Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #161
... inaendelea
Nafasi ya kwanza ilikuwa kubadili muundo wa bunge kwa kuchgua watu wenye uchungu na nchi hii, watu wanaofikiri mtu anawezaje kuishi kwa dola moja.
Ni kwa kupitia bunge pengine tusingeona haya wanayoyafanya viongozi wa bunge hili.
Tumetoa nafasi kwa genge la wahuni kuendeleza mtandao wao wa kulindana ndani ya seikali, katika bunge, vyombo vya sheria na vyombo vya dola.
Laiti kama tungekuwa a bunge linaloweza kupiga kura ya hapana tusingeona bajeti ya vocha za simu za vijana wanaotongozana ikiwa ndiyo chanzo cha mapato. Tumewakabidhi CCM kwa hiari na kwa hila.
Nafasi ya pili ilikuwa ni pale dola ilipoelewa kuwa umma unataka mabadiliko, mabadiliko ya katiba ili tuwe na mfumo unaokidhi haja na matakwa yetu. Tukashangaa kuona wapinzani na wananchi wakikubali genge lile lile lifanye mabadiliko ya katiba. Hebu fikiri miaka 50 hawakutaka iweje leo watake?
Mimi binafsi nawalaumu sana viongozi wa vyama vya upinzani hasa CDM. Hakika walikuwa na 'mass support' ya wananchi kuhusu utengenezaji wa katiba mpya.
Sijui waliingia mkenge gani na kuruhusu mchakato huo uendelee tukijua dhahiri shahiri kuwa wale wasiotaka mabadiliko na waliotufikisha hapa hawawezi kutukwamua.
Nilionya sana na kusema tume ya katiba inayoundwa na Rais na Mwenyekiti wa CCM haiwezi kutupatia kitu mbadala, ni mazingaombwe tu ya kuchezehsa mikono ili tuamini kuwa karatasi imekuwa pesa.
Ni mazingaombwe kama alivyowahi kusema ndugu yangu Mzee Mwanakijiji.
Kuna watu wenye hoja kuwa katiba pekee haiwezi kuwa suluhisho. Mimi napingana nao kwasababu midhali tumeshindwa kulivunja genge hili la 'wahalifu' kwa njia nyingine ikiwemo sanduku la kura, hatuna sababu ya kupoteza miaka 10 zaidi tukisubiri maajabu. Tumeshapoteza miaka 50 kwanini tuendelee kupoteza mingine?
Mimibaba anasema muda si mshiriki mzuri kwetu na tumeshapoteza, kwanini tufikir kupoteza zaidi
Tanzania kwasasa hatuhitaji kufufua viwanda, kuendeleza kilimo, kuhubiri kuhusu nguvu kazi au matumizi ya rasilimali zetu. Hatuhitaji elimu wala uvuvi, madini au nishati. Vyote hivyo vimekwama kwasababu genge la wahalifu limeshika mpini na sisi tumeshika makali. Njia mojawapo ni kutumia nguvu ya umma ili tupate muongozo utakaondoa kimya kimya hili genge huku tukiijenga nchi.
Wizi na uporaji pamoja na uhuni mpya wa kuuana ulioanza kushika kasi siyo matatizo yetu ni dalili za tatizo letu ambalo ni kukosa mfumo utakaombana kila mmoja kuanzia yule Mwanakijiji anayeiba kuku, Waziri anayesaini mikataba ya wizi na mkuu anayetuamnisha kuwa 'huu ni upepeo tu' utapita.
Hivyo ndivyo China walivyoweza, ndivyo Japan wanavyofanya, na ndivyo Marekani wanavyoendelea.
Nchi yao haiongozwi na mtu mmoja aliyelundikiwa madaraka na kuyatumia vibaya.
Matokeo ya kuwa na mfumo mbovu ni kuwa na viongozi dhaifu serikali dhaifu na nchi hovyo! huo ni ukweli hata kama unauma. Hapa ndipo tulipokwama!
