Enyi ndugu Waislamu, funga yenu isifanye wasiofunga wateseke

Enyi ndugu Waislamu, funga yenu isifanye wasiofunga wateseke

Expensive life

JF-Expert Member
Joined
May 2, 2020
Posts
2,971
Reaction score
9,437
Ndugu zangu, juzi nikiwa katika pita zangu mitaa ya Kariakoo, baada ya mizunguko kadhaa nikaona ngoja niingie moja ya maduka makubwa ya Bakhresa yanayouza vinywaji baridi ili nipoze koo kidogo.

Baada ya kuingia katika duka lile nilimkuta muhudumu mmoja hivyo nikamuomba anipatie kinywaji.

Ajabu akaniambia hatuuuzi vinywaji muda huu nikamjibu kwa nini? Akanijibu mwezi wa Ramadhani hatuuzi vinywaji mchana mpaka saa moja usiku.

Nikamuuliza sasa kama hamuuzi mmefungua kwa nini? Jamaa akaendelea kunijibu kwa ukali nimesema hatuuzi chochote muda huu.

Ndugu zangu Waislamu kama mnajua hamtoi huduma kwa kuwa mpo kwenye funga ni bora mkafunga kabisa ili tujue moja.
 
Muslim bwana, nlikutana na mmama muislam anamfokea mlevi, eti unalewaje alafu unajichanganya na sisi. Harufu yako ya pombe inatukera. Mjiangalie jamani to be honest. Mbona kuleta Sheria hivyo?
 
Muslim bwana, nlikutana na mmama muislam anamfokea mlevi , eti unalewaje alafu unajichanganya na sisi. Harufu yako ya pombe inatukera. Mjiangalie jamani to be honest. Mbona kuleta Sheria hivyo?
Kama upo sehemu ya umma (usafiri nk) ukiwa umelewa na miharufu ya pombe kweli sio sawa.

Ila kama ukimkuta mtu kwake au mtaani ukaanza kumfuatilia na kumhoji sio sawa.
 
Ndugu zangu, juzi nikiwa katika pita zangu mitaa ya kariako, baada ya muzunguko kadhaa nikaona ngoja niingie moja ya maduka makubwa ya Bakhresa yanayouza vinywaji baridi ili nipoze koo kidogo.

Baada ya kuingia katika duka lile nilimkuta muhudu mmoja hivyo nikamuomba anipatie kinywaji.

Ajabu akaniambia hauuzi vinywaji muda huu nikamjibu kwa nini? Akanijibu mwezi wa Ramadhani hatuuzi vinywaji mchana mpaka saa moja usiku.

Nikamuuliza sasa kama hamuuzi mmefungua kwa nini? Jamaa akaendea kunijibu kwa ukali nimesema hatuuzi chochote muda huu.

Ndugu zangu waislamu kama mnajua hamtoi huruma kwa kuwa mpo kwenye funga ni bora mkafunga kabisa ili tujue moja.
Kwani mnapata faida gani kuchokoza waislamu humu, kwani duka la bakhresa ni la serikali siuende kwenye duka lingine la John ununue unacho taka, huwezi kupangia mwenye mali utaratibu wako.
 
Tuvumiliane jamani mwezi wa Toba huu na ni wiki ya pili hii bado wiki 2 tu

Mbona tunavumiliana kwa mengi?
Huoni public transport wanapiga nyimbo za dini wakijua fika kuna kila aina ya watu halafu ni public

Ila tunavumiliana tu
Na wewe kata kushoto hapo utamkuta mangi anauza kila aina ya kinywaji shida umeitatua na kiu umekata

Have a nice day buddy
 
Tuvumiliane jamani mwezi wa Toba huu na ni wiki ya pili hii bado wiki 2 tu

Mbona tunavumiliana kwa mengi?
Huoni public transport wanapiga nyimbo za dini wakijua fika kuna kila aina ya watu halafu ni public

Ila tunavumiliana tu
Na wewe kata kushoto hapo utamkuta mangi anauza kila aina ya kinywaji shida umeitatua na kiu umekata

Have a nice day buddy
Kataka kwenda kwa Bakharesa ili aje aanzishe uzi.

Kila siku mada hizi...hawachoki
 
Back
Top Bottom