Eneo la mita 15 kwa 8 linatosha kujenga nyumba ya ghorofa moja?

Eneo la mita 15 kwa 8 linatosha kujenga nyumba ya ghorofa moja?

Kama una uwezo paa linakuwa la zege la flat ambalo utaweza kutumia kupanda majani, kuanika nguo au kupumzika tu. Hata mti unaweza kupanda.

Amandla...
 
Vijana wa 2000 ni wa ajabu sana.... Kama ni wa kiume usijisumbue kujenga kwa sababu zifuatazo;
t1. Tuna amini Tupo kwenye siku za mwisho hapa duniani , Nyumba atakaa nani?
2. Hiyo hela kwa nini usiandae shughuli ya mazishi yako ikiwemo nyumba yako ya milele (kaburi zuri),jeneza zuri na kugharimia shughuli nzima ya mazishi yako yafanyike kifahari badala ya kusumbua watu na michango?
3. Kama uko kwenye ndoa au ukija kuoa hiyo nyumba ataishia kukaa mkeo na hawara yake ambaye ni kiben10 au mshenzi mshenzi wa mtaani ambaye kwa sasa unamdharau
 
Inategemea unajengea wapi. Kama ni eneo la kupimwa, utatakiwa angalau kuacha mita 1.5 na nusu kila upande na hivyo utabaki na upana wa mita 5 za kujenga. Kwa mbele utatakiwa kuacha mita 3 na nyuma mita 1.5 hivyo utabaki na mita 10.5 za kujenga. Nafasi yako ya kujenga itakuwa mita 5 kwa 10.5. Hizi zinatosha kabisa kujenga ghorofa. Changamoto utakayokuwa nayo ni ujenzi wa septic tank na soak pit ambazo kwa kweli nafasi iliyobaki haitoshi. Unachoweza kufanya ni kuinyanyua yote kwa nguzu na kuanza kukata vyumba kuanzia ghorofa ya kwanza. Hiyo nafasi ya chini ya unaweza kuweka septic tank na soak pit yako. Na hata gari unaweza kupaki.

Amandla...
Ni kweli sheria kulingana na planning space standards inataka kuwepo na building setbacks(nafasi Kati ya mwisho wa kiwanja na mwanzo wa linapojengwa jengo)

Lakini naona hii hafanyi kazi kwa bongo yetu hii maana kariakoo hakuna setbacks popote na bado wameweza kupewa vibali na wamejenga na mambo yanaendelea kama kawaida
 

Attachments

  • Screenshot_20240708-164333_1.jpg
    Screenshot_20240708-164333_1.jpg
    194.6 KB · Views: 12
  • Screenshot_20240708-164442_1.jpg
    Screenshot_20240708-164442_1.jpg
    204.2 KB · Views: 16
Ni kweli sheria kulingana na planning space standards inataka kuwepo na building setbacks(nafasi Kati ya mwisho wa kiwanja na mwanzo wa linapojengwa jengo)

Lakini naona hii hafanyi kazi kwa bongo yetu hii maana kariakoo hakuna setbacks popote na bado wameweza kupewa vibali na wamejenga na mambo yanaendelea kama kawaida
Inafanya kazi. Tatizo ni kuwa code zetu hazizungumzii kuhusu vitu vinavyo "cantilever" kwenye hizo setbacks. Kwa sababu hiyo wengi wanaweka balconies hivyo kubakiza nafasi ndogo sana. Kwa mfano, mtu akiweka balcony ya mita 1 anaacha sentimeta 50 tu kutoka kwenye mpaka wake. Wa upande wa pili nae akifanya hivyo utaona inabaki mita moja tu kati ya balcony ya nyumba na nyingine. Ukiwa na ghorofa nyingi ndio hiyo nasi inavyozidi kuonekana kiduchu na kuzuia mwanga kufika katika ghorofa za chini. Ukiangalia nchi nyingine wanaruhusu watu kujenga kwenye mpaka wa upande moja ( wengine pande zote) na hivyo kuruhusu setbacks ya mita 3 upande uliobaki. Hiyo inaruhusu mwanga kufika chini. Majengo ya katikati ya miji hayana sababu ya setback za pembeni.

