DV-2023 program ( bahati nasibu ya kuhamia U.S.A.) inaanza rasmi kuchezwa tarehe 6/10/2021

DV-2023 program ( bahati nasibu ya kuhamia U.S.A.) inaanza rasmi kuchezwa tarehe 6/10/2021

Nimekwambia kwa waliopo Dar kama upo mwanza zipo photo point za kueleweka same na arusha ila mikoa mingine kama mbeya cjaona, ruvuma, rukwa, cjaona weng ni wapiga picha wahuni tu nakwambia kwa experience nilizunguka sana mkoa wa ruvuma kuanzia tunduru, songea, mbinga ckupata photo studio ya maana.
Mbeya kuna majamaa wapo kabwe stand wanaitwa mashada kdgo wanajitahid labda na uhindn kama wapo ila sina uhakika.
Alaf shida sio kupiga picha shida ni dimensions wanazotaka kama unaongea kama motivational speaker pole hii kitu nilishaapply mara 2 mwaka 2013 nikaja kuapply tena 2015 ila sikufanikiwa so najua nachokwambia.
Ungeanzisha Uzi wako ingependeza kweli.
 
Ungeanzisha Uzi wako ingependeza kweli.
Hatushindani kuanzisha uzi maana hatulipw kwa kufanya hvyo ila lengo la kuanzisha ni kutoa nafasi wengine wachangie ingekuwa ni siri ungetuma kwenye PM za watu.
 
Hatushindani kuanzisha uzi maana hatulipw kwa kufanya hvyo ila lengo la kuanzisha ni kutoa nafasi wengine wachangie ingekuwa ni siri ungetuma kwenye PM za watu.
Pole,
 
USHIRIKI, DV-2023 MWISHO TAREHE 9/11/2021- ZIMESALIA SIKU 9 TU.

Tunakumbushana kuwa tarehe ya mwisho kwaajili ya kutuma ushiriki wako kwenye Bahati nasibu ya mwaka huu (DV 2023 lottery) ni TAREHE 9/11.

Kwa maneno mengine zimesalia siku 9 tu kabla ya kufungwa kwa ushiriki kwa msimu huu.

Ndugu, jamaa, rafiki hima tuma ushiriki wako iwapo sifa na vigezo unavyo.
Lakini pia kama yupo yeyote unaemfahamu na ambae unadhani anavyo vigezo,
basi kunjua roho mfahamishe,
hutapungukiwa na kitu.

Hii ni nafasi adimu yenye faida zaidi ya maneno yangu yanavyoweza kukuelezea.

Tafadhali,
Soma maelekezo vizuri,
Kisha jaza form kwa utulivu.
Ukikwama mahali usisite kuwasiliana nami tutasaidiana mawazo na ushauri, -bureeee.

Gharama ni iwapo utahitaji nikujazie mimi ama kuonana ana kwa ana.

Piga/WhatsApp :+255714591548


Nawasilisha.
 
USHIRIKI, DV-2023 MWISHO TAREHE 9/11/2021- ZIMESALIA SIKU 9 TU.

Tunakumbushana kuwa tarehe ya mwisho kwaajili ya kutuma ushiriki wako kwenye Bahati nasibu ya mwaka huu (DV 2023 lottery) ni TAREHE 9/11.

Kwa maneno mengine zimesalia siku 9 tu kabla ya kufungwa kwa ushiriki kwa msimu huu.

Ndugu, jamaa, rafiki hima tuma ushiriki wako iwapo sifa na vigezo unavyo.
Lakini pia kama yupo yeyote unaemfahamu na ambae unadhani anavyo vigezo,
basi kunjua roho mfahamishe,
hutapungukiwa na kitu.

Hii ni nafasi adimu yenye faida zaidi ya maneno yangu yanavyoweza kukuelezea.

Tafadhali,
Soma maelekezo vizuri,
Kisha jaza form kwa utulivu.
Ukikwama mahali usisite kuwasiliana nami tutasaidiana mawazo na ushauri, -bureeee.

Gharama ni iwapo utahitaji nikujazie mimi ama kuonana ana kwa ana.

Piga/WhatsApp :+255714591548


Nawasilisha.
Kumbe muda bado, ngoja tujitahidi
 
E-DV 2023 KUJISAJILI KUMEISHA RASMI TAR. 9/11/2021, MATOKEO TAR. 8/5/2022.

Habari wadau,

Napenda kuchukua fursa hii kuwashukuru mlioufuatilia Uzi huu.

Niwashukuru pia wote mliotoa michango chanya, tulioulizana na kuelekezana pale ambapo palihitaji mawazo ya wenzetu wengine miongoni mwetu,-ilikuwa poa.

