Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #81
Inaendelea.......
Ngome ya kisiasa ya Chadema ni tabaka la wasomi. Kuna sababu nyingi za kutokea hili
1. Ni kutokana na tabaka la wasomi kuona mambo yanavyokwenda CCM. Wamebaini kuwa mabadiliko sasa ni muhimu.
Tabaka hilo lina wale wanaoamini kuwa kuibadilisha CCM lazima mtu awe na fedha.
Miongoni mwao wanaamini kuwa ili uwe sehemu ya 'system' ni lazima uwe ndani ya chama. Hili la pili ndilo liliobaki na CCM
2. Juhudi za Chadema kuwaingiza katika siasa vijana 'recruit' . Vijana hao wameonyesha wazi kuwa kuna tofauti za mitizamo kwa vizazi vilivyopo(wazee na vijana).
Katika ngome hii ya kisiasa tabaka la wasomi linaundwa na vijana. Hii ndiyo inapelekea wasomi wengi makazini na vyuoni kuunga mkono CDM. Kwa hilo tu linazaliwa tabaka la wafanyakazi ambao wengi ni wasomi hasa kada ya kati.
Kada hii ya wasomi vijana imekuwa na ushawishi mkubwa sana kisiasa kiasi cha kugeuza wakulima kuunga mkono. Ndiyo maana CDM sasa inavuna wanachama huko vijijini.
Hata bila kada ya wasomi, kuna jambo moja linaiumiza sana CCM. Mgawanyiko ndani ya chama umekifanya chama kidumae kimaamuzi. Lipo Kundi la wenye chama na pesa na kundi linaloamini chama kimepoteza mwelekeo.
Kibaya zaidi ni uongozi wa CCM kuwatenga na kuwanyanyasa viongozi wazee. Haya yote yamekifanya chama kionekane kama genge la waporaji. Matokeo ya haya ni wanachama kutoona siku za usoni 'future' na hivyo kutafuta mbadala ambao ni CDM kwa wakati tulionao.
Ingawa CDM ina ngome kubwa ya vijana na wasomi, ni lazima ichukue tahadhari. Vijana ni watu wenye matamanio, mbinu na wakosefu wa busara kwa baadhi ya nyakati. Tumeona misuguano ndani ya Chama ikiwa na chanzo cha vijana. Tumeona baadhi wakikosa uzooefu wa kisiasa hasa kwenye majukwaa n.k.
Kibaya zaidi ni CDM kuiga mbinu za CCM katika kushughulikia matatizo hasa ya vijana ndani ya chama.
Migogoro inayoimaliza CCM ni zao la migogoro ndani ya UVCCM. Vijana hao walitumiwa na wazooefu kuleta mtafaruku ambao unafukuta hadi sasa. Tunakumbuka akina Guninita, Nchimbi, Malisa, Masauni, Nape, Mkalla, Francis n.k walivyopita katika mitifuano.
Hali si tofauti ndani ya Chadema, kuna migongano na makundi yasiyo rasmi ndani ya chama.
Makundi ndani ya vyma hayawezi kuepukwa kwa asilimia mia, lakini yanaweza kupunguzwa nguvu yasilete uharibifu.
Habari za ndani ya chama zinavuja na kuna mashambulizi ya chini chini hata hapa JF yanaonekana.
Akina Kafulila hawakufanya waliyoyafanya 'solo' bado wana wafuasi waliojificha.
Kiklichotokea siku za karibuni ni ushahidi kuwa kuna mgogoro ndani ya BAVICHA. Sipendi kurejea kiini cha mgogoro lakini inatosha kusema kuna vita kati ya Mwenyekiti na makamo wake ushahidi wa wazi kuwepo kwa makundi.
Tatizo ninaloliona ambalo ni kubwa ni lile lile la kushughulikia mambo ki-CCM, kwamba kuna tatizo lakini litatafutiwa maelezo, mbinu na hadithi katika utamaduni ule ule wa kulindana.
