Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,413
- 23,592
thedealer, hivi mtu mpaka uitwe mwanasiasa, unatakiwa utimize masharti gani? Unawatenganishaje watu wawili mpaka moja umwite mwanasiasa zaidi ya mwenziwe? Mathalani tuchukue mifano ya watu wawili humu, Nguruvi3 na thedealer...je yupo mwanasiasa kati yenu kuliko mwingine?
Ziko uthibitisho kwamba Donald Trump alianza kuutamani Urais wa Marekani toka miaka ya 1990s ingawa kwa sababu anazozijua yeye, alikuwa anasita kugombea. Je ana tofauti gani kwa mfano na Rais wa sasa wa Marekani Barack Obama ambaye aliamua ghafla bin vuu kugombea Urais miaka ya 2000s?
Je Barack Obama aliyeshindana na Hillary Clinton, yupi ungemweka katika kundi la establishment na iliwezekanaje kwa Obama kuwa mgombea mteule wa Democrats? Pamoja na hilo iliwezekanaje akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa Marekani dhidi ya mgombea wa establisment kutoka chama cha Republicans?
Swali langu la pili kwako ni hili, je kati ya Donald Trump na Hillary Clinton, yupi aliyepitia mashambulizi makali zaidi toka kwa wapinzani na vyombo vya habari kuliko mwingine kwa muda mrefu? Nadhani tofauti kubwa kati yao ni moja nalo ni namna walivyoweza kukabiliana na hayo mashambulizi yalipotolewa.
Je umefanya angalau utafiti kidogo kujua tofauti zao kimaisha toka wakati wakiwa vijana baada ya kumaliza shule na shughuli walizoshughulika nazo? Marekani kila mgombea hupitia tanuru la moto na haijalishi unatokea chama cha upinzani au chama tawala, watu watataka wajue maisha yako ya awali.
Vyombo vya habari hutumika sana katika kuwapasha wananchi wasiokufahamu vizuri, ulivyoendesha maisha yako kabla na wananchi wategemee nini ukipewa madaraka. Yako mambo mengi yatatendeka k.m. mijadala itatayarishwa, maoni yatatolewa, maswali yataulizwa, midahalo itaandaliwa na uchambuzi utatolewa.
Ukweli ni kwamba Donald Trump anawakilisha kundi la Wamarekani wenye chuki dhidi ya watu wanawaona kama si wenzao. Donald Trump ameamsha hisia hatari za wabaguzi ambao hawana nafasi Marekani katika dunia ya leo na tofauti na wewe, naamini hata ikitokea miujiza akashinda Urais hawezi kumaliza kipindi chake.
Ziko uthibitisho kwamba Donald Trump alianza kuutamani Urais wa Marekani toka miaka ya 1990s ingawa kwa sababu anazozijua yeye, alikuwa anasita kugombea. Je ana tofauti gani kwa mfano na Rais wa sasa wa Marekani Barack Obama ambaye aliamua ghafla bin vuu kugombea Urais miaka ya 2000s?
Je Barack Obama aliyeshindana na Hillary Clinton, yupi ungemweka katika kundi la establishment na iliwezekanaje kwa Obama kuwa mgombea mteule wa Democrats? Pamoja na hilo iliwezekanaje akashinda uchaguzi na kuwa Rais wa Marekani dhidi ya mgombea wa establisment kutoka chama cha Republicans?
Swali langu la pili kwako ni hili, je kati ya Donald Trump na Hillary Clinton, yupi aliyepitia mashambulizi makali zaidi toka kwa wapinzani na vyombo vya habari kuliko mwingine kwa muda mrefu? Nadhani tofauti kubwa kati yao ni moja nalo ni namna walivyoweza kukabiliana na hayo mashambulizi yalipotolewa.
Je umefanya angalau utafiti kidogo kujua tofauti zao kimaisha toka wakati wakiwa vijana baada ya kumaliza shule na shughuli walizoshughulika nazo? Marekani kila mgombea hupitia tanuru la moto na haijalishi unatokea chama cha upinzani au chama tawala, watu watataka wajue maisha yako ya awali.
Vyombo vya habari hutumika sana katika kuwapasha wananchi wasiokufahamu vizuri, ulivyoendesha maisha yako kabla na wananchi wategemee nini ukipewa madaraka. Yako mambo mengi yatatendeka k.m. mijadala itatayarishwa, maoni yatatolewa, maswali yataulizwa, midahalo itaandaliwa na uchambuzi utatolewa.
Ukweli ni kwamba Donald Trump anawakilisha kundi la Wamarekani wenye chuki dhidi ya watu wanawaona kama si wenzao. Donald Trump ameamsha hisia hatari za wabaguzi ambao hawana nafasi Marekani katika dunia ya leo na tofauti na wewe, naamini hata ikitokea miujiza akashinda Urais hawezi kumaliza kipindi chake.