Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Kama ulifikiria imekujengea historia yoyote ya maana, basi aliyekushauri amekudanganya/amekupoteza. Hata huyo aliyekupokea naye anaingia katika historia za wanasiasa wa hovyo katika historia ya siasa za Tanzania. Kama kuna historia concrete itaandikwa na wana vyuoni, basi jina lako litaandikwa kwnye karatasi za mawe!
Ungeli retire siasa labda ingelikujengea heshima zaidi. Kashifa za ufisadi unaotuhumiwa nao hakuna mwenye ushahidi usiokuwa na mashaka! Hivyo bado heshima yako ingelisimama
Hapana Retired; usimuone hivi Lowassa na nadhani si haki kumuona hivyo. Wale wote waliomuunga mkono na kumtumia alipokuja inapaswa kumshukuru tu na kumtakia kila la kheri. Haya mengine si ya lazima. Sidhani kama kurudi kwake ni jambo la kushangaza au kushtua vile. Kwamba alibakia kwa miaka mitatu lazima mumpe hongera na shukrani zake.
 
Kwa ukumbusho tu...

Dr. Slaa alihamia Chadema akitokea CCM baada ya jina lake kukatwa kwa namna ile ile Lowassa alivyohamia Chadema kutoka CCM baada ya jina lake kukatwa.

Dr. Slaa baada ya kukaribishwa Chadema alipewa fursa ya kugombea nafasi ile ile aliyoikosa CCM na hivyo hivyo Lowassa naye baada ya kukaribishwa Chadema alipewa fursa ya kugombea nafasi ile ile aliyoikosa CCM.

Tofauti ni kwamba Dr. Slaa alishinda uchaguzi lakini Lowassa alinyimwa ushindi. Naomba tu tuweke kumbukumbu sahihi...wote wawili waliikuta Chadema ikawasetiri na hakuna ajabu wakiamua kwa nyakati tofauti kurudi nyumbani CCM.

Wote wawili hakuna aliyeonja ladha ya kupigania mageuzi nchini, walikuwa wanakula kivulini wanamageuzi wakihangaika juani. Wote wawili hawajui gharama za kudai mabadiliko waliyolipa wana mageuzi.

Nyumbu 😆😆😆😆😅
 
Msiba wa Ruge?

Hapana. Hakuna sababu ya msingi kwa Lowassa "ku-divert attention ya Watanzania kutoka kwenye msiba wa kitaifa wa Ruge."

Hata hisia kuwa "kuna mkono wa mtu kwenye kifo cha Ruge" hazijapata umaarufu kiasi cha kupelekea Lowassa akurupushwe leo ili "azime" suala hilo.

Kuwatenga waliomtosa Lowassa?

Uwepo wa Rostam Aziz katika tukio unaweza kuwa ishara ya uhusika wake katika uamuzi wa Lowassa kurejea CCM. Na uhusika wake unaweza kumaanisha kuwa "mapacha wawili kati ya watatu" wa MTANDAO wa JK (JK mwenyewe, Lowassa na Rostam) sasa wapo kwa Jiwe.

And where does that leave JK? Well, he was the major force behind kutoswa Lowassa. With him were Mkapa na Mwinyi. Sio siri kuwa wote watatu have fallen out of favour with Jiwe.

Nadhani katika hili labda tuache muda uongee.

October surprise?

Katika siasa za uchaguzi huko Marekani, "October surprise" ni tukio la makusudi linalolenga ku-influence matokeo ya uchaguzi.

Ninaazima political jargon hiyo kumaanisha kuwa huenda tukio hilo la leo linalenga ku-preempt tukio jingine kubwa ambalo "mtu flani" anatarajia linaweza "kupozwa" na ujio wa Lowassa huko CCM pindi tukio hilo likitokea.

Ugumu wa kuongelea tukio hili kama ule uliojitokeza katika kujadili uwezekano wa Lowassa kurejea CCM. Kila baadhi yetu tulipofungua mdomo sio tu kubashiri kuwa Lowassa angerudi CCM bali pia kumtuhumu kuwa huenda anakihujumu chama hicho, tuliishia kutukanwa



Kwahiyo to be on the safer side, si vema kuongelea kitu ambacho huenda kikatafsiriwa kuwa ill wish if not sedition. But something is indeed cooking.

Nafsi inakataa sio kuamini kuwa kweli Lowassa karudi CCM (lilikuwa suala la when na sio if) bali kuamini kuwa kurudi kwake CCM LEO ni kwa vile "leo ni siku kama nyingine."

