Ephraim Mrema na Ufisadi TANROADS

Ephraim Mrema na Ufisadi TANROADS

"Serikali yetu ipo makini kwa faida ya wananchi wa Tanzania, hizi ni porojo za wapinzani ambao hawana sera" ( Infact ndege yetu ipo right on track). Kufika 20.. unaweza kutoka na taxi toka mtwara mpaka Biharamulo.
Hizi ndizo sera dhabiti za Chukua Chako Mapema
 
Serikali ilishauriwa imfukuze Mrema kazi kwa sababu zifuatazo

1.Incompetence
2.Kutokana na hilo hapo juu anaiingizia hasara serikali kwenye miradi mingi

Narudia tena.........Mrema aondolewe............kwani toka aingie ameipa hasara kubwa serikali na anaendelea kuipa hasara..........na nilishasema yeye hana tofauti na akina Mramba, Yona na Mgonja.........

It is so sad ile barabara ya kagoma mpaka Lusahunga haijaisha.........poor wananchi wa Muleba na Biharamulo..........
 
Serikali yenu ni sikivu imesikia kilio chenu, naamini litafanyiwa kazi.
 
Ogah,

..kwani huko Tanroads tender zinakuwa awarded kwa uamuzi wa CEO peke yake?

..wakati CEO ni raia wa Ghana utendaji Tanroads ulikuwaje?

..je, huyu mkandarasi alikuwa anaharibu kazi kweli au alikuwa victimized tu?

NB:

..je, CEO wa Tanroads na wasaidizi wake wanapaswa kushtakiwa kwa mashtaka kama yale ya kina Mramba,Yona,na Mgonja?
 
System nzima ya tenda ni mbovu. Makandarasi wazuri wote wamekimbia nchi maana tunachokazania sisi ni bei nafuu na si ubora au ufanisi. Hapo ndipo hizi kampuni za makomredi wenzetu wanapenyea. Tunachosahau ni kuwa ku-terminate contract ni aghali sana ndio maana tunahitaji uangalifu mkubwa KABLA ya kuingia mkataba. Si uwezo wa mkandarasi tu ndio unaotakiwa kuangaliwa bali hata hizo tenda documents zenyewe kuhakikisha kuwa kilichokuwemo ndicho tunachokitaka. Tunakimbilia kusaini mikataba kutokana na ahadi tulizotoa za kisiasa. Tunakimbilia kuvunja mikataba kwa sababu tunadhani kwa kufanya hivyo ndio tutaonekana ngangari na kujizolea sifa za utendaji makini. Itabidi tubadilike kama tunataka maendeleo ya dhati.

Amandla....
 
Fundi Mchundo said:
Makandarasi wazuri wote wamekimbia nchi maana tunachokazania sisi ni bei nafuu na si ubora au ufanisi.

Fundi Mchundo,

..unataka kukumbushia enzi za kina Mowlem,Wade Adams,D B Shapriya,Birdi Constr...?

..kama sikosei Wade Adams waliondoka na ile kashfa ya Meridian Biao Bank.

..hii kampuni ya Kichina nadhani imeshakuwa na matatizo ktk contract zao nyingine.

NB:

..hivi Kajima bado wako nchini?

..Konoike nao walipokuja Tanzania walianza na mradi wa irrigation.
 
Ogah,

..kwani huko Tanroads tender zinakuwa awarded kwa uamuzi wa CEO peke yake?

Ideally NO, I wish ungekuwa unajua authority aliyonayo CEO wa TANROADS na maamuzi anayoweza kuyafanya

..wakati CEO ni raia wa Ghana utendaji Tanroads ulikuwaje?

naweza kusema, sikupata kusikia upuuzi kama unaoendelea hivi sasa, na muda mrefu yule Mghana alikuwepo kipindi cha akina Mh.Magufuli na Mar Mujungi............. non nonsense guys

..je, huyu mkandarasi alikuwa anaharibu kazi kweli au alikuwa victimized tu??
really can't say.........terminating a contract of such magnitude.........inaacha maswali meengi sana, mara zote contractor atakuwa victim kama akiharibu kazi.......
tatizo ni je TANROADS walifuata taratibu za kuterminate contract? inavyoelekea hawakufanya hivyo...........kwa sababu kama TANROADS walikuwa sahihi...........Contractor ange end up paying the Government instead........

