Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

DEMOKRASIA GANI YA 'WAJUMBE' NA SI WAPIGA KURA?

Kabla ya kuiangalia ramani, ni vema tukazungumzia hoja nyepesi inayokuzwa bila sababu

Wapo wanaohoji mtindo wa Marekani ambapo Rais anachaguliwa kupitia wajumbe, na kwamba anaweza kupatikana hata akiwa na kura chache, kuna demokrasia ya kweli?

Swali hilo liliulizwa Wabunge wa conservative Uingereza walipomchagua mrithi wa Cameron bila wananchi kupiga kura. Wapo wanaohoji iweje Malkia awe mkuu wa nchi bila kuchaguliwa? Je, ni demokrasia ya kweli ? Na je wana haki ya 'kuzogoa' wengine?

Majibu ya maswali haya yapo sehemu moja.
Kwamba, demokrasia haiishii katika uchaguzi bali uchaguzi ni sehemu tu ya demokrasia.

Demokrasia ni makubaliano ya kujiendesha, kwa kupanga, kuchagua na kutenda
Demokrasia zinatofautiana, muhimu ni kuwa ili demokrasia ifanye kazi , makubaliano ya jamii husika yanapaswa kutimizwa

Kwa utaratibu wa Marekani, kuanzia mchujo wa wagombea hadi Urais wananchi wanashiriki. Tofauti ni kuwa, ushiriki wao si wa moja kwa moja kama wa wetu

Kwa asiyejitokeza kupiga kura chaguzi za awali (primaries and caucus) na asiyejitokeza kuchagua wajumbe 'electoral college' hatakuwa amemchagua Rais na hilo ni tatizo lake

Ndivyo Uingereza ilivyokubaliana Malkia ni mkuu wa nchi, waziri mkuu ni kiongozi wa serikali anayepewa ridhaa na wananchi.

Tukihoji demokrasia za US na UK zilikomaa, tusiache kujiuliza, iweje makamu wa Rais atoke Zanzibar kwa sababu tu ya uzanzibar ikiwa sisi ni Taifa moja?

Iweje asitoke eneo jingine kubwa kiuchumi na idadi kubwa ya wananchi?

Well, tulikubaliana kiongozi akitoka upande mmoja, makamu anatoka upande wa pili.

Hiyo ndiyo sehemu ya demokrasia yetu, hakuna anayehoji utaratibu huo na atakayehoji atakuwa ametuingilia kwa kiasi na kasi kubwa.

Inapotokea mambo kinyume na makubaliano yetu wenyewe, ndipo wenzetu wanahoji, mbona tunakwenda kinyume na makubaliano yetu?

Kwa mfano, tumekubaliana taratibu za chaguzi zetu ambazo kwa viwango vyetu ndiyo demokrasia tuliyo afiki. Inakuwaje yanatokea kama yale ya kufuta uchaguzi mzima ambayo hayapo katika makubaliano yetu?

Inakuwaje tumeunda vyombo kama msajili wa vyama ili kuratibu shughuli za kisiasa, kinyume chake jukumu hilo linageuka kuwa la mtu au upande chama kimoja?

Tumekubaliana kwa demokrasia yetu matatizo ya vyama vya siasa yana mlezi msajili wa vyama,mbona haonekani kuchukua jukumu lake hili la mikutano kupigwa marufuku?

Jukumu la msajili si kutoa vibali bali kufafanua sharia alizokabidhiwa kama zinawiana na hali iliyopo. Vipi amekaa kimya kana kwamba kila jambo ni shwari?

Mivutano hii ya kisiasa tunatatuaje ikiwa hatuheshimu makubaliano yetu ya uendeshaji wa siasa zetu nchini?

Ni kwa mtazamo huo, kuhojia demokrasia zilizokomaa kama za Marekani au Uingereza ni suala lisilo na mashiko.

Pengine kabla ya kulalamika kuhusu kuingiliwa na nchi za magharibi, ni vema tukajiuliza, je tunatenda tulichokubaliana kama sehemu ya demokrasia yetu!

Tusemezane
 
2016_08_04_pres.png

MAGIC NUMBER 270

Viti 270 humwezesha mgombea kuwa Rais wa Marekani. Hizo namba katika majimbo (state) ndizo electoral college. Idadi yake ni 538, nusu yake ni 269 na anayevuka hapo 270 ndiye Rais

Wajumbe hao hupiga kura jumatatu ya kwanza baada ya Jumatano ya pili ya mwezi December.
Hiyo ni kukamilisha taratibu kwani mwenye wajumbe 270+ atapigiwa kura na wajumbe wake

Ukiangalia ramani utaona maelezo hapo chini

1. Safe D au Safe R:
Hiyo inaeleza kuwa ima Democrat au Republican wapo salama katika maeneo yalioonyeshwa kwa rangi za Blue au Nyekundu. Usalama ni kuwa tangu Enzi dahari yanapigia chama Fulani kura

Ni kama vile utakaposema Dodoma ni safe kwa CCM, Arusha ni safe kwa Chadema na Pemba ni safe kwa CUF.

2. Likely D au Likely R:
Maana yake, majimbo hayo yana asilimia kubwa za kuegemea chama Fulani

3. Lean D au Lean R:
Maana yake kwa wakati husika, majimbo yanaegemea ima Dem au GOP
Haya ndiyo yanayobadilka badilika kila mara na huitwa 'swing states' kwa maana yanayumba

4. Halafu kuna Toss up katikati
Inapotokea hakuna ushahidi wa wazi nani atashinda Likely au Lean, jimbo husika huitwa Toss up kwa maana kuwa ni 'sadakalawe' mwenye kupata.. mwenye kukosa....

Wagombea hutumia mgawanyiko huo katika kampeni kwa maana mbili kuu
a) Kuelekeza nguvu za kampeni kwa ushawishi unaoweza kuleta matunda.

