English Medium mnawachosha watoto wetu.

English Medium mnawachosha watoto wetu.

Ni saa 10 na nusu alfajiri ninaamka kujiandaa kwa ajili ya kwenda harakati, nafuata taratibu zangu za kila siku, napiga goti namshukuru Mungu kwa uzima naingia bafuni kujishikashika na sabuni pamoja na maji ya baridi ili kuzimua akili ikae mguu sawa. Huwa nachukua nusu saa tu kujiandaa na kwenye saa 11 kamili ninakuwa njia kuelekea ofisini ila kuna kitu nimekiona hakipo sawa kwa zaidi ya miaka miwili.

Tokea kumekuwepo na utiritiri wa hizi shule za binafsi maarufu kwa jina la English Mediums basi sio ugeni kukutana na gari la shule (School bus), mabasi ya njano, haswa majira haya ya saa 11 na saa 11 na nusu zikiwa na watoto wadogo wakienda shule. Ni jambo la kufikirisha sana, kiasi kwamba ukitazama ndani ya magari hayo utakuwa kitoto kimeuchapa usingizi bila wasiwasi, hajafunga mkanda, kiufupi usalama ni mdogo kwa watoto wetu.

Masuala ya msingi ambalo nimepata kuona tunawaumiza watoto wetu ni mambo mawili:
  • Suala la kuamka kuwahi shule, kwa hakika ninathubutu kusema kuwa Mtoto anayesoma shule ya Msingi Muungano anaenjoy Maisha ya shule kuliko ambaye anasoma St. X English Medium. Unaweza kukataa ila nitakupa scenario hizi kadhaa uone mtoto wa kidumu na mfagio anaishi huku wenzake wakiishia. Mtoto anayesoma Muungano anaweza kuamka saa 12 na nusu tena kwa bakora za kutosha kutoka kwa Bi Mkubwa na darasani akaingia saa 1 na nusu, Maisha yanasonga. Mapumziko kwake ni kwenda kucheza mpira na kula barafu za mama Aisha. Turejee kwa Mtotoanayesoma St. X English Medium ambapo tokea saa 11 na nusu au saa 12 anazunguka na basi mji mzima na akiingia darasani saa 1 kamili, mapumziko yao watakunywa uji na kupumzika kweli. Wadau wa elimu tazameni kwa ukaribu jambo hilo, binafsi kuna shule zaidi ya tano ambazo saa 12 kasoro mbasi yao yanazunguka na watoto wakiwa wameuchapa usingizi wa kutosha. Montesorri, Jabal Hira, pamoja na Buyegi Archbishop Mayala nimepata kupishana na magari yenu mara kadhaa alfajiri watoto wakiwa wameuchapa.​

View attachment 3052567

  • Suala ya mabegi makubwa na mazito, nina Rafiki yangu ambaye mtoto wake amepata ulemavu kwenye mgongo, mtoto wa darasa la nne ila anabeba begi zito utadhani utingo. Hakuna maana ya uwepo wa ratba za masomo (timetable) halafu wanafunzi wakapewa maelekezo kuwa abebe vifaa vyote vya shule kila siku. Kwanini shule zisitengeneze makabati ambayo watoto watahifadhi vifaa vyao na kutembea na vifaa kiasi tu. Kuna wakati Bismarck na Tulele walikuwa wanaongoza kwa watoto wao kubeba vitu vizito, yaani begi utadhani mkimbizi!? Askari wa Barabarani kuweni makini na mabasi haya kwani sidhani kama ni utaratibu kuendesha watoto kwa mtindo wenye hatari namna hiyo. Simamisha gari kisha ingia watazame watoto waulize kama mikanda inafaya kazi, je kuna Fire extinguisher na vifaa vya usalama, ongea na msimamizi wa watoto upate kujua hali halisi ya watoto.​
View attachment 3052561

Mamlaka husika zifanye jitihada za msingi katika hili, watoto wetu tunawapatia ulemavu kwa uzembe wa kijinga jinga, watoto wapate usingizi wa kutosha, waamke mapema ila sio saa 10 au 11 kwa kigezo cha kuwahi shule! Hakuna tuzo ya mwanafunzi aliyewahi shule. Tuache kuweka pamba masikioni.
SIO KWA UBAYA! TUNAREKEBISHANA TU!
Ki ukweli kabisa kwa wanaojua biolojia na psycholojia ya watoto watakubaliana namimi hii haiko sawa...sisi wazazi tunamatakwa yetu juu ya watoto wetu.

Yaani Mzazi anadictate nini mtoto aweze ku achieve bila kujia madhara na mzigo kwa mtoto.