NB:

..je, CEO wa Tanroads na wasaidizi wake wanapaswa kushtakiwa kwa mashtaka kama yale ya kina Mramba,Yona,na Mgonja?

Mramba, Yona na Mgonja wanashatakiwa kwa matumizi mabaya ya ofisi kutokana na kutofuata ushauri wa kitaalamu.....and this has been the case Mrema kwenye Miradi Mingi tu, toka alivyoingia TANROADS..........demand za 10% zake zinatutokea puani wananchi............trust me there will be more to come...........

This Dude has to go.....damn
 
WAKATI KUKIWA NA MALALAMIKO LUKUKI KUHUSU HALI MBAYA YA MIUNDO MBINU YA BARABARA NCHINI VIGOGO WA WAKALA WA BARABARA TANROADS PAMOJA NA WAKUU WA WIZARANI WAMEMUWA KUPEANA PESA ZA KUPONGEZANA KUPITIA UTARATIBU WA HONORARIA....
MIONGONI MWA MALIPO HAYO NI SH MILLION 40 ZILIZOLIPWA DECEMBER 23 MWAKA JANA KWA VIONGOZI 6 NA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MIUNDO MBINU....MALIPO HAYO YALIFANYIKA KWA BARUA KUMB trd/hq/a/c/03/01 ya dec 17....mgao wa awali unaonyesha KATIBU MKUU WA MIUNDO MBINU BW OMAR CHAMBO ALIPWE SH MILLION 8(8,000,000) LAKINI IKAFANYIWA MAREKEBISHO NA AFISA MTENDAJI MKUU ALIPOIPITISHA DEC 18 AMBAPO ALIMUIDHINISHA MILLION KUMI(10,000,000) BADALA YA NANE....AFISA MMOJA ALIPOULIZWA UMUHIMU WA KUGAIANA PESA HIZO ALISEMA NI AHASANTE KWA WALIOFANIKISHA KUONGEZEKA KWA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI WA TANROADS NA HELA HIZO ZILIIDHINISHWA NA BODI NA MANAGEMENTE....LAAAHAULA...WENGINE KATIKA MGAO HONARIA ALIIDHINISHWA KULIPWA MILION SITA NA AFISA MTENDAJI NI KAMA IFUATAVYO...

1))J.M.E MWAKITOSI

2) LOYCE LUGOYE

3))AGNESS MEENA

4)N.J.KIPANDA

5)PETER MHIMBA


HAWA NDIO MAFISADI HALISI WANAOITAFUNA KAMPUNI YA TANROADS WAKISHIRIKIANA NA KATIBU WA MIUNDO MBINU BW OMY CHAMBO....KAZI KWELI KWELI SASA KIKWETE UTAREKEBISHA WIZARA IPI MBONA ZOTE ZINANUKA UFISADI MTUPU......MMMMHHHKWENU WANANCHI

SRCE

MWANAHALISI NEWSPAPER
 
Vigogo TANROADS wajigawia 'vijisenti'

Mwandishi Wetu Julai 29, 2009


Kigogo wizarani ashirikishwa

WAKATI kukiwa na malalamiko lukuki kuhusu hali mbaya ya miundombinu ya barabara nchini, vigogo katika Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) pamoja na Wizarani wanapongezana kwa kupeana mamilioni ya fedha kupitia utaratibu wa honoraria.

Miongoni mwa malipo ya aina hiyo ni shilingi milioni 40 zilizolipwa Desemba 23, mwaka jana kwa vigogo sita baada ya kuidhinishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS nchini, Ephraem Mrema.

Malipo hayo yalifanyika kufuatia barua kumbukumbu namba trd/hq/a/c/03/1 ya Desemba 17, 2008 ya Kaimu Afisa Utawala, ambaye hata hivyo hakuonyesha jina lake, kwenda kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS.

Katika barua hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari, Honoraria, Kaimu Afisa Utawala huyo (Ag HRA) anatoa sababu za pendekezo lake la kupatiwa vigogo hao honoraria hiyo kuwa ni kutokana na mchango wao mkubwa walioutoa hadi kufanikisha nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa TANROADS.

Mgawo wa awali wa honoraria hiyo unaonyesha kuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo alipwe shilingi milioni nane lakini ikafanyiwa marekebisho na Afisa Mtendaji Mkuu alipoipitisha Desemba 18, 2008 ambapo alimuidhinishia shilingi milioni 10.

