EPA na mambo yake

EPA na mambo yake

Raisi amenena leo huko Arusha, kwamba hili kundi la akina Jeetu ni kundi la kwanza tu. Kuna makundi mengine yatafuatia. Sounds like promising news!
 
EPA071108.JPG

Farijala Hussein (kushoto) na Rajab Maranda ambao ni watuhumiwa wapya wa ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam alhamisi ambako walifikishwa kwa mara ya kwanza. (Picha na Yusuf Badi).
 
....hii sinema mpaka hapa ilipofika inanoga...tume maalum wamejitahidi ..inabidi angalau tuwape sifa za awali......SIFA ZA JUMLA I BEG TO RESERVE HADI SINEMA YOTE IISHE....

....WEKA GEAR WANANGUUU!!!!...TWENDE KAZI!!!!
 
EPA accused now 13 as three more are arraigned
FAUSTINE KAPAMA
Daily News; Thursday,November 06, 2008 @21:15

The number of people accused of stealing money from the Bank of Tanzania (BoT) in connection with the External Payments Arrears reached 13 when three more businessmen appeared in a Dar es Salaam court yesterday charged with stealing a total of 10bn/-. Now 13 people are so far accused of stealing a total of 41bn/- from the central bank.

The three accused - Dar es Salaam residents Farijala Shaaban Hussein and Rajab Shaban Maranda and Arusha resident Japhet Laiyandumi Lima were remanded until today after denying the charges before separate magistrates at the Kisutu Resident Magistrate’s Court.

The trio is accused of conspiracy, forgery, uttering false documents and obtaining credit by false pretences, as alternative count to theft. They will appear in court today in some cases and on November 10, 14 and 20, for either determination of their bail or preliminary hearing.

The prosecution comprising of Principal State Attorney Stanslaus Boniface, Senior State Attorney Frederick Nakulilo and State Attorneys Biswalo Mganga, Daud Momburu, Edgar Luoga, and Assistant Commissioner of Police Charles Kenyela said investigations were ready. The accused are represented by advocates Mpaya Kamala, Martin Matunda, Joseph Tadayo, Mark Anthony and Hashim Rungwe.

Principal Resident Magistrate Euphemia Mingi was told that Lema stole 2.6bn/- on August 25, 2006 and was also charged with alternative count of obtaining credit by false pretences. Lema reportedly obtained a credit of 2.6bn/- from the bank, purportedly showing that Njake Enterprises had been credited by C. ITOH of Japan in consideration for value received.

Before Resident Magistrate Waliarwande Lema, Hussein and Maranda were accused of conspiring in Dar es Salaam and later stealing 3,868,805,757/15, between January 18 and November 3, 2005. On January 15, 2005, the pair allegedly forged certificate of business registration number 462118 with its register extract and later on September 12, 2005, uttered the documents to United Bank of Africa (UBA), showing that the documents were signed and issued by the registrar to Mwibara Farm.

Resident Magistrate Anyimwilile Mwaseba was told that the two men forged similar documents showing that they were partners of business in the company called Money Planners Consultant. On November 29, 2005 they allegedly uttered the documents to the UBA. On September 8, 2005, the accused allegedly forged a deed of assignment between P. Gracel Company Limited of German and Money Planners of Tanzania, showing that one Jonas Back and Fundi H. Kitengo were directors of the companies, respectively.

It was further claimed that on November 2, 2005, the accused uttered the document to the BoT and later on December 7, 2005, they stole 2,266,049,041/25. The accused were also charged with alternative count of obtaining credit of the said amount by false pretences. Resident Magistrate Khadija Msongo was told that that the same people between April 1 and September 2, 2005, conspired and later stole 1,864,949,294/45.

The same accused allegedly forged certificate of business registration number 151025 and its register extract and later tendered the documents to the UBA, showing that they were signed and issued by the registrar to Kiloloma Brothers. Maranda, on the other hand, appeared separately before Resident Magistrate Hezron Mwankenja charged with forging a deed of settlement between Rashish Limited of Tanzania and General Market Limited of India.

