Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

Duru za siasa: Uchaguzi Mkuu USA

Mkuu mag3 wakati tunasubiri analysis ya HC kutoka kwa nguruvi3. Hebu kwa faida ya wanajukwaa wengi tukumbushe mara ya mwisho hawa wamarekani kukipa uongozi chama tawala awamu mbili mfululizo. Hapa namaanisha kwa mfano,Democrat wamepata fursa ya kuongoza miaka yote 8 ya obama. Mara nyingi hapa wamarekani wakikipa chama uongozi wa miaka 8 mfululizo,uchaguzi unaofuata(km huu) mara nyingi huwa wanafanya mabadiliko. Nataka unikumbushe mara ya mwisho chama kupata uongozi kwa miaka 12 au 16 mfululizo ilikuwa mwaka gani!!?? Najua chama kikivurunda huwa kinaishia miaka 4 km ilivyokuwa kwa George bush senior miaka ya 90.
Mkuu magode, Democratic Party (Liberal, left leaning) ilikuwa ya kwanza kuasisiwa mwaka 1828 ikifuatiwa na Republican Party (Conservative, right leaning) iliyoasisiwa mwaka 1854.

Chama cha Republicans kiliweza kufanikiwa kubaki madarakani kwa kipindi cha miaka 12 kuanzia na Ronald Reagan 1981-1989 akifuatiwa na George H. W. Bush pia wa Republicans 1989-1993.

Kabla ya hapo Democrats nao waliweza kuwa madarakani kwa kipindi kirefu zaidi cha miaka 19 na miezi 9 kuanzia Franklin D. Roosevelt 1933-1945 na kupokewa na Harry Truman pia wa Democrats 1945-1953.

Baada ya kifo cha Franklin D. Roosevelt akiwa bado yuko ofisini na akiwa ameanza kipindi chake cha nne, katiba ilibadilishwa kutoruhusu Rais kubaki madarakani kwa vipindi zaidi ya viwili.

Wakisubiri kumpata Rais wa 45 November mwaka huu, USA imekuwa na marais 19 kutoka Republican Party, 16 kutoka Democratic Party na tisa tu kutoka nje nje ya vyama hivi viwili vikubwa.

Marais wanne wameweza kuuawa wakiwa ofisini nao ni Abraham Lincoln (Republican), James A. Garfield (Republican), William Mckinley (Republican) na John F. Kennedy (Democrat)
 
Mkuu magode, Democratic Party (Liberal, left leaning) ilikuwa ya kwanza kuasisiwa mwaka 1828 ikifuatiwa na Republican Party (Conservative, right leaning) iliyoasisiwa mwaka 1854.

Chama cha Republicans kiliweza kufanikiwa kubaki madarakani kwa kipindi cha miaka 12 kuanzia na Ronald Reagan 1981-1989 akifuatiwa na George H. W. Bush pia wa Republicans 1989-1993.

Kabla ya hapo Democrats nao waliweza kuwa madarakani kwa kipindi kirefu zaidi cha miaka 19 na miezi 9 kuanzia Franklin D. Roosevelt 1933-1945 na kupokewa na Harry Truman pia wa Democrats 1945-1953.

Baada ya kifo cha Franklin D. Roosevelt akiwa bado yuko ofisini na akiwa ameanza kipindi chake cha nne, katiba ilibadilishwa kutoruhusu Rais kubaki madarakani kwa vipindi zaidi ya viwili.

Wakisubiri kumpata Rais wa 46 November mwaka huu, USA imekuwa na marais 19 kutoka Republican Party, 16 kutoka Democratic Party na tisa tu kutoka nje nje ya vyama hivi viwili vikubwa.

Marais wanne wameweza kuuawa wakiwa ofisini nao ni Abraham Lincoln (Republican), James A. Garfield (Republican), William Mckinley (Republican) na John F. Kennedy (Democrat)
Ahsante mkuu mag3 kwa kumbukumbu hiyo. Kwa maantiki hii,baada ya kuwekwa ukomo wa Urais baada ya vipindi viwili,yaani baada ya franklin D.Roosevelt democrat hawajawahi kuongoza kwa vipindi 3 mfululizo. Inaonekana wamarekani kwa kiasi kikubwa wanafanya mabadiliko ya vyama kila baada ya miaka 8 ya uongozi wa chama kimoja. Hili ni jambo kubwa la kujifunza juu ya elimu ya wapiga kura. Hili jambo halipo kikatiba,lkn wapiga kura wanaona ni muhimu kubadili uongozi baada ya kuongoza kwa vipindi viwili mfululizo. Lkn wakati huohuo wanaweza kukiondoa chama kwa kipindi kimoja tu km kikivurunda. Uchaguzi wa mwaka huu,pamoja na makandokando ya Donald Trump,lkn nadhani ndo Rais ajaye wa Marekani..!!
 