Wengine katika mgawo huo wa honoraria ambao kila mmoja aliidhinishiwa kulipwa shilingi milioni sita na Afisa Mtendaji huyo wameorodheshwa kama ifuatavyo J.M.E Mwakitosi (Kaimu DAP wakati huo), Loyce Lugoye, Agnes Meena, N. J. Kipanda na Peter Mhimba
 
na barua hiyo, malipo kwa vigogo hao yanaonekana kwenye hati za malipo (nakala zote tunazo) kwa kila mmoja zilizoidhinishwa Desemba 23, 2008 na mtu mwenye jina la Malamla .H. na wadhifa unaoonyeshwa kwa kifupi tu kama HFCA.

Mhuri wa malipo unaonyesha kuwa yalifanyika kwa hudi ambapo Chambo alilipwa kupitia hundi namba 595259, Mwakitosi namba 595260, Lugoye hundi namba 595261, Mhimba namba 595263, Kipanda na Meena 595266.
 
JK unayasikia haya ? Ama bado uko ziarani kujitambulisha ? Watanzania wanakufa watu wako wana pongezana .
 
WAKATI KUKIWA NA MALALAMIKO LUKUKI KUHUSU HALI MBAYA YA MIUNDO MBINU YA BARABARA NCHINI VIGOGO WA WAKALA WA BARABARA TANROADS PAMOJA NA WAKUU WA WIZARANI WAMEMUWA KUPEANA PESA ZA KUPONGEZANA KUPITIA UTARATIBU WA HONORARIA....
MIONGONI MWA MALIPO HAYO NI SH MILLION 40 ZILIZOLIPWA DECEMBER 23 MWAKA JANA KWA VIONGOZI 6 NA KATIBU MKUU WA WIZARA YA MIUNDO MBINU....MALIPO HAYO YALIFANYIKA KWA BARUA KUMB trd/hq/a/c/03/01 ya dec 17....mgao wa awali unaonyesha KATIBU MKUU WA MIUNDO MBINU BW OMAR CHAMBO ALIPWE SH MILLION 8(8,000,000) LAKINI IKAFANYIWA MAREKEBISHO NA AFISA MTENDAJI MKUU ALIPOIPITISHA DEC 18 AMBAPO ALIMUIDHINISHA MILLION KUMI(10,000,000) BADALA YA NANE....AFISA MMOJA ALIPOULIZWA UMUHIMU WA KUGAIANA PESA HIZO ALISEMA NI AHASANTE KWA WALIOFANIKISHA KUONGEZEKA KWA MISHAHARA YA WAFANYAKAZI WA TANROADS NA HELA HIZO ZILIIDHINISHWA NA BODI NA MANAGEMENTE....LAAAHAULA...WENGINE KATIKA MGAO HONARIA ALIIDHINISHWA KULIPWA MILION SITA NA AFISA MTENDAJI NI KAMA IFUATAVYO...

1))J.M.E MWAKITOSI

2) LOYCE LUGOYE

3))AGNESS MEENA

4)N.J.KIPANDA

5)PETER MHIMBA


HAWA NDIO MAFISADI HALISI WANAOITAFUNA KAMPUNI YA TANROADS WAKISHIRIKIANA NA KATIBU WA MIUNDO MBINU BW OMY CHAMBO....KAZI KWELI KWELI SASA KIKWETE UTAREKEBISHA WIZARA IPI MBONA ZOTE ZINANUKA UFISADI MTUPU......MMMMHHHKWENU WANANCHI

SRCE

MWANAHALISI NEWSPAPER

MwanaHalisi la lini? nadhani ni Raia Mwema
Vigogo TANROADS wajigawia 'vijisenti'

Lakini pia jamani hivi mara tumesahau mabilioni ya Kagoda tunaanza kuangalia milioni 8?
 
Tuwatumie viongozi ile picha ya watoto wanaosoma ile shule ya mbavu za mbwa waweke kwenye maofisini mwao labda wanaweza kuona aibu kidogo kabla hawajachota mihela.
 
Mmmmmmmmh wakuu hii imekaa vibaya inastahili kukemewa na wahusika wakawajibishwa sanjari na kurudisha hizo pesa za umma. Mkuu hii naona irushe magazetini iwafikie wahusika kirahisi
 
Duh, Hata viongozi wa serikali wanachukua Bonus!... hii mpya, wakati fedha za ujenzi wa barabara hizo ni mikopo ambayo haijarudishwa wala haitajenga faida in terms of Net Profit..Ama kweli Ubepari umekuja na mengi..
 