The accused allegedly showed that the Indian Company had credited 207,284,391/44 to the Tanzanian firm. On August 15, 2005, the accused uttered the document to the BoT and three days later stole the money. Meanwhile, Jayantkumar Chandubhai Patel, alias Jeetu Patel and nine others accused of stealing 31bn/- in similar offences yesterday failed to meet bail conditions. Before Resident Magistrate Neema Chusi, Jeetu, Devendra Vinodbhai Patel, Amit Nandy, Ketan Chohan each was to deposit 940m/- but none of them managed to do so.

Before Resident Magistrate Eva Nkya, Jeetu Patel and Nandy, the trio was required to deposit jointly half of 4,924,494,477/- and surrender in court title deed of property with equivalent amount. Bahati Mahenge, Manase Mwakale, Davis Kamungu, Godfrey Mosha and the lone woman, Eddah Mwakale also failed to meet bail conditions set by Magistrate Lema, requiring each to deposit 240m/- in cash, or title deed of property with equivalent amount.
 
unaweza vipi kumwadhibu mtu halafu ndio umfikishe mahakamani? la pili; kama watu hawa (na wengine watakaoongezwa labda kesho) wanashtakiwa kwa makosa yale yale lakini katika kesi mbalimbali tofauti (which makes sense). Wanapelekwa kwa mahakimu tofauti n.k

now....mpangilio ulivyo ni rahisi kuona picha inayoandaliwa kufikia mwisho wake, this is brilliant!! mnakumbuka mchezo wa "kioo kioo alikivunja nani".. ?
 
Nakubaliana na wewe mkuu especially kwenye kuhusu watuhumiwa wengine.
Tunajuwa kabisa kuwa watumishi wa BOT walijuwa wazi kuwa documents zote zilkuwa forgery...Deal ilikuwa na vi memo kutoka kwa viongozi wa nchi nk.

Hawa kina Jeetu na Lukaza waliplan deal na walishirikiana kwenye implementation na ndio maana wakawatumia wanasheria wa Malegesi ili kujidai ku "Confirm" kwamba makampuni hayo ni real.

Accompanied by vimemo kutoka kwa watop flani flani dili lilipita na hata Ballali alikiri.

Ni paka anavishwa kengele so tutaona mwisho wa movie..Kama ni kweli haki inatendeka tutajuwa na kama si kweli pia tutajuwa.

Jambo moja namuomba Mh Rais ni kwamba hili lisiwe kiini macho hata mara moja...Kwasababu tunafuatilia kwa karibu sana...

Anayeshikwa na mali ya wizi ndiye mwizi.
Wafanyakazi wa benki kuu kusingizia kuwa walitumwa na watu wa ngazi za juu kuindhinisha huo wizi ni jambo lisilokubalika.Mahakama iwashughulikie kikamilifu ili watu wakiajiriwa wajue wajibu wao kama wasomi wanatakiwa wafanye nini kujenga heshima ya taaluma zao.Naomba mahakama isiwe na huruma nao kabisa ili kukomesha tabia ya wasomi kuwa puppets badala ya kuzingatia taaluma zao.Wakiona hawawezi kuzingatia taaluma zao kwa nini hawakujiuzulu nafasi zao? Wangejiuzulu wangekuwa na heshima na hadhi ya juu sana sasa hivi.Mahakama iwashughulikie ili kutoa onyo kwa wasomi wapuuzi ambao wanapoteza fedha za wazazi wao na umma na baadaye kuishia tu kuwa puppets na vibaka.

Pia Kuna wafanyabiashara waliokamatwa ambao pia wanajidai watatapika cheche kuwataja vigogo wa serikalini au siasa waliowatuma ili akaunti zao zitumike kuiba. Aliyeshikwa na mzigo wa wizi na ahukumiwe kuwa ndiye mwizi ili kutoa funzo kwa wafanyabiashara wengine ili wakome kukubali biashara zao na akaunti zao kutumiwa kuwaibia wananchi.

