EPA, ESCROW na RICHMOND nazo zilitetewa kama inavyotetewa DP World

EPA, ESCROW na RICHMOND nazo zilitetewa kama inavyotetewa DP World

Mkuu ukiwa kama baba ama mama wa familia hapo kwako.

Watoto wako wakiwa watukutu, kufuja mali hovyo, umalaya, wizi mtaani na tabia zote mbaya utamkodisha jirani akusaidie kuchukua hatua dhidi ya wanao.

Wizi, ufujaji wowote ule wa mali za umma ni kutokana na kuwa na serikali yenye viongozi hovyo wasioelewa wajibu zao kwa dhamana waliyopewa.

Serikali hasi duniani kote hujificha kwa udhaifu huo ili wao wajinufaishe.

Tujifunze kuwa wazalendo na wawajibikaji katika mali za umma lakini kuchukua hatua kali kwa wabadhirifu wote na wazembe.
Tatizo lenu kila jambo mnataka kulifanya la kisiasa. Wakati wa raisi Kikwete hao wanaokutuma upige kelele leo ndio waliokuwa wanajifanya kupiga kelele kuwa serikali ya Kikwete imeshindwa kupambana na wauza madawa ya kulevya, na kwamba wao wakiingia watawakamata wote na kuwatupa ndani.

Magufuli alivyoingia akalifanyia kazi swala hilo kwa kuanza kamata kamata. Kilichotokea kila mtu anakijua. Wauza madawa hao hao wakaungana na hao waliokuwa wanapiga kelele kuhujumu oparation ile ili isiendelee.

Kwahiyo hapo bandarini hata serikali ingesema ichukue hatua ambazo unasema, wale wapiga kelele wangehongwa tena ili wapaze sauti ili ionekane wameonewa, na pengine na wewe leo ungekuwa mmoja wa watetezi wao kisa tu kuna mwanasiassa au kiongozi mmoja unaempenda kawatetea.

Kuwafunga watu au kuwatesa kila siku hapo bandarini haiwezi kusaidia kitu. Sana sana vyama vya upinzani na hao jamaa wa haki za binadamu wangelalamika kuwa jamaa wanaonewa na hivyo nchi kutengwa kimataifa na pia kuendelea kupoteza mapato ya bandari.

Ndomaana serikali imeamua kufukuza majizi yote ili tuanze upya.

Hao wanaoalalamika wengi ni wanufaika wa mfumo mbovu uliyopo sasa hivi bandarini.
 
CCM haikwepi lawama, lakini wangemuelewa Samia na malengo yake wasingekuwa na aina hii ya mawazo waliyonayo.
Wapiga madili bandarini, vishoka na wakwepa kodi wao sasa hivi maji yamewafika shingoni. Na ukizingatia wamehonga watu mamilioni ili wawasaidie kupiga kelele.

Sasa mamilioni yameliwa na serikali imewapuuza.

Serikali imeshagundua kwamba ikicheka na nyani itavuna mabua.
 
Wapiga madili bandarini, vishoka na wakwepa kodi wao sasa hivi maji yamewafika shingoni. Na ukizingatia wamehonga watu mamilioni ili wawasaidie kupiga kelele.

Sasa mamilioni yameliwa na serikali imewapuuza.

Serikali imeshagundua kwamba ikicheka na nyani itavuna mabua.
Siku zao zinahesabika.
 
Escrow na Richmond haifanani kabisa na DPW ni vitu viwili tofauti kabisa.

Escrow na Richmond ni wizi wa kimfumo wa viongozi wa ngazi za juu, DPW ni uwekezaji wa pande mbili kwa maana ya biashara ya serikali ya Tanzania na ile ya Dubai.

DPW inahusisha utaalam wa masuala ya upakuaji wa makasha pale bandarini kama ilivyokuwa TICTS wakati Escrow ni wizi wa pesa za masuala ya umeme.

Mwenye uzoefu na masuala ya uongozi wa TZ anajua fika kwamba uzi huu ni wa kujaribu kuendelea kupotosha umaa juu ya malengo mazima ya uwekezaji na faida zake pale bandarini lengo haswa likiwa ni kuwalinda wezi wetu halisi na wahujumu uchumi.

Umeongea vizur Mkuu,

Wala Rushwa na wapiga madeal lazima wapinge sura mpya kuingia pale bandarin
 
Back
Top Bottom