Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #61
YANAYOJIRI ARUSHA KISIASA: KULIKONI?
#65 hapo juu nilieleza kuhusu majimbo moto na yenye ushawishi wa kisiasa nchini. Nilisema CCM itafanya kila iwezalo ili kushinda Arumeru. Kilichotokea ni wingi wa kura uliokuwa dhahiri kuwa CDM wameshinda. Pamoja na ulizini madhubuti wingi huo wa tofauti ya kura uliweka mazingira 'magumu
Kwa msingi huo CCM ilipeleka timu yote tena ikitumia rsilimali za taifa ili kulitwaa jimbo la Arumeru ambalo lilikuwa ni ngome isiyohitaji kampeni kwao.
Arusha ni 'hot spot' kutokana na ushawishi wake katika duru za siasa nchini.
Kama ilivyokuwa kwa Tarime na wimbi la mageuzi kanda ya ziwa, Arusha ni sehemu muhimu sana kisiasa.
Ambukizo lake linatoka Karatu na Kilimanjaro sasa limeingia Arumeru.
Hakuna jimbo salama tena mikoa ya Kilimanjaro na Arusha
Ni muhimu kukumbuka kuwa mbio za urais 2015 zinategemea sana wagombea watakavyojipanga na kuungwa mkono.
Jimbo la Arusha lilikuwa na mgombea mwana mama Matilda Buriani ambaye anahusishwa sana kisiasa na waziri mkuu aliyejiuzulu Lowassa.
CCM wanafahamu kuchukuliwa kwa ngome zao watakuwa wamepoteza ilenafasi ya kwenda vijijini na sehemu nyingine kwasababu itabidi wapige kambi mikoa michache yenye ushawishi kama Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na Mbeya.
Wanaelewa hali haitabiriki Kagera wala Kigoma na Iringa ni tia maji tia maji.
Kwa maneno mengine ngome imeingiliwa na kuvunjwa.Mikoa kama ya Tanga, Mtwara, Pwani, Dodoma, Sumbawanga, Katavi itabaki kuwa mikononi mwao, swali ni je ina wapiga kura wakutosha achilia mbali wenye ushawishi?
Kutenguliwa kwa ubunge wa Mh Lema kumeleta kiwewe sana kambi ya upinzani.
Sote tunaimani na yombo vyetu vya sheria maana hata Chadema wasipotendewa haki huenda huko.
Pamoja na imani yetu hakuna shaka kuwa mfumo wetu wa sheria unawalakini mkubwa sana.
Vongozi na majaji huteuliwa na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM.
Wasi wasi siyo tu unasemwa na watu mitaani, hata jaji mkuu mstaafu Barnabas Samata, Nyalali wameshasema hayo.
Wiki mbili zilizopita jaji mkuu wa Tanzania Mh Othman alikaririwa akisema serikali inaingilia utendaji wa mahakama.
Ingawa hakusema ni vipi lakini inatosha sana kufahamu kuwa kuna tatizo na limesmwa tena ndani ya wiki mbili tu zilizopita
Tukirudi nyuma tunakumbuka hukumu ya marehemu jaji Rugakingira kuhusu mgombea binafsi. Hadi sasa hakuna haki iliyotolewa na mahakama. Jaji Augustino Ramadhani ameingia na kuikuta kesi na amestaafu na kuiacha.
Wazungu wanasema 'justice delayed justice denied' ucheleweshaji wa sheria ni unyimaji wa haki kwa tafsiri isiyo rasmi.
Tumeshuhudia msuguano wa mihimili ya dola kama bunge na serikali na ilifikia mahali mahakama ikawa katika msuguano na bunge. Hii inaonyesha kuwa kuna tatizo katika mgawanyo wa madaraka na serikali ina nguvu sana katika kutunga sheria na kusimamia sheria hizo hizo ikiwa ni pamoja na kutoa haki.
Kilichonishtua kuhusu hukumu ya Lema ni jinsi Ikulu ilivyojibu haraka sana tuhuma hizo chini ya masaa 12 tangu zitolewe.
Ikulu yetu haina utamaduni huo hata kidogo. Hata pale Rais anapohusishwa na kashfa nzito na zenye aibu hatujawahi kuona Ikulu ikijibu au kutolea ufafanunuzi. Hili la Mh Lema lina nini? Kwanini kurugenzi ya mawasiliano iwe 'effective na efficient' kwa Lema? Kwani Lema ni nani zaidi ya mbunge nchi hii. Hapa lipo jambo.
