EPC + F Siyo Muujiza na Hakuna Utawala Ambao Ungeshindwa Kuutumia Kama Ungekuwa ni Absolute Solution

EPC + F Siyo Muujiza na Hakuna Utawala Ambao Ungeshindwa Kuutumia Kama Ungekuwa ni Absolute Solution

Narudia tena, hii dunia haki ya Mungu; acha tu tujimalizie miaka yetu hii michache ya 50-60 tujipitie zetu tukaangalie yanayofuata huko mbele. Unafiki na chuki za mwanadamu, AAACHA KABISA!
 
Huu ni wizi na utaleta mzigo mkubwa sana kwa serikali zi azo kuja

1. Hakuna anaye jua haya makubaliano zaidi ya samia na mbarawa

2. Hakuna anaye jua interest rate iliyo kubaliwa.

3. Hakuna anaye jua gharama halisi za miradi hii .

4. Hakuna uwazi, hawa wachina wasije siku wakazitaka hizi barabara
Bahati mbaya hakuna anayehoji. Hata wale wabunge batili hakuna wanachofikiria zaidi ya kusubiria rushwa ili waisifie mikataba ya hovyo.
 
Ndugu we umeingizwa chaka huyo kilaza hakuna analoju huyo ni mzushi mwongo wa siku zote. We isikilize na kuiamini serikali yako achana na hao wafuasi wa mwendazake wametemwa sasa wanataka kutututmia watanzania kwa maslahi yao. Atapata mazuzu lakini wenye akili wanmfahamu huyo Bams, fuatilia nyuzi zake zote, ni za kizushi zilizojaa chuki na ubaguzi
Yawezekana unakaribia kupagawa. Eti mimi Bams ni mfuasi wa marehemu Magufuli!

Wafuasi wa marehemu Magufuli wanafahamu jinsi nilivyowahi kuzikosoa sana baadhi ya sera na matendo ya marehemu, kiasi cha wengine kunitusi ni kunitaja kuwa mimi ni mpiga debe wa Samia.

Sijawahi na sitakuja niwe mpiga debe wa mtu yeyote bali nina kiapo cha cha kudumu cha kuwa mfuasi wa ukweli. Nitakiishi kiapo hicho milele.
 
Hakuna awamu ambayo hikukopa Tena magufuli ndio aliyekopa kwenye nabenk

Kwaiyo maoni yako ni nini?
Tuache unafiki wa kujisifia na kujipongeza sana kwa mafanikio kiduchu. Kuridhika na kujipongeza sana kwa mafanikio kidogo kunajenga moyo wa kurudhika na kutojishughulisha zaidi na kwa kasi zaidi.
 
Tungekua na kiongizi aina yako hakika tungefika mbali wapo baadhi lakini system haiwaruhusu kutoa maoni Yao wanabk tu kusifia ...rip Magu
Tuungane kupaza sauti, na wakati fulani kupinga kwa nguvu zetu zote, serikali inapotufanyia hadaa.
 
Nasikia kuna watu wanalipwa humu kushambulia serikali...Kwa hiyo usishangae threads za kushambulia Hadi mbinu za kutatua matatizo
DP, serikali na makampuni makubwa yasiyo na uadilifu, ndio wenye pesa za kuwahonga watu.

Hapa hatushambulii bali tunakosoa.
 
Umelewa kwa maana huyu mpuuzi amepotosha saaana
Ni vema ukaja na uzi wenye kuelezea uhalisia wa jambo na kukanusha upotoshaji kwa hoja sahihi, kinyume chake kumtusi mleta mada ww ndie unastahili kupigwa mawe kama kibaka
 
Acha uongo! Angalia Resident engineers wote wanatoka Ethiopia na hata materials nyingi za ujenzi zitatoka nje, nyie Watanganyika mtakuwa vibarua tu na kubaki kuuziana chai na chips!
Crap

Very crappy project haijaanza tayari umeshapanga safu

You are such an ass
 
Crap

Very crappy project haijaanza tayari umeshapanga safu

You are such an ass
I would wonder if a gay person like you could understand! You keep on being sodomized, that is what you can afford!
🖕
 
