DustBin
JF-Expert Member
- Jun 3, 2021
- 609
- 604
Janga la ukosefu wa ajira linaloikumba nchi yetu limepelekea kushuka thamani kwa elimu na kudharauliwa wenye elimu. Watu wamefikia kusema huku mtaani kwamba hakuna haja ya kusomesha watoto kama wakimaliza tunaendelea kukaa nao nyumbani na hawaajiriwi. Lakini kwa upande wa waajiri katika sekta binafsi nao wamezidi kiburi kwa wafanyakazi wao kwa kuona kuwa hawana namna nyingine kwani serikali haitoi ajira ya kuweza kutosha wahitimu wa vyuo. Nimesikitishwa kusikia kwenye shule moja ya binafsi ndugu zetu wahitimu wa vyuo vikuu wanalipwa chini ya laki moja ikiwa ni mshahara wao kwa mwezi. Na hawana chaguo isipokua kuendelea kutumika kama nguvu kazi rahisi (cheap labor).
Sasa kijana ambae wazazi wake walijinyima kwa kumhudumia masomo yake tangu anaanza darasa la kwanza, anamaliza chuo kikuu anapata kazi kwenye sekta binafsi mshahara wake wa kwanza ni chini ya laki moja. Unafikiria ni nini kitakachotokea hapo? Kumbe ndio maana matukio ya kujinyonga, na kujiua kwa sumu yameongezeka, hii inaweza ikawa ni sababu moja wapo. Hali hii ni huko kwenye sekta ya elimu, sijajua huko kwenye sekta zingine hali ipoje.
Nilishangaa sana mwaka jana kusikia kwenye jimbo fulani idadi ya waliochukua fomu ya kuwania ubunge imefika mia moja. Hao ndio vijana wahitimu wa vyuo vikuu baada ya kuona maisha ya mtaani yamezidi kubana wakaona huenda huko kwenye ubunge labda wataweza kupata unafuu. Na hivyo hivyo hali ilikua kwenye ngazi ya udiwani, hasa wakifikiria wabunge hawana kodi kwenye malipo yao ya mshahara basi hamasa inakua kubwa sana.
Wengi wametoa maoni yao kutatua janga hili au kupunguza hii hali. Mimi muono wangu umeakisi kwenye hili la elimu bila malipo (EBM). Ninavyoona ni kana kwamba suala la elimu bila malipo liliwekwa kisiasa lakini kwa namna hali ya utekelezaji unavyoendelea hivi sasa inaonesha kabisa serikali imeelemewa na mzigo huo mzito. Na kwa upande mwingine huku kuna tatizo kubwa la uhaba wa ajira. Na ndio maana serikali inajaribu kubuni namna nyingine ya kuhakikisha inapata fedha angalau ikaweza kujikwamua mpaka tukaletewa tozo za miamala.
Kwa utafiti nilioufanya kwa kutumia sampo ya eneo ninaloishi hapa mjini familia nyingi zinajiweza kugharamia malipo ya shule kama ada itarejeshwa wanao uwezo wa kuwalipia watoto wao na wakasoma bila matatizo yeyote. Ijapokuwa zipo familia chache zinahitaji msaada. Nalisema hili kwa sababu nimeona kwenye baadhi ya shule kunakuwa na sherehe kadhaa katika mwaka ambazo zinahitaji gharama ili uweze kushiriki, kama vile mahafali na wanafunzi wanachangia kwa asilimia kubwa. Safari za kitaaluma zinazofanywa na shule pia wanafunzi huchangia ili waweze kwenda, na wanachangia fedha safari zinafanyika. Hiki ni kiashiria tosha kwamba familia zina uwezo wa kulipa ile ada (karo) ya Ths. 20,000/- kwa mwaka kama itarejeshwa.
Twakwimu za awali wakati zoezi la EBM linaanza mwaka 2016 zilionesha serikali inatoa bilioni 18.8 kila mwezi kwenda mashuleni. Nilikua nawaza endapo nusu ya wanafunzi wangeachwa wajilipie wenyewe alafu nusu tuchukulie ndio idadi ya familia masikini ina maana serikali ingepeleka bilioni 9.4 mashuleni hiyo nusu nyingine inayobaki ingeweza kuingiza kwenye ajira mpya na kulipa mishahara ya walimu/wafanyakazi wengine zaidi ya elfu kumi na tatu wenye kima cha mshahara chini ya shilingi laki saba kwa mwezi.
Katika kuliendea jambo hili la kuiondoa EBM, serikali haina budi kuwa na takwimu za familia zenye umasikini wa kupindukia ambao kwa hakika hawawezi kabisa kukidhi gharama za shule. Taarifa hizo zinaweza kupatikana Tasaf au hata kwenye ofisi za halmashauri zetu.
Kufanya maamuzi haya ya kuondoa EBM ili kuongeza ajira mpya kuna faida na tija kama ifuatavyo;-
DustBin
Sasa kijana ambae wazazi wake walijinyima kwa kumhudumia masomo yake tangu anaanza darasa la kwanza, anamaliza chuo kikuu anapata kazi kwenye sekta binafsi mshahara wake wa kwanza ni chini ya laki moja. Unafikiria ni nini kitakachotokea hapo? Kumbe ndio maana matukio ya kujinyonga, na kujiua kwa sumu yameongezeka, hii inaweza ikawa ni sababu moja wapo. Hali hii ni huko kwenye sekta ya elimu, sijajua huko kwenye sekta zingine hali ipoje.