Waacheni wahandisi wale nchi, hivi wale waliokwiba mabilioni mboni mpo nao hadi bungeni na hamuwafanyi chochote? Yaani watu kula honoraria ya ka-tumiloni 40 tu imekuwa nongwa?

Hivi mnajua TANROADS inafanyaje kazi kimuundo na kimaslahi inatakiwa wajiendesheje au mnabwata ? TANROADS ni agency period. Kama hamjui jambo ni vyema mkauliza kwanza.
 
Mbona haya ni sehemu ya mafao madogo tuu yameandikwa? Kuna mtu aliniambia huyo Mr shotii ... aka..CHAMBO ambaye ni swahiba wake na JK waongea lugha moja ni KICHECHE wa fedha za wizara ya Miundombuni! yaani kwa sasa ana utajiri sambamba na aliyekuwa bosi wake Mzee wa Vijisenti? si mwakumbuka ndiye anahusika pia na Mradi wa KIWIRA?

Yote tisa, kumi ameikalia Wizara hata Waziri wake KAWAMBWA hafurukuti. Yeye na baadhi ya Maswahiba wake wa TANROADS :...Chief, wasaidizi wa Chief wamenenepeana matumbo utafikiri wajawazito ilhali wananchi wanalia barabara mbovu!
 
Vigogo TANROADS wajigawia 'vijisenti'

Mwandishi Wetu Julai 29, 2009


Kigogo wizarani ashirikishwa

WAKATI kukiwa na malalamiko lukuki kuhusu hali mbaya ya miundombinu ya barabara nchini, vigogo katika Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) pamoja na Wizarani wanapongezana kwa kupeana mamilioni ya fedha kupitia utaratibu wa honoraria.

Miongoni mwa malipo ya aina hiyo ni shilingi milioni 40 zilizolipwa Desemba 23, mwaka jana kwa vigogo sita baada ya kuidhinishwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS nchini, Ephraem Mrema.

Malipo hayo yalifanyika kufuatia barua kumbukumbu namba trd/hq/a/c/03/1 ya Desemba 17, 2008 ya Kaimu Afisa Utawala, ambaye hata hivyo hakuonyesha jina lake, kwenda kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TANROADS.

Katika barua hiyo iliyokuwa na kichwa cha habari, Honoraria, Kaimu Afisa Utawala huyo (Ag HRA) anatoa sababu za pendekezo lake la kupatiwa vigogo hao honoraria hiyo kuwa ni kutokana na mchango wao mkubwa walioutoa hadi kufanikisha nyongeza ya mishahara kwa wafanyakazi wa TANROADS.

Mgawo wa awali wa honoraria hiyo unaonyesha kuelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Miundombinu, Omar Chambo alipwe shilingi milioni nane lakini ikafanyiwa marekebisho na Afisa Mtendaji Mkuu alipoipitisha Desemba 18, 2008 ambapo alimuidhinishia shilingi milioni 10.

Wengine katika mgawo huo wa honoraria ambao kila mmoja aliidhinishiwa kulipwa shilingi milioni sita na Afisa Mtendaji huyo wameorodheshwa kama ifuatavyo J.M.E Mwakitosi (Kaimu DAP wakati huo), Loyce Lugoye, Agnes Meena, N. J. Kipanda na Peter Mhimba


THANKS MM kwa kuweka habari yenyewe kama ilivyo kwenye Raia Mwema ya jana na si mwanahalisi kama ilivyokuwa posted awali.

Pamoja na kiwango kuonekana kuwa kidogo ikilinganishwa na vijisenti vya kina kagoda na meremeta, bado ni wizi wa fedha za watanzania masikini.

Ni milioni 40 ngapi zinatolewa kwa mtindo wa aina hiyo! Huu ni ushahidi kwamba viongozi wetu ni wamepindukia kwa ubinafsi, na hata ukichunguza hiyo mishahara utabaini kwamba wenye nyongeza ya maana ni wakubwa na sio wafanyakazi wa chini, kama ilivyo katika tofauti ya vipato vya majaji na watumishi wao wa chini.

Hali hii isiporekebishwa siku moja nchi nzima itaingia kwenye mapigano ya raia na askari kama ilivyokuwa Kyela.
 
Back
Top Bottom