Eti STAMICO wanauza Makaa ya Mawe tani moja kwa Tsh 60,000/= Mkataba huu Uvunjwe

Eti STAMICO wanauza Makaa ya Mawe tani moja kwa Tsh 60,000/= Mkataba huu Uvunjwe

Mawe ya huko ulikotaja yanafanana viwango na haya yakwetu? Lakini Tani 1 sio mengi mbona acha mama afungue nchi. Tim mwendazake mnawivu Sana nyie acheni mama aupige mwingi.
Ndio maana nimewaeleza hapo juu kwamba wangejua Makaa yako kila sehemu ila ni of poor quality Sana, huwezi linganisha na Botswana au South Africa..
 
Mawe ya huko ulikotaja yanafanana viwango na haya yakwetu? Lakini Tani 1 sio mengi mbona acha mama afungue nchi. Tim mwendazake mnawivu Sana nyie acheni mama aupige mwingi.

Aiseee hayo ni makaa ya mawe au mchanga?
 
Tusije kutumia gharama mara mbili kufukia mashimo, ohooo......
 
Kama kuna ukweli kwenye hili, inabidi hawa watu wanayofanya haya mambo wawe wanahukumiwa kupigwa "risasi" ama adhabu zinazofanania na hizo siamini kama mtu anaweza akaagree price chini ya ile ya soko la dunia.
 
Kama ni kweli kuna shida ila ulitakiwa uweke ushahidi wa hicho unachoongea cha kuuza madini Kwa bei hiyo..

Pili kule Ruvuma kuna kampuni ya mzawa ya Ruvuma Coal Mining Limited ndio imekuwa ikisafirisha Makaa ya Mawe kwa mda mrefu,swali Je wao ndio wanauziwa Kwa bei Hiyo na stamico au wao Wana mgodi wao kama wawekezaji wengine wa madini?

Mwisho kuna Hawa jamaa wa Hiyo sekta wanafai makaa yetu yako daraja ya mwisho ndio maana hayana soko la uhakika pengoline hii ndio Sababu kama kuna ukweli.
Elimu please, hivi density ya makaa ya mawe Ni ngapi say per cubic meter and a day on average, zinaweza kuchimbwa cubic meter ngapi
I think you can guess what I want to establish!
 
Taarifa haijakamilika naona imejaa mihemko.

Stamico na makaa ya mawe wapi na wapi?

Ingawa nahisi kwenye hii tenda walamba asali wamepiga parefi sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!
Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya
View attachment 2245667
Resource curse... Makaa ya mawe yanapaswa kubaki ardhini. Kuyachimba kwa matumizi ni kuchochea uharibifu!
 
Kuna kitu bado watu hawajaambiwa...
Kuna mdau aliniambia upanuzi wa bandari Mtwara ulikula zaidi ya Billion 300 ... Na asilimia kubwa ya pesa hiyo ilikuwa mkopo ( mikopo ya haraka haraka) ...japo kuwa tuliambiwa ni pesa yetu...

Kinachofanyika kuna service ya mkopo hapo... Kwakuwa muda wa kulipa umeanza....

Sijajua kama ni kweli tani moja imefika 60,000 ila kuna makato ya asilimia flani yanafanyika kuhudumia mkopo.. Sijajua kwa muda gani..
Ndio maana pia wanajaribu Dangote aitumie kusudi waweze kuserve mkopo kwa haraka..

Sijajua Bandari ya Tanga wanafanyaje.. Ila nahisi mkopo pia ulihusika pakubwa..
 
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!
Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya
View attachment 2245667
Chanzo Cha taarifa juu ya bei yetu kulinganisha na bei iliyopo solo la Dunia,ukizingatia mahitaji ni makubwa kufuatia mgogoro wa nishati uliopo hivi Sasa kutokana Na Nato kupanga kususia nishati kutoka urusi.
 
Mmmh jamii forum wajuzi wengi lakin Daaah..okay,apo inategemea terms wanazouzian CFR,CIF,FOB ,EX MINE etc..Actually Coal CIF china ni $120/MT..mm nafanya trading kama,hyo bei uliotaja ww mteja gani unaemjua amenunua nilitee na mm..Mzigo upo 20,000MT/monthly and price $37/MT ex mine($2/MT my commission)
 
Back
Top Bottom