Itshangaza kama Clinton ataelekeza nguvu zake Texas( TX) ambako ni 'solid Red' au Trump kuelekeza nguvu za ushawishi California (CA) ambako ni 'solid Blue'

b)Kujua waelekeze rasimali wapi katika mikutano na kampeni kwa ujumla kama kulipa wahusika kwa maana hiyo hiyo ya (a) hapo juu

c) Kujua wapi kuna idadi ya wajumbe wengi kati ya hizo Likely na Lean.
Kwa mfano, kama Colarado (CO) ina wajumbe 9 na Arizona (AZ) ina wajumbe 28.

Kwavile ni Likely au Lean ni vema kwa wagombea kuelekeza nguvu Arizona ima kulinda (GOP) au kushambulia (Dem) kwakuwa idadi yake ya 28 inaweza ku off set ya wajumbe 9 Colorado

Ramani hiyo inaonyesha pia kwanini mgombea anaweza kuwa na popular vote kubwa na asiye Rais

Tutafafanua
 
RAMANI NA 'POPULAR VOTE'

Rejea ramani hapo juu. Ukiitazama kwa namba zilizopo utaona kwanini mgombea anaweza kushinda popular vote na bado asiwe Rais wa Marekani

Kwa mfano, mgombea X akishinda majimbo yafuatayo kwa asilimia zote ya popular vote
Idaho (ID- 4
Montana (MT)- 3
North Dakota-3
South Dakota-3
Wayomin-3
New England-5
Kansas- 6

Mgombe X atakuwa amaeshinda majimbo 7 na kuoata viti 27

Mgombea Y akishinda kwa asilimia 55 tu ya popular vote katika jimbo la Florida atakuwa amepata viti 29. Yaani jimbo moja limebeba viti vingi kuliko majimbo 7

Kwa kampeni ya Clinton kuliko kutumia muda na rasilimali kwa majimbo 7 ambayo ni Red states ni afadhali atumie rasilimali hizo na muda Florida tu

Ukichukua population ya majimbo 7 mgombea anaweza kuwa na kura nyingi sana, lakini ana viti 2 pungufu na mgombea Y aliyeshinda Florida tu.

Ndivyo ambavyo Trump hatatumia muda na rasilimali zake Illinoi akijua ni blue state.

Hata hivyo, utawaona wote Trump na Clinton wakizunguka sana maeneo yafuatayo

Nevada- Wajumbe 6
Colorado-9
Indiana-6
New Hampshire-4
Florida-29
North Carolina
Ohio- 18
Pennsylvania-20
Arizona-11
Michigan-16
Minnesota-10
Wisconsin-10
Georgia -16
Missouri-10
Virginia -13

Sababu za kuzungukia maeneo haya ni kama tulizosema. Ni majimbo Likely au Lean to Dem au Rep. Kwa maana,kuna uwezekano wa kushinda, kuyatupa ni kujinyima nafasi

Pamoja na hayo bado kuna mchujo wa majimbo hayo hapo juu.
Kwa mfano, atakayeshinda Ohio (18) na Florida (29) atakuwa na wajumbe 47 wengi kuliko Nevada(6), Colarado(9), Indiana(6), New Hampshire(4) na Arizona(11) Wisconsin(10) kwa pamoja jumla ya 46

Hii ndiyo sababu utawasikia wagombea wakizunguka Ohio, Florida, Pennsylvania, ni eneo dogo la kuwekeza rasilimali lenye malipo makubwa kwa idadi ya wajumbe.

Pia kuna mchezo wa saikolojia unaotumika. Arizona imechukuliwa na George Bush kabla ya Obama.Kiuasili ni jimbo la Republican

Kutokana na sera za Trump dhidi ya wahamiji , jimbo hilo lenye Walatino wengi linabaki kuwa battle ground. Kwa hali ilivyo lina lean kwa Republican

Hapa Clinton ana shot kwa maana anaweza kuchukua ushindi.
Kisaikolojia hiyo itaudhi Republican na hivyo Trump ataelekeza nguvu kulinda jimbo lao. Hapo ataondoa focus na rasilimali Florida, Ohio na Pennsylvania n.k. na kupunguza nguvu ya ushindani

Tutaendelea kuiangalia ramani

Tusemezane
 
WIKI HII KATIKA UCHAGUZI

Awali, tutoe ufafanuzi wa ramani inayoonekan hapo juu.
Namba zinazoonekana ndani ya state ndizo electoral college vote.

Namba zinazoonekana chini (Dem 347) na (Rep 191) zinatokana na tathmini iliyofanywa na UVA na inaweza kubadilika

Tumeeleza haya kwasababu kama magic number ni 270, basi Dem wangeshashinda kwa 347!!!

Katika uhalisia kuelekea uchaguzi Dem huanza na mtaji wa viti 206 na Democrat 191
Ili kufikia 270 mpambano huwa katika hizo 'Likely or Lean'

Utasikia wachambuzi wakisema 'battleground states' au Key state

Kwanini tunazungumzia 'mtaji'
Kwa minajili ya mjadala 'assume' kuwa mtaji wa Dem ni 202 tukuiondoa viti 4 vya New Hampshire.

