Five55
JF-Expert Member
- Jun 14, 2024
- 214
- 241
View attachment 3188723
Roho ya Marehemu ipate rehema kwa Mungu na ipumzike kwa amani -AMINA
Leo baada ya kupata taarifa za kifo cha aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya awamu ya nne (4) Mhe Jaji Werema,
Haraka nikamkumbuka aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kusini Mhe David Zacharia Kafulila namna walivyopambana Bungeni katika kashfa ya uchotaji wa pesa kwenye akaunti ya Tegeta Escrow zaidi TZS321 bilioni.
Sitaki kurejea sakati lile, Ila..
Kafulila pamoja na mapambano yale yote bahati mbaya Kafulila hakuwahi kutambuliwa popote Tanzania kama shujaa wa mapambano ya rushwa na ufisadi zaidi ya watu kupambana kuhakikisha harudi tena Bungeni kabla na baada ya 2015.
Kifo cha Jaji Werema na kusahaulika kabisa kwa David Kafulila kwenye medani za siasa za kupamba na rushwa na ufisadi ni ishara ya nchi yetu kuchukia wanaochukia rushwa na Ufisadi kwa moyo na nguvu zao zote.
Swali, Je, Leo hii hakuna akina Kafulila wengine Bungeni?
2030 kama maamuzi yangekuwa ni yangu basi David Kafulila ningemkabidhi Urais wa JMT mara baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kumaliza muda wake ili apambane na rushwa na Ufisadi ulioota madevu na masharubu.
Je, ni wangapi mnawaza kama Mimi kuhusu Urais na Kafulila?
Mungu ibariki Tanzania,
View: https://youtu.be/Qg5dWRyjVOE?si=ako4Bhu7IRztYfv_
Kafulila anafaa sana jamani
