JokaKuu, hili la nchi za kiarabu zenye utajiri wa mafuta kushinikiza Wapestina wapewe haki yao limeathiriwa sana na vita ya Iraq. Pengine hali ya Palestine ingekuwa na nafuu kuliko ilivyo sasa kama hii vita haikuwepo. Sadam Hussein alikuwa rafiki wa marekani kabla hajawa hasimu wao mkubwa. Vita ya Iraq na kifo chake Sadam Hussein kwanza kilitoa mwanya kwa shia majority ndani ya Iraq kushika madaraka makubwa, lakini kubwa IRAN iliibuka kama big brother fulani wa ukanda huu wa Middle East. Iran watu wake wengi ni Shia, na jirani sasa nako wengi ni shia.
Looser number moja wa huu mtafaruku anakuwa Saudi Arabia (na hata UAE). Hawa ni sunni, na kwa muda walikuwa juu (dominance), sasa wanakuwa challenged na Iran ambayo iko kwenye mkakati wake wa Nuclear. Hili la nuclear linazidi kupandisha mashetani wasaudia na marafiki zake marekani. Na hapa ndipo urafiki wa Saudia na mmarekani unazidi kuimarika kwa sababu wote wana common enemy - Iran. Marekani kwa upande mwingine na muisraeli ni kitu kimoja. Na hapa ndipo tunakuja kwa looser number mbili Palestine.
Saudia ina nafasi kubwa sana kuongoza nchi nyingine middle east ili kuisaidia palestina. Lakini vile vile Saudia na wenzake wanamuhitaji sana mmarekani kupambana na Iran. Mmarekani yuko na Israel na kuna fununu kwamba nyuma za pazia Saudia anakubaliana mambo mengi tu na Israel kupitia kwa middle man - marekani.
Mkuu wangu hizi ni siasa za kwenye luninga, siasa ambazo nchi za magharibi zinataka sisi tuamini lakini ukweli upo wazi kabisa ya kwamba vita kuu ya sasa hivi kidunia ni UKOLONI MAMBOLEO... Hakuna siasa (Uhuru na UTU wa watu) kutangulia Uchumi bali uchumi ndio unaojenga uhuru wa watu wenyewe..
Labda nikueleze tu kwa kifupi, Miaka yote ya Ubepoari Marekani na nchi za magharibi ilikuwa kutawala nchi kiuchumi na hapakuwa na nia rahisi zaidi ya kukamata makoloni..Mataifa mengi yalipojikuta yanaathirika kiuchumi kwa kukoloniwa yalifikiri kufanya mageuzi ya utawla ndio njia pekee ya kuboresha maisha yao kiuchumi wakiwa huru na ndio maana hatua ya kwanza ktk ukombozi wa nchi zetu ilikuwa Uhuru wa Bendera.
Sasa katika mahesabu ya nchi magharibi wakakubali kutoa Uhuru lakini kwa sababu walikuwa wameisha weka mitego yao ktk investment zao wanatafuta njia ya kuzilinda mali zao ndio kina Saadam Hussein, Shah, Mobutu, na wengine wengi tu wakipachikwa kwa maandalizi maalum. Hata Nyerere alikuwa ktk kundi hilo japokuiwa hawakujua undani wake.. yeye alikuwa na mahesabu yake tayari maana alizungukwa na wajamaa kina Abrahaman Babu, Nassor Moyo, Hanga na wengine wengi tu wasomi.
Ndio tukaona Uhuru ukitolewa kama karanga lakini bado nchi nyingi hazikuwa na viwanda isipokuwa utoaji wa mali ghafi - wanasema dhahabu sii dhahabu until imetengenezwa kito kwa maana kwamba Pamba haina thamani kama zao isipokuwa kile kinachotokana na zao hilo ndio thaminisho la Pamba..
Tukapewa Uhuru wetu lakini baadhi ya viongozi wa nchi hizi wakaanza kushtuka na kukoloniwa Kiuchumi, kumbe muda wote wakoloni walikuja nchi hizi kufuata rasilimali zetu na sio kututawala sisi kama watumwa!!!. Maana historia inatuambia Wakoloni walikuja Afrika kuchukua watumwa kama cheap labours, wakafunga utumwa wenyewe lakinni bado wakabakia Afrika kututawala, haya wametupa Uhuru lakini bado maisha ya wananchi hayajabadilika ndio kujua kwamba hawa watu walikuja kuchuma na sii kututawala. Kina Nyerere wakapiga sana kelele ktk vikao vya UN lakini hakuna aliyewasikia..
Likaja vuguvugu la kifikra, viongozi na wanasiasa wetu kuzitazama upya fikra za kina Karl Max na Stalin ambazo muda wote walielewa asili ya kupe ni kunyonya damu na sii kutafuta makazi au usafiri wa bure..Ndio mageuzi yakaanza kuiva kina Nyerere wakatokea na kupigwa vita vikali sana maana waligusa interest zao. Japokuwa imechukua muda mrefu sana kwa wananchi wa nchi mbali mbali kugundua kwamba tumetawaliwa kiuchumi, nguvu ya fikra hizi sasa hivi ni kubwa zaidi kuliko wakati wowote ule hata kupita wakati wa vita baridi..