Tukiunganisha dot yanaweza kupatikana majibu ya kweli na ya uongo lakini yote yakawa ya kweli kimazingira.
Haiwezekani Rais ahusishwe na Kagoda Ikulu ikae kimya, ahusishwe na Richmond Ikulu ikae kimya n.k halafu hili la Lema lijibiwe masaa chini ya 12 tangu kutokea? Why Lema! who is Lema? Kuna jambo
Kisiasa maana yake ni kuwa tuhuma hizo zitatibua mpango mzima wa kulitwaa jimbo la Arusha. Wananchi wataingiwa na hasira na kupiga kura ya hasira endapo tuhuma hizo zitaachwa zienee vichwani mwao.
Huo ndio mtazamo wangu kisiasa na kila mmoja wetu anaweza kuwa na wake.
Chadema wafanye nini?
Ningewashauri CDM wasikate rufaa kwasababu mazingira yanaashiria kutokuwa na haki, yamegubikwa na mazingira yanayotatiza sana. Waitumie fursa waliyopewa na Ikulu kufikisha kesi Mahakama ya juu ya wananchi.
Kitengo chao cha uenezi kifanye kazi hiyo kikamilifu.
Kwa vile bado kuna joto la Arumeru,CDM watumie nguvu hiyo kukabiliana na uchaguzi ndani ya siku 90.
Tatizo la kukata rufaa ni kuwa hukumu inaweza kutolewa mwezi wa 12. Wakati huo suala litakuwa mahakamani na ni kosa la kisheria kulizungumzia. Hapo CDM watakuwa wamefungwa mdomo wakati CCM wakijijenga kutokana na makovu ya Arumeru. Hukumu ikija kama inavyotarajiwa basi CDM watakuwa wamepoteza nafasi iliyo wazi kwa sasa.
Chadema wafikirie sana mtego huu wa CCM na serikali yake. Kinachofanyika ni kupitisha muda 'buy the time' suala likiwa mahakama kuu, wakati huo huo CDM wakiwa wamefungwa midomo kisheria na CCM wakijijenga.
Kupitisha muda kuna maana ya kuua nguvu na moto wa kisiasa walio nao CDM kwa sasa na kampeni zikianza mathalani mwezi wa 12 hakuna atakayekumbuka Arumeru na wote watakuwa wameanza upya.
Tusemezane
#65 hapo juu nilieleza kuhusu majimbo moto na yenye ushawishi wa kisiasa nchini. Nilisema CCM itafanya kila iwezalo ili kushinda Arumeru. Kilichotokea ni wingi wa kura uliokuwa dhahiri kuwa CDM wameshinda. Pamoja na ulizini madhubuti wingi huo wa tofauti ya kura uliweka mazingira 'magumu
Kwa msingi huo CCM ilipeleka timu yote tena ikitumia rsilimali za taifa ili kulitwaa jimbo la Arumeru ambalo lilikuwa ni ngome isiyohitaji kampeni kwao.
Arusha ni 'hot spot' kutokana na ushawishi wake katika duru za siasa nchini.
Kama ilivyokuwa kwa Tarime na wimbi la mageuzi kanda ya ziwa, Arusha ni sehemu muhimu sana kisiasa.
Ambukizo lake linatoka Karatu na Kilimanjaro sasa limeingia Arumeru.
Hakuna jimbo salama tena mikoa ya Kilimanjaro na Arusha
Ni muhimu kukumbuka kuwa mbio za urais 2015 zinategemea sana wagombea watakavyojipanga na kuungwa mkono.
Jimbo la Arusha lilikuwa na mgombea mwana mama Matilda Buriani ambaye anahusishwa sana kisiasa na waziri mkuu aliyejiuzulu Lowassa.
CCM wanafahamu kuchukuliwa kwa ngome zao watakuwa wamepoteza ilenafasi ya kwenda vijijini na sehemu nyingine kwasababu itabidi wapige kambi mikoa michache yenye ushawishi kama Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na Mbeya.
Wanaelewa hali haitabiriki Kagera wala Kigoma na Iringa ni tia maji tia maji.
Kwa maneno mengine ngome imeingiliwa na kuvunjwa.Mikoa kama ya Tanga, Mtwara, Pwani, Dodoma, Sumbawanga, Katavi itabaki kuwa mikononi mwao, swali ni je ina wapiga kura wakutosha achilia mbali wenye ushawishi?
Kutenguliwa kwa ubunge wa Mh Lema kumeleta kiwewe sana kambi ya upinzani.
