Ephraim Kibonde Jahazi Show

Ephraim Kibonde Jahazi Show

Hao mafala wa clouds+THT lazima wajipendekeze kwa Mkwere kwani jamaa kawaonga recording studio which was meant to all Bongo flava artists kimya kimya hata BASATA hawakujua
 
Hivi Clouds hawafungwi na TCRA Policy, Hizi organ zinafanya kazi gani, ukisikiliza kipindi cha kibonde tangu wale wazoefu waondoke sijui wafukuzwe kibonde akaja in, ni porojo zisizo na maana, huwa najiuliza kwani Clouds haina wahariri, je wakurugenzi hawasikilizi upuuzi huu, na je TRCA na ICT/Broadicasting policy wanasemaje huu ya hili.

Si hilo tu usiku kunakipindi na matusi kwenda mbele, je ni leseni hii ya entertainment ndo inawapa kufanya mambo ya hovyo hovyo haya?

Je waziri wa ICT/Broadicasting hapewi hizi feedback je hata yeye hajawahi kusikiliza redio hii? Waziri wa wizara hii anahitaji aamke...
 
huyu jamaa nilikuwa namfagilia sana kipindi cha nyuma kabla ya uchaguzi, nowdays namchukulia kama mpuuzi kijingajinga fulani. nafikiri njaa imemfanya awe hovyo. kikubwa nilichomchukia kila kitu yeye anajua..
 
Maskini jamaa anasumbuliwa na njaa amekuwa akipewa u MC kwenye sherehe za CCM apate chochote na tule tusuti twake twa kijani,tumshauri achague moja siasa au Utangazaji
 
that kibonde is a big disgeace, not worthy to be discussed as a sane being.
 
I am not a hater but yesterday i hated this person to the most!! Mungu anisamehe tu kwani baadaye ilinilazimu kuswali kuondoa hiyo hatredness but naamini nastahili pia kumshauri huyu ndugu.

Kama unapita hapa Ephraim ... ningekushauri sana uwe makini na propaganda zako zisizo na mashiko ... unajipunguzia credibility kwa jamii katika mambo hata yasiyokuhusu ... ina maana wananchi, wanasheria, wanataaluma wote wanaozungumzia uchungu wao juu ya malipo ya dowans ni wehu!!??

Upuuzi ulioongea jana ni wakijinga sana kwa maslahi ya taifa hili ... wanachi wangapi wanataabika kijijini sababu ya matumizi mabaya ya rasilimali zetu?? acha upuuzi ndugu yangu ... sifia vitu vyenye mantiki na huna haja ya kujigeuza kuwa "enemy of the people"! kama ni njaa then do it in a brave way ... kujua sana kutakugharimu uhusiano wako na jamii! watu walikuponda sana a couple of weeks back for your unbalanced arguments, ukajaribu kuficha pumba zako for few days now unarudi kule kule; naamini u can do better than that man ... go out there and do it in a more balanced way ... for sure u'll be praized!! ni ushauri tu!!
 
Ushauri wa bure kwa huyo Kibondeee- ajaribu kufikiri kabla ya kuzungumza na kama ana dini ajue ulimi ni mbaya kuliko upanga ukatao kuwili. Jaribu kwenda kwenye masomo ya juu kidogo uweze kufanya "intelligent analysis" ya hoja mbalimbali zinazotolewa jamvini. Sana sana unajidhihirisha u mtu wa namna gani. JIREKEBISHE.
 
ni kawaida ya malimbukeni wote wanapopata wasichotarajia
 
It is very strange how fast people forget their misery!

Huyu jamaa niliwahi kumkuta pale DTP Mikocheni opp na TMJ hosp; (kile kipindi alichokuwa hasikiki..........sijui nini kilimkuta )

He was in pathetic state....you could hardly hear him talking, so humble na nilimface nikaongea, he seemed to be a gentleman A REAL ONE so to speak!

Lakini ayafanyayo hivi sasa ni kama anajaribu kuikimbia ile hali kila siku akihofu isimkaribie tena! ndg yangu Kibonde............haya yote maisha tu; wajibu unao kwa jamii unayoitumikia maana ni kipawa ulichopewa na Mungu...........sasa ole wako! UTAMJIBUJE ALIYEKUPA KIPAWA HICHO?
 
Si Mpenzi wa kusikiliza kipindi chake cha JAHAZI lakini mara nyingi sana nimebahatika kumsikia Jamaa huyu akiropoka sana, kusema ukweli nilimheshimu sana Kibonde lakini kwa sasa namuona hana maana tena kwa sababu zifuatazo;

Anashabikia mambo yenye ukweli usiopingika, mfano swala la DOWANS ambalo jana alilizungumzia kwa mbwembwe sana, asijue kuwa anazidi kuharibuhali ya hewa, alidai kuwa nchi haiwezi kukosa usingizi kwa sababu ya mtu mmoja anaetaka madaraka kwa nguvu na kwamba kama ni suala la lkutaka kupigiwa kura basi asubiri 2015; sina tatizo na maoni yake kwa hili,, ugomvi wangu ni yeye kujifanya kuwa ndo mwakilishi wa Watanzania wote, aliongea kwa kebehi kubwa sana, je na sisi tutafute au tutumie nafasi zetu kumkebehi?

Pili, Kusisitiza kwake kuwa ni sahihi DOWANS kulipwa na kama kuna anaebisha basi akae kimya, nimemuona ni mtu asie busara kuliko hata mvuta bangi (samahani kama nimekosea)

Tatu, kutaka viongozi wa dini eti wasiingiliea mambo ya nchi ni ujinga kama wanasiasa; na hapa na mimi namuomba kuwa kama yeye si mwana siasa basi aachane na mambo ya siasa la sivyo aondoke kwenye utangazaji aje kwenye siasa.

La mwisho, nawaombeni sana, lugha ya kuwakebehi wengine na kuwaona hawana maana airekebishe upesi; akumbuke alivyokuwa anamponda Mr.Two, lakini yuko wapi sasa, mwenzie ni mbunge na bado yeye ni watch dog tena mropokaji mtaani anaetafuta umaarufu kwa madereva wa daladala na makondakta.

Na kama vipi basi arudi akaendelee na matangazo yake ya Zain yasiyo na impact yoyote.

Narudi tena baadae
 
kama unaoga mtoni na kaja chizi akabenga nguo zako na wewe ukaanza kumkimbiza mpaka mjini basi wewe ndio utaoneka chizi kuliko chizi mwenyewe
Huyu bwana keshajadiliwa sana humu na anaonekana ana upungufu wa Akili wa kujitakia, hivyo na watu tukiendela kumjadili humu basi tutaonekana sisi ni wehu kuliko huyo,
Hana Hadhi ya Kujadiliwa tena humu JF
 
Back
Top Bottom