Time will tell.




Sent using Jamii Forums mobile app


You have to accept the fact that this time you were really caught up by surprise, big time.

This is the real show how these mind games are played.
 
Hujui shost kuwa Lowasa ni mwana CCM kuanzia March 1, 2019
Yaani jana? Mhu mimi naona bora liende. Pole yao watoto wanaokua na watakaozaliwa. Kuna nchi zinasemwa vibaya kisiasa ila kimaendeleo Bongo haioni ndani. Uchumi wao ni wa kiwango cha juu, huku maji bure, umeme unawasha AC mwisho wa mwezi ukilipa nyingi dollar 40, elimu bure na darasani watoto hawazidi 45. Ni nchi inasemekana haina demokrasia ila ni nchi ambayo ukiishi utafikiri upo jimbo mojawapo USA hata viunga vya NY. Huku watu ni wastaarabu ila siasa hawataki kusikia.
 
Viongozi na wafuasi wa Chadema hujiadai wanajitambua na wenye uelewa sana kumbe kinyume chake

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa karudi yule Mnayemuita Fisadi. Imekaaje hapo? Mliyesema hadharani kwenye Kampeni hafai kwenda jumba jeupe alijinyea Geita ni mgonjwa! Pale so wodi ya Wagonjwa kaja. Tusiokuwa na vyama tulikaa mbali tukisikiliza Kashfa kwa EL. Sasa Fisadi anapokelewa na wote. Mbona haambiwi no baki huko huko?
 
Zaidi ya nusu ya viti vya cdm bungeni 2020 havitakuwepo . Anayebisha twende MKEKA BETTING. Najua mijawpo ya agenda cdm 2020 ni Koroshow ,Dollar Ajira na hali ya maisha.
Usanii wa kuyajibu maji yanachemka

Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani kama wana hamu tena ya kuomba kura. Hakika cha Moto wamekipata enzi hii. Mimi naona ni kupoteza fedha. Uchaguzi uwe tu kupita bila kupingwa, because upinzani hawatashinda Popote!
 
1) Wakati Lowasa yupo CCM:
• Chadema walimwita Kubwa la Mafisadi
• CCM wakamwita Msafi


2) Wakati Lowasa anagombea Uraisi Chadema:
• CCM walimwita Kubwa la Mafisadi
• Chadema walimwita Msafi


3) Wakati Lowasa amerudi CCM
• Chadema wanamwita Msafi
• CCM watamwita ????


Hapo ni jibu tosha Kuwa Chadema either ni Mbumbumbu wanafuata upepo tu au Wanajua wanachokifanya Bali ni Wanafiki tu.

Lakini Leo hawajioni kuwa Hata wao Walimsafisha Lowasa na kusema si Fisadi na kutaka kumpa Uraisi..

Lakini Leo Wanaanza kumeza maneno yao.

Vyama vyote vya siasa hapa Nchini ni Wanafiki Watupu na Ndiyomana hata CCM watamsafisha Lowasa waliyemwita Fisadi.
 
Kama ulifikiria imekujengea historia yoyote ya maana, basi aliyekushauri amekudanganya/amekupoteza. Hata huyo aliyekupokea naye anaingia katika historia za wanasiasa wa hovyo katika historia ya siasa za Tanzania. Kama kuna historia concrete itaandikwa na wana vyuoni, basi jina lako litaandikwa kwnye karatasi za mawe!
Ungeli retire siasa labda ingelikujengea heshima zaidi. Kashifa za ufisadi unaotuhumiwa nao hakuna mwenye ushahidi usiokuwa na mashaka! Hivyo bado heshima yako ingelisimama
Hesabu na "timing" ya nhe Lowasa ni zero na inampa taswira halisi.
Lowasa alihamia CHADEMA waliokuwa wamemwandama kwa kumtuhumu kwa ufisadi baada ya Mbowe "kubadili gia angani" ili kupata fursa ya kugombea nafasi ya uras kwa tiketi ya chama hicho. Akashindwa katika Uchaguzi Mkuu. Kumbe kama ilivyokuwa kwa Augustine Mrema, alistahili kushindwa. Naye asingetosha kuongoza nchi. Angewezaje kama hana anayoyaamiji wala msimamo?
Pamoja na nia yake ya kuhami mali zake dhidi ya pokonya pokonya ya mamlaka husika inayoendelea, heshima yake na jeuri ya kikwao viko wapi? Jambo la uhakika ni kuwa amejiabisha, amejimaliza, na hatathaninika na Watanzania.
 
Back
Top Bottom