Kama Dem watashinda Ohio, Florida na Pennsylvania idadi ya viti ni 69
202+ 69= 271 ambayo ni kubwa ya magic number 270

Na vivyo hivyo, tuki assume Trump atashinda New Hampshire, Arizona , Florida, Penny, Florida na Colorado, jumla itakuwa 284 kubwa kuliko 270 ambayo ni magic number

Kwa maana hiyo, hizi battleground states zinaamua nani anafika katika mstari wa mwisho

Wiki hii
Kwa upande wa Dem Hillary Clinton amekiri kuwa 'short circuited ' kwa kuwa na emails mbili
Hii ni katika jitihada ya kumaliza makali ya emails ambayo ynaharibu taswira yake kwa umakini

Ni damage control yenye gharama kwani Trump aliikomalia baada ya wiki nizto wiki iliyopita

Hata hivyo Democrats walifanya timing, kwani wakati Clinton anaongelea hilo, takwimu za ajira zikatoka zikionyesha ajiranzilizotengenezwa ni 250K kinyume na mataraji ya 177K

Mjadala ukawa huo huku masoko ya mitaj, S&P, NASDAQ na DOW JONES yakifika rekodi za juu
Namba za ajira zimesaidia sana, huku bei ya mafuta ikiwa nzuri kwa watumiaji tofauti na miaka mingine hasa wakati huu wa summer

Leo Trump alikuwa anazindua mpango wa sera ya uchumi. Clinton naye anatarajiwa kuzindua mpango wake hapo hapo Detroit.

Hata hivyo hali imebadilika kwa Trump baada ya 50 GOP security expertise walipotoa waraka kuonyesha Trump si wa kuaminiwa nkupewa katika suala la usalama

Hawa 'expertise' ni walioshiriki serikali za Republican zilizopita katika nafasi ya ulinzi na usalama

Kauli hii inamwagia mafuata ile inayoendelea 'Tempartment ya Trump si nzuri kukabidhiwa nuclear code'

Kauli hii inaonekana kumuumiza sana Trump, kwani pamoja na kuaminika kiusalama kma GOP, kwa US suala la nuclear code ni kama ufunguo wa dunia.

Tusemzane
 
Wakati tunaendelea kukufuatilia...juu ya magic numbers na 'security experts' kumruka Trump. Mimi nachomekea vibwagizo vya Bibi Clinton na sintofahamu ya DNC kumbeba Bibi Clinton.
==========
Huyu Bibi Clinton ataaminikaje kwa kutisha na kuzusha mambo kwa kisingizio cha histoaria...!? Ona alivyomtisha wakati wa kampeini. Ona inavyodhaniwa DNC staffers walivyo kwenye hali tete. Fuatilia link.

1.Clinton akimtisha Obama:
=
=That time in 2008 when Hillary Clinton said Obama might be assassinated (VIDEO)

2. DNC saga:
The whistleblowing organization Wikileaks wants to catch those responsible for the murder of Democratic National Committee (DNC) staffer Seth Rich and are now offering a $20,000 reward for information.
The group’s co-founder Julian Assange suggested on Dutch television that if Rich is the source of the 20,000 emails exposing the party’s sabotage of the Bernie Sanders campaign in favor of Hillary Clinton, he may have been killed over it.

However, when asked if Rich was a Wikileaks source, Assange refused to comment, merely saying they were investigating the circumstances surrounding his murder.
Wikileaks offers $20k reward over dead DNC staffer, but won’t confirm he leaked emails
 
Wakati tunsendelea kukufuatilia...juu ya magic numbers na 'security experts' kumruka Trump. Mimi nachomekea vibwagizo vya Bibi Clinton na sintofahamu ya DNC kumbeba Bibi Clinton.
Wikileaks offers $20k reward over dead DNC staffer, but won’t confirm he leaked emails
TUJITEGEMEE, nakubaliana kabisa na wewe kwani una haki kabisa ya kuamini unachoamini ila najiuliza swali moja tu ...$20k ni dola 20,000.00 tu...is Wikileaks serious? Surely this is a joke! Najua jinsi wapinzani wa Clinton walivyo tayari kumshambulia na kwa msingi huo wanaweza wakatoa kiasi chochote kupata habari kama hii, sasa mbona $20,000 ni kiasi kidogo sana?

Donald alivyo anxious kupata info kama hizi, kwa nini Asange atoe tu hizo hela kiduchu, kama kweli kifo cha Seth Rich kinahusishwa na DNC? Nani atahatarisha maisha yake kwa hela ndogo kama hiyo? Si afadhali ingekuwa $20,000,000 sawa na asilimia 0.05% tu ya hazina ya Trump?
 
......

Donald alivyo anxious kupata info kama hizi, kwa nini Asange atoe tu hizo hela kiduchu, kama kweli kifo cha Seth Rich kinahusishwa na DNC? Nani atahatarisha maisha yake kwa hela ndogo kama hiyo? Si afadhali ingekuwa $20,000,000 sawa na asilimia 0.05% tu ya hazina ya Trump?
Sawa Mkuu..ni kweli ela hazitoshi. lakini Wikileaks haifanyi biashara inategemea sana donation kutoka kwa wasomaji wake. bahati mbaya sana wachangiaji wake kwenye hiyo donation waliminywa sana hasa baada ya kutoa taarifa za ukatili wa majeshi ya uvamizi nchini Iraq. Hivyo Assange hana fedha za kutosha kutoa dau nono.

US wanaelekea kui'pin' Russia badala ya Wikileaks kwa udukuzi wa DNC.
Washington considers sanctioning Moscow over DNC email leak - report


Kizungumkuti cha kubebwa H.Clinton na vyombo vya habari kina endelea. CNN sasa wanakanusha kila analolisema Trump. Lakini hao hao CNN hawakanushi wasemalo wale team H.Clinton (mfano wana muita Trump 'unfit' for the US presidential post). Sisi hapa nyumbani magazeti yetu na redio hata na TV tunazilaumu sana kuwa haziko 'impartial' wakati wa kampeni.

