Ellon Musk aitaka Pentagon igharamie vita vyake yenyewe huko Ukraine

Ellon Musk aitaka Pentagon igharamie vita vyake yenyewe huko Ukraine

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Tajiri namba moja duniani anayemiliki mtandao wa Starlink ameiambia wazi wizara ya ulinzi ya Mareknani kuwa sasa itabidi waanze kugharamia mawasiliano hayo kwa Ukwani.Amesema kama ni sadaka tayari keshatoa zaidi ya dola milioni 80 kwa ajili ya vfaa 20000 ambavyo vimekuwa ni nguzo ya mawasiliano ya jeshi la Ukraine baada ya minara yote ya mitandao ya simu za mkononi kubomolewa na Urusi.
Akizidi kuipasha Pentagon Musk amesema iwapo kasi itakuwa hii kwa misaada yake ifikapo mwishoni mwa mwaka itakuwa ametumia dola milioni 100,Siwezi tena.....
Taarifa hiyo si ya mdomo na kupitia twitter yake pekee bali tayari ameshaiandikia Pentagon tangu mwezi uliopita.
Kuonesha jinsi vifaa hivyo vilivyo muhimu kwa Ukraine mshauri wa raisi Zelensky,Mykhailo Podolyak amebainsisha serikali yake itafanya kila juhudi ili mawasiliano hayo yaweze kuendelea.Akasema Musk amewasaidia sana kwa muda mrefu na biashara yake ina haki ya kuendelea kujimudu.
 
Hizi ni habari za kwenye vijiwe vya kahawa
Hamna haja ya kuongea sana.View attachment 2387330
Screenshot_20221014-202011.jpg
 
Elon musk ni nani mpaka awapangie marekani sera Yao ya mambo ya nje, yaan marekani abadilishe sera yake kisa Elon musk, kwa kukusaidia marekani ametumia USD trillion 1 na kukaa miaka 20 Afghanistan na ameshindwa vita sembuse hii ya Ukraine ambayo hapigani direct
 
Elon musk ni nani mpaka awapangie marekani sera Yao ya mambo ya nje, yaan marekani abadilishe sera yake kisa Elon musk, kwa kukusaidia marekani ametumia USD trillion 1 na kukaa miaka 20 Afghanistan na ameshindwa vita sembuse hii ya Ukraine ambayo hapigani direct
Kulipia internet ya Starlink ndio sera ya Mambo ya nchi za nje?

Yeye Elon Musk amewataka wagharamie huduma ya Internet anayotoa hapo Ukraine... Wewe unaruka ruka Kama bisibisi na kuleta habari za sera.
 
Kulipia internet ya Starlink ndio sera ya Mambo ya nchi za nje?

Yeye Elon Musk amewataka wagharamie huduma ya Internet anayotoa hapo Ukraine... Wewe unaruka ruka Kama bisibisi na kuleta habari za sera.
Kwa hiyo washitishe kuwasaidia Ukraine kwa sababu Elon musk anawadai, na hiyo starlink Elon musk si alipeka kwa utashi wake mwenyewe kwani amelazimishwa asitishe huduma
 
Elon musk ni nani mpaka awapangie marekani sera Yao ya mambo ya nje, yaan marekani abadilishe sera yake kisa Elon musk, kwa kukusaidia marekani ametumia USD trillion 1 na kukaa miaka 20 Afghanistan na ameshindwa vita sembuse hii ya Ukraine ambayo hapigani direct
Yeye hajawapangia bali kasema walipie gharama za kuipatia huduma Ukraine maana yy hataweza tena kugharamia.
Hata hivyo kawabeba sana ni sema Ukraine haina shukurani mpaka sasa ametumia gharama ya million 80$ ambayo ni sawa na billion karibia 200 za kitanzania.
 
