Elimu ya Nape Nnauye

Elimu ya Nape Nnauye

unakumbuka mzee Mzindakaya aliwahi kulazimisha kusoma Mzumbe? Unajua matokeo yake walimuondoa pamoja na kuwa alikuwa mkuu wa mkoa wa Morogoro; Nape Nnauye alikuwa na sifa zote za kujiunga na chuo ndio sababu bodi ya chuo ilikubali vyeti vyake.

Chama
Gongo la mboto DSM
Lakini unajuwa kuwa kwa sasa ni Doctor!!!
 
Nani serikalini wenye digrii kutoka Oxford, Yale, Cambridge, na Stanford?

Andrew Chenge na Gavana Balali (RIP?) wamesoma Havard. Lakini angalia madudu waliyoyafanya serikalini. Tatizo si kwamba umesoma wapi, tatizo ni mfumo mbovu uliopo kwenye serikali na jamii yetu kwa ujumla. Hakuna kabisa uwajibikaji.
 
sawa ana masters, je hili la wadogo zake kufeli namna hii anasemaje?
 
Nape Nnauye ana masters John Mnyika ana nini?

Chama
Gongo la mboto DSM

Nape ni kweli ana Masters na Mnyika ni Form Six hilo halina ubishi. Hoja inakuja ilikuwa kuwaje Nape aanzishe hoja ya elimu ili hali yeye akijijua elimu yake yake kaipata kumagumashi na ni system tu uliyombeba??? Kusema una Masters siyo ajabu lakini kama angelikuwa ni mtoto wa mkulima basi tena labda angekuwa askari polisi saizi anatumika kuwadhibiti CDM huko mitaani na angekuwa analalamikia posho au mshahara kuchelewa!!
 
Last edited by a moderator:
Mungu wangu! Nape kumbe alipata DIVISION FOUR kidato cha nne! Sijui ata-comment nini katika matokeo ya kidato cha nne yaliyotangazwa hivi karibuni! Manake wanafunzi wote waliofeli ni wenzake!!
 
Dah Nape Nnauye yupo bize dunia nzima! Tangu juzi hatokei kuzungumza na members wenzake wa JF? Mkuu Ritz unaweza kumpigia simu kaka mwenezi tafadhali?
 
Last edited by a moderator:
Nepi jitokeze hadharani kujibu shutuma
 
Verry simple, NAPE anayo masterz na Mnyika hakumaliza chuo.period

Na pia Nape Nnauye alipata Division 4 ya point 29 wakati John Mnyika alipata Division 1 ya pointi 7 huku akiwa na A tisa.

Kwa mwenye akili timamu anajua nani ni nani kati ya Nape na Mnyika. Nyie kaeni na mavyeti yenu ya ubabaishaji Mnyika anabaki na akili kichwani ambayo imemfanya kuwa mbunge bora 2012 licha ya bunge kuwa na maprofesa kibao.

Nape hakusoma form 5 na 6 bali alisaidiwa na Mzee Makamba kwenda chuo cha chama kivukoni bila kuwa na sifa. Matusi yote Nape amejifunzia KIVUKONI kwenye cguo cha magamba
 
Nape Nnauye ana masters John Mnyika ana nini?

Chama
Gongo la mboto DSM

Mkuu chama naona mapovu kibao ya nini?!!!! hapa mtoa hoja na wanajamvi wanachotaka
kujua si kwamba Nape ana masters au hana hapana,kinachotakiwa ni Nape kujibu aliendaje
A level na four ya point 29? kama siyo alibebwa?
Suala la kuwa na Degree au Masters mbona wako wengi walitolewa list na msemakweli na
mpaka leo hawajakanusha wala kwenda mahakamani kama walivyotishia?!!!
Tunataka Nape aondoe utata huu,maana ni yeye anaanzisha vita ya mawe wakati kumbe
anaishi nyumba ya vioo" Please Nape fanya ka Mnyika"
 
Back
Top Bottom