Edo Kumwembe: Ningekuwa mshauri wa Mbowe, ningemshauri ajiondoe katika kinyang'anyiro

Edo Kumwembe: Ningekuwa mshauri wa Mbowe, ningemshauri ajiondoe katika kinyang'anyiro

Ubaya Ubwela

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2024
Posts
1,353
Reaction score
3,060
Mtangazaji wa kipindi cha Jana na Leo kutoka Wasafi Fm, Edo Kumwembe amesema angekuwa mshauri wa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Freeman Mbowe angemshauri kujiondoa katika kinyang'anyiro cha Uenyekiti kisha atangaze kumuunga mkono mpinzani wake Tundu Lissu

Edo amesema “ningekuwa mshauri wa Mbowe ningemwambia Mbowe ajiondoe kwenye kinyang'anyiro na ajiondoe kable ya boksi la kura na atangaze kumuunga mkono Lissu”

Soma: Godbless Lema: Namuomba Mbowe apumzike, amuachie Lissu afanye kazi ya Uenyekiti CHADEMA

Edo ameeleza sababu ya yeye kuwaza hivyo ni kutokana na Lissu kuungwa mkono na watu wenye ushawishi na nguvu katika siasa za upinzani hasa CHADEMA.

“watu ambao wanatangaza kuwa upande wa Lissu ni watu wazito sana kwa CHADEMA, John Heche Heche na ana kanda yake, Lema kwa kaskazini lema na kama angesema anamuunga mkono Mbowe kidogo watu wangeyumba, Lissu hao wote ni watu wazito sana kwenye hicho chama”

Ameongeza kuwa kama Mbowe atashinda atakuwa na wakati mgumu kuongoza bila uwepo wa watu hao watatu “fanya Mbowe umeshinda unaongozaje bila hao makamanda, na hao makamanda wana vitu moyoni ukiwasikiliza kulikuwa na mipango ya kuwaondoa kutoka kwa Freeman aweke watu wengine”

Pamoja na hayo amejaribu kuelezea namna watu hao walivyopambania CHADEMA kwa kukaa jela pamoja na kupigwa na polisi wakati mwingine.

Aidha amekumbusha kuwa moja ya pigo alilopata Mbowe ni kushinda kwa Wakili Deogratius Mahinyila Adv Mahinyila kuwa Mwenyekiti wa BAVICHA ambapo pia anamuunga mkono Lissu
 
Mbowe hana washauri wazuri amezungukwa na wapiga dili.
Pili hayupo kwa maslahi ya CHADEMA zaidi bali kwa mama wa maridhiano, kitendo cha kutaka kuwaweka kando wapinga maridhiano na kupata support kutoka makada wa CCM ina maana ameamua kugombea kwa maslahi ya CCM
 
Kwahiyo akishinda heshima yake itashuka?

Mbowe hataki kugeuka jiwe, fuatilia hadithi hii alitusimulia Baba wa Taifa.
Possibility za kushinda ni ndogo mno kwa nini asikae pembeni kwa heshima kubwa aliyojijengea?
Angalia hata uchaguzi wa BAVICHA shangwe la wajumbe kwa Lissu na Mbowe utajua amepoteza haiba ya uongozi CHADEMA
 
Possibility za kushinda ni ndogo mno kwa nini asikae pembeni kwa heshima kubwa aliyojijengea?
Angalia hata uchaguzi wa BAVICHA shangwe la wajumbe kwa Lissu na Mbowe utajua amepoteza haiba ya uongozi CHADEMA
Hilo tukio lilinifurahisha lakini kiukweli nilihuzunika sana, Mbowe sio wa kufikia hatua ile.

Mbowe anatupa wakati mgumu wa kumkataa kwa heshima aliyoijenga juu yetu.
 
Mbowe hana washauri wazuri amezungukwa na wapiga dili.
Pili hayupo kwa maslahi ya CHADEMA zaidi bali kwa mama wa maridhiano, kitendo cha kutaka kuwaweka kando wapinga maridhiano na kupata support kutoka makada wa CCM ina maana ameamua kugombea kwa maslahi ya CCM
Hawa ndiyo aina ya washauri wa Mbowe
 

Attachments

  • GgorHp4XUAAE0_u.jpeg
    GgorHp4XUAAE0_u.jpeg
    51.3 KB · Views: 2
  • GfMNLpyXYAA8ucg.jpeg
    GfMNLpyXYAA8ucg.jpeg
    58.9 KB · Views: 2
Jinsi upepo unavyovuma ndani ya CHADEMA kwa asilimia kubwa Mhe. Mbowe hana chake tena. Mhe. Mbowe kubali yaishe na ujitoe kwenye uchaguzi wa tarehe 21.1.2025. Wanachama bado wanakupenda na utaendelea kupendwa kwa sababu umekitoa CHADEMA mbali.
 
Back
Top Bottom