Juzi natoka Kinondoni nasindikiza Mgeni wangu anayesafiri na Basi la Esta linampitia njiani saa kumi na moja nakutana na watoto wa dogo wa Aidha Nursery au La Kwanza wako njiani na mabegi.

Nilisikitika sana kwani hata mimi na utu uzima wangu kuamka usiku ni mbinde kwa sababu tu ya shida.

Kama mtoto saa kumi na moja yuko barabarani je huyu kaamka saa ngapi?

Je tunajali kwamba watoto lazima wapate haki yao ya Utoto? Wacheze, walale muda wa kutosha, wajifunze lugha na tabia za jamii yao na kupumzika?

After all umempeleka mtoto Kwenye hiyo Nursury yako je akimaliza anapata nini? Kunq faida kubwa kiasi gani mpaka ku jeorpadize haki ya mtoto?
 
Changamoto ilioko hapo ni shule kutokuwa na usafiri wakutosha unakuta usafiri mmoja unachukua watoto mitaa zaidi ya 20 hapo unategemea dereva aamke saangapi paka anakuja kumaliza mtaa wa mwisho ni saa ngapi na shule anaingia saa ngapi na masomo yanaanza saa ngapi. Mamlaka husika kabla ijaipa kibali shule iangalie idadi ya usafiri ili kuepusha hii kero mtt hapati muda wa kutosha wa kupumzika kwa kweli anatoka amechelewa na kurudi anachelewa vilevile
 
Tunafeli sana! Tunawachosha watoto kabla ya kuwa watu wazma
Hizo shule zenyewe sasa hata akimaliza hakuna anachojua zaidi ya English.

English nayo ambayo haina makubwa/maajabu sana kwenye maisha yao.

Wazazi tunajifurahisha kupitia mateso ya watoto. Unajisikia raha kuona Mwanao anaonge Ngeli.
 
Nadhani wazazi ndio mnachagua kutesa watoto. Dudu liumalo halipewi kidole, ninyi mbona mnawapa shule za namna hiyo watoto.
 
Yani sahv shule kibao tena karibu na makazi,kumpeleka mtoto wa nursery au shule ya msingi private shule ambayo ni mbali na makazi yako na inabidi aamke saa 10 huko,huo ni uzembe wa mzazi, dogo anaamka saa 1 na 1 na nusu yupo shule
Kila mtu ana mapenzi yake na namna ya kulea watoto.

Nilipiga Stop kupeleka mtoto Boarding hadi aanze Sekondari sijali watu wanasemaje. Kwanza nalinda Uchumi wa mtoto hapo baadae.

Siwezi kumsomesha shule ya mamilioni kwa hela hizi hizi na uchumi wa tozo.

Wenye nazo wawapeleke watoto wao wanapotaka mimi nawekeza akimaliza awe na pakukimbilia.

Nimesoma na nimejifunza mengi kwenye haya maisha ya Elimu.
 
Mzazi analipa nauli ili mtoto akae kwenye kiti au asafirishwe kwa hali yoyote ile mradi afike shule??
Usalama ni jambo muhimu sana! Mtoto anaamka asubuhi na kulala tena! Sidhani kama ni jambo jema!
 
Kila mtu ana mapenzi yake na namna ya kulea watoto.

Nilipiga Stop kupeleka mtoto Boarding hadi aanze Sekondari sijali watu wanasemaje. Kwanza nalinda Uchumi wa mtoto hapo baadae.

Siwezi kumsomesha shule ya mamilioni kwa hela hizi hizi na uchumi wa tozo.

Wenye nazo wawapeleke watoto wao wanapotaka mimi nawekeza akimaliza awe na pakukimbilia.

Nimesoma na nimejifunza mengi kwenye haya maisha ya Elimu.
Tusiruhusu watoto wetu wapitie mitihani migumu ambayo tumepitia sisi!
 
Ni saa 10 na nusu alfajiri ninaamka kujiandaa kwa ajili ya kwenda harakati, nafuata taratibu zangu za kila siku, napiga goti namshukuru Mungu kwa uzima naingia bafuni kujishikashika na sabuni pamoja na maji ya baridi ili kuzimua akili ikae mguu sawa. Huwa nachukua nusu saa tu kujiandaa na kwenye saa 11 kamili ninakuwa njia kuelekea ofisini ila kuna kitu nimekiona hakipo sawa kwa zaidi ya miaka miwili.

Tokea kumekuwepo na utiritiri wa hizi shule za binafsi maarufu kwa jina la English Mediums basi sio ugeni kukutana na gari la shule (School bus), mabasi ya njano, haswa majira haya ya saa 11 na saa 11 na nusu zikiwa na watoto wadogo wakienda shule. Ni jambo la kufikirisha sana, kiasi kwamba ukitazama ndani ya magari hayo utakuwa kitoto kimeuchapa usingizi bila wasiwasi, hajafunga mkanda, kiufupi usalama ni mdogo kwa watoto wetu.