Nimeona mnajadiliana kuhusu ukubwa wa vyumba. Ni kweli inategemea sehemu unapojenga. Mara nyingi wanasema upande mmoja usipungue mita 2.4. Hiyo ya mita 3 inatokana na vyumba vya nyumba za NHC za vyumba 6 kuwa na ukubwa wa futi 10 ( mita 3.3) kwa futi kumi kutumika kama standard. Sisi kwetu tunapenda dari lisiwe chini ya mita 3 kwa sababu ya mahitaji ya mzunguko wa hewa na kuruhusu kufunga ceiling fan. Katika maeneo ya baridi mita 2.7 ( hata 2.4 kwa mbinde) inatosha ili kuhifadhi joto ndani ya chumba.

Amandla...
 
Inafanya kazi. Tatizo ni kuwa code zetu hazizungumzii kuhusu vitu vinavyo "cantilever" kwenye hizo setbacks. Kwa sababu hiyo wengi wanaweka balconies hivyo kubakiza nafasi ndogo sana. Kwa mfano, mtu akiweka balcony ya mita 1 anaacha sentimeta 50 tu kutoka kwenye mpaka wake. Wa upande wa pili nae akifanya hivyo utaona inabaki mita moja tu kati ya balcony ya nyumba na nyingine. Ukiwa na ghorofa nyingi ndio hiyo nasi inavyozidi kuonekana kiduchu na kuzuia mwanga kufika katika ghorofa za chini. Ukiangalia nchi nyingine wanaruhusu watu kujenga kwenye mpaka wa upande moja ( wengine pande zote) na hivyo kuruhusu setbacks ya mita 3 upande uliobaki. Hiyo inaruhusu mwanga kufika chini. Majengo ya katikati ya miji hayana sababu ya setback za pembeni.

Nimeona mnajadiliana kuhusu ukubwa wa vyumba. Ni kweli inategemea sehemu unapojenga. Mara nyingi wanasema upande mmoja usipungue mita 2.4. Hiyo ya mita 3 inatokana na vyumba vya nyumba za NHC za vyumba 6 kuwa na ukubwa wa futi 10 ( mita 3.3) kwa futi kumi kutumika kama standard. Sisi kwetu tunapenda dari lisiwe chini ya mita 3 kwa sababu ya mahitaji ya mzunguko wa hewa na kuruhusu kufunga ceiling fan. Katika maeneo ya baridi mita 2.7 ( hata 2.4 kwa mbinde) inatosha ili kuhifadhi joto ndani ya chumba.

Amandla...
Bado haifanyi kazi, maghorofa mengi hasa kariakoo hayana balcony both sides, balcony zipo kwa mbele tu. Ukiangalia picha namba mbili utaona kuna ghorofa hapo hazina balcony left and right sides, balcony zipo mbele tu
Lakini pia kwa floor ya chini huwezi kuona space ya mita tatu ipo wazi Kati ya ghorofa na ghotofa.

Kuendelea kuthibitisha hii sheria haifuatwi angalia pia front setbacks kwa kkoo, standard na sheria inataka kuwe na mita si chini ya 5. Je maghorofa ya kkoo yana space kwa mbele kwa mita 5 au zaidi?

Kwenye bedroom standard ulichosema ni kweli, japo hata sehemu zenye baridi wanazidisha urefu wa 2.7 hasa wale wenye A house design, au wale wanaojenga loft apartments, unakuta kutoka kwenye floor mpaka ceiling ni mita karibu 6😂
 
Ukienda Japan au sehemu za India hiki ni kiwanja kikubwa tu.

Amandla...
Bila kusahau Singapore, Singapore hata kiwanja Cha mita 5 kwa 10 watu wanatoa ghorofa moja Kali Sana, inajengwa cube ya maana sana
Bongo watu wamekariri ndio maana wanauziwa sqm 1500 au zaidi kwa pesa nyingi kweli alafu mwisho wa siku wanashindwa kufanya maintenance
 
Bado haifanyi kazi, maghorofa mengi hasa kariakoo hayana balcony both sides, balcony zipo kwa mbele tu. Ukiangalia picha namba mbili utaona kuna ghorofa hapo hazina balcony left and right sides, balcony zipo mbele tu
Lakini pia kwa floor ya chini huwezi kuona space ya mita tatu ipo wazi Kati ya ghorofa na ghotofa.