Nihitimishe hapa kwa kusema, tunahitaji katiba mpya na kwa tume iliyopo tumebofoa sana! Katiba inayotokana na sisi wananchi ingetuwezesha kupata wananchi wanaowajibika, bunge linalowajibika, serikali inayowajibika, vyombo huru vya sheria na dola. Hapo tungevunja uti wa mgongo wa genge linaloiumiza nchi. Tungeweka misingi ya utaifa na thamani za taifa ili kila achukuae dola ajue huo ndio muongozo kinyume chake ni out na sheria kuchukua mkondo wake.
Endapo tungefanikiwa kwa hilo basi tungeweza kukaa na kuamua mfumo gani tunaoona unafaa kwa mazingira yetu na wala si copy and paste ya Ubepari au Ujamaa.
Kisha basi, tungekaa na kuangalia ili twende mbele ni kipi tukipe kipaumbele na ni vipi tutumie rasilimali zetu kuwasadia wananchi wetu. Hapo ndipo tungejadili kuhusu Ujinga, maradhi na Umasikini. Tungejadili sekta ya afya, elimu, madini nk zinatusaidiaje kujikwamua.
Ninasikitika kusema kwa bahati mbaya fursa zote mbili tumeshindwa kuzitumia.
Bado tuna nafasi kidogo sana hata hivyo ya kuwa 'empower' wananchi wetu kuhusu tatizo halisi na si dalili.
Tuna nafasi ya kusema katiba inayotengenezwa si yetu ni ya Rais na CCM. Tunanafasi ya kuwaambia wapinzani (CDM) kitendo cha kukubali tume inayowajibika kwa Rais na CCM ni usaliti na warejee kwenye 'drawing board'.
Tuangalie tatizo na si dalili. Kuumwa kichwa na homa siyo tatizo la mgonjwa wa malaria, tatizo ni kuwa wadudu wa malaria wameshambulia mfumo wa kawaida wa mwili wa mwanadamu. Vivyo hivyo, kukwama kwetu kimaendeleo, umasikini, ujinga, maradhi, uporaji na wizi hayo siyo matatizo, tatizo letu ni mfumo mbaya wa utawala ulioshambulia mfumo wa nchi yetu. Suluhu ya kwanza ni kutengeneza mfumo mpya wa utawala kwa muongozo mpya unaotokana na sisi
Tusemezane
Nafasi ya kwanza ilikuwa kubadili muundo wa bunge kwa kuchgua watu wenye uchungu na nchi hii, watu wanaofikiri mtu anawezaje kuishi kwa dola moja.
Ni kwa kupitia bunge pengine tusingeona haya wanayoyafanya viongozi wa bunge hili.
Tumetoa nafasi kwa genge la wahuni kuendeleza mtandao wao wa kulindana ndani ya seikali, katika bunge, vyombo vya sheria na vyombo vya dola.
Laiti kama tungekuwa a bunge linaloweza kupiga kura ya hapana tusingeona bajeti ya vocha za simu za vijana wanaotongozana ikiwa ndiyo chanzo cha mapato. Tumewakabidhi CCM kwa hiari na kwa hila.
Nafasi ya pili ilikuwa ni pale dola ilipoelewa kuwa umma unataka mabadiliko, mabadiliko ya katiba ili tuwe na mfumo unaokidhi haja na matakwa yetu. Tukashangaa kuona wapinzani na wananchi wakikubali genge lile lile lifanye mabadiliko ya katiba. Hebu fikiri miaka 50 hawakutaka iweje leo watake?
Mimi binafsi nawalaumu sana viongozi wa vyama vya upinzani hasa CDM. Hakika walikuwa na 'mass support' ya wananchi kuhusu utengenezaji wa katiba mpya.
Sijui waliingia mkenge gani na kuruhusu mchakato huo uendelee tukijua dhahiri shahiri kuwa wale wasiotaka mabadiliko na waliotufikisha hapa hawawezi kutukwamua.
Nilionya sana na kusema tume ya katiba inayoundwa na Rais na Mwenyekiti wa CCM haiwezi kutupatia kitu mbadala, ni mazingaombwe tu ya kuchezehsa mikono ili tuamini kuwa karatasi imekuwa pesa.
Ni mazingaombwe kama alivyowahi kusema ndugu yangu Mzee Mwanakijiji.
