Engine oil gani ni nzuri kwa Gari aina ya IST?

Engine oil gani ni nzuri kwa Gari aina ya IST?

Msaada kwann ukitumia sae 40 kwa Magari makuu aina shida
Kiuhalisia Sae 40 ni mzito ua kwa lugha rahisi in viscosity kubwa.... Hivyo inaweza kutoa protection nzuri zaidi kwa injini za zamani ambazo zimeshachakaa baadhi sehemu zenye misuguano...pia ni nzuri kwa mazingira ya joto na injini inayofanya kazi masaa mngi kila siku mfano dala dala.

Pia ni nzuri kwa injini za kizamani za vintage cars...

Modern engines zinapendekezwa multi grade mfano 5w30 au 10w 30.
 
nimeipata total 5w30 synthetic, japo kwa tabu sana, afu kibei kimechangamka kidogo lkn at least i have a peace of mind. ule mlio mkubwaa wa dk kadhaa mara tu ya kuwasha ulikuwa unanipa tabu sana. huku kitaa kwetu wamejaza sae 40 hatari. afu wanavyozisifia sasa. once again thanks boss
Hilo ni kweli, huku mtaani habar za 5w30 mafundi wetu hawazielewi.

Wao wameshakaririshwa SAE40 Ndio oil.

Hiyo hiyo SAE40 inawekwa kwenye trekta, Kenta, fuso mpaka IST na vits.
 
Mwezi June nmemvua Voltz Mzee mmoja mstaafu kwa bei chee.

Yeye kazoea service za bei rahisi na gar ilkua inatoa moshi mwingi Mara tu inavowashwa na kuunguruma mno.

Baada ya kuichukua nikainunulia orijino CASTROL OIL 5w30 kwa elfu 80 Lita 5.

Aisee, gar ilbadilika na kua smooth mno.
Moshi na muungurumo vikakata.

Baadae nkaenda kuirudia rangi.

Mzee tulikutana kwenye bar, aliishangaa sana jins ilivobadilika kuanzia muungurumo mpk mwonekano
 
Hilo ni kweli, huku mtaani habar za 5w30 mafundi wetu hawazielewi.

Wao wameshakaririshwa SAE40 Ndio oil.

Hiyo hiyo SAE40 inawekwa kwenye trekta, Kenta, fuso mpaka IST na vits.
Fundi haruhusiwi kukuambia kuhusu oil yeye kazi yake ni kumwaga oil na kukukabidh gari yako na tambua engine ya gari ndio gari yenyewe tusiwasingizie mafundi hata sisi wahusika ndio chanzo oil ya sae40 ni oil cheap sana kuliko oil zozote zile sasa wewe ukifika dukani ukiambiwa 5w30 au 5w40 na 10w30 au 10w40 ni 65-80 kwa dumu la Lita 4/5 unaona kuwa unapigwa wakati sae 40 inauzwa 40 unaona y nisumbuke na cha garama wakati cheap ipo lkn kumbuka hivyo unaiua engine yako taratibu taratibu ushauri wangu kwa wenye magari mpendelee kusoma manual za magari yenu kuhusiana na aina ya oil

Pia mpende kupokea ushauri kwa sisi wauza oil kuna baadhi ya vitu tunafundishwa kuhusu kumpa mteja oil sahihi kulingana na oil sahihi na ukifika dukani kwangu kitu cha kwanza nakuuliza gari inaitwaje na imetengenezwa mwaka gani ili nikupe oil iliyo sahihi na yenye API inayoendana na mwaka wa gari mwisho karibuni sana JO GENUINE SPARE PARTS AND ACCESSORIES tupo Kinondoni vijana karibu na meridian hotel upate oil sahihi kwa gari yako +255762263074/+255719263074
 
Fundi haruhusiwi kukuambia kuhusu oil yeye kazi yake ni kumwaga oil na kukukabidh gari yako na tambua engine ya gari ndio gari yenyewe tusiwasingizie mafundi hata sisi wahusika ndio chanzo oil ya sae40 ni oil cheap sana kuliko oil zozote zile sasa wewe ukifika dukani ukiambiwa 5w30 au 5w40 na 10w30 au 10w40 ni 65-80 kwa dumu la Lita 4/5 unaona kuwa unapigwa wakati sae...
Hahaha. umeeleza vizuri sana...ila hapo mwisho plzzzzz lipia tangazo la biashara [emoji3][emoji3]
 
