Elimu ni ufunguo wa Maisha, Diamond anamsomesha mtoto wake Braeburn International school, chekechea ada milioni 20

Unapaswa ufahamu kuwa Feza hiyohiyo unayoijua wewe Kuna upande wa pili wanafata mtaala wa Cambridge na ada zao huwa ndefu pia.
Wazazi pia vizuri kuzijua hizo shule vizuri zingineni huitwa International School lakini huwa na matokeo mabaya sana mitihani ya. Kimataifa ya Cambridge

Shule nzuri mfano zinazotumia mfumo wa NECTA huwa tunazijua kwa kuangalia matokeo ya mitihani ya NECTA

Ni vizuri pia mzazi kujiridhisha na matokeo ya mitihani ya Cambridge ya Shule husika kabla kujitosa kichwa kichwa kupeleka mtoto

Uzuri shule za kimataifa ziko nchi nyingi pesa akiwa nayo aweza peleka iliyo nzuri yenye matokeo mazuri mitihani ya Cambridge popote Africa hata nje

Kuna wazazi hilo hata huwa hawaangalii akiona ina kibao International School anaishia hapo

Vizuri kucheki
 
Sema kweliii.
Yaani, we acha tu...😂
Hata kama ukipata viza ya kusoma UK, unaweza kuleta familia yako na watasoma bure
Wahindi wanapambana hasa kwenda Europe kwa dhumuni moja tu, kusomesha watoto wao.
Wafanyakazi wa balozi za bongo, huwa wanasomba mpaka vitukuu, lakini wakitumbuliwa ndio mwisho wake🤣
 
Unapaswa ufahamu kuwa Feza hiyohiyo unayoijua wewe Kuna upande wa pili wanafata mtaala wa Cambridge na ada zao huwa ndefu pia.
Ukisoma mtaala wa Cambridge yaani ndio unakuwa so powerful ama just Ile human ego distinguished in classic.yaani mfano mathematics amaa physics Ni mbali na hii ya necta,hii mie nimeuliza nielezewe. Mie Kuna watu wamemaliza hapa necta wakaenda Oxford , Cambridge,Yale, Massachusetts,havard ,mit, hapo huwa inakuwaje wandugu
 
Uzi wote huu umeandika kisa mtoto wa Chibu au kuna lingine??

Kazi ipo.
 
Education is better than money

v/s

Money is better than education


Ukiwa shuleni unapangwa
v/s
ukiwa mtaani uhalisia unajulikana

Mwambieni mtoto wa Mo apambane abadilishe ile hali ya maisha pale kwao ni dhiki kubwa ile [emoji16]
 
Na kwa hiyo katiba ni uongo kabisa inavyoelekeza kuwa mtu kugombea urais anatakiwa kuwa na miaka 40 na pia awe na akili timamu.. kumbe kuna masharti mengine yapo😄
 
Kila mtoto anaesoma Braeburn ni mtoto wa kishua haswa pengine huyo Diamond ndo miongoni mwa maskini hapo kwahiyo kila mtoto hapo ni hela lakini jiulize kwanini hawaendi kuteka
Suala la ulinzi limezingatiwa labda akatekwe akiwa mikononi kwa babaake
Sana,
Hapo ni wakishua tu,

Hivi kwanini international school nyingi zipo Arusha ? ,Niliwai angalia list zao ni Arusha na Dar ya pili ,
Sijajua kwanini nyingi ziko Arusha,
 
Mawazo ya kimasikini haya yanayohubiriwa na wachungaji wanaotembeea ma V8 huku waumini hawana uhakika hata wa mlo wa usiku.

Maarifa ni muhimu na Mungu nae ni Muhimu
Hata Mimi ,nampingaaa
Eti ,
"Usisomeshe watoto kuwa Matajiri"

Huo,itakuwa ni upungufu wa akili,

Kuna ,
Utajiri WA Maarifa ya kimwili
Utajiri WA Maarifa ya kiroho

Vyote Muhimu, vinategemeana,pia
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…