CNN called out for (incorrect) onscreen ‘fact check’ of Trump’s claim Obama founded ISIS

Pia amefanikiwa kutotiwa hatiani mara tano (H. Clinton). Lakini kwetu hapa tunalalamikiwa (na hao hao US pamoja baadhi ya wanaharakati wetu hapa nyumbani na hata waandishi nguli nchini - Generali so to speak) kuwa watanzania tunawapa furusa za kugombea na kushinda na kisha kuwapa madaraka baadhi ya viongozi watuhumiwa wa 'ufisadi'. Na wanasema hii ni kufifisha demokrasia na utawara bora wa sheria. Sasa huyu Mama amewezaje kuruka viunzi hivi katika utawala bora uliotukuka wa US ? Ni huyu mama anayetuhumiwa kuwa extremely 'careless' (inasemekana ilidhibitika hivyo) katika kuhifadhi 'nyaraka' za nchi, uwenda akakabidhiwa 'Nuke Code'

5 times when the Clintons escaped federal charges

Hillary's Great Escape: FBI Email Scandal Dismissal
FBI: No evidence Clinton sought to violate laws in email case | News | DW.COM | 05.07.2016
 
Mkuu jitegemee
Nadhani unawatuhumu CNN kwa kuripoti habari na kuzifanyia mjadala

Kuwa 'unfit' si neno baya kwa kiswahili ,hafai, na siyo CNN waliosema bali Kampeni ya Clinton. Hivi majuzi GOP security experts wamerudia kauli hiyo

Kama ambavyo Trump anamwita HC 'crooked' au Obama 'stupid'

Tazama vyombo vya habari vya wenzetu kisha ulinganishe na vyetu utaona ipo tofauti. Kuwalaumu CNN si sawa

Ukiangalia kwa undani, HC amekuwa katika media kwa kiasi kikubwa sana kiasi kwamba habari zake zingine zinajirudia. Tofauti na Trump yeye anajaribu ku minimize asiendelee kuwepo katika media katika hali ya utata

Matahalanim ukiacha suala la emails linalojirudia rudia kwake, wiki nzima hajasema neno tofauti. Trump katika wiki hii tu kazua utata mara 2

1. Kusema ' ....may be 2nd amendment people,there is' ilileta utata mkubwa kuwa anachochoe mauaji. US ina matukio mengi sana ya marasi kuuawa. Hivyo, habari kama hiyo ni habari kubwa

2. Kwamba aliyeasisi ISIS ni Obama.
Hata alipotakiwa arudi mstarini na mwandishi wa conservative, alikataa.

Sasa ukiangalia mantiki yake inaweza kuwa haina tatizo, kauli yake ina tatizo

Kama tulivyowahi kusema, Trump ndiye analisha vyombo vya habari 'news'

Kuhusu HC kuruka viunzi, tuelewe sheria zinasemaje hapa.

Mfano, Trump amehojiwa na secret service kuhusu 'second ammendment' hakushtakiwa. Kwa wenzetu haijalishi how many times utakuwa accused, muhimu ni je,umekuwa convicted?

Ndio utata wa OJ Simpson wa mara ya kwanza.
Juzi, askari waliomuua Freddie wameachiwa huru.

Ukifanya ulinganifu na mauza uza yetu utakuwa unakosea.

Vetting system yao inaacha kila kitu wazi. Je, sisi si level hiyo ikiwa hata bunge limezuiliwa kutaja baadhi ya maneno kama nyumba za serikali?

Tupo miaka 150 na wenzetu, tusijaribu kufananisha chungwa na jiwe
 
Mkuu TUJITEGEMEE, ninaposoma post zako kuhusu uchaguzi Marekani nabaki nacheka tu kwa sababu ni wazi kuwa unatazama huo uchaguzi kwa macho na akili za kibongo. Umeamua kujiaminisha kuwa yanayowezekana kufanyika hapa Tanzania yaweza kufanyika hivyo hivyo Marekani na umejaribu sana tu kulinganisha siasa za Marekani na za dunia ya tatu. Nadhani hapa unakosea sana na hivyo naomba ufungue macho, uutazame uchaguzi wa Marekani kwa jicho lisilo na tongo tongo za Kibongo.

Uchaguzi wa marekani mwaka huu umeweka historia ambayo haikuwahi kushuhudiwa huko nyuma na yote ni kwa sababu ya mgombea moja anayeitwa Donald Trump. Hakuna hata siku moja mgombea wa Urais Marekani aliwahi kupewa mteremko na vyombo vya habari kama Donald Trump alivyobebwa katika uchaguzi huu. Wakati wagombea wenzake wanatumia mamilioni kujitangaza yeye lolote alilotamka na chochote alichofanya, vyombo vya habari vilimpa kipaumbele cha bwerere.

Mpaka sasa watu wanajiuliza ni kitu gani kilifanya vyombo vya habari vya Marekani kumpa free ride Donald Trump na kuripoti matamshi yake bila kuhoji. Lakini sasa vyombo vya habari vinapoanza kuhoji uropokaji wake, ukurupukaji wake, uongo wake, utapeli wake...anaanza kulalama. Donald Trump, kama ingekuwa uwezo wake, angevifungia vyombo vyote vya habari na kuwakamata wapinzani wake wote wanaomkosoa na kuhoji uwezo wake na temperament yake kama mgombea Urais.

Donald Trump alilikoroga na sasa itabidi alinywe...alikuwa anafurahi sana anapokuwa habari wakati anapewa sifa na sasa lazima avumilie anapokuwa habari anapokosolewa, hiyo ndiyo siasa ya Marekani. TUJITEGEMEE, naoma pia unasahau kuwa ni yeye anasababisha hali hiyo kwani kila wakati vyombo vinataka kuwaandama wapinzani wake, anashindwa kukaa kimya kuwapa nafasi. Badala yake huzusha jambo ambalo hulazimisha attention kuhamia kwake kwa kutoa matamshi ya hovyo ya kukurupuka.
 