Hii kesi ikiamuliwa vizuri wasomi na wafanyabiashara hawatakubali hata siku moja kutumiwa kama puppets wa wanasiasa au vigogo wa serikali au mashirika ya umma kuwaibia wananchi.Wasomi walioajiriwa watafanya kazi kwa kujiamini bila woga wa mheshimiwa kasema tuibe na wafanyabiashara watakaa mbali na EPA zingine kuogopa yaliyowapata akina Jeetu Patel,Lukaza na wengineo.

Hii kesi yaweza badilisha kabisa ethics za utendaji kazi na za wafanyabiashara kama itaamuliwa vizuri.Mahakama isisikilize porojo na mabomu ya wafanyakazi wa benki kuu wanaotuhumiwa na hao wafanyabiashara kwani walikuwa wapi muda wote kulipua hayo mabomu?

Walisubiri hadi wasumbue bunge,serikali na mahakama iwatie ndani ndipo wajifanye raia wema walio tayari kulipua mabomu?

Wananchi hatuko tayari kusikiliza mabomu ya hawa vibaka wafanyakazi wa benki kuu na hao vibaka wafanyabiashara.

Kwanza Kikwete amewamehurumiwa mno.Hebu fikiria mtu umeiba pesa kuanzia 2005 leo 2008 miaka mitatu toka umeiba hayo mabilioni.Ina maana kwa miaka mitatiu umezungusha hiyo hela kwenye biashara na umepata faida kubwa sana.Leo serikali inasema rudisha zile hela ulizochukua na kuziingiza bila riba wala faida urudishe tu principal amount na wanakupa miezi sita hutaki.Hivi hawa mafisadi kama si wapuuzi ni nini.Ingekuwa mimi ningerudisha chap chap hiyo principal amount nikabaki na faida maana ulikuwa kama mkopo usio na riba wa miaka mitatu ambao unapewa uzungushe kwenye biashara bure.

Kitendo chao cha kukataa kurudisha ni uhalifu mkubwa ambao hata chizi hawezi kuwasamehe.Pesa hawarudishi eti wana mabomu watalipua.Siko tayari kusikiliza mabomu yenu shenzi nyie nasikiliza mahakama tuu inaamua nini.

Mafisadi hao wafanyabiashara na hao wafanyakazi wa Benki kuu wangekuwa wazalendo wangelipua hayo mabomu siku nyingi si kusubiri wafike kizimbani ndio wajitie wana breaking news kwa mheshimiwa jaji au hakimu.
 
mkuu wa kaya nakupongeza kwa hii hatua inayotia moyo, hata mimi sasa nasema yes we can, sema manji na wengineo wengi tu wanaohusika wasikose. nawasikia wakisema sema na methali yao heti wewe ni lile zimwi, kwahiyo wanahope wenzio.
 
Tukishindwa kumpongeza JK na hatua hii tutakuwa sio wastaarabu na tutaonekana ni walalalamishi wasio na upeo. Give Credit where credit is due!!!!!

Jk has performed above any standard known in dealing with MAFISADI.

Alichofanya JK ni kwanza kuwadhoofisha mafisadi kwa kuwaambia warudishe hela kila kitu kitakuwa powa.

Kumbuka kama mafisadi wangepelekwa Mahakamani kwanza kama wengi tulivyotaka humu ndani, basi wasingekosa hiyo 50% ya hela walizoiba kupewa dhamana according to the law. Kwa kuwaambia warudishe hela kwanza, umeona inavyokuwa kazi kwa mafisadi kutoa hela sababu hata kama walikimbiza hela nje, sasa itakuwa vigumu hela hizo kuwasaidia kutoka ndani.

Nasikia serikali imeweka mkwala kuwa kila hela itakayoletwa kuwekwa dhamana lazima ijulikane imetoka wapi na wazee wa TRA wako hapo mahakamani wakiangalia kwa ukaribu.

Ukileta nyumba nayo uchunguzi unaendelea kama kila kitu kiko clean.

Hapa wazee hata kama ni sinema basi tukubali kwenye trailer JK kashinda.