Masuala ya msingi ambalo nimepata kuona tunawaumiza watoto wetu ni mambo mawili:
  • Suala la kuamka kuwahi shule, kwa hakika ninathubutu kusema kuwa Mtoto anayesoma shule ya Msingi Muungano anaenjoy Maisha ya shule kuliko ambaye anasoma St. X English Medium. Unaweza kukataa ila nitakupa scenario hizi kadhaa uone mtoto wa kidumu na mfagio anaishi huku wenzake wakiishia. Mtoto anayesoma Muungano anaweza kuamka saa 12 na nusu tena kwa bakora za kutosha kutoka kwa Bi Mkubwa na darasani akaingia saa 1 na nusu, Maisha yanasonga. Mapumziko kwake ni kwenda kucheza mpira na kula barafu za mama Aisha. Turejee kwa Mtotoanayesoma St. X English Medium ambapo tokea saa 11 na nusu au saa 12 anazunguka na basi mji mzima na akiingia darasani saa 1 kamili, mapumziko yao watakunywa uji na kupumzika kweli. Wadau wa elimu tazameni kwa ukaribu jambo hilo, binafsi kuna shule zaidi ya tano ambazo saa 12 kasoro mbasi yao yanazunguka na watoto wakiwa wameuchapa usingizi wa kutosha. Montesorri, Jabal Hira, pamoja na Buyegi Archbishop Mayala nimepata kupishana na magari yenu mara kadhaa alfajiri watoto wakiwa wameuchapa.​

View attachment 3052567

  • Suala ya mabegi makubwa na mazito, nina Rafiki yangu ambaye mtoto wake amepata ulemavu kwenye mgongo, mtoto wa darasa la nne ila anabeba begi zito utadhani utingo. Hakuna maana ya uwepo wa ratba za masomo (timetable) halafu wanafunzi wakapewa maelekezo kuwa abebe vifaa vyote vya shule kila siku. Kwanini shule zisitengeneze makabati ambayo watoto watahifadhi vifaa vyao na kutembea na vifaa kiasi tu. Kuna wakati Bismarck na Tulele walikuwa wanaongoza kwa watoto wao kubeba vitu vizito, yaani begi utadhani mkimbizi!? Askari wa Barabarani kuweni makini na mabasi haya kwani sidhani kama ni utaratibu kuendesha watoto kwa mtindo wenye hatari namna hiyo. Simamisha gari kisha ingia watazame watoto waulize kama mikanda inafaya kazi, je kuna Fire extinguisher na vifaa vya usalama, ongea na msimamizi wa watoto upate kujua hali halisi ya watoto.​
View attachment 3052561

Mamlaka husika zifanye jitihada za msingi katika hili, watoto wetu tunawapatia ulemavu kwa uzembe wa kijinga jinga, watoto wapate usingizi wa kutosha, waamke mapema ila sio saa 10 au 11 kwa kigezo cha kuwahi shule! Hakuna tuzo ya mwanafunzi aliyewahi shule. Tuache kuweka pamba masikioni.
SIO KWA UBAYA! TUNAREKEBISHANA TU!
Mpeleke mwanao St kayumba acha hizi siasa
 
Tusiruhusu watoto wetu wapitie mitihani migumu ambayo tumepitia sisi!
Kutafuta Elimu na kuhaso ni mtihani mgumu? Dont be negative....... That was learning and not torturing.

Kuna watu wana madeni wanashindia mchicha na mihogo ukimuuliza kwanini anakwambia eti anasomesha😅😅
 
Kutafuta Elimu na kuhaso ni mtihani mgumu? Dont be negative....... That was learning and not torturing.

Kuna watu wana madeni wanashindia mchicha na mihogo ukimuuliza kwanini anakwambia eti anasomesha😅😅
Hapa ila tujitahidi mtoto asione kama amekuja kuteseka! Kuna watu wengi wana maisha mazuri sana ila wanavyowalea watoto wao ni kipuuzi sana! Sina maana kwanza ni vibaya mtoto kuona na kusihi kwenye ugumu ila isiwe kwenye dhana ya kukomoa!
 
Hapa ila tujitahidi mtoto asione kama amekuja kuteseka! Kuna watu wengi wana maisha mazuri sana ila wanavyowalea watoto wao ni kipuuzi sana! Sina maana kwanza ni vibaya mtoto kuona na kusihi kwenye ugumu ila isiwe kwenye dhana ya kukomoa!
We mlee kwa uwezo wako. Usije ukafa njaa bure kwa kujikamua vitu ambavyo huna. mwisho wa siku utaishia kwa kiboko ya Wachawi
 
Back
Top Bottom