vita inaanzia ndani mwenu kwa kuwatumia wananchi wenyewe dhidi ya serikali au kiongozi anayepingana na ukoloni mamboleo. It is this factor which makes neo colonialism such a serious threat to world peace.

Wakoloni wana kila aina ya mbinu na wataendelea kubuni mbinu za kuingia nchi zenye maliasili kama zetu kwa sababu makwao hawana malighafi na uchumi wao unategemea malighafi kutokana nchi maskini..Na kwa UJINGA wetu sisi tumeuvaa mkenge wa demokrasia na utandawazi wakati they control stock market na utandawazi hauna sura wala thamani pasipo stock market..Tumeliwa pande zote na ukoloni mamboleo.. Nawaomba sana mfikirie zaidi UKOLONI MAMBOLEO kama ndio mfumo unaotumika kuendesha wiuzi, Ulafi na Uhasidi woote tunaouona kutoka nchi tajiri kwa sababu kumpunguzia kodi Bakhresa kuna uwezo zaidi wa kukuza biashara zake ndani na kuzalisha kazi..Utajiri wake unashuka hadi kwa vijana kupata ajira na kuwawezesha kununua bidhaa zetu mahitaji yao (money to spend)..Hivyo mzunguko wake ndio makuzi ya uchumi wetu badala ya kuibiwa na wawekezaj toka nje kam akina Barriks ambao kesho wanakimbia TZ pasipo kulipa corporate tax na kutuachia mahandaki..
 
Wakuu,
Mnakasha ni mtamu na nawashukuru sana sana. Kila ninapowasoma siachi kudokoa kitu.
Nina hakika jinsi mvutano ulivyo ndivyo unaakisi mvutano katika jamii yetu, ingawa nina uhakika viongozi wetu wamechanganyikiwa na hili halipo katika ajenda zao isipokuwa uchaguzi na dili.

Nionavyo mimi tumefika mahali penye mduara, kila tukienda mbele na mjadala tunarudi tulipoanzia.
Hili lina afya yake lakini ningeomba twende mabali zaidi na pengine tuvunje mduara uliopo.

Kwa vile kuna mchakato wa kuandika katiba mpya (ingawa sikubaliani nao kwa vile najua matokeo yake mabaya) inabidi tukubali kuwa upo japo kwa kufumba macho.

Kutokana na tuliyojadili, ningependa niulize mambo yafuatayo yanayohusiana na mada yetu.
a) JingalaFalsafa, Mkandara, jmushi1, Mwalimu, Mimibaba na yoyote awaye :
Endapo ungepewa nafasi ya kutoa mapendekezo ya kuandika kifungu cha katiba kinachohusu siasa na uchumi wa Tanzania (i)ungekiandika kisomeke vipi (ii) Unakiaanisha vipi (analyze) kwa mustakabali wa taifa letu.

b) Kwa vile uchumi ndio unatawala siasa za dunia ya leo
(i) Ungeshauri Wananchi wafanye nini kujikomboa kiuchumi
(ii)kukabiliana na ukoloni mamboleo, ubepari au ujamaa usiolingana na hali zetu au kukubaliana na hayo kama yanalengo la kutuinua na kutuondoa tulipo tufanye nini
(ii)Kwa vile tunakubaliana kuwa umasikini,ujinga na maradhi ni maadui zetu, ni mfumo gani (wowote unaoufikiri) unadhani utatuwezesha kupambana na maadui hawa katika mazingira ya dunia ya leo.
 
Back
Top Bottom