East African Federation (EAF) public Views

East African Federation (EAF) public Views

Chinga!

Kilichowatisha UK ni kwamba wao wanatoa graduate 400,000 kwa mwaka wakati China wanatoa 4,000,000. Na sasa hivi celebrity culture imetawala UK, watoto hawataki kuhangaika na sayansi kabisa, si unajua hivi karibuni University of Reading wametangaza kufunga idara yao ya fizikia in a few years time. Vilevile waajiri wanacomplain sana kuwa vijana are not fit for purpose, hesabu na kiingereza vinasumbua sana.
 
Mtz
sikutaka kwenda mbali, kutokana na kundi la wapinga elimu ninao ongea nao humu akina Lunyungu n.k
Brown AMEFANYA utafiti kwa nchi ya India ambapo hawapunguwi graduate milion 2, kwa mwaka na tena akafanya utafiti wa china na kuona hao milion 4.

....Amesema hadi kichina kifundishwe shuleni kukabiliana na ushindani huu. siwezi kusema mengi hapa.
nimefuarahi kuona nawe elimu inakukuna kama mimi na Mnyika.
 
Chinga,

Ninasikitika sana jinsi tunavyoichezea shule pale nyumbani. Unajua longolongo zote za maisha bora haziwezi kuja bila kuwekeza kwenye elimu. Unajua ukuaji wa uchumi unategemea sana mambo ya innovation ambayo yanakuwa driven na science and technology.

Sasa hebu kaangalie kwenye vyuo vyetu, vinapata pesa kiasi gani ya kufanyia research? hamna hata kidogo, kwa nini sasa Maprof wasikimbile kwenye politiki? inasikitisha sana leo hii mwanafunzi wa chuo kikuu kupata lecture akiwa amekaa kwenye sakafu. Yaani tunadhihaki elimu kwa kiasi kikubwa sana. We really need to invest in education at all levels. Kwa wana academia wa bongo, hebu angalia leo hii inavyotia udhia kusoma essays za wanafunzi wa chuo kikuu kwa jinsi wasivyojua kiingereza na jinsi wanavyoshindwa kutoa critical analysis as expected. Je ni kweli graduates wetu wataweza kucompete kwenye globalised labour market kwa mwendo huu?
 
Mwanasiasa,

Heshima yako mkuu, nimekusikia na Mzee Chinga, lets move on to the next topic, unless JJ akija na mpya then turudi hapa kumkoma nyani giladi!
 
Chinga una yako,
Nimesema hakuna mtu mwenye akili timamu ambae hataki kutafuta maarifa zaidi. Ndio maana nimekubaliana na hoja za Mzee ES na Mwanasiasa. Ya kwamba Elimu ni nyezo muhimu ya ukumbozi na Mnyika ni lazima amelizie shule na hata aongeze daraja.

Ikiwa Mnyika ni kiongozi mwenye akili timamu, huwezi kusemwa ana shauriwa vibaya, hayo mwachie JK na Lowassa, wana wa miungu ambao huwa hawakosei, wakichemka husemwa wameshauriwa vibaya!
 
Dr WHO,

Nasema kwamba Mnyika hawezi kuwa kibraka wa mtu yoyote kama ambavo chinga anaonyesha kwamba wakina Mtei na Mbowe ndio wanamzuia kusoma. Mnyika anajua analofanya,anashaurika na anajua jema na baya. Anasimama kwa miguu yake mwenyewe. Si kweli kwamba anaendeshwa endeshwa kirahisi na watu.
 
Chadema wapo kwenye hii bodi, wako wapi? Mbona hawajibu masuala yaliyoulizwa kuhusu helikopta pamoja na msimamo mzima wa Chadema kuhusu Education?

Waliotumwa na Chadema waache mashambulizi yasiyo na msingi bali wajibu hoja.

Jibuni hoja …..hoja………hoja…..
 
Mwanakijiji
tunaomba wimbo wa vunja mifupa bado meno ipo.

'peleka mtoto shule apate elimu itamsaidia kwa maisha yake'

Mwanakijiji nimeusahau huu wimbo tuweke, una mafunzo makubwa sana.
 
Sawa,
Mnyika, weka 'priorities' zako sawa: shule, shule, tena haraka kabisa, na isiwe shule ya kiduchuduchu; kwani inaelekea uwezo unao mzuri tu wa kukufikisha hatua yoyote utakayopenda kuifikia. Siasa utaikuta, na tena ndio itakuwa inanoga haswa.
Huna sababu yoyote ya maana zaidi ya kuendelea kukupoteza muda wako.

Kuhusu hayo mambo mengineyo, sasa nimeelewa maana ya akina CHADEMA wengi kumcharukia Chinga.
 
No way can can janjaweed be allowed in this community!! Wanapaswa kujua we can comfortably torelate interahamwe na banyamulenge kwani the're easily contained lakini siyo janjaweed. ISITOSHE SHARIA KWETU NI UCHURO...
 
It is just amazing how some Tanzanians think that Rwanda and Burundi is a burden to the East African Community.

