Ephraim Mrema na Ufisadi TANROADS

Ephraim Mrema na Ufisadi TANROADS

Waacheni wahandisi wale nchi, hivi wale waliokwiba mabilioni mboni mpo nao hadi bungeni na hamuwafanyi chochote? Yaani watu kula honoraria ya ka-tumiloni 40 tu imekuwa nongwa?

Hivi mnajua TANROADS inafanyaje kazi kimuundo na kimaslahi inatakiwa wajiendesheje au mnabwata ? TANROADS ni agency period. Kama hamjui jambo ni vyema mkauliza kwanza.

Hebu eleza maana hasa ya agency?, maana naona umelipuka na taarifa nusu nusu. Mimi ninavyojua kuna "Government agencies", sasa hizi zinaweza kuwa "quangos" - quasi-non government organizations ambazo zina semi-autonomy lakini zinategemea most of their resources from public (hapa naamanisha pesa za walipa kodi, au kwa bongo tunasema wanapewa pesa toka hazina), Kwa kuwa TANROADS ni agency iliyo chini ya serikali, ni dhahiri kabisa kuwa pesa walizogawana zimetoka hazina na ndiyo maana wamempa hata katibu mkuu wa wizara Shs 10m kama ahsante ya kuidhinisha malipo hayo.

Huu ni ufisadi tosha, hasa ukizingatia barabara nyingi hazipitiki na nyingine hata maintenance hazifanyiwi kama hazina mwenyewe vile. Wizi ni wizi tu uwe wa kuku au ng'ombe. Wewe unayesema watu wameiba mabilioni tunawaacha wakati wengine wanaiba tu-milioni 40 tunawakomalia unatakiwa kujua kuwa baya kubwa halihalalishi baya dogo kuwa zuri. Watu kama hawa wasiojali resources walizopewa kuzilinda hawastahili kuendelea na nafasi hizi, kwani wakipewa nyingi wataiba zaidi.

hebu fikiria hizo Shs 40m zingetumika kutengeneza madimbwi yalipo barabarani hata kama ni mita 20 watu wangapi wangepata ajira?. Hatukatai kupongezana kupo makazini ila si kwa style hii ya bonus za kurudisha nyuma maendeleo. Unakumbuka Maghufuli alipokuwa wizara ya miundombinu alivyokuwa anawapasha hawa TANROADS, wanalipana mishahara mikubwa bila kuwa na tija. Huu ni wizi wa pesa za walipa kodi na ingekuwa kwa wenzetu wangezirudisha zote kwa wenyewe wananchi.
 
jamaa pale TANROADS kazi anayo ...maana aliwatinua wote akaweka matangazo gazetini ya nafasi za kazi lakini by the look of things inabidi anipe contract ya kusort out mambo pale

Tatizo lake ni kuwa wanamdharau sasa he needs to stamp his authority
 
tutendelea kula nyasi wana JF, kwani bado tunaongea sana na kutoa majibu rahisi kwa maswali magumu. Tatizo lipo katika kuwajibishana, tusisahau kuwa TANROAD ni agence ya serikali, na serikali haina mkono wake moja kwa moja kiuwajibishanaji, so kazi ipo kweli. INANIUMA SANA, NIKIFIKIRIA, HUWAGA NINALIA,INANIUMA SANA UFISADI HUU....................................
 
Unajua kama vile kama vile zile skendo za EPA..wengine wana EPA ndogo ndogo na wengine epa zao ni kubwa kubwa

Of course hii ni kama asymetrical war...tunapiga vita UFISADI wa SPIKA SAMUEL SITTA, wengine wamelekeza makombora MEREMETA, wengine WIZARA YA ARDHI na wengine wamelekeza TRA na bila kusahau BANDARI YETU YA DAR

Lakini hii ya TANROADS inatisha maana yule bosi pale (bwana MREMA) nakumbuka mwanzoni mwa mwaka alitumia almost menejimenti yake nzima kisha akaweka matangazo ya nafasi za kazi kwenye daily news...zilikuwa kurasa 3 mfululizo sasa leo nashangaa kuona haya:

anywa najua si kila mtu ana interest ya kusoma article nzima lakini dondoo ni hivi:


-Cost za kutengeneza kilomita moja ya barabara ya lami acording to TANROADS zimeruka na kufikia 1.9 billion yaani 1.46million dollars.