Ahsante mkuu mag3 kwa kumbukumbu hiyo. Kwa maantiki hii,baada ya kuwekwa ukomo wa Urais baada ya vipindi viwili,yaani baada ya franklin D.Roosevelt democrat hawajawahi kuongoza kwa vipindi 3 mfululizo. Inaonekana wamarekani kwa kiasi kikubwa wanafanya mabadiliko ya vyama kila baada ya miaka 8 ya uongozi wa chama kimoja. Hili ni jambo kubwa la kujifunza juu ya elimu ya wapiga kura. Hili jambo halipo kikatiba,lkn wapiga kura wanaona ni muhimu kubadili uongozi baada ya kuongoza kwa vipindi viwili mfululizo. Lkn wakati huohuo wanaweza kukiondoa chama kwa kipindi kimoja tu km kikivurunda. Uchaguzi wa mwaka huu,pamoja na makandokando ya Donald Trump,lkn nadhani ndo Rais ajaye wa Marekani..!!
Ni kweli usemavyo ila kumbuka kuwa uchaguzi wa mwaka huu si wa kawaida, ni tofauti kabisa na chaguzi nyingi zilizopita kwani kuna mambo matatu makubwa ya kuzingatia kwa pande zote mbili;

Republicans
  • Mgombea, Donald Trump, hawajawahi kuwa kiongozi kisiasa katika ngazi yoyote ile wala historia ya kuwatumikia wananchi kijamii wakati wowote ule.
  • Pili mgombea ni tajiri aliyerithi mamilioni ya fedha na hajui kabisa maisha wanayoishi wananchi wa kawaida (middle class) na hajawahi kuonja machungu ya kulitetea taifa.
  • Tatu, haungwi mkono na makada wa awali wa chama kwa kukurupuka na kuyumba linapotokea hoja ya kutetea itikadi na misingi ya chama chake.
Democrats:
  • Mgombea, Hillary Clinton, anayo nafasi ya kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kugombea Urais tangu kuanzishwa kwa taifa la USA.
  • Clinton anayo sifa ya uongozi katika medani za kisiasa kwa ngazi mbalimbali na anayo historia ya kuwatumikia kijamii tangu akiwa kijana.
  • Anaungwa mkono na makada wengi wa chama chake pamoja na Rais Obama aliyeweka rekodi ya kuwa mweusi wa kwanza kushinda Urais.
magode, ukisoma niliyoyandika unaweza kusema naonekana kumtetea mgombea wa Democratic Party kuliko yule wa Republican au hata kumchukia Donald Trump. Unaweza pia kujiuliza kwa nini nimezungumzia zaidi mapungufu ya mgombea wa GOP kuliko wa DNC...najibu hivi, ni kweli wagombea wote wawili wana mapungufu yao kama binadamu, lakini hapa nimejikita katika sifa na uzoefu kiuongozi na si sifa kiutendaji kwa sababu Marekani Rais hawi mungu-mtu kama hapa kwetu Tanzania.

Nchini Marekani Rais peke yake, hawezi kuleta mabadiliko bila ya wananchi kupitia wawakilishi wao. Viongozi wote serikalini, pamoja na wale wa kuteuliwa, wanapatikana pale tu wananchi wanaporidhia teuzi zao kupitia wawakilishi wao. Udikteta hauna nafasi Marekani na mtu moja hawezi kufanya maamuzi yanayopingana na Katiba kwani vyombo vimewekwa kuhakikisha hatumii nafasi yake vibaya. Trump hajawahi kuwa chini ya mtu au watu lakini akiwa Rais lazima awe chini akiwatii na kuwatumikia watu.
 
Ni kweli usemavyo ila kumbuka kuwa uchaguzi wa mwaka huu si wa kawaida, ni tofauti kabisa na chaguzi nyingi zilizopita kwani kuna mambo matatu makubwa ya kuzingatia kwa pande zote mbili;

Republicans
  • Mgombea, Donald Trump, hawajawahi kuwa kiongozi kisiasa katika ngazi yoyote ile wala historia ya kuwatumikia wananchi kijamii wakati wowote ule.
  • Pili mgombea ni tajiri aliyerithi mamilioni ya fedha na hajui kabisa maisha wanayoishi wananchi wa kawaida (middle class) na hajawahi kuonja machungu ya kulitetea taifa.
  • Tatu, haungwi mkono na makada wa awali wa chama kwa kukurupuka na kuyumba linapotokea hoja ya kutetea itikadi na misingi ya chama chake.
Democrats:
  • Mgombea, Hillary Clinton, anayo nafasi ya kuweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kugombea Urais tangu kuanzishwa kwa taifa la USA.
  • Clinton anayo sifa ya uongozi katika medani za kisiasa kwa ngazi mbalimbali na anayo historia ya kuwatumikia kijamii tangu akiwa kijana.
  • Anaungwa mkono na makada wengi wa chama chake pamoja na Rais Obama aliyeweka rekodi ya kuwa mweusi wa kwanza kushinda Urais.
magode, ukisoma niliyoyandika unaweza kusema naonekana kumtetea mgombea wa Democratic Party kuliko yule wa Republican au hata kumchukia Donald Trump. Unaweza pia kujiuliza kwa nini nimezungumzia zaidi mapungufu ya mgombea wa GOP kuliko wa DNC...najibu hivi, ni kweli wagombea wote wawili wana mapungufu yao kama binadamu, lakini hapa nimejikita katika sifa na uzoefu kiuongozi na si sifa kiutendaji kwa sababu Marekani Rais hawi mungu-mtu kama hapa kwetu Tanzania.