Tsh. 100,000/=
IMG_20190917_144542.jpeg
 
Fundi haruhusiwi kukuambia kuhusu oil yeye kazi yake ni kumwaga oil na kukukabidh gari yako na tambua engine ya gari ndio gari yenyewe tusiwasingizie mafundi hata sisi wahusika ndio chanzo oil ya sae40 ni oil cheap sana kuliko oil zozote zile sasa wewe ukifika dukani ukiambiwa 5w30 au 5w40 na 10w30 au 10w40 ni 65-80 kwa dumu la Lita 4/5 unaona kuwa unapigwa wakati sae 40 inauzwa 40 unaona y nisumbuke na cha garama wakati cheap ipo lkn kumbuka hivyo unaiua engine yako taratibu taratibu ushauri wangu kwa wenye magari mpendelee kusoma manual za magari yenu kuhusiana na aina ya oil pia mpende kupokea ushauri kwa sisi wauza oil kuna baadhi ya vitu tunafundishwa kuhusu kumpa mteja oil sahihi kulingana na oil sahihi na ukifika dukani kwangu kitu cha kwanza nakuuliza gari inaitwaje na imetengenezwa mwaka gani ili nikupe oil iliyo sahihi na yenye API inayoendana na mwaka wa gari mwisho karibuni sana JO GENUINE SPARE PARTS AND ACCESSORIES tupo kinondoni vijana karibu na meridian hotel upate oil sahihi kwa gari yako +255762263074/+255719263074
Sae 40 ni Tsh.28,000 tu huku mtaani,ila kwny gari yangu ni marufuku.
 
Elimu ya bure..
Kwa gari lako na kwa mazingira ya Tanzania tumia 5w 30,
Ukikosa nenda 10w 30.....
.Anayekuambia hizi oil ni za nchi za baridi amekariri bila kusoma...

Iko hivi..
5w 30 ina uwezo wa kuhimili baridi kali kuanzia -30°C bila kupoteza viscosity yake...pia oil hii ina uwezo wa kuhimili kiwango cha juu cha joto ambacho ni +40 °C bila kupoteza viscosity yake..
Hiki kiwango cha joto nilichotaja ni joto la mazingira unayoishi (outside temperature)

10w 30 ina iwezo wa kufanya vizuri kuanzia joto la -20°C mpaka joto la +40°C...

Hii ina maana kwamba oil 5w30 na 10w 30 zina uwezo wa kusambaa haraka sehemu za injini hata kama gari limewashwa kwenye mazingira ya baridi sana kibongo bongo tunasema Arusha, Iringa, Mbeya na maeneo mengine yenye baridi.
Pia inahimili joto kali kama la Dar, Zanzibar nk.

Kwa hiyo hizi oil zinamudu mazingira yote na ndiyo maana car manufacturers wa siku hizi wana recommend oil hizi zaidi siyo Nissan, Toyota,Honda, Subaru,Mazda n.k...

Ukinunua nunua full synthetic ukikosa ndiyo ununue hizi mineral oil ambazo usivushe 3000 km.

Synthetic unaweza ukaenda km 5000 na zaidi kama umefunga oil filler genuine ndiyo ufanye service nyingine..

Full synthetic inahimili dhoruba ngumu kama milima, matope, joto, baridi, racing bila kupoyeza viscosity yake....na bei yake imesimamia kucha.

Agalia fundi wa mwembeni asikushauri uweke SAE 40 ya kawaida...hii oil ni nzito sana na utakuwa unalitesa gari bila wewe kujua...

Oil ndiyo DAMU ya engine.....zingatia if you love your car.
Wewe una weledi kwenye masuala ya oil. Safi sana, hujawa mchoyo wa elimu
 
Na kwa kuongezea tu oil filter genuine bei yake haipungui 20000 ukikuta unauziwa chini ya hapo hiyo sio genuine na mafundi wengi wanawashauri wateja kutumia sae 40 kwa sababu bei yake ipo chini sana na wengi wa mafundi wa uswahilini hawana elimu ya kutosha kuhusu hii oil
Mimi nimeenda kwa dealer Toyota Arusha Oilfilter ya Corolla runx sh.31,000.
 
Mimi nimeenda kwa dealer Toyota Arusha Oilfilter ya Corolla runx sh.31,000.
Ni sawa kabisa...
Mimi huwa nanunua za Nissan kwa 15000/-

Sasa unakuta mtu gari la milioni 10 anaweka oil filter ya 3500/-
Hizi cheap oil filters ndiyo zile ambazo ukisafiria safari ndefu zinaziba yale machujio ya ndani yapo kama karatasi, kisha zinavimba....hapo oil inashindwa kupanda juu kwa wingi unaotakiwa..