-Wakati huo huo cost of construction of one kilometre of tarmac road in countries like Kenya and Zambia ranges from $500,000 to $600,000.
pale BANDARINI

Bwana Mporogomyi aliomba apewe ufafanuzi mwaka jana akaambiwa subiri na sasa mwaka mzima ushapita nahakuna aliyeweka ufafanuzi kuhusu hizi gharama si KAWAMBWA na WIZARA yake wala si TANROADS wenyewe...sasa cha kujiuliza hapa whats so difficult kwenye hili? si kiasi cha kwenda kwenye huo michanganua yao kwenye computer na kuweka wazi kwa nini tunatumia 1.5 million dollars kunjenga barabara ya lami wakati wenzetu wanatumia dola laki 5 tuu?

Unajua hawa watu saa zingine ovyo sana na wenyewe wana invite flies un necessarily kwa sababu wangekuwa o[pen haya yote yasingetokea

Anyway...

Hapa kuna taarifa kuwa hata huyo mrema Mwenyewe analipwa mapesa mengi bila sababu na ilihali HANA hizo qualifications za kufanya kazi hiyo na mbaya zaidi hakuwepo kwenye short list of eligible candidates!!

Mbaya zaidi wakati bara bara zetu hazipitiki lakini Ephraim Mrema analipwa marupu rupu kuliko hata ma EXPATRIATES wanaofanyakazi Tanzania!


Ohh kwa msio jua ni kuwa bwana Mrema anachukua pesa zifuatazo:

BASI SALARY KWA MWEZI: $8,500

HOUSE ALLOWANCE KWA MWEZI: $2,200

PENSION KWA MWEZI: $850

TRAVEL ALLOWANCE: $500

MEDICAL COVER KWA MWEZI: $400

ANNUAL PERFORMANCE BONUSES $102,000

ANNUAL LEAVE PAYMENT $3,000

GOLDEN HANDSHAKE AKIMALIZA CONTRACT: $10,000

COMMENCEMENT au START UP ALLOWANCE: $ 9,000



By the way Ma ENGINEERS ambao waliachwa na kuchukuliwa unqualifies Mrema ni akina BONIFACE NYITI,VENANCE NDYAKUMANA na mtu mwingine kwa jina la CHACHA na icing on the cake ni kuwa bwana Mrema ana BSc in Construction Economics and MSc in Project Management na kabla ya hapo alikuwa procurement consultant kule Unguja

Na si hivyo tuuu kumbe ile fukuza na kuweka matangazo ya kazi kwenye kurasa tatu za DAILY NEWS ilikuwa ni kuondoa kiwingi cha watu aliokuwa akiwaona maadui zake na kwa kukata mzizi wa fitna aliamua kibabe babe kuanzisha ONE YEAR CONTRACTS!!!

UFISADI wa Bwana Mrema no pamoja na yeye binafsi kuwa mstari wa mbewe kweneye ma dili ya rushwa kama vile kumngoa ofisa pale kwenye mizani Kibaha baada ya yule afisa kuimpound ma truck yaliyozodi tani 70

anyway zaidi muulizeni huyo bwana Kilonsi Mporogmyi kwa mnaotaka mijidataz zaidi


http://www.ippmedia.com/
 
Unajua kama vile kama vile zile skendo za EPA..wengine wana EPA ndogo ndogo na wengine epa zao ni kubwa kubwa

Of course hii ni kama asymetrical war...tunapiga vita UFISADI wa SPIKA SAMUEL SITTA, wengine wamelekeza makombora MEREMETA, wengine WIZARA YA ARDHI na wengine wamelekeza TRA na bila kusahau BANDARI YETU YA DAR


hahaha...bongo kila mtu inabidi akomalie eneo lake la ufisadi. Umekuwa mchezo wa paka na panya sasa.
 