Nchini Marekani Rais peke yake, hawezi kuleta mabadiliko bila ya wananchi kupitia wawakilishi wao. Viongozi wote serikalini, pamoja na wale wa kuteuliwa, wanapatikana pale tu wananchi wanaporidhia teuzi zao kupitia wawakilishi wao. Udikteta hauna nafasi Marekani na mtu moja hawezi kufanya maamuzi yanayopingana na Katiba kwani vyombo vimewekwa kuhakikisha hatumii nafasi yake vibaya. Trump hajawahi kuwa chini ya mtu au watu lakini akiwa Rais lazima awe chini akiwatii na kuwatumikia watu.
Nakubaliana na ww mkuu Mag3 kwa sehemu na hata ulichosema ndiyo ukweli wenyewe. Lkn maelezo ya mwisho yanathibitisha ukweli kwamba,pamoja na kukosa kwake uzoefu ktk uongozi kwa ngazi yoyote ile,bado taasisi ya urais inaweza kuongozwa na mtu yeyote...!

Kumbuka pia uongozi wa kisiasa kwa ngazi yoyote hauhitaji uzoefu kwa sababu majukumu ktk kila wadhifa yanatofautiana. Na hii ya kutokuwa na uzoefu wa uongozi,inampa sifa pia bwana trump. Dosari pekee inayoshadadiwa na wengi ni matamshi yake,na hilo naamini washauri wake watamjengea uwezo wa kujiepusha na matamshi yatakayochochea chuki dhidi ya wapiga kura.

Hilary clinton,ni bora angekuwa neutral km trump,kashfa zote anazotuhumiwa nazo ni zile zinazotokana na yy kuwa uongozini. Na jambo lingine lisilosemwa sana wala kuandikwa sana wamarekani wanaona kumpa Urais bi hilary ni kumrudisha bill clinton ikulu. Ni kweli uchaguzi utakuwa na ushindani mkali sana,lkn hakuna njia ya kumzuia bwanyenye huyo kuwa Rais wa Taifa kubwa Duniani. Mark my words...!!



Sent from my GT-I9190 using JamiiForums mobile app
 
Ahsante mkuu mag3 kwa kumbukumbu hiyo. Kwa maantiki hii,baada ya kuwekwa ukomo wa Urais baada ya vipindi viwili,yaani baada ya franklin D.Roosevelt democrat hawajawahi kuongoza kwa vipindi 3 mfululizo. Inaonekana wamarekani kwa kiasi kikubwa wanafanya mabadiliko ya vyama kila baada ya miaka 8 ya uongozi wa chama kimoja. Hili ni jambo kubwa la kujifunza juu ya elimu ya wapiga kura. Hili jambo halipo kikatiba,lkn wapiga kura wanaona ni muhimu kubadili uongozi baada ya kuongoza kwa vipindi viwili mfululizo. Lkn wakati huohuo wanaweza kukiondoa chama kwa kipindi kimoja tu km kikivurunda. Uchaguzi wa mwaka huu,pamoja na makandokando ya Donald Trump,lkn nadhani ndo Rais ajaye wa Marekani..!!
Kumbu kumbu, kama sharia ingeruhusu vipindi vitatu Regan angeweza kuongoza vipindi Zaidi ya viwili
Ndivyo ambavyo Clinton angeweza kuongoza vipindi vitatu pia

Kwa upande wa elimu ya umma, suala sidhani ni vipindi viwili na kubadili
Siasa za Marekani zinaongozwa na nyakati

2012 hoja kubwa ilikuwa ni uchumi, employment n.k.
Hoja imepoteza nguvu si kwasababu uchumi ni mzuri, bali mwelekeo hauwezi kubezwa.

Hoja imegeuka kuwa ujira kwa wafanyakazi.
Na kwa umaarufu wa hilo, hata Republican wanaingia kati, ingawa haijawa sera yao

Hoja nyingine ni usalama. Kutokana na matukio ndani na nje ya Marekani, hayo yana influence sana mwenendo wa uchaguzi kwa ujumla.

Tukio lolote la usalama nchi Marekani, litabadili upepo wa kisiasa

Somo la kujifunza ni jinsi demokrasia ya wenzetu inavyofanya kazi hasa kutoa nafasi kwa wananchi kushiriki katika kuamua hatma yao.

Ni jinsi Rais anavyopitia mchujo mzito kabla ya kupatikana.
Na jinsi kulivyo na 'impartiality' kwa vyombo vya umma

Tujifunze namna ya kuwa na power balance. Kwamba, kama hutawapenda wagombea bado kuna Senati na Congress ambazo ni sehemu muhimu ya utawala.

Na somo la tatu ni jinsi wenzetu wanavyosoma katiba waliyoandika, wanavyoiheshimu na wanavyoifuata.

Katiba ni mali ya wananchi na nchi , si ya mtu , kundi au chama fulani na kwamba haiwezi kuchezewa na mtu bila sababu za maana

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3 na @Mag3,kwanza niwashukuru sana sana kwa uchambuzi wenu,japo kila siku nafuatilia kupitia CNN llakini pana vitu vya ziada navipata kupitia Uzi huu.
Nini mtazamo wenu kwa swala la Trump na Mr .Khan (Baba wa yule Muslim Solder).Inaonekana kama limemnyong'onyeza sana Trump na hata jinsi alivyojibu,yale makeke yake hajaweza kuyaonyesha kama anavyokuwa anawajibu wengine
 
Hii imenikera, sijapitia post za nyuma...nitazipitia baadaye. Hii si sahihi.
------------------------------
Kwa nini wako 'desperate' kumuangusha Trump kwa mbinu za 'kifedhuli'...! Ndiyo demokrasia kweli ya kujifunza namna ya kupiga kampeini?

