EONII 2023 movie ya kwanza kali ya Technology Tanzania, kama Hollywood vile

Ni nzuri japo nimeona quality yake sio HD pia wanaozungumza Kiswahili wanakosea sehemu ya kutamka R anatamka L. Hayo ni makosa makubwa sana.

Either way kama ni kweli basi ni mwanzo mzuri. Ila kwanini watumia gharama kubwa kutengeneza Sci-Fi kwanini wasitafute script writers wazuri wakaandika story nzuri na kutengeneza movies/series za kawaida kuliko haya mautopolo yao ya kila siku sijui Kitimtim mara Huba mara Pazia.

Tasnia ya filamu Tanzania badilikeni sio kila siku theme kubwa ni mapenzi na comedy za kitoto za kitimtim, yani hamna jipya.
 
Siwezi kutoa maoni yyte kuusu hii movie hadi nitazame yote ila nimesikia gharama ya hii movie imegharimu 400million za kitanzania ila sina na uwakika coz sijaona sehemu yyte ya usibitisho wa iyo pesa kama imetumika nafikir nasubili kwanza hadi niione na niwasikie kwenye interview za waandaji ndio tutapata jibu sahii
 
Anyway kwa vile ni ya kibongo, tuseme tu wamejitahidi. Ila kiuhalisia hilo trailer daaah chenga tu 😁😁😁😁 ☆☆ 2/10
 
Nimeona IST humo inazurula [emoji16][emoji16][emoji847][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Watu wanashangaa IST imefuata nini mwaka 2061 [emoji38][emoji38]
Kusema ukweli wabongo ni much know sana na clueless simultaneously.
Jaribu hata kutumia common sense, Toyota IST imetoka 2002 miaka 21 imepita lakini je leo hauzioni barabarani? Hapana mpaka leo 2023 bado zipo barabarani, je kitu gani kifanye zisiwepo 2061? Hizi comment zenu zinawachoresha upeo wenu kichwani.

For the sake of the argument, katikati ya story ni lazima protagonist awekwe kwenye mazingira au situation ngumu na helpless labda hizo futuristic vehicles zimerun out of electricity na possibilities, nyingine, hivyo kwa desperation atafanya chochote kile kutoka kwenye situation hiyo hata kwa kutumia bajaji lakini in this case old vehicles kama IST sababu movie imesetiwa 2061. Kuonyesha kwamba chochote kinaweza kuwa useful in difficult situation. Ukibanwa na njaa jangwani utakula hata siafu.

Na nani amekwambieni 2061 kutakuwa hakuna Toyota ISTs duniani? Hollywood na wazungu wanajivunia vya kwao na ninyi jivunieni vya kwani acheni kuwa suckers wa vitu vya watu. Na kwa akili primitive za watanzania Genre ya Sci-Fi itakuwa ngumu kustawi kama reasoning yenyewe ndio kama za hawa watu.

Hii ndio sababu situmii JamiiForums siku hizi, lazima utakuta clueless mjuaji mmoja anayejikuta ana akili nyingi anaandika pumba bila kujua tena kwa kujiamini kabisa.
 
na mandhari yake ni ya Teknolojia na muonekano ni wa Tanzania baada ya 2061.

Dak 1.16 -1.17 ya trailler

Inaonekana Toyota IST old model, sasa sijui kama ifikapo 2061 kutakuwa na IST old model...
 
Inaonyesha mambo yetu ya asili - kichawichawi?
 
Mkuu acha nongwa na ukike.yaani ushaanza tafuta makosa.jamaa wamejitaidi mnooo tunatakiwa tutoe support kufika mbali sio hiv jmn

Kuna mahali popote nimetoa tusi kwako au kwa mtu mwingine?

Comment yangu imekaa kuonesha kosa la kiufundi ambalo muongoza filimu hakupaswa kulifanya...

Hiyo filamu haijawa released officially, hivyo waandaaji wanawaweza rekebisha baadhi ya scenes kutoka na positive reviews kama hizi...
 
Mkuu acha nongwa na ukike.yaani ushaanza tafuta makosa.jamaa wamejitaidi mnooo tunatakiwa tutoe support kufika mbali sio hiv jmn
Wakati Sonic the hedgehog ya kwanza inaachiwa trailer watu wali-criticize muonekano wa Sonic, waandaaji wakaubadilisha na baada ya hapo (huo muonekano mpya) ukapendwa na kuifanya Sonic the hedgehog kua moja ya movie iliyokubalika ambayo ime-base kutokana na game.

Movie kibao Hollywood b4 hazijawa released watu hukosoa trailers kuanzia CGI yenyew iliyotumika mpaka baadhi ya details ambazo wanaona haziko sawa

Watu wanapoonyesha makosa haina maana eti hawataki kukisapoti, hiyo ni njia nzuri ya waandaaji wa filamu kuonyeshwa makosa katika bidhaa yao na kuyarekebisha kabla muvi haijaachiwa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…