I would wonder if a gay person like you could understand! You keep on being sodomized, that is what you can afford!
🖕
Losing argument kijinga Hivi only works for idiots

Issue za matusi Hivi only comes from assholes
 
Nasikia kuna watu wanalipwa humu kushambulia serikali...Kwa hiyo usishangae threads za kushambulia Hadi mbinu za kutatua matatizo
Umesikia vibaya. Sifa kuu ya JF ni kukosoa bila kuogopa. Aidha, ni sehemu ambapo anaekosolewa ana haki ya kujitetea bila kuogopa. Ndivyo ilivyokuwa. Hapa hapakuwa mahali pa vuvuzela. Kiongozi makini anathamini wale wanaomueleza ukweli wao kuliko wale ambao wanaona kuwa wajibu wao ni kumsifia hata pale ambapo dhahiri amekosea. Watu kama nyie ambao badala ya kuitetea serikali kwa kujibu hoja kwa hoja mnakimbilia kumwaga matusi na kuwashutumu wenzenu kuwa wamenunuliwa mnatia doa platform hii.

Amandla....
 
Ni kitu sahihi na kitu chema kwa sababu zifuatazo
1. Miundombinu ijengwe tunaihitaji, kuhusu kulipa tutajua mbele ya safari
2. ni heri kufanya maamuzi hata kama yana makosa kuliko kutofanya maamuzi kabisa
3. Tukidaiwa deni kubwa tutaumiza kichwa na kutafuta vyanzo vipya vya mapato
4. Hata tusipo kopa kwa miundombinu basi tutakopa kwa vitu vingine vya kijinga kama mishahara, posho na kampeni
5. Makosa ni sehemu ya maisha hivyo tusiogope kukosea ndo kujifunza huko, maisha hayaji na user manual
6. Mtu hawezi kosa cha kupinga hata uwe na plan nzuri vipi
7. Uthubutu ndo msi gi wa mafanikio naipongeza serikali kwa uthubutu wa kuboresha miundombinu hata kama kuna makosa yatarekebishwa na vizazi vijavyo
 
Duh watanzania mna nongwa sana, hata mfanyiwe nini hamridhiki.

Huo mtindo wa ujenzi ni mahususi kwa ajili ya kuboost uchumi kwa maana serikali italipa zaidi lakini hela itawafikia watu kupitia hao wakandarasi. Kupitia huo ujenzi kuna vibarua, wafanyakazi mbalimbali wataajiriwa, wauza materials watapata pesa n.k so pesa mtaani itakuwepo.
Acha kujitoa ufahamu. Njoo waone vibarua wa SGR wanalipwa kiasi gani ni shilingi unaiona mtaani. Hamnaga kitu kama hichoeti fesa zitajaa mtaani. Labda uchumi wa kwenye karatasi.

Vibarua wa SGR wanalipwaa Shilingi elfu sita kwa siku na mtaani hata tunaaoishi pembeni mwa kambi za mturuki hatuzioni hizo pesa zinazosemwa.
kwa ufupi utaratibu wa ujenzi kwa mtindo wa EPC + F ni janga kwa Taifa.
 
Tunawapongeza wale wote ambao kila siku, usiku na mchana, wanafikiria namna ya kutatua matatizo ya nchi na wananchi.

Lakini watu watambue kuwa hakuna muujiza wa kuifanya nchi ipate maendeleo, na kulala na kuamka, matatizo ya nchi na wananchi yakaisha, zaidi ya kufanya kazi kwa bidii, kujinyima, umakini wa mipango na usimamizi, kuzuia ufisadi na miradi yenye mikataba ya hovyo, weledi na uadilifu wa wasimamizi na watendaji wa Serikali.

Nchi yetu ina vitu vingi vya kuisaidia ipige hatua kwenda mbele. KIKUBWA INACHOKIKOSA NI SERIKALI MAKINI, ILIYOJAA WATU WAADILIFU NA WENYE WELEDI. Hilo ndiyo tatizo kubwa la nchi yetu, kuliko mengine yote.