Pekua New York Post uone wanavyojaribu kumuharibia Trumps kupitia the First lady to be.
nypost.com
 
Mkuu Nguruvi3 na @Mag3,kwanza niwashukuru sana sana kwa uchambuzi wenu,japo kila siku nafuatilia kupitia CNN llakini pana vitu vya ziada navipata kupitia Uzi huu.
Nini mtazamo wenu kwa swala la Trump na Mr .Khan (Baba wa yule Muslim Solder).Inaonekana kama limemnyong'onyeza sana Trump na hata jinsi alivyojibu,yale makeke yake hajaweza kuyaonyesha kama anavyokuwa anawajibu wengine
Nyamizi, uchaguzi wa mwaka huu ni tofauti kabisa na chaguzi zote zilizowahi kufanyika Marekani tangu taifa hili lipate uhuru wake July 4, 1776. Hebu msikilize huyu bwana akijaribu kuelezea anavyouona uchaguzi wa mwaka huu;



Kwenye swala la Ghazala Khan na mkewe Khizr kuhusu kifo cha mtoto wao Captain Hamayun Khan akiipigania na kuitetea nchi yake, mambo yamekuwa mazito kidogo. Donald Trump kama kawaida yake anajua fika anao wafuasi ambao hawayumbishwi na tamko lolote analokurupuka nalo hata likiwa la kipuuzi na la kijinga namna gani. Lakini safari hii sacrifice ya kijana na uchungu walio nao wazazi wake, umewagusa wengi na eneo lingine kabisa na hivyo kuzusha maswali kadhaa.

Donald Trump alikwepa kuji-elist jeshini wakati wa vita vya Vietnam akisingizia afya, kitu ambacho kimegundulika halikuwa na ukweli wowote. Wakati vijana wenzake wanajitolea kulitetea taifa kijeshi, yeye alikuwa anaponda maisha jijini New York akitafuna mabilioni aliorithi kutoka kwa babake. Hivi sasa anao watoto ambao hakuna hata moja aliyepitia jeshini lakini yuko tayari kuwaponda mashujaa waliolipigania taifa la Marekani kama John Mccain na wengine kupoteza maisha.

Donald Trump, bila aibu, anadai na yeye alitoa sacrifice kwani aliweza kutumia mamilioni ya kurithi kuunda makampuni na kuwaajiri watu wengi huku akiwatapeli wafanya biashara wadogo wadogo. Hadi leo ameshindwa kutoa kinachoitwa tax returns, kitu ambacho ni unprecedented kwa mgombea Urais nchini Marekani lakini mashabiki wake hata hawahoji kulikoni. Kuna mambo chungu nzima amefanya na kuyatenda ambayo yangeweza kabisa kumuondolea sifa za uongozi lakini si Donald Trump.
 
Hii imenikera, sijapitia post za nyuma...nitazipitia baadaye. Hii si sahihi.
------------------------------
Kwa nini wako 'desperate' kumuangusha Trump kwa mbinu za 'kifedhuli'...! Ndiyo demokrasia kweli ya kujifunza namna ya kupiga kampeini?

Pekua New York Post uone wanavyojaribu kumuharibia Trumps kupitia the First lady to be.
nypost.com
TUJITEGEMEE, tarehe 2 Julai mwaka 1776, Wamarekani walipiga kura ya kudai uhuru kutoka Uingereza na siku mbili baadaye tarehe 4 Julai 1776 walijitangazia uhuru. Ni uhuru ambao haukupatikana mezani, ni uhuru uliopatikana kupitia vita na umwagaji damu, ni uhuru ulioitangazia dunia kwamba Marekani ni Republic. Republic ni demokrasia ambayo pamoja na kuheshimu maoni ya wengi, haipuuzii maoni ya wachache, hapana, huheshimu, huzingatia na kulinda uhuru wa wachache.

Donald Trump, kwa maoni na matendo, ameonesha kutoheshimu uhuru wa walio wachache na ndio maana katika maisha yake ametumia ujanja ujanja kuwakandamiza wanyonge. Republican party iliundwa na watu ambao baada ya kuona Democratic Party inakumbatia utawala wa wengi bila kuheshimu haki ya wachache, waliamua kuasi na kuanzisha chama kipya. Nyakati hizo Democratic party ndio ilikuwa haiwajali minorities ikiwa ni pamoja na kutetea utumwa uliowakandamiza weusi.

Miaka ilivyokwenda misingi ya vyama hivi viwili ilibadlika na Democratic Party ndio ikaanza kuheshimu na kujali maslahi ya wachache badala ya Republican Party. Ni hivi karibuni GOP imegundua kwamba inapotea na hivyo kuanza kujirudi kukirudisha chama katika mstari kwa kujenga uhusiano bora na minorities. Ujio wa Trump na kwa matamko anayoyatoa umekirudisha chama katika miaka mingi tu nyuma na ndio maana establiment ya GOP imejitenga kabisa naye na kuamua kukaa kando.