Donald Trump alilikoroga na sasa itabidi alinywe...alikuwa anafurahi sana anapokuwa habari wakati anapewa sifa na sasa lazima avumilie anapokuwa habari anapokosolewa, hiyo ndiyo siasa ya Marekani. TUJITEGEMEE, naoma pia unasahau kuwa ni yeye anasababisha hali hiyo kwani kila wakati vyombo vinataka kuwaandama wapinzani wake, anashindwa kukaa kimya kuwapa nafasi. Badala yake huzusha jambo ambalo hulazimisha attention kuhamia kwake kwa kutoa matamshi ya hovyo ya kukurupuka.
Na alidhani primaries au caucus ni sawa na uchaguzi mkuu. Hapo standard inabadilika

Kwa hili la kuzusha mambo, wiki iliyopita angelikuwa mtulivu suala emails lilirudi kwa kasi likichagizwa na GOP.
Nani amelifunika! ni Trump kwa kauli zake mwenyewe

Huwezi kulinganisha emails za watu na tishio la kuua 'Rais' au mgombea

Jitegemee atambue, Rais wa Marekani ni wa 'Dunia' kwa nguvu ilizo nazo

Marekani imeshuhudia mauaji makubwa ya Marais wao, hivyo tishio lolote linabeba uzito kuliko habari nyingine. Nani anazua hayo, ni Trump
 
Na alidhani primaries au caucus ni sawa na uchaguzi mkuu. Hapo standard inabadilika

Kwa hili la kuzusha mambo, wiki iliyopita angelikuwa mtulivu suala emails lilirudi kwa kasi likichagizwa na GOP.
Nani amelifunika! ni Trump kwa kauli zake mwenyewe

Huwezi kulinganisha emails za watu na tishio la kuua 'Rais' au mgombea

Jitegemee atambue, Rais wa Marekani ni wa 'Dunia' kwa nguvu ilizo nazo

Marekani imeshuhudia mauaji makubwa ya Marais wao, hivyo tishio lolote linabeba uzito kuliko habari nyingine. Nani anazua hayo, ni Trump
Trump sasa hivi amejenga uadui si na Democrats tu bali na Republicans waliochoka na matamshi yake ya kipuuzi na pia vyombo vya habari vilivyochoka kutetea ujinga wake. Hata watoto wake wa kiume ni muda sasa waliamua kukaa mbali naye, wawili wakichukua likizo kwenda kuwinda. Binti yake Ivanka aliyem-introduce kwanye Convention naye kaamua kukaa mbali na vyombo vya habari.

Si hivyo tu viongozi wa GOP 75 wameamua kumwandikia barua mwenyekiti wa chama wakitaka pesa za kampeni zielekezwe zaidi kwa wagombea wa Congress badala ya kuzipoteza kwa mwenda wazimu Trump. Leo kuna mkutano mkubwa kati ya viongozi wa GOP na watu wake ambao unaweza kuamua hatma yake. Tetesi ni kwamba kuna hofu ya Donald Trump kujitoa katika kugombea.
 
Nimekutana na hii pahala...

X: I think it would be safe to say that Donald Trump is the greatest asshole in American history.
Y: Not quite...assholes are generally aware that their shit stinks. Trump on the other hand...
Z: Trump is fast food for fools.

Ha ha haaa...!
 
Tatizo Trump anafikiri style ile ile ya uropokaji ovyo iliompa ushindi kwenye caucus dhidi ya kina Ted Cruz, Jeb Bush basi itafanya kazi mpaka sasa kumbe mambo yamekuwa ni kinyume. Huyu bwana hana breki ya mdomo kabisa chochote kinachomjia kichwani anaropoka tu. Republicans wamekuja kushituka too late kwamba huyu jamaa ni janga na anahatarisha kukizamisha chama chote kwenye matope.
 
Tatizo Trump anafikiri style ile ile ya uropokaji ovyo iliompa ushindi kwenye caucus dhidi ya kina Ted Cruz, Jeb Bush basi itafanya kazi mpaka sasa kumbe mambo yamekuwa ni kinyume. Huyu bwana hana breki ya mdomo kabisa chochote kinachomjia kichwani anaropoka tu. Republicans wamekuja kushituka too late kwamba huyu jamaa ni janga na anahatarisha kukizamisha chama chote kwenye matope.
Wakati wa chaguzi za awali, Trump alipata 'shield' ya wagombea wengine 16.

Kwamba, kusema chochote hakukuathiri taswira yake. Kwasasa wamebaki wawili na mmoja lazima awe Rais.

Kinachoangaliwa ni sera, hakuna 'shield' . Fyongo zinaonekana wazi kwa Wagombea.

Kilichomsaidia kushinda kama tulivyowahi kujadili ni kundi lake ambalo lipo naye 100%.

Wagombea wengine walikuwa wanagawana wapiga kura.

Mwishoni ilionekana wazi John Kasich alikuwa sahihi kubeba bendera.

Chaguo jingine ni Marco Rubio ambaye kama angezingatia domestic policy badala ya kumshambulia Obama kwa siasa za nje, na kujikita na siasa za Israel angekuwa mbali

Rubio alijua Jumuiya ya Waisrael Marekani ingemsaidia sana kwa influence yake.

Akajisahau kuzungumzia agenda zinazogusa wananchi. Hilo lilikuwa kosa

Ted Cruz alikuwa chaguo badala ya kuona Trump atakuwa mgombea.

Kiuhalisia hakuwa chaguo la GOP kwasababu ya mikwaruzano Capitol hill na wazee.
Hata hivyo, alionekana kunyooka ikitokea kuliko ilivyokuwa kwa Trump

GOP walipoteza kadi kubwa sana kwa John Kasich. Leo hadithi ingekuwa tofauti sana

Republican walitambua udhaifu wa Trump. Kwa bahati nzuri au mbaya, demokrasia ya wenzetu inaacha wananchi wafanye maamuzi.

