Eti unajenga bandari ya Karema Ili upunguze Malori Tunduma, kwa Jiografia ipi hiyo?

Eti unajenga bandari ya Karema Ili upunguze Malori Tunduma, kwa Jiografia ipi hiyo?

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Hawa wanaopanga na kufanya hii miradi Huwa wanajua wanachokifanya au wanakurupuka tuu?

Yaani Mizigo Mingi inayopita Tunduma inaenda DRC(Lubumbashi), Zambia na Zimbabwe ambako route Yao fupi ni via Tunduma..

Sasa inawezekanaje mizigo itoke Dar iende Karema then ivuke Ziwa itafute Barabara ndio iende huko nilikotaja..

Kwa Jiografia Ipi? Hivi huko Wizarani hakuna Wataalamu Hadi kufanya miradi ya kukurupuka isiyo na Tija?

Imeshindikana Kwa Bandari ya Kasanga ambayo nayo ilijengwa Kwa mabilioni na lami ikafikishwa Bandarini lakini hakuna hata Lori Moja linatumika njia hiyo na kupunguza msongamano Tunduma..

Serikali acheni blaa blaa zisizo na msingi,Jenga Sgr Dar Hadi Zambia Hadi Lubumbashi na njia zote ziwe Dual Carriage ndio walau utapunguza msongamano Tunduma sio hizo hadithi na blaa blaa zisizo na msingi.

----
Ubovu wa barabara na kutokuwepo kwa reli kutoka Mpanda kwenda Bandari ya Karema iliyopo Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi imetajwa kuwa sababu ya bandari hiyo kuzorota kinyume na matarajio.

Akizungumza mara baada ya kuzuru mradi huo wa kimkakati wa bandari ya Karema, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC), Jerry Silaa, amesema tangu ilipofunguliwa rasmi mwezi Septemba 2022 hadi sasa, bandari hiyo imeingiza kiasi cha shilingi milioni nne na laki nane tu ambazo amesema ni kiasi kidogo ukilinganisha na uwekezaji uliofanyika wa shilingi Bilioni 47.97

Amesema kukamilika kwa miundombinu hiyo itasaidia malori yanayopeleka mizigo DRC badala ya kupitia Tunduma yatapitia Mpanda hadi Karema na baada ya kufika Bandari ya Karema ni rahisi kufika Bandari ya Karemii iliyopo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na baadaye Lubumbashi, jimbo kubwa la kibiashara nchini humo.

Silaa amesema Mpango wa serikali uliopo sasa ni kujenga barabara ya kilomita 110 kutoka Kijiji cha Kagwira hadi bandari ya Karema pamoja na kujenga reli kutoka Mpanda hadi Karema.

Ujenzi wa mradi wa Bandari ya Karema uliogharimu kiasi cha shilingi Bilioni 47.97, ulianza kutekelezwa Oktoba 2019 na kukamilika mei 2022 na kuanza kazi rasmi Septemba 2022


 
KWA kusini Mwa afrika, Njia ya Tunduma haikwepeki.

Kwanini wasijenge njia nne toka Mpemba hadi Tunduma, kwann wasijenge Yard kubwa Mpemba pale mizigo na uvukaji wote ukamilishwe Mpemba pale Tunduma iwe ni kuvuka tu.
 
KWA kusini Mwa afrika, Njia ya Tunduma haikwepeki.
Kwann wasijenge njia nne toka Mpemba hadi Tunduma, kwann wasijenge Yard kubwa Mpemba pale mizigo na uvukaji wote ukamilishwe Mpemba pale Tunduma iwe ni kuvuka tu
Kalema sio kwa ajili ya kukwepa Tunduma. Ni kwa ajili ya kuisadia Tunduma na wadau wake.
 
Mnaokosoa mnakuwa mnaangalia soko lililopo tu. Je, soko litakaloibuka kwa maeneo ya DRC yaliyopo kando kando au karibu na ziwa Tanganyika kwa upande wa DRC?
 
KWA kusini Mwa afrika, Njia ya Tunduma haikwepeki.
Kwann wasijenge njia nne toka Mpemba hadi Tunduma, kwann wasijenge Yard kubwa Mpemba pale mizigo na uvukaji wote ukamilishwe Mpemba pale Tunduma iwe ni kuvuka tu
Njia 4 zinatakiwa kutoka Dar Hadi Zambia na DRC Congo plus reli sio hizo hadithi wanazofanya
 
Kuhusu upanuzi wa barabara kutoka Mpemba hadi Tunduma, ipo kwenye mradi wa upanuzi wa TANZAM highway kutoka Igawa hadi Tunduma.
Tenda imetangazwa na mkataba umeshasainiwa na pande zinazohusika.
KWA kusini Mwa afrika, Njia ya Tunduma haikwepeki.
Kwann wasijenge njia nne toka Mpemba hadi Tunduma, kwann wasijenge Yard kubwa Mpemba pale mizigo na uvukaji wote ukamilishwe Mpemba pale Tunduma iwe ni kuvuka tu
 
Mnaokosoa mnakuwa mnaangalia soko lililopo tu. Je, soko litakaloibuka kwa maeneo ya DRC yaliyopo kando kando au karibu na ziwa Tanganyika kwa upande wa DRC?
Unajua litaibuka lini? DRC ya vita Haionekani kupata amani in a near future na kumbuka wao concentration ya Maendelea Iko Upande wa Masgharibi na Kusini Magharibi iliko Katanga..