Donald Trump hapigwi vita, hapana, anajimaliza mwenyewe kwa kujipiga vita na Marekani ninayoijua haiwezi kufanya makosa tena kama ilivyowahi kutokea huko nyuma. Kama unaamini Trump anaweza kuwa Rais wa Marekani, subiri mvua vuli zianze, hivi sasa ameweza kutembea katika barabara ya lami isiyo na mashimo wala mawe. Ngoja atakapoanza kuonja joto la jiwe siku zinavyokwenda, ni rahisi ngamia kupitia tundu la sindano kuliko mdhulumiaji na mkurupukaji kuukwaa Urais Marekani.

TUJITEGEMEE, hicho kinachofanyika Marekani ndiyo demokrasia, ndio uhuru wa maoni na ndio unasikia ukiitwa first amendment. Ni ajabu wewe kusema wanamfanyia Trump ufedhuli huku unasahau anavyotukana watu kila leo hadi Rais wa Marekani, Obama. Hatukani tu watu, anatukana hadi taasisi kama jeshi akidai ni la hovyo, anamwita mgombea mwenzake crooked Hillary na serikali nzima ya Obama stupid. Yaani yeye ni kama vile uhuru wa kusema lolote ni wake yeye peke yake, wakisema wengine unaita ufedhuli.
 
Hii imenikera, sijapitia post za nyuma...nitazipitia baadaye. Hii si sahihi.
------------------------------
Kwa nini wako 'desperate' kumuangusha Trump kwa mbinu za 'kifedhuli'...! Ndiyo demokrasia kweli ya kujifunza namna ya kupiga kampeini?

Pekua New York Post uone wanavyojaribu kumuharibia Trumps kupitia the First lady to be.
nypost.com
TUJITEGEMEE nadhani una maanisha ile picha ya Melania akiwa uchi wakati ni model huko kwao.
Kuna habari pia hakumaliza chuko kikuu alichosema amefuzu

Mkuu siasa za Marekani zaina akili na mbinu pia. Kampeni huendeshwa na tone ya wagombea wenyewe, wananchi wanachambua pumba na kweli
Kampeni zinaangaliwa na vyombo vya habari kwa undani ili kupata ukweli

Mkuu, Dald Trump huyu unayesema , ndiye alimwa attack Heide Cruz kwa kutumia tweet ya kulinganisha Melania na Heide

Ni Donald huyu alitusi baba yake Ted Cruz , pamoja na wenzake wakati wa chaguzi za awali. Hakuna aliyesalimika na kashfa zake

2008 kampeni ya Obama ilianza kumshambulia mtoto wa Mcain ambaye mambo yake ya kijinisia yana utata. Obama alisimama na kukemea kampeni na wafuasi wake kuwa family matter ni nje ya kampeni

2012 Romney kampeni ilianza mashambulizi dhidi ya Michelle kuwa anataka kufundisha watu namna ya kulisha watoto. Mitt Romney akakemea hilo na kusema familia ziwe nje ya mambo ya kampeni

2016 Trump alimdhalilisha Clinton kwa harusi ya Chelsea. Akaanzisha suala la Monica Lewenski akimtuhumu Bill kama fuska la karne

Haya ya Melania kayakaribisha yeye mwenyewe, tena si kutoka kampeni ya Hillary bali vyombo vya habari.

Unaweza kuona tone ya kampeni inaweza kuwa set na akina nani

Ukiingiza mambo ya nje, vyombo vya habari vinafuatilia kwa ukaribu kama ambavyo vinafanya kazi ya kuchambua sifa za Melania

Ninachotaka kukuonyesha ni mwenendo wala si uetetezi wa upande wowote
Ni katika kuonyesha kampeni za wenzetu na demokrasia yao

Kama utakumbuka, nimewahi kusema demokrasia ni makubaliano ya jamii Fulani. Endapo kwetu mambo ya familia hatuyakubali, hiyo haiwezi kuwa standard ya dunia nzima. Muhimu ni kuwa jamii husika inaheshimu makubaliano waliyojiwekea?

Sisi hatuheshimu hata katiba, tunawezaje kukerwa na picha za Melania wakati upana wa demokrasia yao tunaoona dhahiri shahiri?
 
Mkuu Nguruvi3 na @Mag3,kwanza niwashukuru sana sana kwa uchambuzi wenu,japo kila siku nafuatilia kupitia CNN llakini pana vitu vya ziada navipata kupitia Uzi huu.
Nini mtazamo wenu kwa swala la Trump na Mr .Khan (Baba wa yule Muslim Solder).Inaonekana kama limemnyong'onyeza sana Trump na hata jinsi alivyojibu,yale makeke yake hajaweza kuyaonyesha kama anavyokuwa anawajibu wengine
Mkuu suala la Mr Khan halikuanza naye leo
Ni kwavile Trump hawezi kusoma mazingira

2012 secretary of state Collin Powell alieleza kwa uchungu sana kuhusu matumizi ya neon Islamic terrorist yaliyokuwa yanatumiwa sana na Rudi Guliani na Republican kwa ujumla. Hayo yalifanyika kumfungaminisha Obama/Uislam/ Terrorism na ndiyo maana walimwita B.Hussein Obama

Collin Powell ambaye ni Jenerali na ndiye aliyeongoza majeshi ikiwemo operesheni ya Somalia. Powell anaheshimika sana katika jeshi la Marekani na kama ujuavyo ni mweusi

Collin alisema, alipotembelea makaburi ya mashujaa pale Arlington aliona majina ya Waislam. Akauliza ikiwa wote watakuwa terrorist vipi wale waliolipa gharama kubwa kutetea Marekani wakiwa Waislam 'pay ultimate price'

Hilo liliwaingia sana Wamerekani na mjadala ukabadilika na kuwa radical Islamic terrorist as opposed to Islamic terrorist.