While Uganda and Kenya are very welcoming new members, some Tanzanian's news papers are busy trying to argue how ujambazi has been the fruit of illegal immigrants from these two nations!! One of the author mentions how Kagera and Kigoma regions have been affected by these two neigboring nations. One of Charactestics of xenophobia is trying to blame everything on foreigners when in actual fact have nothing to do with whatever happens. The statistics show that Dar-es-salaam has the more crimes than Kagera and Kigoma combined.

Now, is Dar's crimes linked to Rwanda and Burundi? Doesn't the Kilimanjaro and Arusha crime rates including using weapons higher than Kigoma and Kagera? It think it is high time to deal with the problem at hand than blaming foreigners for everything that happens within the country.
 
Eric
Mnyika mawazo yake ni ya kushikiwa, hana maamuzi yeyote na kibaya waliomzunguuka hawana upeo wa shule, ndio sisi wapenda maendeleo na mabadiliko ya kweli tuna mshikia bango akasome.
fikiria Eric hayo mabadiliko na maendeleo yatakuja bila elimu?

Naamini katika hizi posts zangu nimsaidia Mnyika kama Mnyika na pia chama kutoka kwenye NGO na kuwa chama chenye sura ya kitaifa.
najua naweza kuumizwa na wanachama wa chadema, lakini ukweli lazima usemwe.

kuna bosi waTRA alipelekwa Kilimanjaro kusimamia ushuru pale Holili maana kuna vuja sana kodi, jamaa wa kaskazini walivamia nyumba yake na kuinyoma moto ili wamuuwe yule afisa TRA aliyekuwa akifanya kazi kama taratibu zinavyotakiwa.

na mimi siogopi hata kunikuta yalimkuta jamaa wa Holili ambaye amerudishwa makao makuu TRA.

nAjua ukweli unauma sana, na jina langu litatajwa sana humu. ndio unaona kila dakika members wapya wana join forum, kuja kupambana na chinga.
hata waje elfu nitawashinda kwani hoja zangu za msingi hawajibu.
 
Kwanza nina furaha kubwa kwa sababu baada ya miaka karibu 30,
wanainchi wa Afrika Mashariki wamepata fursa ya kurejesha umoja wao
amboa siasa na ujeuri iliharibu. Shukurani zangu ni kwa wanainchi wa
nchi hizi tatu amboa bila idhini na nia yao, hatungekuwa na Jumuia
hiyo.

Lakini ningependa kuwaonyeni na kuwatahadharisha juu ya wanasiasa
ambao tusipo chunga wataharibu umoja wa Afrika Mashariki. Naanza na
Kenya:

Katika Kenya, wanasiasa wamekuwa maarufu kwa kupenda na kukuza
mamlaka yao sana. Kwa mfano wabunge wamejiongezea mishahara na
marupurupu kufika kiwango cha fedheha kubwa kwa nchi nzima. Raisi wa
nchi na wanasiasa marafiki zake wangependa aendelee kuongoza nchi
mpaka siku ya kwenda kwake ahera. mwongozo kama huo kamwe hawendi
sambamba na umoja wa jumia. Taifa kujiunga katika umoja na mataifa
mengine ni kwanza hilo taifa kujinyima na kuwapa mataifa wenzake
zaidi. Kwa hivyo Kenya haiko tayari kutupilia mbali siasa za ndani,
uhuru wake na uchumi wake bora ili kukubali jumuia. Wanainchi wa
taifa la Kenya wangependa Jumuia ya Afrika Mashariki, lakini serikali
haitaki sababu wanasiasa watapoteza raha zao.

Uganda
Kuna woga mwingi Uganda juu ya Jumuia. Hata ingawa raisi Museveni
amesimama msitari wa mbele katika kutafuta umoja wa Jumuia ya Afrika
Mashariki, wanainchi wake wameonyesha woga kwamba wakenya watanunua
mali na kutwaa uzalishaji wa nchi. Wanahofia kwamba viwanda vya
Uganda havitaweza kushindana na vile vya Kenya. Jee, kama kuna Dola
moja la Afrika Mashariki, Mkenya au mganda atakuwa ni nani? Kama
kiwanda hakiwezi kushindana na kiwanda kilicho Kenya, je hicho
kiwanda kitaweza mashindano na viwanda vya madola ya Ulaya na
Merekani? Umoja gani ambao waweza kuendelea mbele bila wanainchi wake
wote kuwa na haki sawa ya kutembea, kununua na kutia rasmali popote
pale wanapotaka?

Tanzania

Hapa, uwongozi umeanguka dafrau. Porojo kali inachapishwa kwenye
magazeti na majarida ya nchi hio ikitoa madai yasiokuwa ya kweli
kwamba wakenya watanunua nchi nzima na kazi zote zitachukuliwa na
waganda na kadhalika. Cha kushangaza ni kwamba serikali ya nchi hio,
imeamua kunyamaza badala ya kujibu propaganda hiyo kali kwa ukweli na
kwa ufasaha. Kwa mara nyingene tena twaona woga ukitawala juu ya
ukweli.