Kuendelea kuthibitisha hii sheria haifuatwi angalia pia front setbacks kwa kkoo, standard na sheria inataka kuwe na mita si chini ya 5. Je maghorofa ya kkoo yana space kwa mbele kwa mita 5 au zaidi?

Kwenye bedroom standard ulichosema ni kweli, japo hata sehemu zenye baridi wanazidisha urefu wa 2.7 hasa wale wenye A house design, au wale wanaojenga loft apartments, unakuta kutoka kwenye floor mpaka ceiling ni mita karibu 6😂
Sheria za setbacks za mita 5 ni kwa ajili ya residential areas. Maeneo ya mjini hayapaswi kuwa na setback ya mbele kwa sababu maduka n.k. yanatakiwa yaingiwe moja kwa moja kutoka kwenye side walk. Hakuna mji wa maana wenye setbacks za mbele kwenye majengo ya biashara katikati ya mji. Kunatakiwa kuwa na continuity kutoka jengo moja kwenda lingine.
Ukiangalia picha ya kwanza, balconies za pembeni ziko wazi kabisa na nafasi kati ya kuta na kuta inawezekana kabisa kuwa mita 3.

Amandla...
 
Sheria za setbacks za mita 5 ni kwa ajili ya residential areas. Maeneo ya mjini hayapaswi kuwa na setback ya mbele kwa sababu maduka n.k. yanatakiwa yaingiwe moja kwa moja kutoka kwenye side walk. Hakuna mji wa maana wenye setbacks za mbele kwenye majengo ya biashara katikati ya mji. Kunatakiwa kuwa na continuity kutoka jengo moja kwenda lingine.
Ukiangalia picha ya kwanza, balconies za pembeni ziko wazi kabisa na nafasi kati ya kuta na kuta inawezekana kabisa kuwa mita 3.

Amandla...
Bado zinaangukia kwenye general standards.
Lakini pia sio wote wenye ghorofa wameweka fremu, wapo walioweka chini offices na wengine hotel mwanzo mwisho lakini bado hakuna setbacks. Tena kwa standards za hotel setbacks ni kubwa
 
Bado zinaangukia kwenye general standards.
Lakini pia sio wote wenye ghorofa wameweka fremu, wapo walioweka chini offices na wengine hotel mwanzo mwisho lakini bado hakuna setbacks. Tena kwa standards za hotel setbacks ni kubwa
Nadhani unachanganya vitu. Hamna general standards. Kinachozungumzia setbacks ni development conditions. Pamoja na setbacks kunakuwa pia na miongozo ya kiasi gani cha kiwanja kinaweza kufunikwa ( coverage) na umla ya eneo linaloweza kujengwa katika kiwanja hicho ( Floor Area Ratio) na urefu wa jengo unaoruhusiwa. Hizi zote zinaongozwa na malengo ya Manispaa katika maeneo husika. Je wanataka nyumba moja moja, majengo yanayoweza kukaliwa na wengi, majengo yenye mchanganiko wa matumizi n.k. Hamna setbacks maalum kwa ajili ya hoteli au aina ya jengo lolote. Setbacks zinazowekwa ni minimum kwa hiyo kama unataka kuwa na garden kubwa mbele ya nyumba yako basi unaongeza setback. Hii ni tofauti katikati ya miji ambapo mara nyingi nia inakuwa majengo yawe katika msitari mmoja ( majengo yz zamani ya Acacia/Independence Avenue ambayo siku hizi inaitwa Samora Avenue). Majengo haya pia mara nyingi yanaruhusiwa kubanana ( sio hapa kwetu siku hizi) kwa kuwa na "party walls". Kuna miji mingine ilikuwa inadai hata ghorofa ziwe zinarudishwa nyuma ili kuruhusu mwanga kufika chini. Kwa kifupi setbacks n.k. hazina standards bali ni uamuzi wa mamlaka zinazohusika na mipango miji ya kila eneo. Mamlaka zetu kwenye hili eneo ziko nyuma sana ndio maana wanatumia miongozo ya maeneo ya makati katika maeneo ya biashara. Hilo ni kosa na litaharibu miji yetu.

Amandla...
 