Unajua kama vile kama vile zile skendo za EPA..wengine wana EPA ndogo ndogo na wengine epa zao ni kubwa kubwa

Of course hii ni kama asymetrical war...tunapiga vita UFISADI wa SPIKA SAMUEL SITTA, wengine wamelekeza makombora MEREMETA, wengine WIZARA YA ARDHI na wengine wamelekeza TRA na bila kusahau BANDARI YETU YA DAR

Lakini hii ya TANROADS inatisha maana yule bosi pale (bwana MREMA) nakumbuka mwanzoni mwa mwaka alitumia almost menejimenti yake nzima kisha akaweka matangazo ya nafasi za kazi kwenye daily news...zilikuwa kurasa 3 mfululizo sasa leo nashangaa kuona haya:

anywa najua si kila mtu ana interest ya kusoma article nzima lakini dondoo ni hivi:


-Cost za kutengeneza kilomita moja ya barabara ya lami acording to TANROADS zimeruka na kufikia 1.9 billion yaani 1.46million dollars.


-Wakati huo huo cost of construction of one kilometre of tarmac road in countries like Kenya and Zambia ranges from $500,000 to $600,000.
pale BANDARINI

Bwana Mporogomyi aliomba apewe ufafanuzi mwaka jana akaambiwa subiri na sasa mwaka mzima ushapita nahakuna aliyeweka ufafanuzi kuhusu hizi gharama si KAWAMBWA na WIZARA yake wala si TANROADS wenyewe...sasa cha kujiuliza hapa whats so difficult kwenye hili? si kiasi cha kwenda kwenye huo michanganua yao kwenye computer na kuweka wazi kwa nini tunatumia 1.5 million dollars kunjenga barabara ya lami wakati wenzetu wanatumia dola laki 5 tuu?

Unajua hawa watu saa zingine ovyo sana na wenyewe wana invite flies un necessarily kwa sababu wangekuwa o[pen haya yote yasingetokea

Anyway...

Hapa kuna taarifa kuwa hata huyo mrema Mwenyewe analipwa mapesa mengi bila sababu na ilihali HANA hizo qualifications za kufanya kazi hiyo na mbaya zaidi hakuwepo kwenye short list of eligible candidates!!

Mbaya zaidi wakati bara bara zetu hazipitiki lakini Ephraim Mrema analipwa marupu rupu kuliko hata ma EXPATRIATES wanaofanyakazi Tanzania!


Ohh kwa msio jua ni kuwa bwana Mrema anachukua pesa zifuatazo:

BASI SALARY KWA MWEZI: $8,500

HOUSE ALLOWANCE KWA MWEZI: $2,200

PENSION KWA MWEZI: $850

TRAVEL ALLOWANCE: $500

MEDICAL COVER KWA MWEZI: $400

ANNUAL PERFORMANCE BONUSES $102,000

ANNUAL LEAVE PAYMENT $3,000

GOLDEN HANDSHAKE AKIMALIZA CONTRACT: $10,000

COMMENCEMENT au START UP ALLOWANCE: $ 9,000



By the way Ma ENGINEERS ambao waliachwa na kuchukuliwa unqualifies Mrema ni akina BONIFACE NYITI,VENANCE NDYAKUMANA na mtu mwingine kwa jina la CHACHA na icing on the cake ni kuwa bwana Mrema ana BSc in Construction Economics and MSc in Project Management na kabla ya hapo alikuwa procurement consultant kule Unguja

Na si hivyo tuuu kumbe ile fukuza na kuweka matangazo ya kazi kwenye kurasa tatu za DAILY NEWS ilikuwa ni kuondoa kiwingi cha watu aliokuwa akiwaona maadui zake na kwa kukata mzizi wa fitna aliamua kibabe babe kuanzisha ONE YEAR CONTRACTS!!!