Hatuwezi kuingia katika jumia ya Afrika Mashariki na ukabila na
utaifa. Yafaa wanaichi wawe huru kuhama na kwenda mahali popote
kwenya dola. Kwa mfano, hakuna mhehe hata mmoja sehemu niliyo zaliwa.
Ninge penda wahehe wahamie huko ili watu wangu wasiwe wanadhania
wahehe ni watu walio kaitka simulizi za zamani
 
Chinga nimekuuliza kwenye thread ingine, lini utaacha kuwa simplistic na propagandist?

Wacha: helikopta ni chombo cha usafiri kitachorahisisha ujumbe wa CHADEMA kufika katika sehemu mbalimbali za nchi kwa muda mfupi na kwa gharama nafuu. Kuna cha kujibu zaidi hapa? Lakini unaweza ukatoa tafsiri ingine unayopenda. Hata kwa gari ya kawaida, kuna watu wengine wanaona gari kama chombo cha usafiri kukutoa sehemu moja kwenda nyingine. Kuna wengine wanaona gari kama symbol of status. So, it is the question of perception, na hamna kitu kigumu kama kumzuia binadamu kufikiri anavyotaka!
 
Wacha: Nilisahau swali lako kuhusu education:Hili ni swali kubwa linalohitaji muda na nafasi zaidi, labda ungekuwa specific. Kuhusu nini katika elimu: ubora, gharama, na elimu gani: ya msingi, sekondari au ya juu?

Kwa sasa nikwambia tu kuwa CHADEMA hairidhishwi na ubora wa elimu tuliyo nayo. Moja ya sera za CHADEMA ni kuongoza fedha kwenda katika mashule. Kwa mawzo yangu kama mwana CHADEMA na wala sio kama chama (maana hili linahitaji kiongozi) ningependa pesa zaidi ziende mashuleni sio kubaki pale makao makuu ya wizara ya elimu. Ni rahisi sana kusema bajeti ya elimu imeongezeka. Kitu kigumu kujua ni pesa kiasi gani hasa imefika mashuleni. Ningependa pesa zaidi zitengwa kwa ajili ya mafunzo ya walimu, vitendea kazi, kulipa walimu mishahara yenye hadhi, nk. Hasa katika ku-train walimu katika kiwango kinachokubalika. Kwa kuanzia, kiwango cha chini cha mwalimu kiwe diploma katika elimu inayopatikana kwa mafunzo yasiyopungua miaka miwili. Serikali ya awamu ya nne ilianza na kuitukana fani ya ualimu na elimu kwa ujumla kwa kuwafundisha vijana waliomaliza form siksi kwa wiki 4 na kuwapatia kazi ya kufundisha. Haya ni matusi, lakini kama kawaida ya wtanzania tuliona hamna neno maadamu athari zake sio za papohapo kama za umeme.

Mpango wa muda mrefu ni kuwa na walimu wenye ngazi ya kuanzia shahada. Shahada za ualimu lazima ziwe kwa ngazi husika. Kwa mfano shahada katika elimu ya msingi, sekondari, nk. Mtindo wa sasa hivi wa kutoa shahada ya ualimu tu inatupa walimu walio bora katika taaluma (academics) lakini sio katika ujuzi wa ualimu (professional teachers).

Kubwa sana katika walimu, itabidi kulipa walimu mishahara itakayowawezesha angalau kumudu maisha ya kawaida. Sio lazima kuwalipa mishahara itakayowafanya wawe matajiri, bali mishahara yenye kuipa ualimu hadhi. Watanzania tuna shida sana katika hili. Tumekubali kukabidhi watoto wetu watu ambao serikali inawadharau na iliyowafikisha mahala pa kutokuthamini kazi zao. No wonder, tunatoa vijana wa ajabuajabu katika mashule yetu. Kwa hiyo hatua moja kubwa ni kurudisha heshima ya walimu kwa kuwalipa mishahara kama wafanyakazi wengine wa serikali au zaidi. Ni kwa njia hii tutavutia vijana wanaofaulu vizuri kujiunga na vyuo vya ualimu.

Kama nilivyosema hapo juu, swali lako Wacha ni pana mno; inabidi ujifunze kuuliza maswali, usiwe kama waandishi wa habari wa bongo! if you ask a too general question, you get a too general answer!
 
Mwanasiasa.
Tunataka sera ya chama sio mawazo yako? au mkiingia madarakani, mtakuwa na special arrangement kama akina Mbowe na Mnyika?
 
Mnyika.
wewe ni mkurugenzi wa chama ina maana huna access za mtandao? ulisema utakuja kujibu humu tarehe 5 na leo 11.
chama utaendesha vipi? kama huwezi kufanya vitu within a deadline?
kuna kazi huko chadema.
 
Written by Eric Shimoli and David Mugonyi, The Nation

PRESIDENT Kibaki on Wednesday turned down the hefty salary increase given to him by Parliament last week. The President said he had weighed the implications of the increase and decided to reject the Sh3.2 million monthly pay package.

"I thank the National Assembly for seeing it fit to award the President the salary increment. I have taken note of the decision reached and weighed its implications under the current economic conditions prevailing in the country, and do hereby turn down the offer," he said in a statement last night.

Get the whole story thru: http://jambotanzania.net/v2/content/view/948/2/
 
Back
Top Bottom