Mimibaba
JF-Expert Member
- Jul 1, 2009
- 4,557
- 1,294
Kwa hiyo hoja yangu baso ipo palepale, Uzalendo kwa viongozi na wananchi umepotea na hili linatugharimu sana iwe kwa Viongozi, Madaktari, walimu na hata mitaani kwa sababu hatuwandaa watu ktk misingi ya kibiashara. Kutoka Ujamaa kuingia Ubepari ni sawa na mtu alokwenda kuhbadilisha dini kutoka Uislaam kuingia Ukristu au kinyume lazima atakuwa na tafisri mbovu za faradhi za sunna za imani aloingia. Kwa hiyo nitaenbdelea kupinga mfumo huu wa Afya nchini na pengine nitasema Madkatri ni victims wa mfumo huu uloanzishwa na Mwinyi na Lowassa in 1992 and we are paying for that. the one
Nianze kuomba samahani kwa kuwa sijapitia thread zote, ila nitachangia kwa kutoa uzoefu wangu.
Ninachokiona ni viongozi kujaribu kukidhi matakwa ya kisiasa kwenye uendeshwaji wa serikali kitaalam. Ukidodosa kabla ya 1967 civil service chini ya Central establishment hapakuwepo tofauti ya mishahara kwa misingi ya taalum badala yake kigezo kilikuwa ni "qualifications and experience". Promotions zilikuwa scheduled. Lakini kilichokuwa wazi wakati huo lazima ukidhi na kujipambanua kwa ufanisi.
1972 nchi yetu ilikumbwa na ombwe la Mwongozo (Ambao in a nutshell uliondoa Technical Management based on evidence and delivery) ambao ulijenga dharau kwa baadhi ya taaluma. Lakini wakati huo huo ukasimika chama kushika hatamu na maamuzi ya kichama yaliyojitenga na utendaji wa kitaalamu (professional) pamoja na maamuzi yenye misingi ya mantiki kwa ajili kujikidhi uwezo duni na mdogo wa washika hatamu. (Mlinzi getini ambaye alikuwa mwenyekiti wa chama alikuwa na madaraka ya kuamua hatma ya taasisi zaidi ya Meneja (nimebana ieleweke ni mfano wa kweli). Maana yake hapo ilipandwa mbegu ya kuanza kubagua na kutoheshimu taaluma.
Kilichofuatia ni kusomeshwa na kulipwa kulingana masomo yako. Nakumbuka vizuri mimi binafsi 1972 nilipata scholarship ya Jeshi kwenda Canada kuwa Fighter Pilot. Kulingana na mahitaji ya nchi kwa walimu wa hisabati, nilichuliwa na FFU toka uwanja wa ndege na kupelekwa UD nikasomee ualimu wa hisabati. Nilipomaliza walimu wa hesabu tulikuwa tunalipwa mshahara wa juu kuliko mtu ye yote (Tshs 1400 1974/5). Yaani hata Mkuu wa Mkoa hakutufikia. Mwanzo wa ubaguzi huo.
1977 ikazaliwa CCM ndani ya misingi ya kibaguzi ya taaluma. Akaingia mdudu anaitwa "Rare Profession" pamoja na Registration za Professional Cadres zilizojibainisha na kujipambanua kuwa ni Rare Profession. Hapo zikauondoa msingi wote wa utumishi serikalini. Kwa mfano nina ushahidi kuwa kwa sasa kuna kada zinapaa kwa promotions pamoja na ngazi za mishahara kwa sababu wao wanaaccess ya mafaili ya maamuzi kwa hiyo kwao ni lazima wawe juu. Hoja hapa ni kuwa when the center can not hold things fall apart.
Kwa hoja namantiki ya uzoefu nilioutoa ona yafutayo:-
1. Mind set ya utumishi imebadirika kuwa rare professionalism yaani ubora wa kimimi kwa fani yangu. Swali mind set hii inarandana vipi na utumishi wa umma? Jibuni wenyewe
2. Wanasiasa wamefanikiwa kuonekana wao ndio watumishi wa umma wasiolala kwa vile wanafanya maamuzi yanayohusu mstakabali wa nchi kwa hiyo they are rarest professional lazima walipwe tofauti na wengine na hasa kwa vile wao ni waamuzi wa mwisho Swali kibinadamu matumizi ya msingi yanatofautiana? Kwa nini tutofautiane kwa kigezo ambacho si kazi bali nani ana nafasi gani ya kuamua juu ya mwingine? Hii inajidhihirisha na maumbile ya kibinadamu kutaka haki na usawa.
3. Kama vilivyo viungo vya mwanadamu hakuna kisicho na umuhimu. Hata vidole pamoja na utofauti wake vinaheshimiana wakati wa utendaji. Serikali hufanya kazi kama mwili wa mwanadamu kila kiungo kina umuhimu wake na mchango wake. Si msomi wa biolojia ila najua mahitaji ya kila kiungo cha mwanadamu yanakidhiwa sawa sawa vinginevyo kiungo kitakachopungukiwa kitasababisha mwili kuuma. Hoja na swali hapa maana halisi ya utumishi bado ipo? Na kila mtumishi anaielewa sawa sawa na mwenzake? Na watumikiwa nao wanaonaje kinachoendelea? Ni wazi kunahitaji ku redifine utumishi wa umma (naomba nieleweke utumishi wa umma ni regardless na utumishi wa serikali kwa maana ya delivery ya service kwa public)
Changamoto
Mwalimu ambaye ni daktari, injinia na kiongozi kwa taaluma zote hizo adai mshahara kiasi gani? Na mwananchi uelewa wake wa huduma za kiumma (afya, elimu, usafiri, biashara/uchumi) azilinganishe na fani na kuzigharamia kifani.
Hitimisho
Kuna kujiona fani fulani ni bora kuliko nyingine. Hili limejengeka kwa historia ya utawala wa nchi yetu. Pia kuna maamuzi yanayofanywa kisiasa kwenye masuala ya kitaalamu k.m. kuendesha serikali kama serikali ni taaluma na kama taaluma haitofautiani sana duniani. Tulichokosea ni kufanya na kuruhusu maamuzi bila kuzingatia mahitaji ya kitaalamu ambayo hayatofautiani kwa serikali makini dunia nzima. Tusisahau mtoto umleavyo ndivyo akuavyo
KWA VILE WATAWALA WAMELIKOROGA LAZIMA WALINYWE HATA KAMA CHUNGU mKWA KUFANYA MAAMUZI MAGUMU