Trump amejinasibu kuwapenda Veteran na hata kufikia kuchangisha milioni 5 kwa ajili yao. Kama ulimsikia Jenerali aliyeongea katika DNC convention, huo nao ulikuwa uongo, Trump hakuchangisha kiasi hicho na hajakanusha

Mara zote ameishambulia serikali ya Obama kuwa imewatelekeza veteran akitumia mianya kama wa kashfa ya VA hospital iliyowahi kutokea

Kisanga kimeanza pale aliposema atapiga marufuku 'Waislam' kuja US
Ndipo akina Khan wakajiuliza, je, wao ambao watoto wao wamelipa gharama kubwa sana kutetea Marekani vitani wanasimama wapi katika hili?

Kauli ya Mr Khan ilijaa hisia na ukweli ambao kila mmoja ameuona. Ni kweli mtoto wake amepoteza majina na kaburi lake lipo katika upande wa mashujaa

Swali analoulizwa Trump, kijana huyo angekuwa amejrehiwa, je angepata zile pesa 'anazochangisha' Trump au angewekwa pembeni kwa Imani yake?

Mr Khan kwa muda mfupi amekuwa star katika TV, na hilo limemnyong'eza sana Trump. Washauri wake wamemshauri akae kimya kwani kuendelea kuliongelea ni sawa na kutia chumvi katika kidonda kinachovuja damu

Hata Veteran hawakubaliani nalo, na hapo anaona amepoteza sehemu nyingine muhimu. Hivyo, kunyong'onyea si kwasababu hana la kusema, ni kuogopa kumwagia mafuta katika moto unaowaka.

Ni tatizo alilotengeneza mwenyewe.
 
"Mag3, post: 17050731,member: 10873"]TUJITEGEMEE,Ni uhuru ambao haukupatikana mezani, ni uhuru uliopatikana kupitia vita na umwagaji damu, ni uhuru ulioitangazia dunia kwamba Marekani ni Republic. Republic ni demokrasia ambayo pamoja na kuheshimu maoni ya wengi, haipuuzii maoni ya wachache, hapana, huheshimu, huzingatia na kulinda uhuru wa wachache.
Hata ndani ya convention zote, watu waliruhusiwa kuonyesha hisia zao. Waliondolewa pale tu ilipoonekana kuna mtafarauku, na hakuna aliyeshtakiwa. Ni katika kutekeleza first amendment na kusikiliza wachache
Miaka ilivyokwenda misingi ya vyama hivi viwili ilibadlika na Democratic Party ndio ikaanza kuheshimu na kujali maslahi ya wachache badala ya Republican Party. Ni hivi karibuni GOP imegundua kwamba inapotea na hivyo kuanza kujirudi kukirudisha chama katika mstari kwa kujenga uhusiano bora na minorities. Ujio wa Trump na kwa matamko anayoyatoa umekirudisha chama katika miaka mingi tu nyuma na ndio maana establiment ya GOP imejitenga kabisa naye na kuamua kukaa kando.
Baada ya Obama kumpiga vibaya Romney kinyume na matarajio ya GOP, Republican waliandaa mkutano kutahmini hali ya mambo
Moja ya maazimio yao ilikuwa kurudisha minorities katika Republican kwani wamekuwa vulnerable sana eneo hilo. Ironically minorities kama black America walitakiwa kuunga mkono Republican kutokana na historia.

GOP ndio walipinga utumwa na ni kipindi cha uongozi wao civil rights zilipitishwa.
Zote ilikuwa kuwajali minorities. Ujio wa akina Trump unaonyesha kurudisha nyuma jitihada ambazo the establishment waliziita progressive. Kwamba, mazingira yanabadilika, ushoga unazungumziwa makanisani na wapo makasisi.

Kwamba, abortion ni mambo yanayoonekana kuchukua sehemu kubwa, hivyo wanapaswa kufanya adjustment kulingana na hali ilivyo. Kama ulivyosema, the establishment walisusia kwa kuona hiyo si Republican wanayotaka kujenga.
TUJITEGEMEE, hicho kinachofanyika Marekani ndiyo demokrasia, ndio uhuru wa maoni na ndio unasikia ukiitwa first amendment. Ni ajabu wewe kusema wanamfanyia Trump ufedhuli huku unasahau anavyotukana watu kila leo hadi Rais wa Marekani, Obama. Hatukani tu watu, anatukana hadi taasisi kama jeshi akidai ni la hovyo, anamwita mgombea mwenzake crooked Hillary na serikali nzima ya Obama stupid. Yaani yeye ni kama vile uhuru wa kusema lolote ni wake yeye peke yake, wakisema wengine unaita ufedhuli.
Well said mkuu.