Kuna watu wenye hoja kuwa katiba pekee haiwezi kuwa suluhisho. Mimi napingana nao kwasababu midhali tumeshindwa kulivunja genge hili la 'wahalifu' kwa njia nyingine ikiwemo sanduku la kura, hatuna sababu ya kupoteza miaka 10 zaidi tukisubiri maajabu. Tumeshapoteza miaka 50 kwanini tuendelee kupoteza mingine?
Mimibaba anasema muda si mshiriki mzuri kwetu na tumeshapoteza, kwanini tufikir kupoteza zaidi
Tanzania kwasasa hatuhitaji kufufua viwanda, kuendeleza kilimo, kuhubiri kuhusu nguvu kazi au matumizi ya rasilimali zetu. Hatuhitaji elimu wala uvuvi, madini au nishati. Vyote hivyo vimekwama kwasababu genge la wahalifu limeshika mpini na sisi tumeshika makali. Njia mojawapo ni kutumia nguvu ya umma ili tupate muongozo utakaondoa kimya kimya hili genge huku tukiijenga nchi.
Wizi na uporaji pamoja na uhuni mpya wa kuuana ulioanza kushika kasi siyo matatizo yetu ni dalili za tatizo letu ambalo ni kukosa mfumo utakaombana kila mmoja kuanzia yule Mwanakijiji anayeiba kuku, Waziri anayesaini mikataba ya wizi na mkuu anayetuamnisha kuwa 'huu ni upepeo tu' utapita.
Hivyo ndivyo China walivyoweza, ndivyo Japan wanavyofanya, na ndivyo Marekani wanavyoendelea.
Nchi yao haiongozwi na mtu mmoja aliyelundikiwa madaraka na kuyatumia vibaya.
Matokeo ya kuwa na mfumo mbovu ni kuwa na viongozi dhaifu serikali dhaifu na nchi hovyo! huo ni ukweli hata kama unauma. Hapa ndipo tulipokwama!
Nihitimishe hapa kwa kusema, tunahitaji katiba mpya na kwa tume iliyopo tumebofoa sana! Katiba inayotokana na sisi wananchi ingetuwezesha kupata wananchi wanaowajibika, bunge linalowajibika, serikali inayowajibika, vyombo huru vya sheria na dola. Hapo tungevunja uti wa mgongo wa genge linaloiumiza nchi. Tungeweka misingi ya utaifa na thamani za taifa ili kila achukuae dola ajue huo ndio muongozo kinyume chake ni out na sheria kuchukua mkondo wake.
Endapo tungefanikiwa kwa hilo basi tungeweza kukaa na kuamua mfumo gani tunaoona unafaa kwa mazingira yetu na wala si copy and paste ya Ubepari au Ujamaa.
Kisha basi, tungekaa na kuangalia ili twende mbele ni kipi tukipe kipaumbele na ni vipi tutumie rasilimali zetu kuwasadia wananchi wetu. Hapo ndipo tungejadili kuhusu Ujinga, maradhi na Umasikini. Tungejadili sekta ya afya, elimu, madini nk zinatusaidiaje kujikwamua.
Ninasikitika kusema kwa bahati mbaya fursa zote mbili tumeshindwa kuzitumia.
Bado tuna nafasi kidogo sana hata hivyo ya kuwa 'empower' wananchi wetu kuhusu tatizo halisi na si dalili.
Tuna nafasi ya kusema katiba inayotengenezwa si yetu ni ya Rais na CCM. Tunanafasi ya kuwaambia wapinzani (CDM) kitendo cha kukubali tume inayowajibika kwa Rais na CCM ni usaliti na warejee kwenye 'drawing board'.
Tuangalie tatizo na si dalili. Kuumwa kichwa na homa siyo tatizo la mgonjwa wa malaria, tatizo ni kuwa wadudu wa malaria wameshambulia mfumo wa kawaida wa mwili wa mwanadamu. Vivyo hivyo, kukwama kwetu kimaendeleo, umasikini, ujinga, maradhi, uporaji na wizi hayo siyo matatizo, tatizo letu ni mfumo mbaya wa utawala ulioshambulia mfumo wa nchi yetu. Suluhu ya kwanza ni kutengeneza mfumo mpya wa utawala kwa muongozo mpya unaotokana na sisi
Tusemezane