Edward Lowassa arejea CCM, apokelewa na Uongozi wa juu wa chama

Tatizo wanajua kucheza na upinzani hawajui kucheza na wanainchi.

sisi wanainchi lowasa au mbowe kuhamia ccm kwetu sio jambo kubwa. kwetu sisi tunataka nafuu ya maisha. tufanye biashara vizuri tulime tusipangiwe kwenye uuzaji.
 
Ni ufinyu mkubwa wa akili kudhani kwamba kuondoka kwa fisadi lowassa chadema imevunjwa uti wa mgongo. Hakuwahi hata kwa sekunde moja huyu fisadi kuwa uti wa mgongo. Acha UZUSHI wa kuandika pumba humu. Hebu twambie positive impact ya huyu muongo mkubwa na fisadi aliyekubuhu katika miaka mitatu na ushee akiwa chadema, ambaye kipindi kirefu alikuwa kimya.


 
Ruge huyu jamaa itakuwa ameuwawa na sumu kali sana sana kama polonium-210 tena itakuwa alikula, aliivuta au alikunywa huenda ilikuwa ni dozi ndogo aliyopewa na mtaalam wa hali ya juu. Mazingira yanaonyesha kabisa maana tangia mwaka jana alipoanza kujisikia vibaya akiwa kwenye hafla fulani.

Dalili za kupewa sumu ndo hizo kujisikia vibaya kuharisha, kutapika na baadhi ya organ za mwili kushindwa kufanya kazi vizuri na mwishowe kifo. Anyway hii inaonyesha serekale tuliyonayo ni ya aina gani.

Kwenye kumuaga Ruge kuna watu watalia sana kuliko wenye msiba ila ili ku shift attention wakaona wafanye wanamleta mzee Lowassa ila watambue CCM makada ipo siku watakuwa wakimbizi. Waanze kuandaa sehemu z kukimbilia maana sasa mambo yamekwiva

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karibu tena nyumbani.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
siasa ni mchezo wa hovyo sanaa nakumbuka wale waliokuwa wakiimba siku ile dodoma ktk ule ukumbi wao walikuwa wakiimba '' ninaa imaniii na Lowasaaaa nina imaniiii na Lowasaaaaa '' ss sijui itakuwaje
 
ila Lisu hawezi itikisa CCM ni mwepesi kama karatasi..hakuna aliyewahi kuwa naye Karibu kwenye mfumo. .Lowasa alitikisa na bado hakufurukuta..
 
Mwacheni Lowassa ahamie CCM ni haki yake ya kikatiba. 2020 kuna mtu atarudi tena Chadema.

Sent using Jamii Forums mobile app
Marekebisho ya sheria ya vyama vya siasa vinataka mgombea wa kitaifa awe amejiunga na chama zaidi ya mwaka. Hivyo muda mwafaka wa wanasiasa kuhama ndio huu kama wana nia ya kuteuliwa kugombea nafasi yoyote ya kitaifa na chama husika.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dr slaa cyo ccm.
mbowe anapaswa kuwajibika kwa aibu lake hili.
tulimwonya akakaidi haya ndyo matunda yake yakutema big g kwa karanga ya kuonjeshwa
 
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) nchini Tanzania kimesema kuondoka kwa mwanachama wake, Edward Lowassa na kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM) hakutakuwa na madhara yoyote.

Hayo yamesemwa leo Ijumaa Machi 1, 2019 na Katibu Mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani Tanzania, Dk Vicent Mashinji alipozungumza na Mwananchi muda mfupi baada ya Lowassa ambaye ni waziri mkuu wa zamani kutangaza uamuzi huo.

“Tunamtakia maisha mema huko aendapo, yeye ni mtu mzima anajua anachokifanya,” amesema Dk Mashinji.
Alipoulizwa iwapo uamuzi wa Lowassa unaweza kukitetelesha chama hicho kikuu cha upinzani Dk Mashinji amejibu kwa kifupi “It will never happen"(haiwezi kutokea).

Na Tausi Mbowe, Mwananchi
CHADEMA YAFUNGUKA LOWASSA KUREJEA CCM..."YEYE NI MTU MZIMA ANAJUA ANACHOKIFANYA"

Neno la Sumaye baada ya Lowassa kurejea CCM

Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani, Frederick Sumaye ameeleza maoni yake baada ya kusikia Edward Lowassa kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Sumaye amesema "Mimi haunipi shida, mtu akiamua kuhama chama na kwenda kingine ni uamuzi wake,” alisema Sumaye.

"Kama kaamua acha aende, sisi tutaendelea kujenga chama na hicho unachokisema cha kuhama ni ndoto ambayo haipo,” amesema Sumaye alipoulizwa kama na yeye ni miongoni mwa watakaorejea CCM.

Edward Lowassa alijiunga CHADEMA Julai 2015 baada ya jina lake kuenguliwa kwenye mchakato wa kutafuta mgombea wa Urais ndani ya CCM


Neno la Sumaye baada ya Lowassa kurejea CCM - MUUNGWANA BLOG
 
Mwenye ile hotuba nzuri Dkt.Lowassa ya leo aitupie tafadhali...

Nasikia kamwaga nondo za kufa mtu.
 
ila Lisu hawezi itikisa CCM ni mwepesi kama karatasi..hakuna aliyewahi kuwa naye Karibu kwenye mfumo. .Lowasa alitikisa na bado hakufurukuta..

Kama akisimama lowasa au membe Lkn si huyu ccm mpya,
 
Watu wa huku JF nimewavulia kofia maana wanajua kufukua makaburi humu na wakikudaka utajuta kuzaliwa. Bora ku lay low tuu. Wasalimie mama zangu wadogo wote nimewamiss sana ila wasipotee sana[emoji4]

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaniumiza kichwa ujue mbili haikai moja inapotea,unakuja na kupotea hahahaha, sikubali nakufata ulipo!!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…