Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama


Naheshimu kutofautiana mawazo maana ndio afya ya mijadala.
 
Huu mwandiko ukiusoma kwa makini zaidi unaweza kujiwa na hisia kuwa Mzee mwanakijiji ni Dr Slaa mwenyewe . Hisia hizi zimetokana na baadhi ya hoja kwenye hili andiko kuwa ni hoja za kujitetea lakini zisizo na misingi yoyote.

Kwa mfano Mwanakijiji anasema eti Dr Slaa ni mwanasiasa bora kuliko mwanasiasa mwingine yoyote kwa sasa ,hii ni hoja dhaifu sàna . Ni hoja ya kihisia na kijipendelea zaidi kuliko uhalisia mwenyewe.


Hoja nyingine anasema eti kuwa balozi si lazima uwe mwana ccm ,hii ni hoja kituko kabisa . Tangu lini ccm ikachagua mpinzani wa kweli kuwa balozi. eti Dr Mkumbo alikuwa mpinzani na akachaguliwa kuwa katibu wa wizara ,hiki nacho ni kichekeho tangu lini Mkumbo alikuwa mpinzani?

Tatu Mwanakijiji anasema kuwa hajaona tatizo lolote kwenye awamu hii . Hii inashangaza sana . Kwani kwa hali ilivyo sasa katika sekta zote hata mtoto wa darasa la saba anajua kuwa liko tatizo.

La mwisho kabisa naomba nikubaliane na baadhi ya hoja za Mwanakijiji( Dr Slaa) kwa mfano ni kweli kabisa Chadema lazima wawe makini zaidi linapokuja swala la kupokea wageni kutoka upande wa pili. Nadhani tukio hili la mzee wetu kurudi nyumbani kwao limeacha fundisho kubwa kwa upinzani.

Hongera mzee wetu . Uwe na mapumziko mema huko nyumbani kwako , maana upande huu wa pili umejaa mateso na mahangaiko mengi sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mzee mbona maneno mengi ,kuondoka kwa Lowasa Hakuna hasara yoyote ile zaidi ya faida ,Mzee hebu Fanya formative and summative evaluation , acha ushabiki .
 
Mzee mbona maneno mengi ,kuondoka kwa Lowasa Hakuna hasara yoyote ile zaidi ya faida ,Mzee hebu Fanya formative and summative evaluation , acha ushabiki .
 
Shikamoo mkuu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nikiri wazi Mkuu kuwa Umenenena Vyema Na Nakubaliana Na Mawazo yako,unajua Hawa Kenge Aina Ya Mzee Mwanakijiji wamekuja Na Makala Ndeefu ambazo Mtu Ukizivamia Kwa Pupa unaweza Ukadhani Jamaa Wamekuja Na Recovery Plan Kwa ajili ya Upinzani Kujikwamua na Mkwamo Uliopo Sasa ila naomba nikuhakikishie Ndg.kitaturu Upo Sahihi 100% tangu Lini Magamba Kama Mzee Mwanakijiji wakautakia Mema Upinzani?? Waache Kutuhadaa Aisee kila Mtu apambane Na Hali ya Kwenye Chama Chake..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tz kuna wapinzani watatu kuwahi kutishia ccm...

Wakwanza ni Maalim Seifu
Wapili ni Dr Slaa
Watatu ni Tundu Lissu...

Sasa kabakia Lissu, sema walichompatia ni kumvunja miguu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Huna jipya
 
Ccm bana wanapenda siasa nyepesi eti, wameandaa maandamano kesho ya kuuga mkono kutoka Lowasa kuondoka sebuleni kuhamia chooni
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…