Sioni kwanini hatua za nidhamu hazijachukuliwa kwa Juliana Shonza ambaye ni wazi kwa vigezo vyovyote vile ni mkosefu na mtovu wa nidhamu. Ni mtumiwa wa kuleta vurugu
Tumeona jitihada za kumlinda kwa maneno matamu kama vile, bado ni mdogo, afundwe n.k. Ni kulindana kule kule kwa CCM kulikodhoofisha ngome yao.
Matarajio ya wengi ni kuona mbadala wa CCM kwa vitendo na si maneno. Kwa hili la kulinda watovu wa nidhamu kama Juliana kuna madhara mengi yatokanayo
1. Kuendeleza makundi kwasababu tayari makamu mwenyekiti amejihakikishia ulinzi ndani ya chama
2. Kudhoofisha nguvu za ngome ya vijana kwa kuwagawa, kutofanya kazi pamoja n.k.
Leo ni uongo kujidanganya kuwa Heche na Juliana wanaweza kufanya kazi pamoja hapo ndio mwanzo wa mparaganyiko
3. Kuwavunja nguvu wote wanaodhani CDM inaweza kuja na jipya. Kama hawawezi kumwadhibu mtovu wa nidhamu wa maneno sijui watawezaje kumwadhibu fisadi aliyebobea. Swali linabaki je CDM wana preach what they do!
4. Inaondoa uhalali wa CDM kuikemea CCM kwasababu utawezaje kumwambia JK amwajibishe Waziri mkuu ikiwa wewe huwezi kumwadhibu simple person Juliana Shonza makamu wa BAVICHA?
Ni malizie kwa kusema kuwa wenzetu wanathamini sana 'political base' zao katika siasa. Na hakika kama chama kinataka kuanguka kisiasa basi kianze na ku-demoralize ngome zake. CCM ilipo ni matokeo ya kudharau ngome zilizoifanya isimame kama chama kwa nusu karne.
Nitahadharishe tu kuwa kuchanua kwa Chadema kutakuwa na maana kama ngome yao itaridhika na mwenendo wa chama.Migogoro ya chini chini inakiweka chama mahali pa gumu hata kama si dhahiri.
Tusemezane
Ngome ya kisiasa ya Chadema ni tabaka la wasomi. Kuna sababu nyingi za kutokea hili
1. Ni kutokana na tabaka la wasomi kuona mambo yanavyokwenda CCM. Wamebaini kuwa mabadiliko sasa ni muhimu.
Tabaka hilo lina wale wanaoamini kuwa kuibadilisha CCM lazima mtu awe na fedha.
Miongoni mwao wanaamini kuwa ili uwe sehemu ya 'system' ni lazima uwe ndani ya chama. Hili la pili ndilo liliobaki na CCM
2. Juhudi za Chadema kuwaingiza katika siasa vijana 'recruit' . Vijana hao wameonyesha wazi kuwa kuna tofauti za mitizamo kwa vizazi vilivyopo(wazee na vijana).
Katika ngome hii ya kisiasa tabaka la wasomi linaundwa na vijana. Hii ndiyo inapelekea wasomi wengi makazini na vyuoni kuunga mkono CDM. Kwa hilo tu linazaliwa tabaka la wafanyakazi ambao wengi ni wasomi hasa kada ya kati.
Kada hii ya wasomi vijana imekuwa na ushawishi mkubwa sana kisiasa kiasi cha kugeuza wakulima kuunga mkono. Ndiyo maana CDM sasa inavuna wanachama huko vijijini.
Hata bila kada ya wasomi, kuna jambo moja linaiumiza sana CCM. Mgawanyiko ndani ya chama umekifanya chama kidumae kimaamuzi. Lipo Kundi la wenye chama na pesa na kundi linaloamini chama kimepoteza mwelekeo.
Kibaya zaidi ni uongozi wa CCM kuwatenga na kuwanyanyasa viongozi wazee. Haya yote yamekifanya chama kionekane kama genge la waporaji. Matokeo ya haya ni wanachama kutoona siku za usoni 'future' na hivyo kutafuta mbadala ambao ni CDM kwa wakati tulionao.