UFISADI wa Bwana Mrema no pamoja na yeye binafsi kuwa mstari wa mbewe kweneye ma dili ya rushwa kama vile kumngoa ofisa pale kwenye mizani Kibaha baada ya yule afisa kuimpound ma truck yaliyozodi tani 70

anyway zaidi muulizeni huyo bwana Kilonsi Mporogmyi kwa mnaotaka mijidataz zaidi

http://www.ippmedia.com/
HII NI KIBOKO!hata la kusema sinalo
 
Hiyo annual perfomance bonuses imenilazimu nikaitafute miwani yangu ambayo nilishaanza kusahau kuitumia.Nway,its da same old bulsh!t on a new day...
 
Kuhusu hayo malipo Mrema hana kosa kwani hakujipangia mwenyewe, package ipo kwa yeyote atakayeshika nafasi hiyo. Swali ni kwanini nchi maskini inakuwa na mishahara na marupurupu ya kuua namna hiyo? duh! sina hamu na Tz.
 
Kuhusu hayo malipo Mrema hana kosa kwani hakujipangia mwenyewe, package ipo kwa yeyote atakayeshika nafasi hiyo. Swali ni kwanini nchi maskini inakuwa na mishahara na marupurupu ya kuua namna hiyo? duh! sina hamu na Tz.


Nziku hapo ndipo watu wanakosea; wanaangalia malipo ya Spika, Maximo, Mrema, mkuu wa TRA n.k na kusema kwanini tunaweza kuwalipa hawa hivi vyote wakati sisi ni maskini? - the answer is wao wanajua kuwa sisi si maskini!
 
Nziku hapo ndipo watu wanakosea; wanaangalia malipo ya Spika, Maximo, Mrema, mkuu wa TRA n.k na kusema kwanini tunaweza kuwalipa hawa hivi vyote wakati sisi ni maskini? - the answer is wao wanajua kuwa sisi si maskini!

kwi kwi kwi😱
 
Nakumbuka wakati anaajiriwa maswali yalikuwa hayahaya, sasa yanarudi tena nahisi haya ni majungu, Am ready to be proved wrong kwa kujibiwa maswali haya.

1.Mabosi wa tanroads waliotangulia walikuwa wanalipwaje? (Walikuwa wageni)
2.Vipi tuone mtanzania mwenzetu kulipwa vizuri ni kosa? Si sisi wote tuna hasira kwa sababu mishahara yetu haikidhi mahitaji yetu?
3.Majina ya waliotajwa ni kweli walikuwa wanaitaka nafasi, wangepata je mambo haya yangekuwepo?
4. Tupeni mapungufu yake katika utekelezaji ili tupime kama malipo yanalingana na deliverables zake au la.

Kama tutafikia mahali pa kumhukumu kila mmoja tukitokea kwenye kona ya maslahi binafsi, naamini hatutashinda vita hii ya mafisadi. Ni vizuri tusimame vyema katika haki na ukweli. ( HUU NI USHAURI WA BURE)
 
Nakumbuka wakati anaajiriwa maswali yalikuwa hayahaya, sasa yanarudi tena nahisi haya ni majungu, Am ready to be proved wrong kwa kujibiwa maswali haya.

1.Mabosi wa tanroads waliotangulia walikuwa wanalipwaje? (Walikuwa wageni)
2.Vipi tuone mtanzania mwenzetu kulipwa vizuri ni kosa? Si sisi wote tuna hasira kwa sababu mishahara yetu haikidhi mahitaji yetu?
3.Majina ya waliotajwa ni kweli walikuwa wanaitaka nafasi, wangepata je mambo haya yangekuwepo?
4. Tupeni mapungufu yake katika utekelezaji ili tupime kama malipo yanalingana na deliverables zake au la.