Sote tunaimani na yombo vyetu vya sheria maana hata Chadema wasipotendewa haki huenda huko.
Pamoja na imani yetu hakuna shaka kuwa mfumo wetu wa sheria unawalakini mkubwa sana.
Vongozi na majaji huteuliwa na Rais ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM.
Wasi wasi siyo tu unasemwa na watu mitaani, hata jaji mkuu mstaafu Barnabas Samata, Nyalali wameshasema hayo.
Wiki mbili zilizopita jaji mkuu wa Tanzania Mh Othman alikaririwa akisema serikali inaingilia utendaji wa mahakama.
Ingawa hakusema ni vipi lakini inatosha sana kufahamu kuwa kuna tatizo na limesmwa tena ndani ya wiki mbili tu zilizopita
Tukirudi nyuma tunakumbuka hukumu ya marehemu jaji Rugakingira kuhusu mgombea binafsi. Hadi sasa hakuna haki iliyotolewa na mahakama. Jaji Augustino Ramadhani ameingia na kuikuta kesi na amestaafu na kuiacha.
Wazungu wanasema 'justice delayed justice denied' ucheleweshaji wa sheria ni unyimaji wa haki kwa tafsiri isiyo rasmi.
Tumeshuhudia msuguano wa mihimili ya dola kama bunge na serikali na ilifikia mahali mahakama ikawa katika msuguano na bunge. Hii inaonyesha kuwa kuna tatizo katika mgawanyo wa madaraka na serikali ina nguvu sana katika kutunga sheria na kusimamia sheria hizo hizo ikiwa ni pamoja na kutoa haki.
Kilichonishtua kuhusu hukumu ya Lema ni jinsi Ikulu ilivyojibu haraka sana tuhuma hizo chini ya masaa 12 tangu zitolewe.
Ikulu yetu haina utamaduni huo hata kidogo. Hata pale Rais anapohusishwa na kashfa nzito na zenye aibu hatujawahi kuona Ikulu ikijibu au kutolea ufafanunuzi. Hili la Mh Lema lina nini? Kwanini kurugenzi ya mawasiliano iwe 'effective na efficient' kwa Lema? Kwani Lema ni nani zaidi ya mbunge nchi hii. Hapa lipo jambo.
Tukiunganisha dot yanaweza kupatikana majibu ya kweli na ya uongo lakini yote yakawa ya kweli kimazingira.
Haiwezekani Rais ahusishwe na Kagoda Ikulu ikae kimya, ahusishwe na Richmond Ikulu ikae kimya n.k halafu hili la Lema lijibiwe masaa chini ya 12 tangu kutokea? Why Lema! who is Lema? Kuna jambo
Kisiasa maana yake ni kuwa tuhuma hizo zitatibua mpango mzima wa kulitwaa jimbo la Arusha. Wananchi wataingiwa na hasira na kupiga kura ya hasira endapo tuhuma hizo zitaachwa zienee vichwani mwao.
Huo ndio mtazamo wangu kisiasa na kila mmoja wetu anaweza kuwa na wake.
Chadema wafanye nini?
Ningewashauri CDM wasikate rufaa kwasababu mazingira yanaashiria kutokuwa na haki, yamegubikwa na mazingira yanayotatiza sana. Waitumie fursa waliyopewa na Ikulu kufikisha kesi Mahakama ya juu ya wananchi.
Kitengo chao cha uenezi kifanye kazi hiyo kikamilifu.
Kwa vile bado kuna joto la Arumeru,CDM watumie nguvu hiyo kukabiliana na uchaguzi ndani ya siku 90.
Tatizo la kukata rufaa ni kuwa hukumu inaweza kutolewa mwezi wa 12. Wakati huo suala litakuwa mahakamani na ni kosa la kisheria kulizungumzia. Hapo CDM watakuwa wamefungwa mdomo wakati CCM wakijijenga kutokana na makovu ya Arumeru. Hukumu ikija kama inavyotarajiwa basi CDM watakuwa wamepoteza nafasi iliyo wazi kwa sasa.
Chadema wafikirie sana mtego huu wa CCM na serikali yake. Kinachofanyika ni kupitisha muda 'buy the time' suala likiwa mahakama kuu, wakati huo huo CDM wakiwa wamefungwa midomo kisheria na CCM wakijijenga.
Kupitisha muda kuna maana ya kuua nguvu na moto wa kisiasa walio nao CDM kwa sasa na kampeni zikianza mathalani mwezi wa 12 hakuna atakayekumbuka Arumeru na wote watakuwa wameanza upya.
Tusemezane