Nadhani unachanganya vitu. Hamna general standards. Kinachozungumzia setbacks ni development conditions. Pamoja na setbacks kunakuwa pia na miongozo ya kiasi gani cha kiwanja kinaweza kufunikwa ( coverage) na umla ya eneo linaloweza kujengwa katika kiwanja hicho ( Floor Area Ratio) na urefu wa jengo unaoruhusiwa. Hizi zote zinaongozwa na malengo ya Manispaa katika maeneo husika. Je wanataka nyumba moja moja, majengo yanayoweza kukaliwa na wengi, majengo yenye mchanganiko wa matumizi n.k. Hamna setbacks maalum kwa ajili ya hoteli au aina ya jengo lolote. Setbacks zinazowekwa ni minimum kwa hiyo kama unataka kuwa na garden kubwa mbele ya nyumba yako basi unaongeza setback. Hii ni tofauti katikati ya miji ambapo mara nyingi nia inakuwa majengo yawe katika msitari mmoja ( majengo yz zamani ya Acacia/Independence Avenue ambayo siku hizi inaitwa Samora Avenue). Majengo haya pia mara nyingi yanaruhusiwa kubanana ( sio hapa kwetu siku hizi) kwa kuwa na "party walls". Kuna miji mingine ilikuwa inadai hata ghorofa ziwe zinarudishwa nyuma ili kuruhusu mwanga kufika chini. Kwa kifupi setbacks n.k. hazina standards bali ni uamuzi wa mamlaka zinazohusika na mipango miji ya kila eneo. Mamlaka zetu kwenye hili eneo ziko nyuma sana ndio maana wanatumia miongozo ya maeneo ya makati katika maeneo ya biashara. Hilo ni kosa na litaharibu miji yetu.

Amandla...
Naelewa wala sichanganyi, space standards zimewekwa kwenye sehemu specific na wakacategorize na yapo matumizi yanabaki na kuingia kwenye general standards
So general standards zipo, rejea UPA Act iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2018
Kaangalie planning space standards utaona zinazokua regarded as general na zilizo specific

Halmshauri(mamlaka za miji) zinaweza kuandaa waraka kulingana na aina ya matumizi na ukawa Kama muongozo wa ujenzi kwenye hiyo halmashauri lakini bado wata-adhere na ile UPA act ya 2018

Setbacks maalum zipo kulingana na aina ya matumizi, hiko kilichowekwa ni minimum tu

Mfano halmashauri ya jiji ilala wanao waraka wa ujenzi kkoo, tafuta huo waraka uone kama unafatwa kwenye ujenzi. Au mfano rahisi vituo vya mafuta kaangalie standards zake na masharti yake alafu ingia mtaani kaangalie kinachoendelea

Ni kweli Kuna kosa kutumia standards za residential kwenye maeneo ambayo ni commercial kama kkoo, lakini kumbuka hao wengi kkoo walikua ni residential wala hawakua na plot za makazi biashara
 
Naelewa wala sichanganyi, space standards zimewekwa kwenye sehemu specific na wakacategorize na yapo matumizi yanabaki na kuingia kwenye general standards
So general standards zipo, rejea UPA Act iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2018
Kaangalie planning space standards utaona zinazokua regarded as general na zilizo specific

Halmshauri(mamlaka za miji) zinaweza kuandaa waraka kulingana na aina ya matumizi na ukawa Kama muongozo wa ujenzi kwenye hiyo halmashauri lakini bado wata-adhere na ile UPA act ya 2018

Setbacks maalum zipo kulingana na aina ya matumizi, hiko kilichowekwa ni minimum tu

Mfano halmashauri ya jiji ilala wanao waraka wa ujenzi kkoo, tafuta huo waraka uone kama unafatwa kwenye ujenzi. Au mfano rahisi vituo vya mafuta kaangalie standards zake na masharti yake alafu ingia mtaani kaangalie kinachoendelea