Niongezee, kuna heshima za watu hata kama hawakubaliani. Utasikia seneta so and so, Gavana so etc. Trump alimwita Seneta Rubio, little Rubio.
Hakujaribu kumwita Seneta bali Little Rubio.

Jitegemee ajiulize, kama inakera vipi kule ambapo hata mikusanyiko iliyo ndani ya sharia na katiba hairuhisiwi? Nadhani anaweza kuona upana wa demokrasia ya wenzetu.
 
WIKI NGUMU KWA TRUMP

Baada ya mkutano mkuu wa DNC uliootoa nafasi kwa Familia ya Khan kuzungumza, hoja imeibuka tena baada ya Trump kuimwagia mafuta. Trump alihoji ukimya wa Mrs Khan

Hilo limeibua mjadala takribani masaa 72 na ushee likijadiliwa na vyombo mbali mbali.

Chama cha Veteran wa Amerika kimetoa kauli ya kulaani kauli za Trump.

Familia za waliokufa vitani 'Gold star' wamemjia juu Trump

Wakati huo huo GOP hasa the establishment kama Mcain wamepinga kauli za Trump

Mgombea mwenza, Mike Pence amekutana na swali kama hilo lililompa wakati mgumu

Katika wiki hii kumekuwepo na tukio la Mrs Trump kuonekana katika picha za utupu
Melania alikuwa ni model, na picha zake katika mgazeti hazikuwa na stara

Wachunguzi wa mambo wanashangaa kampeni ya Trump kutoliongelea kabisa kana kwamba tukio halikuwepo.

Wapo wanaosema pengine picha hizo zimetolewa katika jitihada za kuua hoja ya veteran.
Hayo yamebaki maoni tu, ingawa inashangaza kampeni kukaa kimyaa!

Katika tukio jingine katika masaa machache ni pale Trump alipoeleza kuhusu Russia
Trump alisema atazuia Russia kuingia Ukraine eneo la Cremea

Hadi sasa Raussia wapo huko na hilo limeweka weledi wa Trump katika wakati mgumu

Ieleweke,Trump hupenda vyombo vya habari na habari nyingi ziwe za utata au vinginevyo huanzishwa naye na si kama wengi wanavyodhani vyombo vya habari vinamwandama

Lakini pia ana tatizo, kwamba damage control yake ni mbaya. Suala la veteran angesema kwa urahisi tu, anawaheshimu wote na asingependa mjadala Zaidi! Hakufanya hivyo

Tusemezane
 
Kwanza nitoe pongezi kwa wadau wote wa hili jukwaa waandishi na wasomaji!

Heshima kubwa zimwendee mkuu Nguruvi3 kwa umaridadi wake wa kuchambua na kubainisha mambo makubwa makubwa ya kitaifa na kimataifa. Jamaa una uwezo mkubwa sana, binafsi ninaona hivyo. Keep it up! Ilifikia mahali nikataka kukufahamu personally, sikufanikiwa, ila nitafanikiwa. Thanks kwa jamaa mmoja anayekufahamu kanipa hints chache kuhusu wewe! Wanasema if you hang with five stupid men then you will be the sixth...........hahahaha!

Well, naomba ku declare interest. Namshabikia Donald John Trump. Ninazo sababu zangu za msingi sana, lakini moja kubwa ni hili. Sio establishment hata sio mwanasiasa. Huyu ni somo kubwa sana kwa wanasiasa wanaodhani nchi inamilikiwa na wanasiasa na kila neno lao ni sheria. Najua Nguruvi3 na team yake kubwa ni Hillary Clinton usiniulize nimejuaje!

Napenda namna Trump anavyoshambuliwa kila pahali, na hatimaye ashinde. Naogopa namna anavyoshindwa kusoma upepo wa kampeni kwenye nafasi ya urais kiasi cha kusababisha mkanganyiko usio wa lazima hasa hasa kwa wale ambao bado hawajaamua kura zao zinaenda kwa nani. Lakini namuelewa vema, ndivyo alivyo.

Hata hivyo siamini kama ataleta mabadiliko yoyote chanya akiwa rais lakini napenda ashinde kwa sababu ya hasira nilizo nazo dhidi ya 'establishment'; bado pia siamini kama Clinton naye ataleta la maana kwenye u presidency wake. Kama Trump anavyosema ni 'Crooked' nami nakubaliana naye 100%. Kama Hillary Clinton atashinda, naona kama atakuja kutumika kama 'uchochoro' wa kuimaliza USA na manyang'au wakubwa kama akina Putin na EURO kwa ujumla. Hata akishinda siamini kuwa atamaliza muda wake wa miaka 4 madarakani.

Kwa jinsi hali ya Dunia ilivyo kwa sasa, ninaona watu wanaofit kuwa kwenye nafasi kubwa kubwa za kisiasa wanakaa pembeni na kutazama Dunia inavyodidimizwa na wanasiasa. Wengi hawagombei, na hata wakigombea wananchi hawawaelewi kwa kuwa wananchi nao ni 'crooked' hasa kwa nchi zetu za Afrika.
 
TheDealer ahsante kwa mchango wako
Yapo mengi umeongelea, nitajaribu kuyapitia kwa kadri

1. Tunapoongelea 'the establishment' hawa ni wa Washington.
Sijui magavana ni sehemu yao au la. B.Clinton, R.Reagan, Bush jr walikuwa ni magavana.