JK OYEEE!! JK OYEE! ahahahahhhhhhh
 
Sioni cha maana hapa! Mpaka atishiwe kiasi hiki ndio apeleke watu mahakamani! hakukuwa na haja ya kuwachelewesha kiasi hiki!!! Wezi ni wezi tu! Sasa sijui credit anachukuaje JK wakati wananchi including wana JF kumkalia vibaya JK na wenzie! Lazima tukubali JK na kundi lake wametikiswa sana na wananchi! Na bado, asipoeleweka hakuna kipindi cha pili! Kama kesi hizi ni kiini macho ajue atakuwa anatukana mamba na mto hajavuka! Na atakaposhindwa kuvuka naye atajumuishwa kwenye kundi hilohilo! Heko wananchi mliosimama kidete!

Kama JK anadhani anaweza kucheza na waTz watamwonyesha kazi! Atawafunga hao na bado atatoswa na yeye pia! The same trick aliyotumia na anayosifiwa kwayo na baadhi ya watu hapa, yaani kuwaahidi watakaorudisha hela atawaacha lakini akawatosa!
 
Tukishindwa kumpongeza JK na hatua hii tutakuwa sio wastaarabu na tutaonekana ni walalalamishi wasio na upeo. Give Credit where credit is due!!!!!

Jk has performed above any standard known in dealing with MAFISADI.

Alichofanya JK ni kwanza kuwadhoofisha mafisadi kwa kuwaambia warudishe hela kila kitu kitakuwa powa.

Kumbuka kama mafisadi wangepelekwa Mahakamani kwanza kama wengi tulivyotaka humu ndani, basi wasingekosa hiyo 50% ya hela walizoiba kupewa dhamana according to the law. Kwa kuwaambia warudishe hela kwanza, umeona inavyokuwa kazi kwa mafisadi kutoa hela sababu hata kama walikimbiza hela nje, sasa itakuwa vigumu hela hizo kuwasaidia kutoka ndani.

Nasikia serikali imeweka mkwala kuwa kila hela itakayoletwa kuwekwa dhamana lazima ijulikane imetoka wapi na wazee wa TRA wako hapo mahakamani wakiangalia kwa ukaribu.

Ukileta nyumba nayo uchunguzi unaendelea kama kila kitu kiko clean.

Hapa wazee hata kama ni sinema basi tukubali kwenye trailer JK kashinda.

JK OYEEE!! JK OYEE! ahahahahhhhhhh


....yaani unataka tumpongeze huyu kichekesho kwa kutekeleza wajibu wake? Ni mitazamo potofu kama hii ndio inatufanya watanzania tushindwe kuwawajibisha viongozi wetu kwa kuona kwamba wanapotimiza wajibu wao kama kusimamia ujenzi wa barabara, mahospitali na mashule tunaona wametufanyia favour. Amka wewe! Bado upo usingizini tu.
 
EPA071108.JPG

Farijala Hussein (kushoto) na Rajab Maranda ambao ni watuhumiwa wapya wa ufisadi wa fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam alhamisi ambako walifikishwa kwa mara ya kwanza. (Picha na Yusuf Badi).

du! huyu farijala alikuwaga kaka mkuu forodhani primary in the 80s.
 
Ina maana Raia Mwema walijua kabla? Maana hii habari ilitoka Jumatano siku ambayo walifikishwa mahakamani.

Ukisoma baadhi ya sentesi utaona kuna jambo na wanaonyesha wazi kuwa Jeetu Patel na wengine watapelekwa mahakamani na RA na Manji bado kuna mvutano.

Mafisadi wa EPA hakuna wa kupona

Mwandishi Wetu
Novemba 5, 2008

DPP asema sheria itawabana wahalifu

Wamejichimbia Mbezi Beach kupitia mafaili

SIKU chache baada ya Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kukabidhiwa majalada ya watuhumiwa wa wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), imefahamika kwamba waliolipa fedha hawatakwepa mkono wa sheria ikibainika kuwapo jinai wakati wa kuchota fedha hizo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya Serikali ambazo Raia Mwema imezipata zimeeleza kwamba hakuna mhalifu atakayesalimika ikiwa kutakuwapo ushahidi wa kuweza kufungua mashitaka; licha ya kuwapo mgawanyiko mkubwa kuhusiana na baadhi ya watuhumiwa kuendelea kutaka kukingiwa kifua na watendaji wa ndani ya serikali na wengine kutolewa kafara.