Ni kweli Kuna kosa kutumia standards za residential kwenye maeneo ambayo ni commercial kama kkoo, lakini kumbuka hao wengi kkoo walikua ni residential wala hawakua na plot za makazi biashara
Space standards ni kwa ajili ya maeneo ya ndani ya majengo wakati hizo setbacks n.k. ni kwa ajili ya maeneo ya ujenzi na zinakuwa kwenye "Development conditions". Development conditions za Tanzania ni arbitrary ndio maana hata zinapozungumzia setbacks hazitoi ufafanuzi wa projections juu yake. Waraka wa ujenzi wa Manispaa kuhusu ujenzi katikati ya hauona miongozo yoyote ya maana maana una miongozo ya residential area. Ukiifuata hamna jengo litajengwa katikati ya mji. Kwa kuwa Kariakoo ilikuwa zamani sehemu ya makazi hakumaanishi development conditions zibaki zile zile kila wakitayarisha Master plan mpya. Masterplan iliyopo ya Oysterbay inaruhusu ujenzi wa mixed use buildings ( residential/commercial) pembezoni mwa barabara wakati eneo lote lilikuwa kwa ajili ya makazi ya viongozi wa serikali!

Suala la vituo vya mafuta linatakiwa kuwekwa kwenye Masterplan. Naamini utitiri wake ni kutokana na masterplan iliyopo kutoa mianya kibao ambayo wajanja wanatumia. Sidhani kama kuna miongozo yeyote rasmi kuhusu ujenzi wa vituo vya mafuta au aina yeyote ya majengo. Dar es Salaam kulikuwa na ghala za silaha za kivita katikati ya makazi sembuse vituo vya mafuta!!!?

Tatizo la mipango miji ni zaidi ya yanayo endelea Kariakoo.

Amandla....
 
Ukiangalia Urban Planning Act 2007 iliyoongezewa 2018 haitoi miongozo yeyote kuhusu petrol stations isopokuwa kuziweka kwenye User Group D inayohusu maduka. Hilo ni pungufu kubwa.

Amandla....
 
Space standards ni kwa ajili ya maeneo ya ndani ya majengo wakati hizo setbacks n.k. ni kwa ajili ya maeneo ya ujenzi na zinakuwa kwenye "Development conditions". Development conditions za Tanzania ni arbitrary ndio maana hata zinapozungumzia setbacks hazitoi ufafanuzi wa projections juu yake. Waraka wa ujenzi wa Manispaa kuhusu ujenzi katikati ya hauona miongozo yoyote ya maana maana una miongozo ya residential area. Ukiifuata hamna jengo litajengwa katikati ya mji. Kwa kuwa Kariakoo ilikuwa zamani sehemu ya makazi hakumaanishi development conditions zibaki zile zile kila wakitayarisha Master plan mpya. Masterplan iliyopo ya Oysterbay inaruhusu ujenzi wa mixed use buildings ( residential/commercial) pembezoni mwa barabara wakati eneo lote lilikuwa kwa ajili ya makazi ya viongozi wa serikali!

Suala la vituo vya mafuta linatakiwa kuwekwa kwenye Masterplan. Naamini utitiri wake ni kutokana na masterplan iliyopo kutoa mianya kibao ambayo wajanja wanatumia. Sidhani kama kuna miongozo yeyote rasmi kuhusu ujenzi wa vituo vya mafuta au aina yeyote ya majengo. Dar es Salaam kulikuwa na ghala za silaha za kivita katikati ya makazi sembuse vituo vya mafuta!!!?

Tatizo la mipango miji ni zaidi ya yanayo endelea Kariakoo.

Amandla....
Hapana planning space standards sio kwa ajili ya ndani ya majengo, ni nje na setbacks inaingia ndani ya space standards, rejea UPA act 2018. Uzuri sheria zetu zimetoa tafsiri vizuri

Master plan hata ikibadilika na kusema sehemu hii iwe for commercial purpose bado ili kuendeleza hiyo sehemu kutafata detailed scheme zinavyotaka. Master plan Ni mpango wa jumla tu, ndio maana nikakuuliza je waraka au muongozo wa halmashauri unasemaje kuhusu kkoo?

Vituo vya mafuta vinatakiwa kuwekwa kwenye master plan? Vituo vya mafuta vinawekwaje kwenye master plan? Vituo vya mafuta vinawekwa kwenye detailed plan mfano neighbourhood plan.