Matatizo yetu kwa kiasi kikubwa yanasababishwa na mipango mibovu, sera mbaya, sheria mbaya, usimamizi mbaya, wizi, ufisadi, ubadhirifu na weledi mdogo wa wafanya maamuzi na watunga sera.

Serikali yetu imekuwa ni Serikali ya hadaa kwenye mambo mengi. Ni Serikali inayofanya jambo dogo halafu kelele za kujisifu ni kubwa kupindukia. Hata inapofanya makosa, ni mwiko kukiri kuwa imefanya makosa, badala yake ni kuongeza nguvu na jitihada za kujisifu. Ni Serikali defensive, yaani kulinda kwa gharama yoyote yale makosa ambayo inakuwa imefanya.

Angalia hata mkataba wa DP, ni dhahiri kwa mtu yeyote mwenye akili timamu, mkweli wa nafsi na mwadilifu, ataona kwa uwazi kabisa mkataba huo ulivyo wa hovyo na mapungufu mengi, lakini Serikali na watu wake wanapambana usiku na mchana kuwahadaa wananchi kuwa ni mkataba mzuri sana, utakaoondoa tatizo la ajira, na kuifanya nchi iwe tajiri, na kuwezesha kufutwa kwa kodi nyingi na tozo.

Sasa limekuja suala la ujenzi wa barabara kwa kutumia utaratibu wa EPC + F. Wanavyousifia utaratibu huo ni kama nchi imevumbua muujiza mkubwa utakaomaliza matatizo yote ya ujenzi wa barabara, na kama vile tawala nyingine zote zilizotangulia zilikosa ubunifu.

Ukweli ni kwamba EPC + F, hakuna utawala ambao ungeshindwa kujenga barabara kwa kufuata utaratibu huo kama ungeonekana ni rahisi na wenye tija.

Kwa mchumi mzuri, siyo mchumi wa makaratasi, ujenzi wa barabara kwa utaratibu huu, ndiyo aghali kuliko utaratibu mwingine wowote ambao nchi imewahi kutumia.

Kwa wasioelewa, utaratibu huu wa EPC + F, mjenzi anajenga barabara kwa kutumua pesa yake, halafu Serikali itakuwa inamlipa yule mjenzi taratibu kwa kiwango kilichokubaliwa.

Mjenzi wa barabara anapata wapi pesa?
Mjenzi wa barabara anachukua pesa toka kwenye mabenki na taasisi mbalimbali za fedha.

Mjenzi wa barabara anazichukua pesa toka benki kwa utaratibu gani?
Mjenzi anachukua pesa benki kwa njia ya mkopo. Mkopo ni lazima uwe na riba maana mkopeshaji naye anatafuta faida.

Mjenzi kwa nini akubali kutujengea barabara halafu alipwe taratibu?
Mjenzi ni mfanyabiashara. Anatafuta faida. Hivyo nchi italazimika kumlipa mjenzi kwa kiwango ambacho mjenzi lazima apate faida.

Mjenzi atapataje faida?
Lazima atahakikisha nchi inalipa kufidia riba ya benki alikochujua pesa, plus faida ya kwake yeye mjenzi. Na tukichelewesha, tutalipa na penalty.

Kwa hiyo utaratibu huu wa EPC + F, utatufanya tujenge barabara zetu kwa gharama kubwa kuliko kipindi chochote kile. Kwa wasioupendelea utaratibu huu wangeweza kuuliza, kwa nini ukalipe riba kwa taasisi mbili, yaani kwa benki na mjenzi, wakati kuna uwezekano wa kukopa benki moja kwa moja, ukaokoa riba ambayo ungemlipa mjenzi?