Sasa hapo utaona ni namna gani unavyoisaga injini yako pole pole..
 
Ni sawa kabisa...
Mimi huwa nanunua za Nissan kwa 15000/-

Sasa unakuta mtu gari la milioni 10 anaweka oil filter ya 3500/-
Hizi cheap oil filters ndiyo zile ambazo ukisafiria safari ndefu zinaziba yale machujio ya ndani yapo kama karatasi, kisha zinavimba....hapo oil inashindwa kupanda juu kwa wingi unaotakiwa..

Sasa hapo utaona ni namna gani unavyoisaga injini yako pole pole..
Hebu hizo za 15000 mkuu hebu ziangalie huku chini kwenye tred sio nyeusi kweli? Maana og bei yake ni 30?
 
Ni sawa kabisa...
Mimi huwa nanunua za Nissan kwa 15000/-

Sasa unakuta mtu gari la milioni 10 anaweka oil filter ya 3500/-
Hizi cheap oil filters ndiyo zile ambazo ukisafiria safari ndefu zinaziba yale machujio ya ndani yapo kama karatasi, kisha zinavimba....hapo oil inashindwa kupanda juu kwa wingi unaotakiwa..

Sasa hapo utaona ni namna gani unavyoisaga injini yako pole pole..
Mimi watumiaji wengi wa magari siwalaumu kws kutumia vitu feki ila shida ni mafundi ndio wanaharibu magari yao Nina uhakika mmiliki wa gari akija ukamwambia genuine oil filter ni 20000 na fake yake ni 10000 na ukamwelekeza na madhara yake sijui kama atanunua hiyo
 
Hebu hizo za 15000 mkuu hebu ziangalie huku chini kwenye tred sio nyeusi kweli? Maana og bei yake ni 30?
Huku chini ina raba nyeusi....ila kwa mujibu wa user manual ya gari yngu, part number inayosoma kwenye hiyo filter ndiyo iliyopendekezwa.....na huwa zina rangi flan kama nyeupe na maandiahi mekundu...zile za bei rahisi zaidi namba hazioani bali size tu ndiyo inaoana....
 
Huku chini ina raba nyeusi....ila kwa mujibu wa user manual ya gari yngu, part number inayosoma kwenye hiyo filter ndiyo iliyopendekezwa.....na huwa zina rangi flan kama nyeupe na maandiahi mekundu...zile za bei rahisi zaidi namba hazioani bali size tu ndiyo inaoana....
Part no ni sawa ila genuine kabisa inakua na tred za silver kwa ndani ukiangalia vzr hiyo ya 15 tred zake ni nyeusi pia yaani wanatoa kopi kama ambavyo Toyota zinatolewa ila genuine filter lazima tred yake iwe ya silver!
 
Kumbe unazungumzia tred...kwa mfano wiki mbili zilizopita nimefanya service....hii filter ina tred za silver...si nyeusi....ila sehemu nyingi inauzwa 15000 mpka 20000 kwa huku Arusha...sijui sehemu nyingine...
Part no ni sawa ila genuine kabisa inakua na tred za silver kwa ndani ukiangalia vzr hiyo ya 15 tred zake ni nyeusi pia yaani wanatoa kopi kama ambavyo Toyota zinatolewa ila genuine filter lazima tred yake iwe ya silver!
 
Mkuu
Nakushauri Iwapo Una Nafasi Yaani Eneo Ulilopo Tayota Tanzania Limited Wana Ofisi Nenda Na Engine Number
Wanauza, Wanatoa Ushauri Aina Ya Vitu Vya Kuweka Kwenye Gari Yako


Kuna Jamaa Ana Toyota Max X AliwekA Oil Aipendayo Hasa Akizingatia Kuwa Ataibadili Baada Ya Kilometres 10000
Gari Yake Ikawa Nzito Sana Hasa Anapotaka Kuondoka


Aliwatembelea Toyota Tanzania Limited
Akapewa Ushauri Na Oil Sahihi

Alichoambiwa Anaweza Kununua Kipuri Toyota Tanzania Limited Halafu Akaenda Kufungiwa Kwa Fundi Wake Mtaani Iwapo Ataona Hatamudu Gharama
 
Wakuu nataka msaada kidogo.
Gari yangu ninapo ipaki pahala na kuwasha AC na kutulia kidogo, tatizo linakuja wakati wa kuondoa, gari inakuwa nzito kuchanganya mpaka kama dakika moja hivi na nikiizima AC ile hali inapotea kabisa Nini tatizo? Assnte
 
Back
Top Bottom