Kwa mujibu wa habari hizo, kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na wasiolipa ndio watakaochukuliwa hatua, imekuwa ikitumika na sasa imeibua mgawanyiko kwa wahusika wa ndani na nje ya Serikali; huku kila upande ukiitumia kwa mtazamo tofauti na kwa nia ya kulinda ama kupigania maslahi maalumu.

DPP, Elieza Feleshi, aliliambia Raia Mwema, jana Jumanne, kwamba ofisi yake ni asasi huru inayoendesha shughuli zake kwa kuzingatia sheria, na kwamba hakuna nguvu yoyote itakayoweza kuwafanya wafanye jambo kinyume cha sheria.

Alipoulizwa kuhusu kufikishwa au kutofikishwa mahakamani kwa baadhi ya watuhumiwa waliolipa mabilioni ya fedha za EPA, Feleshi alisema, "hatujajua kwa sasa, kwani ndio kwanza tuko kazini," na alipoulizwa kuhusiana na kusamehewa kwa wezi, alisema, "ofisi yangu inaendeshwa kwa kufuata sheria zilizopo na hatuwezi kufanya jambo lolote nje ya sheria."

Kuhusiana na uhuru wa ofisi yake kufanya maamuzi, Feleshi alisema, "Ofisi hii (DPP) iko huru tokea tunapata uhuru kwa kuwa iliwekwa wazi katika katiba yetu ya kwanza na hadi katiba ya sasa iko hivyo, hiki ni chombo huru."

Maelezo ya Feleshi na watendaji wengine serikalini yanaonyesha uwezekano wa serikali kubadili mwelekeo kwa kuepuka kuwalinda watuhumiwa waliobainika kushiriki vitendo vya jinai wakati wa mchakato wa kuchukua fedha za EPA, jambo ambalo limeelezwa ni kutokana na msukumo mkubwa nje ya mfumo rasmi serikalini.

"Unajua hata Rais Kikwete kama kiongozi anayeongoza kwa kufuata sheria hawezi kusema lolote kuhusiana na watu watakaochukuliwa hatua kwani kazi hiyo inahusu vyombo vya kisheria ambavyo ni lazima akwepe kuwapa nafasi ya kuweza kujitetea watakapofikishwa mahakamani kwamba walishahukumiwa," anasema mtu aliyekaribu sana na serikali.

Habari za uhakika zinaeleza kwamba kuanzia Jumatatu wiki hii, wanasheria wa Serikali wamejichimbia katika hoteli moja ya ufukweni, maeneo ya Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam, wakipitia majalada yaliyowasilishwa ofisi ya DPP kutoka katika kikosi kazi (task force) kilichokuwa kikichunguza watuhumiwa wa EPA.

"Wameongeza nguvu kwa kuleta wanasheria makini baadhi kutoka nje ya Dar es Salaam kwa ajili ya kazi hiyo na wamepewa wiki mbili tu wawe wamemaliza kazi na hivi tunavyozungumza wako Mbezi wakifanya hiyo kazi kwa makini kuweza kukamilisha kabla ya kwisha kwa muda waliopewa," kinasema chanzo chetu chenye mahusiano ya kikazi na wanaofuatilia sakata hilo serikalini.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, kwa sasa kumeibuka kwa hali ya wasiwasi miongoni mwa baadhi ya watu waliohusika kwa namna moja au nyingine na sakata la EPA, hata wale ambao walikuwa wanaamini kuwa wamejificha nyuma ya watu wengine katika kampuni zilizohusika na wizi huo.

" Nakuhakikishia hakuna atakayepona pamoja na kuwa wale mnaowataka mmoja anaweza kufikishwa mahakamani lakini wengine bado kazi kubwa inafanyika kupata ushahidi usio na shaka kutokana na nguvu kubwa waliyonayo watuhumiwa hao. Nakwambia hakuna atakayepona na wasidhani kuna msamaha kwa wahalifu. Msamaha unaweza kuwapo kwa waliochukua fedha bila kutenda kosa la jinai," kinaeleza chanzo hicho.