Hata yalipoibuka makundi ya 'Never Trump' na lile la Mitt Romney bado demokrasia ilitoa nafasi kwa aliyepewa mamlaka na wananchi, Trump

Ukitaka kuona jinsi GOP walivyoshtuka mapema, ni pale walipofanya 'coalition' ya John Kasich na Ted Cruz. Illikuwa move ' engineered' na GOP kumzuia Trump technically.

Tunarudi pale pale demokrasia iliyokamaa haikutoa nafasi, Trump akawa mgombea

Pili, kususia mkutano mkuu ilikuwa dalili njema kuwa GOP hawakukubaliana na Trump

Siyo suala la 'the establishment' , ilikuwa wazi Trump hakuweza kutetea hoja au kuzifungamanisha na sera za GOP. Kauli zilitia shaka hasa ugomvi na makundi ya jamii

GOP walimpa benefit of doubt, kadri muda unavyosonga mbele uvumilivu unawatoka.

Baadhi wameanza kuondoa 'endorsement' zao na wengine kumpinga wazi wazi kama kundi la security experts 50 waliosema Trump hafai katika suala zima la ulinzi na usalama

Baada ya tamko la hao experts kura za maoni zinaonyesha pengo kati yake na Hillary

RNC chair, Reince amezungumzia kuelekeza pesa chaguzi za congress na senate
Wanatambua kwa mwendo wa Trump labda litokee jingine lisilotarajiwa, hali ni tete sana.

Hofu ya GOP ni kuunganishwa kwa message au fyongo za Trump na uchaguzi wa maseneta na wabunge (congress).

Wana wasi wasi uwezekano wa kupoteza seneti na congress unazidi kuongezeka.

Njia nyepesi ni 'kutosa' mzigo baharini meli iendelee na safari
 
TRUMP ABADILI 'MENEJA'

LOISIANA NI TATIZO KWA DEM

Trump amebadili manager wa kampeni Bw Manifort.
Huyu alimrithi Lawandowiski aliyeenguliwa pia.

Ingawa Manifort kajiuzulu, ni wazi kampeni 'shake up' imemlazimu

Katika wiki hii, Trump amebadilika kikauli.
Ukilinganishwa na siku takribani 27 za dhoruba, inaonekana tofauti kubwa

Trump anaongelea sera na hata kuomba radhi kwa baadhi ya matamshi

Hili linakuja wakati kura nyingi za maoni zikionyesha kuelemewa, si katika battleground states tu bali red states kama Utah, Arizona na Colarado

Kuna nyakati GOP walimtaka Trump amwachie Pence kama mwenendo wa kampeni hautabadilika. Mabadiliko hayo yanafuatia shinikizo hilo.

DEM NA LOUISINA

Kumetokea mafuriko makubwa na kuua watu trakribani 12 Louisiana.
Haya ni kumbu kumbu ya Katrina ya miaka ya nyuma

Katrina ilikuwa doa kubwa kwa Bush aliyechelewa kuwafikia wananchi

Obama ingawa ametoa maelekezo ikiwa ni pamoja na kutangaza hali ya hatari na kuwasiliana na FEMA(kitengo cha maafa) mara kwa mara, akiwa mapunzikoni Martha Vineyard, hainekani kama inajibu haja

Gazeti maarufu Louisiana katika tahiriri limesema ni wakati Obama aende kuona madhara mwenyewe.

Wakati huo huo Trump na Pence wanaelekea Lousiana

Hili la Louisiana ni la Obama, hata hivyo akiwa Democrat litaleta tabu sana kwa kampeni ya Clinton. Kwanini hakujifunza kutoka kwa Bush na Katrina?

Tusemezane
 
TRUMP ABADILI 'MENEJA'

LOISIANA NI TATIZO KWA DEM

Trump amebadili manager wa kampeni Bw Manifort.
Huyu alimrithi Lawandowiski aliyeenguliwa pia.

Ingawa Manifort kajiuzulu, ni wazi kampeni 'shake up' imemlazimu

Katika wiki hii, Trump amebadilika kikauli.
Ukilinganishwa na siku takribani 27 za dhoruba, inaonekana tofauti kubwa

Trump anaongelea sera na hata kuomba radhi kwa baadhi ya matamshi

Hili linakuja wakati kura nyingi za maoni zikionyesha kuelemewa, si katika battleground states tu bali red states kama Utah, Arizona na Colarado

Kuna nyakati GOP walimtaka Trump amwachie Pence kama mwenendo wa kampeni hautabadilika. Mabadiliko hayo yanafuatia shinikizo hilo.

DEM NA LOUISINA

Kumetokea mafuriko makubwa na kuua watu trakribani 12 Louisiana.
Haya ni kumbu kumbu ya Katrina ya miaka ya nyuma

Katrina ilikuwa doa kubwa kwa Bush aliyechelewa kuwafikia wananchi

Obama ingawa ametoa maelekezo ikiwa ni pamoja na kutangaza hali ya hatari na kuwasiliana na FEMA(kitengo cha maafa) mara kwa mara, akiwa mapunzikoni Martha Vineyard, hainekani kama inajibu haja

Gazeti maarufu Louisiana katika tahiriri limesema ni wakati Obama aende kuona madhara mwenyewe.

Wakati huo huo Trump na Pence wanaelekea Lousiana

Hili la Louisiana ni la Obama, hata hivyo akiwa Democrat litaleta tabu sana kwa kampeni ya Clinton. Kwanini hakujifunza kutoka kwa Bush na Katrina?