Lakini kipekee kabisa nachukuwa fursa hii kuwashukuru waliodiriki kutenga muda wao kuwasiliana nami moja kwa moja kupitia simu (+255714591548) pamoja na mtandao wa WhatsApp,- 'haikuboa'

Aidha shukrani za dhati ziwaendee walionitafuta na kunana nao ana kwa ana kwa kushauriana lakini pia kipekee zaidi kwa wale walioona umuhimu na uhitaji wao kwangu kwa mimi kuwachezea Bahati nasibu ya mwaka huu ingawa hata kabla ya mimi kuonana nao kila mmoja nilikiwa nikimsisitizia kuwa cha muhimu asome maelekezo na akiweza acheze mwenyewe hukohuko aliko lakini wao wakasisitiza wanione tu, guys, nimewapenda bure.

Sasa kwa-wale niliowahi kuwachezea miaka iliyopita na bado mkaona umuhimu wangu na kutaka niwacheze tena nyie mnayo sehemu yenu maalum na tulivu kule Mbinguni🤪
Kwani na 'Ankara' zenu pia zimenifanya nisikie vizuri🤸

Aidha niwape kongole pia wachache ambao mliona tushauriane tu kupitia simu kisha mjaze wenyewe huko mlipo pasi kuonana nanyi, mbarikiwe pia kwani kupanga ni kuchagua na kufanya ni kutaka kama mlivyoamua👍

Tuombe Mungu basi atufikishe salama tarehe 8, Mei 2022. ambapo ndipo rasmi matokeo ya Bahati nasibu yatakuwa tayari kwa kutazamwa na watakao bahatika kuendelea na mchakato kuienendea Viza ya kudumu ya U.S.

Uzi haujafungwa

Na tuendelee kuelimishana.

Ahsanteni.
 
Hii green card lottery mara nyingi watu wenye nafasi kubwa kushinda ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 25 kushuka chibi maana hawa wanabitajika Sana kwenda kutumika jeshini.

Kundi la pili ni wale wanaojua kuwa wana watoto hawa pia hupewa kipaumbele.
 
Hii green card lottery mara nyingi watu wenye nafasi kubwa kushinda ni wale wenye umri wa kuanzia miaka 25 kushuka chibi maana hawa wanabitajika Sana kwenda kutumika jeshini.

Kundi la pili ni wale wanaojua kuwa wana watoto hawa pia hupewa kipaumbele.
Hii taarifa umeitoa wapi mkuu?

Hakuna kipau mbele katika hii kitu,
Haya ni Matango poli yaliyoiva kabisa🤣

Kwanza umri kwa mshiriki si kigezo,
Kama sifa unazo hata ukiwa na miaka 100 ruksa kucheza na ukishinda wanakupa Viza na unaenda.

Kuhusu Jeshi,
Tangopoli hili ni kubwa zaidi.
Unadhani Wamarekani wanaokotaokota tu watu na kuwaingiza sekta nyeti kama Jeshi, mna masikhara nyie.

Huo mchujo wa kuingia jeshini sio wa kitoto,
Ni kweli umri mdogo ni mzuri ila haimaanishi kuwa utaingia kirahisi kama unavyojaribu kusema.

Tiketi yako;
Kuwa raia wa Tanzania
Kuwa na Elimu inayotakiwa
Fuata taratibu basi.

Ukichaguliwa hata na mkongojo wako unaingia Marekani.
 
Hii taarifa umeitoa wapi mkuu?

Hakuna kipau mbele katika hii kitu,
Haya ni Matango poli yaliyoiva kabisa🤣

Kwanza umri kwa mshiriki si kigezo,
Kama sifa unazo hata ukiwa na miaka 100 ruksa kucheza na ukishinda wanakupa Viza na unaenda.

Kuhusu Jeshi,
Tangopoli hili ni kubwa zaidi.
Unadhani Wamarekani wanaokotaokota tu watu na kuwaingiza sekta nyeti kama Jeshi, mna masikhara nyie.

Huo mchujo wa kuingia jeshini sio wa kitoto,
Ni kweli umri mdogo ni mzuri ila haimaanishi kuwa utaingia kirahisi kama unavyojaribu kusema.

Tiketi yako;
Kuwa raia wa Tanzania
Kuwa na Elimu inayotakiwa
Fuata taratibu basi.

Ukichaguliwa hata na mkongojo wako unaingia Marekani.
Hivi unadhani ukishinda tu unapewa Visa eeeh.
Kwa taatifa yako unaweza ukashinda lottery na bado usipewe visa; kitu unachotakiwa kujua lazima uende kwenye interview. Fuatilia itawkewa ni nini namaanisha.

Jwa kifupi naona tunajaribu kupungua kitu ambacho huna uelewa nacho. Kwa taatifa yako watu wote chini ya miaka 25 ukienda lazima ujiunge na kesho na usipofanya hivyo ujue itakusumbua baadae. Nina mifano mingi hai katika Hili.
 