Siku tatu za mwisho kabla ya Oktoba 31, 2008 ziku ambayo Rais Kikwete alitoa kuwa mwisho wa waliochukua fedha za EPA kuzirudisha, baadhi ya wafanyabiashara walipeleka benki mabilioni ya fedha, sehemu ikiwa ni fedha taslimu.

"Hivi nchi hii kweli kuna sheria zinafanya kazi! Haiwezekani mtu anaweza kuwa na fedha taslimu kwa mabilioni na anawezaje kuzipeleka kwa mara moja benki. Waliziweka wapi, au ndio zile zinazodaiwa kuchapishwa?" alisema.

Baadhi ya wafanyabiashara walikimbilia kulipa fedha kupitia benki mbalimbali jijini Dar es Salaam, baadhi wakipeleka fedha taslimu katika maboksi na mabegi wakiwa na imani ya kupata msamaha, imani ambayo imeelezwa kuweza kuwagharimu.

Zaidi ya Sh bilioni 69 zumekusanywa kutoka kwa waliochota fedha za EPA,kiasi ambacho kilitangazwa na Rais Kikwete alipohutubia taifa mwisho wa mwezi uliopita.

Kumekuwapo na mjadala mzito kuhusiana na kauli za Serikali kuhusiana na malipo ya fedha za EPA kuwa kinga ya kufunguliwa kwa mashitaka ya kijinai kwa wahusika.

Wanasheria, wanasiasa na wananchi wengine wamekuwa wakisisitiza kwamba baadhi ya watuhumiwa wa wizi wa fedha za EPA walighushi nyaraka na hivyo wanapaswa kushtakiwa.

Hata hivyo, bado ni kitendawili kuhusiana na nani hasa atakayefikishwa mahakamani huku kukiwa bado na hofu ya kulindwa kwa baadhi ya watu 'wazito' walioko nyuma ya kampuni 13 zilizochota sehemu kubwa ya Sh. bilioni 90 ambazo zimethibitishwa kuchotwa kwa njia ya kihalifu.

Ripoti ya Wakaguzi wa Kampuni ya Ernst and Young waliofanya kazi kwa niaba ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ilionyesha kwamba kiasi cha Shilingi 90,359,078,804.00 zililipwa kwa kampuni 13 ambazo zilitumia kumbukumbu, nyaraka na hati zilizo batili na za kugushi na kwamba kampuni hizo zilifanya uhalifu na hazikustahili kulipwa chochote.

Wakaguzi hao na Ikulu kupitia taarifa iliyotolewa na Luhanjo, Januari 9, 2008, walipendekeza wahusika wa kampuni hizo 13 wachukuliwe hatua za kisheria ndani yake ikiwamo Kagoda Agricultural Limited na kampuni tisa za mfanyabiashara mwenye asili ya Kiasia, Jeetu Patel.

Kampuni ambazo Jeetu Patel anahusika nazo ni Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.

Nyaraka za serikali zinaonyesha Kagoda Agriculture Limited inamilikiwa na John Kyomuhendo mwenye hisa 40 na Francis William anayemiliki hisa 60 katika kampuni hiyo, huku kukiwa na nyaraka nyingine muhimu zinazotaja wahusika zaidi ambao wanaelezwa kuwa na nguvu kubwa ndani ya mfumo wa.utawala.

Kampuni nyingine ni V.B & Associeties Company inazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel na Changanyikeni Residential Complex Limited inayomilikiwa na Jose Van de Merwe, Samson Mapunda na Charles Mabina ikiwa na makao yake, Sinza, Kumekucha, Dar es Salaam.

Katika orodha ya kampuni 13 zilizoghushi nyaraka zimo kampuni nyingine za Money Planners & Consultants inayomilikiwa na Paul Nyingo na Fundi Kitungi na kampuni ya Njake Hotel & Tours Limited inayomilikiwa Japhet Lema, Anna Lema, Abel Lema, Derick Lema na Benard Lema wa Arusha.