Ingawa CDM ina ngome kubwa ya vijana na wasomi, ni lazima ichukue tahadhari. Vijana ni watu wenye matamanio, mbinu na wakosefu wa busara kwa baadhi ya nyakati. Tumeona misuguano ndani ya Chama ikiwa na chanzo cha vijana. Tumeona baadhi wakikosa uzooefu wa kisiasa hasa kwenye majukwaa n.k.
Kibaya zaidi ni CDM kuiga mbinu za CCM katika kushughulikia matatizo hasa ya vijana ndani ya chama.
Migogoro inayoimaliza CCM ni zao la migogoro ndani ya UVCCM. Vijana hao walitumiwa na wazooefu kuleta mtafaruku ambao unafukuta hadi sasa. Tunakumbuka akina Guninita, Nchimbi, Malisa, Masauni, Nape, Mkalla, Francis n.k walivyopita katika mitifuano.
Hali si tofauti ndani ya Chadema, kuna migongano na makundi yasiyo rasmi ndani ya chama.
Makundi ndani ya vyma hayawezi kuepukwa kwa asilimia mia, lakini yanaweza kupunguzwa nguvu yasilete uharibifu.
Habari za ndani ya chama zinavuja na kuna mashambulizi ya chini chini hata hapa JF yanaonekana.
Akina Kafulila hawakufanya waliyoyafanya 'solo' bado wana wafuasi waliojificha.
Kiklichotokea siku za karibuni ni ushahidi kuwa kuna mgogoro ndani ya BAVICHA. Sipendi kurejea kiini cha mgogoro lakini inatosha kusema kuna vita kati ya Mwenyekiti na makamo wake ushahidi wa wazi kuwepo kwa makundi.
Tatizo ninaloliona ambalo ni kubwa ni lile lile la kushughulikia mambo ki-CCM, kwamba kuna tatizo lakini litatafutiwa maelezo, mbinu na hadithi katika utamaduni ule ule wa kulindana.
Sioni kwanini hatua za nidhamu hazijachukuliwa kwa Juliana Shonza ambaye ni wazi kwa vigezo vyovyote vile ni mkosefu na mtovu wa nidhamu. Ni mtumiwa wa kuleta vurugu
Tumeona jitihada za kumlinda kwa maneno matamu kama vile, bado ni mdogo, afundwe n.k. Ni kulindana kule kule kwa CCM kulikodhoofisha ngome yao.
Matarajio ya wengi ni kuona mbadala wa CCM kwa vitendo na si maneno. Kwa hili la kulinda watovu wa nidhamu kama Juliana kuna madhara mengi yatokanayo
1. Kuendeleza makundi kwasababu tayari makamu mwenyekiti amejihakikishia ulinzi ndani ya chama
2. Kudhoofisha nguvu za ngome ya vijana kwa kuwagawa, kutofanya kazi pamoja n.k.
Leo ni uongo kujidanganya kuwa Heche na Juliana wanaweza kufanya kazi pamoja hapo ndio mwanzo wa mparaganyiko
3. Kuwavunja nguvu wote wanaodhani CDM inaweza kuja na jipya. Kama hawawezi kumwadhibu mtovu wa nidhamu wa maneno sijui watawezaje kumwadhibu fisadi aliyebobea. Swali linabaki je CDM wana preach what they do!
4. Inaondoa uhalali wa CDM kuikemea CCM kwasababu utawezaje kumwambia JK amwajibishe Waziri mkuu ikiwa wewe huwezi kumwadhibu simple person Juliana Shonza makamu wa BAVICHA?
Ni malizie kwa kusema kuwa wenzetu wanathamini sana 'political base' zao katika siasa. Na hakika kama chama kinataka kuanguka kisiasa basi kianze na ku-demoralize ngome zake. CCM ilipo ni matokeo ya kudharau ngome zilizoifanya isimame kama chama kwa nusu karne.
Nitahadharishe tu kuwa kuchanua kwa Chadema kutakuwa na maana kama ngome yao itaridhika na mwenendo wa chama.Migogoro ya chini chini inakiweka chama mahali pa gumu hata kama si dhahiri.
Tusemezane