Eti STAMICO wanauza Makaa ya Mawe tani moja kwa Tsh 60,000/= Mkataba huu Uvunjwe

Eti STAMICO wanauza Makaa ya Mawe tani moja kwa Tsh 60,000/= Mkataba huu Uvunjwe

Kama nikweli inasikitisha sana,tozo kibao halafu watu wanajichotea tu maliasili yetu
 
Nadhani mtoa mada hujui ihalisia wa hizo bei za makaa ya mawe, hapa kwetu hiyo ni bei ila kuna ushuru na gharama nyingine juu yake, japo sio kiivyo ila zinafika elfu 30 kwa tani moja.

Pia namna ya usafirishwaji inachangia sana, by the time makaa ya mawe yanafika iwe Mtwara kwa Dangote, Tanga Cement & Rhino Cement Tanga, etc bei ya makaa inakuwa ishapaa kutoa 1.8mil kwa semi moja, hadi 6.3mil kwa semi moja. Kuna gharama kubwa sana kwenye usafiri. Sasa 6.3mil tayari bei inakuwa ipo juu.
Inahitajika reli toka Mtwara hadi ziwa nyasa.
 
Mpaka hapa hajatokea mtaalamu kwenye hii sekta akatoa ufafanuzi. Kwa sie tusiojua kuhusu makaa ya mawe inawezekana tukaona ni kitu chenye thamani kubwa kumbe ni kitu cha kawaida kabisa. Na pia ikawa ni bidhaa inayopatikana kwa wingi duniani. Na uchimbaji wake ukawa sio wa gharama kubwa kama wengi tunavyo jaribu kufikiri.
Naamini kabisa kwenye hii mikataba kuna harufu ya upigaji lakini ukiangalia na bei za nchi nyingine tumezisiwa kwa nusu. (Kwa mujibu wa mleta mada)

Kumbe kina Mkapa RIP walipojimilikisha migodi ya kiwira walijimilikisha miradi ya kawaida kabisa. Lakini kelele zake kuuubwa.

Ningependa kuona mtaalamu kwenye hili eneo, aje atoe ufafanuzi. Sio wanasiasa na wale walamba viatu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] aiseee hichi nacho ni kituko cha mwaka yani tani moja kwa elfu sitini jamani hii nchi hii inabidi iwe na sheria ya kunyonga kabisa!

Hivi ndio kufungua nchi huku? Hakika inachekesha na kuhuzunisha kwa wakati mmoja! Tunajisifu kwa meli kubwa eti imetia nanga kumbe makaa ya mawe ni kama yanaondoka bure kabisa na no one cares aiseeeee

Ngoja ni lale tuuu
Dhambi kunyongana mkuu
 
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!

Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya.

View attachment 2245667
sasa kama yanauzwa bei ya kutupwa si ukayanunue ukauze huko dola 500 kwa tani, wavunje mkataba uyanunue wewe? watu wengine sijui waliugua degedege utotoni?
 
Tani moja ya makaa ya mawe kwa bei ya mifuko mitatu ya simenti! Huku kama siyo kulogwa ni nini?
 
Kama ni kweli kuna shida ila ulitakiwa uweke ushahidi wa hicho unachoongea cha kuuza madini Kwa bei hiyo..

Pili kule Ruvuma kuna kampuni ya mzawa ya Ruvuma Coal Mining Limited ndio imekuwa ikisafirisha Makaa ya Mawe kwa mda mrefu,swali Je wao ndio wanauziwa Kwa bei Hiyo na stamico au wao Wana mgodi wao kama wawekezaji wengine wa madini?

Mwisho kuna Hawa jamaa wa Hiyo sekta wanafai makaa yetu yako daraja ya mwisho ndio maana hayana soko la uhakika pengoline hii ndio Sababu kama kuna ukweli.
Uko sahihi,

Ushahidi wa bei upo wapi!?!
Je, ubora wa haya makaa ya mawe upoje!?!

Hata mkaa na kuni tu zinatofautiana bei kufuatana na aina ya mti,
Kuni za mpingo ni gharama kuliko kuni za mkaratusi,
Mkaa wa Mkorosho au Iringa. Ubora wake ni tofauti na mkaa wa miti pori!
 
Mkuu, swali kama hili siyo level yako, usijishushe kiasi hicho, please.
Bei hutegemea current market demand, haitegemei awamu ya 5 au 4 waliuza kiasi gani.
Tuna mawazo ya kisiasa Sana, very sad! Kuna vitu vipo nje ya uwezo wa wanasiasa na watawala,
Watu hatuelewi hata kuwa haya mambo yanaendana kufuatana na soko la dunia.
Nafikiri watu tuelimishwe, tokea primary, soko

Mfano, kwanini vitunguu nyanya bei hupanda na kushuka.
Kwamba waweza kufika sokoni ukakuta Kkoo nzima zipo fusso 3 Tu za nyanya, hapa bei itapanda!
Na unaweza kufika sokoni ukakuta fusso 100 za nyanya! Hapa bei inaporomoka!
 