Miongoni mwa wanaotajwa kushirikiana na Jeetu Patel kupitia kampuni ya Ndovu Soap Limited ni Jayantulal Chandubhai Patel na Sidik Yacoubu.

Kampuni ya Bora Hotels and Apartments wamiliki wake wamo Jayantkumar Chandubhai Patel na Devandra Patel wakati Bina Resort Limited iliyosajiliwa Machi 31, 2005, wamo Jayantikumar Chandubhai Patel na Devendra Patel.

Kampuni ya Maltan Mining Company iliyosajiliwa Machi 8, 1993 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Hariharier Radhakrishna wakati Navy Cut Tobacco iliyosajiliwa Oktoba 12, mwaka 1995 inamilikiwa na Jantkumar Chandubhai Patel na Radakrishna.

Kampuni nyingine ni Bencon Limited, B.V Holdings, Venus Hotels na V.B & Associeties Company zinazomilikiwa na Devendra Patel na Jantkumar Chandubhai Patel, ambazo zote zilisajiliwa Aprili 4, 2005.

Katika orodha ya BRELA imo pia kampuni ya Excellent Service Limited inayomilikiwa na Emil Samanya, Peter Sabas na Elisifa Ngowi. Kampuni hiyo ilisajiliwa Mei 13, 1992 na kupewa namba 26959.

Ngowi anahusishwa pia katika kampuni nyingine ya Clyton Marketing iliyosajiliwa Juni 6, 2005 akiwa na mwenzake Edwin Mtoi.

Wamiliki wengine waliofahamika ni Rajabu Maranda na Thabit Katunda ambao wanatajwa kumiliki kampuni ya Liqiud Service Limited ambayo usajili wake ulifanyika Desemba 12, 2004 na kupewa namba 15007.

Wamo pia Johnson Lukaza na Mwesigwa Rutakyamilwa Lukaza ambao wao wanamiliki kampuni ya Karnel Meals Holdings Ltd, Mibale Farm ambayo inamilikiwa na Kizza Selemani na Farijala Hussein na Malegesi Law Chambers inayomilikiwa na Beredy Malegesi.

Wamiliki wengine ni Paul Nyingo na Fundi Kitungi, wanaomiliki Kampuni ya Money Planners & Consultants iliyosajiliwa Machi 22, 2005 na Kiloloma & Bros Enterprises inayomilikiwa na Charies Kissa, ambayo ilisajiliwa Aprili 8, 2005.

SOURCE: Raia Mwema - Mafisadi wa EPA hakuna wa kupona
 
Mzee naona kama tuliambiana makala yangu ya Jumatano kwenye Tanzania Daima ilikuwa "Ujumbe kwa DPP: Washitaki wote, au waachie wote".. Ninachoshindwa kuelewa hadi hivi sasa ni kuwa hawa jamaa na familia zao hawana wasiwasii na hawakuonesha kushtuka sana habari hii ilipokuja. Na zaidi ya yote, kwamba wote walikuwa mahali ambapo ilikuwa ni rahisi kupatikana...

Ila Raia Mwema sasa inatisha mzee... kudos kwa hawa jamaa..
 
Halisi Bravo
kwa kila kitu. Jambo moja la msingi sasa ni kujua pesa zilizokusanywa zilipo maana hizo dhamana wanazoambiwa waweke zinaweza toka kwenye makusanyo hayo hayo waliyotoa-

So Mwanyika et al, ni wakati sasa wa kuweka repoti ya hadharani waliona nini, nani alipata mgao kiasi gani, amerudisha na kiasi gani, kiasi gani hakijarudishwa.

Rais alisema by last jumamosi habari itakuwa wazi but hadi leo Ijumaa hakuna lolote.... kulikoni Mwanyika na team yakoo:..:::????
 
......na wale waliotoa vimemo ili pesa za EPA zitoke kwa hawa MATAPELI.........wasiachwe
 
Halisi Bravo
kwa kila kitu. Jambo moja la msingi sasa ni kujua pesa zilizokusanywa zilipo maana hizo dhamana wanazoambiwa waweke zinaweza toka kwenye makusanyo hayo hayo waliyotoa-

So Mwanyika et al, ni wakati sasa wa kuweka repoti ya hadharani waliona nini, nani alipata mgao kiasi gani, amerudisha na kiasi gani, kiasi gani hakijarudishwa.