Muonngozo wa ujenzi wa vituo vya mafuta upo, ndio maana nikasema ungerejea UPA act inasemaje. Kiuto Cha mafuta linatakiwa kuwa mita 200 kutoka kimoja hadi kingine kwa maeneo ya mjini(planned) na kwa maeneo ya pembeni(unplanned) linatakiwa kuwa mita 500 kutoka kimoja hadi kingine. Lakini bado wengi hawafuati hii, hata waziri wa sasa wa Ardhi Jerry Silaa hivi karibuni katoka kupambana na hili jambo huko mikocheni.
 
Ukiangalia Urban Planning Act 2007 iliyoongezewa 2018 haitoi miongozo yeyote kuhusu petrol stations isopokuwa kuziweka kwenye User Group D inayohusu maduka. Hilo ni pungufu kubwa.

Amandla....
Si kweli, inatoa muongozo vizuri tu na ndio kitu hata huyu waziri wa sasa anapambana nacho
 

Attachments

  • Screenshot_20240709-174333_1.jpg
    Screenshot_20240709-174333_1.jpg
    234.5 KB · Views: 14
Uko sahihi.
1. Mimi nilichoangalia ni hii hapa:
https://www.lands.go.tz/uploads/documents/sw-1682061038-GN. 91 USE GROUPS AND USE CLASSES.pdf.

Sikuangalia hii hapa:

https://www.lands.go.tz/uploads/documents/sw-1682059395-GN. 93 Town Planning Space Standards.pdf

ambayo inazungumzia User Groups peke yake.
2. Na ni kweli petrol stations zinatakiwa kuwa identified katika detailed plans na sio Master Plan.
3. Ingawa regulations za ujenzi wa majengo zimewekwa kwenye hii GN 93 ni makosa kwa sababu majengo yanatakiwa kuwa na regulations zinazosimama peke yake. Detailed plans zinatakiwa zionyeshe maeneo ambayo majengo tofauti yanayoruhusiwa kujengwa pamoja na planning conditions za hayo maeneo. Kilichofanyika ni kuunganisha space na planning conditions na hivyo kuleta matatizo. K.m. wanasema jengo lolote la ibada ni lazima lijengwe katika kiwanja cha kati ya sqm 1500 na 10,000. Ina maana ukiwa na kiwanja chini au zaidi ya hapo hautaruhusiwa kujenga msikiti au kanisa?
4. Tukija kwenye hivyo vituo vya mafuta, hizi regulations zinasema pawe na mita 200 ( urefu wa viwanja viwili vya mpira) kati ya kituo na kituo. Regulations hazizuii watu kujenga ndani ya hizo mita 200. Na unaweza kuwa na vituo hata 10 vikiongozana ili mradi umeacha mita 200 kati ya kituo na kituo. Na kwa vile vinavyoangaliwa sharti ni kuwa vitenganishwe na right of way ya barabara. Aidha, vituo vinatakiwa kuwa na uzio wa zege (sio matofali bali zege na nondo). Uzio wa aina hiyo una sababu gani? Regulation zinasema pia kuwa vituo vitenganishwe kwa mita 500 katika highly concentrated unplanned areas. Ina high density planned areas hazihusiki?

Ninachosema mimi ni kuwa hizi space planning conditions hazitoshelezi mahitaji ya uendelezaji wa miji. Hizi plans zinatoa mpaka masharti ya ujenzi wa Post/Telecom college! Kuna kitu gani maalum kuhusu vyuo vya aina hiyo? Zinasema hoteli inatakiwa kujengwa katika eneo la hekta 2.4. Hawajasikia kuhusu Boutique Hotels ambazo zinajengwa katika maeneo madogo katikati ya miji?

Ndio maana nilisema zina mapungufu makubwa ikiwa pamoja na kutumia terms ambazo sio sahihi.

Ila asante kwa kunisahihisha pale nilipokosea. Na mimi nimejifunza.

Amandla....
 
Hizi regulations zinazungumzia metro, airports, njia za maji, njia za umeme n.k. lakini hazizungumzii sewage systems!

Amandla...
 
Wataalamu na mainjinia majibu tafadhali.
Unaweza kujenga Ndugu.

Ni ishu ya design tu.

Japokuwa design Yako itakuwa Iko Limited na space uliyonayo.Ni space ndiyo itaamua jengo lako likaeje,kipi kiwepo na kipi kisiwepo.

I'm a designer so far,I know.
 
Back
Top Bottom