KAMA bao la penalti laini ya Saido Ntibazonkiza dhidi ya Asec Mimosas lingesimama kwa dakika zote tisini si ajabu mashabiki na viongozi wa Simba wangerudi katika dunia yao ya njozi kwamba bado wana timu bora kwa ukanda huu wa Afrika mashariki.
Si ajabu pia wangeendelea kuota ile njozi maarufu kwamba wao wanakuwa kitu tofauti linapokuja suala la michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika. Safari hii walikumbushwa tu kwamba timu yao ni ile ile tu ya kawaida ambayo wamekuwa wakiishuhudia katika miaka ya karibuni.
Ilianzia katika pambano dhidi ya Yanga. Lilikuwa ni suala la muda tu kabla Simba haijapokea kichapo kile cha mabao matano kutoka kwa mtani. Kibinadamu kama wachezaji wa Simba wangehisi kwamba wamewaangusha mashabiki wao basi wangejibu mapigo katika pambano lililofuata dhidi ya Namungo kwenye uwanja wa zamani wa Taifa.
Mwanaspoti
Si ajabu pia wangeendelea kuota ile njozi maarufu kwamba wao wanakuwa kitu tofauti linapokuja suala la michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika. Safari hii walikumbushwa tu kwamba timu yao ni ile ile tu ya kawaida ambayo wamekuwa wakiishuhudia katika miaka ya karibuni.
Ilianzia katika pambano dhidi ya Yanga. Lilikuwa ni suala la muda tu kabla Simba haijapokea kichapo kile cha mabao matano kutoka kwa mtani. Kibinadamu kama wachezaji wa Simba wangehisi kwamba wamewaangusha mashabiki wao basi wangejibu mapigo katika pambano lililofuata dhidi ya Namungo kwenye uwanja wa zamani wa Taifa.
Mwanaspoti