Kama tutafikia mahali pa kumhukumu kila mmoja tukitokea kwenye kona ya maslahi binafsi, naamini hatutashinda vita hii ya mafisadi. Ni vizuri tusimame vyema katika haki na ukweli. ( HUU NI USHAURI WA BURE)
Malipo kwa mtaalam mgeni tunayemhitaji na ambaye hatuna hapa kwetu na malipo kwa mtaalam mwananchi hayawezi kufanana, hasa kwa kua sisi bado masikini.
Malipo KWA MREMA ya USD102,000 ni batili hata kama anafanya kazi sawa sawa ama bora zaidi ya mgeni aliyekuwepo. Mgeni alilipwa hivyo kwa kua hatukua na namna. Utashangaa Mrema kasoma kwa scholarships za umma nk.
 
Malipo kwa mtaalam mgeni tunayemhitaji na ambaye hatuna hapa kwetu na malipo kwa mtaalam mwananchi hayawezi kufanana, hasa kwa kua sisi bado masikini.
Malipo KWA MREMA ya USD102,000 ni batili hata kama anafanya kazi sawa sawa ama bora zaidi ya mgeni aliyekuwepo. Mgeni alilipwa hivyo kwa kua hatukua na namna. Utashangaa Mrema kasoma kwa scholarships za umma nk.

Mgeni analipwa hivyo ni kwa sababu tunataka kumshawishi aje kufanya kazi katika mazingira tofauti na ya huko kwao. Na vile vile nchi za kwao huwa wanachangia. Bosi wa kwanza alitoka Norway na sehemu ya mafao yake yalichangiwa na wenyewe wa-Norway. Mghana tulimlipa hivyo kwa sababu lengo likikuwa ni kumpata mtu aliyebobea kimataifa. Mtu mwenye uzoefu katika mashirika ya kimataifa na mwenye uwezo wa kufanya kazi popote duniani. Kumpata mtu wa namna hiyo, malipo yalitakiwa kuwa competitive.

Sasa kwa sababu tumeamua kuchukua mmoja wetu, ningedhani kuwa tungeangalia zaidi uwezo wetu na hali ya nchi yetu. Hao wote tunaowalipa mishahara ya kufuru, tunafanya hivyo kwa kuwapunguzia wananchi wa kawaida. Kwa maoni yangu ni dhambi kumlipa mwenzetu mishahara ya namna hiyo wakati tunashindwa kumlipa mwalimu wa shule ya msingi mshahara ambao utamtosheleza kwa mahitaji yake basic ya maisha. Tunampa mtu bonasi ya dola 102000 wakati tunashindwa kuokoa maisha ya wakina mama lukuki wanapojifungua! Kufanya hivyo ni kukufuru na si kingine.

Amandla........
 
Bonus ya USD 102000 inatokea wapi?? au ndiyo haya mambo ya kuigaiga tu bila kuangalia uzalishaji na faida. Naona huu ndiyo mwanzo wa kufirisika wa Tanroad. May be hawajaali kwa vile wako quaranteed serikali itawachotea mabillion mwakani hata kama barabara haziishi kujengwa.
 
Annual bonus ya dola laki moja na alfu mbili? Please! Most likely ni typo hiyo, na kiasi sahihi ni dola 10,200

Inaelekea wewe uko nje ya Tanzania muda mrefu sana

possibly ado unafikiri Majambo bado yupo .....


ushaambiwa jamaa analipwa bonus ya kiasi hicho wewe hutaki sasa ukiambiwa utuletee ushahidi zaidi unaleta mambo ya most likely

Hivi unjua Mgawe pale Bandarini analipwa kiasi gani?
 
Back
Top Bottom