Sio kweli,
Kama Ni hivyo basi dangote asingeagiza makaa ya mawe kutoka afrika kusini wakati Hapa ya Bei Chee yapo.
Kwani nguzo za umeme zinatoka wapi?? Je Tz hakuna nguzo?
 
Sio kweli,
Kama Ni hivyo basi dangote asingeagiza makaa ya mawe kutoka afrika kusini wakati Hapa ya Bei Chee yapo.
Bei ya bidhaa yoyote hutegemea ubora, gharama za uzalishaji na usafirishaji.
Pili chimbo letu bado jipya kuuza duniani.
Huenda ni bei ya matangazo...nawaza tu.

Tatu...niliwahi kusikia Dangote akisema kuwa anaagiza hayo makitu nje ya nchi kwasababu makaa yetu hayana ubora.
 
Salaam Wakuu,

Imedaiwa Eti, Tanzania kupitia Stamico tumesaini mkataba wa kuuza Madini ya Makaa ya Mawe kwa dola 29.5 ambayo ni sawa na Shilingi 69,444 (Elfu sitini na tisa na Mia nne arobaini na nne tu) kwa Tani moja!

Bei ya Soko la Makaa ya Mawe kwenye Market Insider ni dola 315 sawa na shilingi za Kitanzania 740,250 (laki saba na elfu arobaini na mia mbili na hamsini).

Reuters wameripoti kuwa bei ya Madini ya Makaa ya Mawe inatazamiwa kupanda kwa mwaka 2022 kufikia dola za Kimarekani 500 sawa na shilingi za Kitanzania 1,175,000 (Milioni moja na laki moja na elfu sabini na tano)

Afrika Kusini wanauza makaa ya Mawe kwa bei ya Dola za Kimarekani 140.07 ambayo ni sawa na shilingi 329,164 hii ni bei iliyoporomoka toka kwenye bei ya Dola 214.27 sawa na shilingi 503,534 ya mwezi uliopita!

Ukiangalia bei ya Soko la Madini haya na wastani wa bei inaashiria dhahiri pasi na shaka kuwa Mkataba huu una viashiria vikubwa mno vya Rushwa!

Haiwezekani Madini yetu ya Makaa ya Mawe yauzwe kwa bei inayolingana na bei ya Kifusi cha Udongo/Mchanga!

Watoto na wajukuu zetu watakuta mapango na mashimo watatuuliza hapa palifanyika jambo gani?

Tukiwaambia palikuwa na Madini ya Makaa ya Mawe ambayo yaliuzwa kwa Tani elfu 69,444 watatulaani, watatutukana na kutuadhibu!

Ni heri haya Madini tuyaache vizazi vijavyo viyakute kuliko kuyachimba na kuyauza kwa Mikataba iliyojaa rushwa na Ufisadi!

Haiwezekani Mbuzi mmoja awe na thamani kubwa kuliko Tani moja ya Madini ya Makaa ya Mawe!

Naiomba Serikali kupitia vyombo vyake iuchunguze mkataba huu , iuvunje na ichukue hatua kali kwa kila aliyehusika kuruhusu Mkataba wa kifisadi kama huu ili iwe fundisho kwa watumishi wa Umma wote na wanasiasa wasio waadilifu!

Wizara ya Madini.

Napenda kupata kauli ya STAMICO ilikuwaje wakaingia huu Mkataba

Pia, soma;

Thread 'Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya' Meli nyingine iliyobeba makaa ya mawe yaondoka kutokea Mtwara kwenda Ulaya.

View attachment 2245667
Stamico to the best of my knowledge anamiliki mgodi wa kiwira coal , coal ya kiwira ni moja ya coal zenye ash content kubwa na low calorific value , kiufupi ni coal dhaifu sokoni, inawezekana bei hiyo ni sahihi kulingana na ubora wa makaa yale.
 
Bei ya bidhaa yoyote hutegemea ubora, gharama za uzalishaji na usafirishaji.
Pili chimbo letu bado jipya kuuza duniani.
Huenda ni bei ya matangazo...nawaza tu.

Tatu...niliwahi kusikia Dangote akisema kuwa anaagiza hayo makitu nje ya nchi kwasababu makaa yetu hayana ubora.
Kwa sasa duniani sisi ndo tuna coal bora ,
 
Kwa Tsh 60,000 kwa tani [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hakika nchi imefungukooooooooooooo
Hiyo ni bei ya stamico kama mtoa mada anavyosema, stamico hajaanza kusafirisha mkaa kama sijakosea , anaye lsafirisha mkaa kwa meli hizi mbili za mwisho ni Ruvuma coal ma hasafitishi kwa bei hiyo
 
Tunamshinda Mrusi?
Siwezi kujua ila sisi ndo tunaanza kuchimba , wezetu walianza siku nyingi na almost ile coal bora washamaliza , hata coal ya southern Africa ni shallow kwa ubora
 
Back
Top Bottom