Rais alisema by last jumamosi habari itakuwa wazi but hadi leo Ijumaa hakuna lolote.... kulikoni Mwanyika na team yakoo:..:::????

Kimsingi kazi bado kubwa kwa kuwa wahusika wanapambana sana na kwa sasa waliosalia wamechanganyikiwa maana hata jamaa wa Arusha hadi juzi usiku alikuwa anajiamin hatoguswa lakini jana akashitukizwa na kuchukuliwa na baadaye kupelekwa Dar, moja kwa moja mahakamani. Unajua kwa hili jamaa wamefanya kazi serious kishenzi na walikuwa wasiri kishenzi. Kwa kweli this time makachero waliotumika katika kazi ya kuwachukua na kuwapeleka mahakamani ni watu makini na wenye maadili ya hali ya juu. Sasa mpira unahamia katika mhimili mwingine wa dola, MAHAKAMA baada ya Watawala kujivua na kutoa pasi kwa DPP kabla ya yeye kutoa pasi mahakamani.

Lakini kabla ya kushangilia magoli, tunasubiri wahusika wa KAGODA, vinginevyo tutabadilika na kusema, "Jeetu katolewa kutuzuga, kwa kuwa tu ni Mhindi, ili tuone kuna kinachofanyika. Hatukutaka Jeetu kwa kuwa ni Mhindi, tumemtaka Jeetu kwa kuwa ni mmoja wa waliochota zile Bilioni 90 ambazo hazina shaka kwamba ni za wizi na kuna jinai ya wazi kabisa na hakuwa peke yake na hao kina Lukaza, Maranda na wenzake. Tunawataka watu wa KAGODA"

Jeetu Patel ni mtu mwenye uzoefu wa kukaa jela na ndio maana wamemtosa na inawezekana wamekubaliana.
 
Mode angalia kama inaweza kuunganishwa na ile ya mashitaka
 
Mkapa........ Mramba....... Mgonja....... etc
Mkuu Halisi

uUkimgusa Mkapa tu Nchi itashindwa kutwalika and am so worried kama Balali angekuwapo ila kwa watu kama Mgonja na Mramba it is easy kuwafikisha mahakamani.

Watu wagumu na mpaka upate ushauri wa kutosha ni kama kumgusa Daniel Yona,ukimgusa yona basi umemfikia na Muungwana sababu Yona alirithi mabaya ya Muungwana na anajua fika madudu katika vitabu.

Dont connecting to the dot ukianzia na mkapa.

Ishu nyingine ni kumjibu mtu juu anayelalamika kwamba tumeshindwa kumpongeza mkulu sababu ya kile alichokifanya.

Ukiangalia kwa undani watu wanaotakiwa kupongezwa ni sisi (Jamii forums) sababu bila sisi mkulu asingekuwa na uwezo wa kuwafikisha amahakamani hawa watu.

We said it here first and we are leading them to do what we want thou they might do what they wish.But we have power if they will do different from what we want...a ballot box 2010

Siye tutajipongeza mpaka pale watu wa Kagoda Kilimo Limited watakapowekwa ndani na tuambiew pesa ile ilienda wapi?

we dont need who took it we need to know who use it
 
Last edited:
Mzee naona kama tuliambiana makala yangu ya Jumatano kwenye Tanzania Daima ilikuwa "Ujumbe kwa DPP: Washitaki wote, au waachie wote".. Ninachoshindwa kuelewa hadi hivi sasa ni kuwa hawa jamaa na familia zao hawana wasiwasii na hawakuonesha kushtuka sana habari hii ilipokuja. Na zaidi ya yote, kwamba wote walikuwa mahali ambapo ilikuwa ni rahisi kupatikana...

Ila Raia Mwema sasa inatisha mzee... kudos kwa hawa jamaa..

Asipoibuka Salva mwingine kwenye gazeti hili litakuwa mwiba kwa viongozi mafisadi.
 
Back
Top Bottom