Katika chaguzi za awali, walikuwepo akina Dr B.Carson, Gavana Christie, Gav John Kasich, outsider Carl Fiorina, Jef Bush, Donald Trump, Rick Perry

The establishment walikuwa Seneta Sanders, Hillary, Ted Cruz, Seneta Rubio,Walker kwa uchache wa kuwataja

Mchujo ulionyesha wananchi wana machaguo mawili, moja ni outsider Trump na mwingine ni The Estab. Clinton.
Kwa Dem hakukuwa na option bali the establishment

Chaguzi zimefanyika state zote kwa uwazi na matokeo ndiyo hayo

Kwa wenzetu demokrasia ndiyo inaamua, pamoja na mizengwe yote Trump ndiye mgombea wa GOP. Hakuna ujecha

Wakati gani wanahitaji mtu wa aina gani, demokrasia yao ndiyo itasema.
Trump akichaguliwa, Obama hana choice atamkabidhi oval office.

Hivyo nguvu ya Demokrasia ndiyo inayosema, awe outsider au insider Wamarekani ndio wataamua kwa mustakabali wa Taifa lao.

Inaendelea..
 
2. Kuhusu Team 'Hillary Clinton'
Kwa mtazamo wa haraka inaonekana kweli. Ungepitia uzi wa uchaguzi wa Marekani ungeona tofauti.

Nilisema wazi, kwa GOP chaguo langu lingekuwa John Kasich.
Ni mgombea aliyeeleza mambo kwa mantiki, aliyejua domestic and international affairs

Sen Rubio ni mzuri, tatizo anapenda ku appease badala ya kusimama katika ukweli. Kilichoangusha kampeni yake ni hoja dhidi ya Obama si siasa za ndani.

Ted Cruz ni mwepesi wa hoja. Hakuwa na mbadala,hoja zake zilikuwa dhidi ya Obama. Aliwahi kuuliza, kama Trump afanya surveillance kwa neighborhood za waislam nini msimamo wake?

Jibu la Cruz ni kumshambulia Obama kuhusu ziara ya Cuba.
Huo ukawa mwanzo wa mwisho wake.

Trump: Huyu amekuwa katika vyombo ya habari akikosoa kwa dakika chache
Katika uchaguzi wa awali hakuonyesha chochote zaidi ya kutumia fear mongering kupata kura.

Alifanikiwa kwasababu 'base' yake, sehemu kubwa ni supremacist ni intact
Hakutegemea independents waliogawanyika kila mara

Trump inapofikia hoja, anataja sera hana details. Hapo ndipo utaona kuna tatizo. Amekuwa anageuka geuka kila siku. Hawezi kupambanu jambo kwa mantiki kisera kama anavyoweza John Kasich au Sanders au Clinton.
 
Mkuu Nguruvi3 sijakuelewa vema unavyomujumuisha Bernie Sanders kwenye kundi la establishment, ninavyomfahamu mimi ni kama 'independent' ambaye amekaribishwa ndani ya chama cha 'Democrat' kama kujaribu bahati yake ya kutafuta u-nominee kwa tiketi ya Democrat. Lakini pamoja na hayo bado kwa sehemu kubwa ameegemea mawazo ya outsiders yaani upande wa Donald Trump.

Nimependa hapo kwa 'demokrasia'. Kwamba wanaacha demokrasia yao iwaamulie wanachokitaka. Iwe wanamtaka mtu kutoka establishment ama outsider demokrasia yao itaamua. Mungu aendelee kuwabariki wamarekani na Marekani yao!
 
Democrat
Kwa upande huu walikuwepo wawili. Tatizo tuliloeleza si sera zao ni zaidi
Habari nyingi za Sanders zilihusu kubadili Dem ili ikidhi matakwa yake

Hapo ndipo muda mwingi tumeonyesha tatizo lake, na ndiyo iliyopelekea ku draw conclusion ya 'Team Hillary'.

Tuliwahi kusema Sanders atakuwa tatizo kwa Dem mbele ya safari, na ndilo limetokea na litaendelea kuwa na madhara kwa Dem kwa muda mrefu

Trump vs Clinton
Napo utaona Trump anazungumziwa sana katika uzi huu pengine kwa mabaya tu. Well, mazuri yake hayana kina. Trump ndiye chanzo cha matatizo yake

Mfano, Juzi kazusha tatizo na Gold star family.
Badala ya kufanya damage control yeye anachochea moto.

Kuua hoja inasemekana katumbukiza picha za mkewe, haikusaidia.

Jana kaingiza hoja ya kuwaunga mkono wapinzani wa McCain na Spika Ryan kubadili mweleko, haikuuua hoja.

Jioni ya jana kaingia katika ugomvi na 'katoto' kalikolia katika mkutano wake

Ana create controversy kama means za kuwa katika media, kuua hoja au kupoteza directions ya maongezi.

Kufanya hivyo anatoa chakula kwa media zote duniani.
Yeye anakaribisha matatizo si kuwa matatizo yanamfuata

Hatukutaka kuzungumzia mgogoro na gold star, Nyamizi akauliza hili lipoje?
Tukachangia hoja na hapo ndipo unaona kuna ''bias''
 
Back
Top Bottom