Nirudi kwa Saadam HUssein, huyu mkuu wangu tatizo lake alitangaza kubadilisha mauzo yake na kutumia Euro badala ya dollar, alianza kuweka mikataba na Wachina badala ya Marekani. hana Tofauti na Ghadaffi ambaye aliweka mkataba na Wachina tena baada ya kutaka kuwatosa Wafaransa kwa mara ya pili. Maana ktk makubaliano ya kuondoa vikwazo Libya walikubali kurudisha mashirika ya mafuta ya Shell na yale ya Ufaransa na kwa muda wa miaka minne waliweza kujua ngome zote za Ghadaffi..Hivyo kuondolewa watu hawa ilikuwa Lazima na sii swala la vita na Israel au urafiki na Palestine.
Saudi Arabia on the other hand wanatawaliwa kiuchumi, kwa miaka 35 walikuwa hawapati kitu toka machimbo ya mafuta hadi mkataba ulipokwisha ndio mali ile imerudi kwa Sultan. Kuna tatizo kubwa la uhasama baina ya Sunni na Shia na huu ndio mtaji mkubwa wa Marekani.. The more Shia becomes a threat to Saudia the more they depends on western world ambao wamewahakikishia usalama lakini wakati huo huo hawa west wanahakikisha Saudia inazungukwa na Shias hivyo bado Marekani na nchi za magharibi wana investment zao nyingi sana na kubwa Saudia. Jiulize ikiwa baba yake Osama ni mmoja wa matajiri wakuba Saudia lakini kibiashara ni mbia wa familia ya Bush, unategemea kuna kina Bush wangapi Saudia?.
Nchi ya pili duniani kwa kutoa mafuta ni Iran, toka mapinduzi ya Khomein, nchi za magharibi wamepoteza utajiri mkubwa sana toka nchi hiyo, na nakuhakikishia sio swala la Nuclear hata kidogo isipokuwa ni flash tulotupiwa machoni ghafla limetupumbaza hatuoni mbali. Wanachotaka ni Utajiri wa Iran na watafanya kila hila kuhakiisha anaingia kibaraka wao kama walivyofanya Afghanstan, Pakistan, Misri pengine na kwetu vile vile who knows maana dalili zote zipo. Palestine is another catch 22. Jiulize kwani Palestine wakipewa Uhuru wao kutatokea nini?..As a fact, Israel kuwepo ndio tishio kubwa la Waarabu kuliko kutokuwepo na hivyo wanahitaji ulinzi na Technologia zaidi kujilinda wao. Where will they get all this - Western Countries!.. More money more power to the west!..Palestine wakiupata Uhuru wao kuna sababu gani ya waarabu kujilinda tena maana hakuna mgonvi kila mtu kapata alichokitaka. Nchi za magharibi hawatauza vifaa vya kivita na ndio walipowekeza zaidi na kupiga mabillioni ya fedha - Fear is the Key!
Kama kweli Marekani na nchi za magharibi wanaogopa Iran kuwa na Nuclear head bomb mbona wanashirikiana na Pakistan nchi ambayo haina kabisa muamana kutengeneza nuclear bomb. Ebu tufikiri kwa undani zaidi, ikiwa Iran ina utajiri mkubwa hivyo na kumetokea vita unafikiri wanashindwa kununua nuclear head missile lililokwisha tengenezwa toka nchi hizo hizo kama wanavyonunua vifaa vingine vya kivita? maana silaha zote hizi zinatengenezwa ili viuzwe na sii kusubiri vita kaa itatokea. Iran walipokuwa wakipigana na Iraq, Marekani aliwauzia Iraq mabomu ambayo hayaruhusiwi vitani wakati Iraq walikuwa hawawezi kutengeneza mabomu hayo. Sisi hatutengenezi vifaa vya kivita lakini tunaweza kununua vifaa vyovyote na technologia tuitakayo kama fedha ipo..
So if they can sale all war machine of distruction what makes us think Russia, Pakistan, India, UK, USA wont sale nuclear head missle if the price is right ---They have used it before why care now! kwa hiyo kama kweli wanaogopa Nuclear bomb inatakiwa zote ziteketezwe pasiwepo na nuclear bombs..Again nitasisitiza sana ndugu zangu mkumbuke hili moja.. Marekani are not inerested in anything other than your Resources...
Uranium yetu haina bei hadi itengeneze bomu au nguvu za umeme na hapo ndipo utajiri ulipo..Kama sisi Afrika tusingekuwa na Utajiri huu, ninakuhakikishieni no single Western country would have been interest in us, Iran or Saudia. Economic power rules the world today na sio mabavu au ushujaa wa kina Umsolopagas - You can buy them..