Yeye hajawapangia bali kasema walipie gharama za kuipatia huduma Ukraine maana yy hataweza tena kugharamia.
Hata hivyo kawabeba sana ni sema Ukraine haina shukurani mpaka sasa ametumia gharama ya million 80$ ambayo ni sawa na billion karibia 200 za kitanzania.
Marekani ameshapoteza Zaid trillions of usd Afghanistan na akafeli sembuse hio mill 80 na pentagon wamekuambia wameshindwa kugharamia hizo gharama
 
Marekani ameshapoteza Zaid trillions of usd Afghanistan na akafeli sembuse hio mill 80
Ndio walipe sasa hii habari hata aljazeera na bbc wameirusha.
Walimwomba apeleke satelite zake pale ukraine mwanzoni mwa vita tu kama ambavyo kaombwa azipeleke Iran ili waandamanaji waendelee kupata internet.
Sasa kumbe anatoa msaada tu wakati yeye mfanyabiashara now either walipie huduma au asitishe, na ni njia ya mawasiliano wanyoitegemea na ndio maana mrusi kapeleka mtambo wa kujam mtandao wa hizo satelite
 
Ndio walipe sasa hii habari hata aljazeera na bbc wameirusha.
Walimwomba apeleke satelite zake pale ukraine mwanzoni mwa vita tu kama ambavyo kaombwa azipeleke Iran ili waandamanaji waendelee kupata internet.
Sasa kumbe anatoa msaada tu wakati yeye mfanyabiashara now either walipie huduma au asitishe, na ni njia ya mawasiliano wanyoitegemea na ndio maana mrusi kapeleka mtambo wa kujam mtandao wa hizo satelite
Wamekuambia hawalipi kwani
 
Narudia kwani kudai ni ajabu na wamekuambia hawalipi
Narudia tena kuna sehemu imeandikwa ni ajabu, hapa tunaandika alichosema na kilichotamgazwa kwenye media, sasa sijui unabisha kuwa hakusema hivyo, au hakupeleka satelite zake kuwapa mawasiliano ukraine, au unabisha kuwa anaonge uongo kuwa mpaka sasa hajalipwa.
Hebu nieleze hapa unabisha nini au ni kosa kuzungumzia musk alichosema juu ya hayo malipo?
 
Narudia tena kuna sehemu imeandikwa ni ajabu, hapa tunaandika alichosema na kilichotamgazwa kwenye media, sasa sijui unabisha kuwa hakusema hivyo, au hakupeleka satelite zake kuwapa mawasiliano ukraine, au unabisha kuwa anaonge uongo kuwa mpaka sasa hajalipwa.
Hebu nieleze hapa unabisha nini au ni kosa kuzungumzia musk alichosema juu ya hayo malipo?
We ndo nakushangaa unaposhupalia kwamba wanadaiwa Kwan ni ajabu mtu kudaiwa, unashangaa Elon musk kuwadai pentagon huku nchi za kiafrika zikiwa zinanuka madeni na huku ni maskini wa kutupa tuacheni unafki yaan unashangaa mtu kudai ajabu ni nin
 
Narudia tena kuna sehemu imeandikwa ni ajabu, hapa tunaandika alichosema na kilichotamgazwa kwenye media, sasa sijui unabisha kuwa hakusema hivyo, au hakupeleka satelite zake kuwapa mawasiliano ukraine, au unabisha kuwa anaonge uongo kuwa mpaka sasa hajalipwa.
Hebu nieleze hapa unabisha nini au ni kosa kuzungumzia musk alichosema juu ya hayo malipo?
Huyo jamaa ni mbishi tu hawezi kukuelewa
 
Watamnyoosha. USA sio wajinga, they always have a contingency plan, ukileta za kuleta ndio utajua kuwa kuna sheria nyingi tu uliwahi kuzifunja na wanazengo wakaweka kwenye mafaili.

Kuna dogo mmoja bilionea wa pharmaceutical companies alikomaa kupandisha bei ya dawa flani muhimu ya HIV, mwanzoni serikali ilimbembeleza sana lakini akakomaa, kilichompata ...
 
Tukiacha ushabiki Elon yupo sahihi,yeye ameshajitoa vya kutosha,pia yeye ni mfanyabiashara hafanyi kazi ya kabisa. Marekani hana budi abebe hizo gharama au asitishe huduma.
 
Back
Top Bottom