Wakati Waziri Mbarawa akiusifia utaratibu huu kama vile amegundua sayari mpya, hakutoa mchanganuo wowote. Kwa mfano alitakiwa kusema:
1) kwa wakati huu ambao barabara zimekuwa zinajengwa kwa taratibu tofauti na EPC + F, kilometer 1 ya barabara ya lami, gharama ya ujenzi ni sh. ngapi?
2) Kwenye utaratibu huu wa EPC +F, kilometer 1 ya barabara ya lami, itagharimu kiasi gani?

Mkopo siyo pesa ya bure. Na wala huwezi kujisifia kuwa umegundua mbinu mpya ya kukopa. Mateso ya mkopo utayajua wakati wa ulipaji. Uganda wanalalamika sasa hivi, maana kwa mara ya kwanza mwaka huu wa fedha, karibia 40% ya bajeti yao yote itakuwa inagharamia kulipa madeni. Na sisi kwa sababu ni watu ambao uwezo wetu unaishia kushangilia na kupongeza, tunaelekea huko huko. Ifahamike tuna mikopo ya kugharamia miradi kama SGR, bwawa la Mwalimu Nyerere, daraja la Busisi, mikopo ya miaka mingi ya huko nyuma, sasa inakuja na hii ya EPC + F, na kutakuwa na mikopo kuziba pengo la bajeti kila mwaka. Hatuwezi kukwepa kukopa, lakini mwenye weledi anakopa kwa umakini, na siyo kurundika mikopo mingi kwa wakati mmoja kwa sababu tu amepatikana wa kukukopesha.

Nchi nyingi zinazotumia utaratibu wa EPC + F, zinatumia wakandarasi wa ndani. Kwao, hata kama barabara zitajengwa kwa gharama kubwa, mabenki yanayokuwa yamenufaika kutokana na riba ni ya nchini mwao. Wajenzi walionufaika kutokana na riba ni wa nchini mwao. Kwa hiyo hela inakuwa imetoka Serikalini imeenda kwa watu wao. Sisi hela itatoka Serikalini kwenda kwenye mabenki ya nje, pesa itatoka Serikalini kwenda kwa makampuni ya ujenzi ya nje.

Utawala wa Samia japo unajitahidi kwenye ujenzi wa miundombinu lakini tusizidishe sifa za uwongo. Siyo kweli kuwa utawala huu utajenga barabara nyingi kuliko tawala zote. Ukweli ni kwamba, hakuna utawala uliojenga kilometa nyingi za barabara za lami kuliko awamu ya 4. Zaidi ya 60% ya barabara zote ndefu za lami zimejengwa wakati wa awamu ya 4. Hakuna utawala uliojenga taasisi nyingi na kubwa mbalimbali kama vile viwanda, hospitali na vyuo, tena vyenye ubora wa hali ya juu, kama utawala wa Mwalimu Nyerere. Hakuna utawala ulioanzisha miradi mingi mikubwa kwa wakati mmoja, kama utawala wa Magufuli. Hakuna utawala uliojenga mifumo mizuri ya uchumi, na aliyeweza kushusha mfumko wa bei kutoka two digits mpaka single digit, kama Mkapa.

Mpaka sasa, hakuna kipya, hata kama kuna mambo mazuri yanafanyika.

Tupunguze sifa za hadaa, tufanye kazi. Nchi bado ni maskini, watu bado ni maskini. Katiba yetu na sheria zetu bado ni mbaya. Uadilifu ndani ya Serikali bado ni hafifu sana. Ubunifu, weledi na umakini ndani ya Serikali bado ni duni. Spidi ya miradi ya maendeleo na ongezeko la pato la Taifa ni ndogo kuliko ongezeko la watu.

Sifa nyingi tunazoipa serikali ni sifa bandia. Tunachotakiwa ni kuzidi kuisukuma serikali kuongeza speed zaidi ili iendane na ongezeko la mahitaji ya nchi.
Wivu baada kupigwa za uso.Unatumia EPC+F kama una pesa na akili,wajinga wajinga kama Wajamaa hawawezi kutumia..

Hiki ni kiwewe baada ya kuona legacy inaenda kufunikwa..

Mengine ni blaa blaa na ujinga wa kujifariji tuu.
 
Back
Top Bottom