Huku Mashariki hawana hata Mpango,hakuna Barabara Wala hakuna Miji inayoeleweka..
 
Kuhusu upanuzi wa barabara kutoka Mpemba hadi Tunduma, ipo kwenye mradi wa upanuzi wa TANZAM highway kutoka Igawa hadi Tunduma.
Tenda imetangazwa na mkataba umeshasainiwa na pande zinazohusika.
Hata ikipanuliwa na ikaishia Tunduma bila Zambia na Congo kufanya hivyo ni kazi bure
 
Njia 4 zinatakiwa kutoka Dar Hadi Zambia na DRC Congo plus reli sio hizo hadithi wanazofanya
Bado sana kusema njia nne zitoke Dar hadi Tunduma. Tutakuwa tumeshindwa kufanya mobilization ya resources. Kuanzia Morogoro hadi Makambako, njia 2 zinatosha.
 
Unajua litaibuka lini? DRC ya vita Haionekani kupata amani in a near future na kumbuka wao concentration ya Maendelea Iko Upande wa Masgharibi na Kusini Magharibi iliko Katanga..

Huku Mashariki hawana hata Mpango,hakuna Barabara Wala hakuna Miji inayoeleweka..
Ziwa Tanganyika lipo kusini mashariki, sio mashariki mwa DRC. Mashariki ya DRC yenye changamoto ni kule mpakani mwa Burundi, Rwanda na Uganda.
 
Lile jizi lilikuwa linaanzisha miradi ili lipate kuiba fedha tu na wala halikuwa na muda wa kusikiliza ushauri wa wataalamu,nchi ilifikia pabaya sana mtu mmoja alijiona akili zote za Watanzania anazo yeye hivyo aliona mawazo yake ndio sahihi na aliamua atakavyo.
 
Hawa wanaopanga na kufanya hii miradi Huwa wanajua wanachokifanya au wanakurupuka tuu?

Yaani Mizigo Mingi inayopita Tunduma inaenda DRC(Lubumbashi), Zambia na Zimbabwe ambako route Yao fupi ni via Tunduma..

Sasa inawezekanaje mizigo itoke Dar iende Karema then ivuke Ziwa itafute Barabara ndio iende huko nilikotaja..

Kwa Jiografia Ipi? Hivi huko Wizarani hakuna Wataalamu Hadi kufanya miradi ya kukurupuka isiyo na Tija?

Imeshindikana Kwa Bandari ya Kasanga ambayo nayo ilijengwa Kwa mabilioni na lami ikafikishwa Bandarini lakini hakuna hata Lori Moja linatumika njia hiyo na kupunguza msongamano Tunduma..

Serikali acheni blaa blaa zisizo na msingi,Jenga Sgr Dar Hadi Zambia Hadi Lubumbashi na njia zote ziwe Dual Carriage ndio walau utapunguza msongamano Tunduma sio hizo hadithi na blaa blaa zisizo na msingi..


Mkitaka kupunguza foleni ya Tunduma boresheni reli ya tazara huo hilo ndio suluhisho kinyume na ni UONGO..yani hii inadhihika wazi wazi wasomi wetu elimu yao haiwasaidii kupambana na changamoto..
 
Lile jizi lilikuwa linaanzisha miradi ili lipate kuiba fedha tu na wala halikuwa na muda wa kusikiliza ushauri wa wataalamu,nchi ilifikia pabaya sana mtu mmoja alijiona akili zote za Watanzania anazo yeye hivyo aliona mawazo yake ndio sahihi na aliamua atakavyo.
Chuki inaua.
 
Lile jizi lilikuwa linaanzisha miradi ili lipate kuiba fedha tu na wala halikuwa na muda wa kusikiliza ushauri wa wataalamu,nchi ilifikia pabaya sana mtu mmoja alijiona akili zote za Watanzania anazo yeye hivyo aliona mawazo yake ndio sahihi na aliamua atakavyo.
Bandari ya Kasanga,Kabwe,Karema nk zote zimetumia Mabilioni ila hakuna kitu zinaingiza.

Zaidi ya Bil.200 zimepotea Kwa kukurupuka
 
Tuwajengee? Tuwe donor country? Hata hivyo Tanzania na Zambia wana makubaliano ya Zambia kuboresha kpande kile kibaya sana cha Nakonde kuelekea (wapi pale, nimesahau).
Bado kama itakuwa ni single carriage way ni kazi bure
 
Mkitaka kupunguza foleni ya Tunduma boresheni reli ya tazara huo hilo ndio suluhisho kinyume na ni UONGO..yani hii inadhihika wazi wazi wasomi wetu elimu yao haiwasaidii kupambana na changamoto..
Si ilikuwepo kwenye zile Items, Bw HH wa Zambia alipofanya ziara Tanzania? Sasa ya nini kufanya duplication ya maoni na ushauri usioisha? Tusubiri kwanza tuone kama walimaanisha.
 
Back
Top Bottom