Tusemezane
Mkuu Nguruvi3 kuna taarifa pia suala la e-mail wabunge wa republican bado wamelivalia njunga. Hivi wanaweza kuwashinikiza FBI kubadili maamuzi ya awali na kumfungulia mashitaka bi HR.!? Km ikitokea hivyo,nini itakuwa hatima ya mgombea huyo wa Dem?? Ikitokea mgombea akaenguliwa au kujitoa kwa wakati km huu,chama kinaruhusiwa kuweka mgombea mwingine na mchakato wa kupata mgombea mwingine unakuwaje??
 
Mkuu Nguruvi3 kuna taarifa pia suala la e-mail wabunge wa republican bado wamelivalia njunga. Hivi wanaweza kuwashinikiza FBI kubadili maamuzi ya awali na kumfungulia mashitaka bi HR.!? Km ikitokea hivyo,nini itakuwa hatima ya mgombea huyo wa Dem?? Ikitokea mgombea akaenguliwa au kujitoa kwa wakati km huu,chama kinaruhusiwa kuweka mgombea mwingine na mchakato wa kupata mgombea mwingine unakuwaje??
Mkuu suala la emails linaoenekana kuitesa sana kampeni ya Hillary Clinton. Linajirudia kwa namna tofauti. Ingawa inaoenekana Republican wamelivalia njuga, kama utakumbuka tulieleza jinsi kampeni ya Sanders inavyoimaliza Democrat

Suala la emails limeibuliwa na Sanders baada ya 'kufa'. Kila Sanders alipolitumia lilionyesha kumeletea mafanikio katika kampeni. Republican wakalichukua na hata tunapoandika, kuna 'hisia na tete' kuwa kampeni ya Sanders ailishandaa kuibua hoja hiyo kama uchaguzi ungeenda mkutano mkuu Philly

Kwavile uchaguzi haukufika huko, kampeni ya Sanders ikiongozwa na akina Jeff Weaver 'imeuza' issue kwa Republican. Na katika kumkwamisha Clinton, Republican wanaitumia vema

Si kuwa wanataka matokeo ya mwisho kwa uhakika, wanachotaka ni kuvuruga kampeni ili isijikite katika hoja. Kama utakubuka, siku 27 baada ya mikutano mikuu, kampeni ya Trump ilivurugwa sana na matatizo aliyosababisha. GOP wanafanya hivyo ili kuondoa focus ya Clinton kampeni.

Hata hivyo, kuna hoja muhimu sana ambayo hatujawahi kuijadili kwa undani. Je, ikitokea mgombea kuondolewa kama Republican walivyotaka kumfanyia Trump mwezi wa 9 kama habadiliki, au emails zikamletea Clinton matatizo ya kushtakiwa, nini kitafuata katika kupata mgombea?

Tutalijadili suala hili, lakini ni muhimu sana tukaelewa kwa ufupi hatua zinazofuata baada ya convention na kupata nominee wa vyama. Hili litatupa urahisi wa kuelewa mchakato mzima

1. Presidentia candidates : Hapa ni wagombea waliojitokeza kushiriki hatua za awali za chaguzi ndani ya vyama vyao. Ndio akina Rubio, Sanders, Bush, Cruz, Kasich n.k.

2.'Presumable nominee': Baada ya kushinda na kabla ya kuelekea uchaguzi mkuu wa vyama'conevntion'

3. Party nominee: Baada ya kuidhinisha na kukubali uteuzi wa mkutano mkuu wa chama
Hawa watabaki hivyo hadi uchaguzi mkuu tulioeleza huko nyuma unapangwaje kitarehe

4.Uchaguzi hufanyika November kuchagua Rais. Kura zake zinapatikana kutokana na wajumbe
Idadi ya wajumbe inaitwa 'states' electors' . Hawa ndio wataomchagua Rais katika kile kinachoitwa electoral college. Uchaguzi wa electors katika electoral college hufanyika katika state level.

Mgombea huchaguliwa na wajumbe waliopatikana katika states na siyo popular vote za states

5. President elect: Huitwa hivyo baada ya electoral college kumaliza kazi ya kumchagua Rais na makamu wake. Ikumbukwe, hawa wajumbe wanatokana na popular vote za wananchi, hivyo upigaji kura wao unaakisi matakwa ya waliowachagua. Wanachofanya ni kukamilisha mchakato

6. President: Huapishwa January 20 na hapo kuwa na mamlaka kamili.

Baada ya kuona mtiririko huo ndipo tunaweza kujibu hoja, inatokea nini kama lipo jambo litakalomsibu presumable nominee, nominee, president elect au president?

Inaendelea
 
YAKITOKEA YASIYOTARAJIWA

Tumeona hatua iliyopo ni ya nominee. Ikumbukwe, hawa nominee huchagua makamu (VP) ambao nao huthibitishwa na mkutano mkuu. Tusisitize, hawa ni chaguo la mgombea (nominee) si la chama, hata hivyo huwa kiungo muhimu katika shuguhuli za chaguzi

HISTORIA
Historia ya Marekani inaonyesha hakuna presumable nominee, nominee au president elect aliyewahi
kufariki, kujiuzulu au kuondolewa wakati mchakato unaendelea.

Hata hivyo, imeshatokea mwaka 1872 Vice-president kufariki kabla ya uchaguzi(Horace Geeley)
Mwingine ni Bw Eagleton (1972) wakati wa McGovern wa Democrat akigombea. Huyu alijiuzulu siku 18 baada ya kuteuliwa kutokana na historia yake iliyoonyesha aliwahi kuwa na maradhi ya akili 'depression' katika miaka 1960 na alitibiwa kwa electrotherapy. Hivyo hakuwa fit kwa nafasi hiyo

Hapa kuna hali mbali mbali kutokana na mtiririko wa bandiko lililotangulia hili

1. Kama mgombea akifariki , kuondolewa au kujiuzulu kabla ya uchaguzi mkuu November, vyama vyote Dem na Republican vina sharia za kuziba pengo kwa kushirikiana na mamlaka za states na Federal

Kumbuka Makamu wa Rais mtarajiwa (VP) na kwa hali ya leo, Tim Kaine au Mike Pence hawawezi kuwa wagombea automatic. Kama utakumbuka, bandiko la wali tulisema hawa wameteuliwa na mgombea na si chama ingawa wanabeba bendera za chama

Hivyo National Committee iwe Dem au Rep vitalazimika kuchagua jina jingine

Kwa mantiki hiii, bado Bernie Sanders wa Democrat ana 'shot' ndiyo maana kwa njia za siri sana anaungana na Republican kuhakikisha Clinton anaenguliwa.