Nilishangaa sana mwaka jana kusikia kwenye jimbo fulani idadi ya waliochukua fomu ya kuwania ubunge imefika mia moja. Hao ndio vijana wahitimu wa vyuo vikuu baada ya kuona maisha ya mtaani yamezidi kubana wakaona huenda huko kwenye ubunge labda wataweza kupata unafuu. Na hivyo hivyo hali ilikua kwenye ngazi ya udiwani, hasa wakifikiria wabunge hawana kodi kwenye malipo yao ya mshahara basi hamasa inakua kubwa sana.
Wengi wametoa maoni yao kutatua janga hili au kupunguza hii hali. Mimi muono wangu umeakisi kwenye hili la elimu bila malipo (EBM). Ninavyoona ni kana kwamba suala la elimu bila malipo liliwekwa kisiasa lakini kwa namna hali ya utekelezaji unavyoendelea hivi sasa inaonesha kabisa serikali imeelemewa na mzigo huo mzito. Na kwa upande mwingine huku kuna tatizo kubwa la uhaba wa ajira. Na ndio maana serikali inajaribu kubuni namna nyingine ya kuhakikisha inapata fedha angalau ikaweza kujikwamua mpaka tukaletewa tozo za miamala.
Kwa utafiti nilioufanya kwa kutumia sampo ya eneo ninaloishi hapa mjini familia nyingi zinajiweza kugharamia malipo ya shule kama ada itarejeshwa wanao uwezo wa kuwalipia watoto wao na wakasoma bila matatizo yeyote. Ijapokuwa zipo familia chache zinahitaji msaada. Nalisema hili kwa sababu nimeona kwenye baadhi ya shule kunakuwa na sherehe kadhaa katika mwaka ambazo zinahitaji gharama ili uweze kushiriki, kama vile mahafali na wanafunzi wanachangia kwa asilimia kubwa. Safari za kitaaluma zinazofanywa na shule pia wanafunzi huchangia ili waweze kwenda, na wanachangia fedha safari zinafanyika. Hiki ni kiashiria tosha kwamba familia zina uwezo wa kulipa ile ada (karo) ya Ths. 20,000/- kwa mwaka kama itarejeshwa.
Twakwimu za awali wakati zoezi la EBM linaanza mwaka 2016 zilionesha serikali inatoa bilioni 18.8 kila mwezi kwenda mashuleni. Nilikua nawaza endapo nusu ya wanafunzi wangeachwa wajilipie wenyewe alafu nusu tuchukulie ndio idadi ya familia masikini ina maana serikali ingepeleka bilioni 9.4 mashuleni hiyo nusu nyingine inayobaki ingeweza kuingiza kwenye ajira mpya na kulipa mishahara ya walimu/wafanyakazi wengine zaidi ya elfu kumi na tatu wenye kima cha mshahara chini ya shilingi laki saba kwa mwezi.
Katika kuliendea jambo hili la kuiondoa EBM, serikali haina budi kuwa na takwimu za familia zenye umasikini wa kupindukia ambao kwa hakika hawawezi kabisa kukidhi gharama za shule. Taarifa hizo zinaweza kupatikana Tasaf au hata kwenye ofisi za halmashauri zetu.
Kufanya maamuzi haya ya kuondoa EBM ili kuongeza ajira mpya kuna faida na tija kama ifuatavyo;-
- Tukumbuke kuwa fedha za EBM ni fedha ambazo zikipelekwa shuleni hazirudi, tofauti na mishahara ya wafanyakazi ambayo zikishawekwa kwenye akaunti zao baada ya muda zinarudi tena serikalini kwa njia ya kodi, tozo na ankara mbalimbali ambazo wafanyakazi hulazimika kulipa kwa hali yeyote ile.
- Wingi wa ajira utaongeza uwezo wa familia nyingi kuweza kuhudumia wanafamilia wakiwemo na hao wanafunzi wanaosoma kwenye shule za serikali. Hivyo vijana hawa watakaoajiriwa itawasaidia kuwalipia ada ndugu zao.
- Kupunguza mzigo kwa serikali kwa gharama zisizo na ulazima. Kuna watu wanalipiwa gharama za elimu na serikali lakini wala hawakuhitaji huo msaada hivyo kulipiwa na serikali ni kama vile serikali inaingia gharama isiyo ya lazima.
- Kupunguza manung’uniko ya baadhi ya wakuu wa shule na walimu wakuu wenye shule zenye idadi ndogo ya wanafunzi. Namna fedha zinavyogaiwa mashuleni kigezo kikubwa kinachozingatiwa ni idadi ya wanafunzi, hivyo kufanya shule yenye wanafunzi wengi kupata mgao mkubwa ukilinganisha na shule zenye wanafunzi wachache. Wakati kuna baadhi ya gharama ni sawa kwa shule zote bila kujali una idadi kubwa au ndogo ya wanafunzi. Na hili ndilo lilipelekea kuwepo kwa wanafunzi hewa.
DustBin
Upvote
5