Hivi unadhani ukishinda tu unapewa Visa eeeh.
Kwa taatifa yako unaweza ukashinda lottery na bado usipewe visa; kitu unachotakiwa kujua lazima uende kwenye interview. Fuatilia itawkewa ni nini namaanisha.

Jwa kifupi naona tunajaribu kupungua kitu ambacho huna uelewa nacho. Kwa taatifa yako watu wote chini ya miaka 25 ukienda lazima ujiunge na kesho na usipofanya hivyo ujue itakusumbua baadae. Nina mifano mingi hai katika Hili.
Baadhi ya Watanzania tuna shida,
Kugopa usichokijua na kukihubiri utadhani unakijua na mishipa ya shingo inakutoka.

Sasa unapotosha wasiojua maskini🤔

Tafadhali Soma, Soma nasema Soma.

Nachelea kusema hujui unachokisema hapa.

Mimi najua, nina uhakika na ninachokizungumzia lakini kwa sababu zilizo ndani ya uwezo wangu siwezi kuleta ushahidi hapa.

Lakini narudia kusema tena wewe hujui, na kibaya zaidi masikini hujui kuwa hujui.
Sasa nakushauri uishie hapahapa.
Usiwaaminishe watu ambacho si sahihi sababu ninao uhakika wa 110% hujui hata hii kitu ilianzishwa kwa malengo gani.
Achilia mbali kama maelekezo ya kila mwaka unayafuatilia.

Usikomae sana mkuu unazidi kupotosha.
Narudia tena huna taarifa sahihi acha kupotosha.
 
Hivi unadhani ukishinda tu unapewa Visa eeeh.
Kwa taatifa yako unaweza ukashinda lottery na bado usipewe visa; kitu unachotakiwa kujua lazima uende kwenye interview. Fuatilia itawkewa ni nini namaanisha.

Jwa kifupi naona tunajaribu kupungua kitu ambacho huna uelewa nacho. Kwa taatifa yako watu wote chini ya miaka 25 ukienda lazima ujiunge na kesho na usipofanya hivyo ujue itakusumbua baadae. Nina mifano mingi hai katika Hili.
Kama ni kweli unacho chanzo Cha taarifa, uwe makini na hicho chanzo.

Hapo palipokolezwa;
Hakuna kitu kama hicho.

Wageni hasa wenye umri mdogo huwa wanakimbilia Jeshini kutokana na fursa wanazozipata wakilitumikia Jeshi lakini si kuwa wanalazimishwa.

Narudia tena hulazimishwi,
hushawishiwi wala kubughudhiwi uingie Jeshi,
Wageni wenyewe ndio wanaopenda na pia si mserereko kuingia jeshi, ni mchakato ambao wengi wanachemsha pamoja na kutamani kuingia.

Kuhusu umri;
Anaeruhusiwa kushiriki DV maelekezo kwa mujibu wa rejea dvlottery.state.gov/instructions (chanzo pekee cha taarifa sahihi)
Ni kuanzia umri wa miaka 18 na kuendelea.
Haijatamkwa ukomo.

Maelekezo haya kila mwaka yatoka na huwa kunakuwa na maboresho madogomadogo ila sijawahi kuona ukomo wa umri hata mwaka mmoja Kati ya mingi iliyopita ambayo huwa Mimi nafuatilia.-
Ukihitaji pdf ninazo naweza kukupatia miaka mingi tu.

KWAHIYO HAKUNA UKOMO WA UMRI KUSHIRIKI UWE NA VIGEZO TU, UMEO/KUOLEWA/UNA WATOTO/ HUNA HAIJALISHI NA HAIKUNYIMI NAFASI.

Upendendeleo;
Kuhusu upendeleo/kipaumbele kwa mujibu wa maelekezo rasmi Hakuna kundi lolote linalopewa upendeleo kwa sababu yoyote Ile.

Labda tueleweshane kidogo;
Hii Bahati nasibu inachezwa kwa Komputa na Komputa yenyewe inachagua kwa style wanaita 'random' haiangalii nani, wawapi,mwenye rangi gani wala anaumri gani.

Kingine,
Ingekuwa lengo lao ni umri fulani tu unadhani wao ni wajinga kusema yeyote anaweza kucheza?
Kwani wanashindwa nini kusema wanataka vijana waende Jeshini kwao moja kwa moja?
Ili Mtu aamue mwenyewe mapema.
Kingine;
Hivi ina maana vijana wote waliowahi kupata DV wapo Jeshini huko Marekani sasahivi?
Someni Maelekezo rasmi kwa lengo la kuelewa.

Rai: Usimuamini sana mtu kwa kila anachokisema eti kwakuwa tu yupo Marekani hayo mambo ya zamani sana.
 
Back
Top Bottom