Kama mgombea atafariki baada ya uchaguzi November na kabla ya kura za electoral college, suala hilo klitaamualiwa na congress na supreme court. Inaweza kuwa mgogoro mkubwa sana wa kikatiba

Kama mgombea akifariki baada ya electoral college kumaliza kupiga kura December 20 na kabla ya kuapishwa January 20, makamu wa Rais anakuwa Rais moja kwa moja

Hapa ukubuke kuwa tayari electoral college vitakuwa vimemchagua Rais na Makamu wakisubiri congress ithibitishe January 6 na kuapishwa January 20. Hivyo Makamau wa Rais anapata ''uhalali''

Mkuu Magode, nadhani kwa mabandiko mawili umeweza kupata picha ya nini kinaendelea

Tusemezane
 
UFAFANUZI ZAIDI

Maswali ya mkuu magode kuhusu nini kitatokea ikiwa kuna linguine kubwa inatupeleka katika ufafanuzi Zaidi ya mambo kadhaa yanayohusiana na uchaguzi mkuu wa USA

Hili tunalifanya ili tuone wenzetu wamefikaje walipo na walikutana na vikwazo gani

1. Kuhusu wagombea wakifikwa na majanga kama kifo au kutoweza kutimiza majukumu (incapacitated) tumeonyesha bandiko 458 mtiririko.

Hillary na Trump wamevuka stage ya presumable nominee, wapo katika party nominee.

Yoyote akipatwa na jangwa kati ya November na uchaguzi wa eletral college December, sheria haielezi VP atakuwa na role gani.

Sheria inasema baada ya congress kuhesabu kura za electoral college January 6, mgombea na VP wake wataitwa president elect na Vice president elect

Katika kipindi hicho cha Januray 6 hadi January 20 wakati wa kuapishwa, mgombea akifariki au kuwa incapacitated VP anakuwa Rais automatic

VP anachukua jukumu kwasababu tayari electoral college na congress vimeshamthibitisha

Swali linatokea, Je VP ana nafasi gani ikiwa electoral college itatoa matokeo ya 269 kwa kila mgombea na ili mshindi apatikane lazima mmoja awe na 270 au Zaidi?

Electoral college ina jumla ya viti 538, ukigawa kwa 2 ni 269.

Sasa kunawezakanaje kuwa na kufungana kwa 269 au 268 au 266?

Jibu lake linachanganya na hapa twende pamoja taratibu.

Electoral college za states zinatofautiana kutoka state moja hadi nyingine, katika majimbo 50 ya Marekani hutumia utaratibu wa wainner take all, kwa maana mwenye viti vingi katika states atapata wajumbe wote au anashinda hiyo state

Kuna majimbo mawili yanatumia uwiano, kwamba district za majimbo hayo zitagawanywa kwa ushindi wa kila mgombea.

Halafu kuna eneo linaitwa DC lina viti 3 .
Haya maeneo ndiyo yanayeza kuleta kufungumana kwa viti kwa kura za Urais

Lakini pia usisahau kuwa kuna chama cha Green Party au kuna uwezekano wa kuwa na mgombea binafasi anayeweza kushinda jimbo moja na kuvuruga hesababu ya 270.

Kwa mfano, Green Party wakishinda jimbo la Florida lenye wajumbe 20, Trump na Clinton wakakaribiana sana, uwezekano wa kutopata 270 upo. Rais hawezi kupatikana

Kinachofuata ni suala kupelekwa Congress ambapo kura zitapigwa kuamua mshindi.
Kila state itakuwa na kura moja, kwamba aliyeshinda atapata kura 1 ya state

Congress hawatamchagua VP, kama tulivyosema VP hupigiwa kura na electoral college separate na Rais. Congress itamchagua Rais na Senate itampigia kura VP

Hili limewahi kutokea mwaka 1836 ambapo VP wa Martin Van Buren VP Richard Johnson ulikwama katika uchaguzi wa electoral college kwa kura 1.

Kwamba alikuwa short kwa kura 1.
Ilibidi uchaguzi wa VP uende Senate na VP wote wawili waliingia katika uchaguzi tena

Kwa bahati nzuri Johnson alimshinda Francis Granger ndani ya Senate

Swali la kujiuliza, kwanini Senate imachague VP na si Congress kama ilivyo kwa 'Rais'
Yaani kunapokuwa na kufungana kwa kura za urasi ima 270 au chini na ikiwa wote walipigiwa kura na electoral college?

Kwa Marekani, VP ana role ceremonial katika Senate.
Yupo kiongozi wa Senate wakimwita Senator majority ambaye kwasasa ni Michel McNeill. Halafu yupo Minority Leader ambaye alikuwa H.Reid

Kura katika Senate zinapofungana ''tie' VP ana kura moja inayoweza kuwa break tie.

Hivyo role ya VP ipo katika Senate ndiyo maana upataikaji wake katika hali ambayo ni ya utata kama kushindwa kupatikana katika hatua za awali inatatuliwa na Senate

Kwa kauli nyingine, anawajibika kwa seneti kuliko Congress,Rais ana uhusiano na vyote

Tusemezane
 
Back
Top Bottom