EWURA: Nchi ina hifadhi ya Mafuta inayojitosheleza, Petrol inatosha kwa siku 19 na Diesel siku 18

EWURA: Nchi ina hifadhi ya Mafuta inayojitosheleza, Petrol inatosha kwa siku 19 na Diesel siku 18

Eti siku 19 CCM mmetufikisha mahali pabaya sana
Kuna mwingine alijitokeza hadharani eti kuna uhaini
Nashukuru watalii hawakumsikia yule mlevi.
 
Huyo bila shaka Hana akili au anatufanya wananchi hatuna akili na ni wajinga..

Kama yapo ya kutosha iweje sasa kuna maeneo ya nchi hayana nishati hii kwa zaidi ya wiki 4 na kule ambako yanapatikana bei iko juu kuliko kawaida..!

Hawa viongozi wetu Wana shida gani kwenye vichwa vyao??
Wewe ndo huna akili mkuu.. fuatilia habari vizuri
 
Sijasikia vizuri amesema siku 19 au miezi 19 maana ukiwa chini ya miezi 4 mpaka sita Tayari unakuwa na shortage sasa unapokuja hadharani na kusema kuhusu siku dah inafikirisha sana
Mkuu!

Kuna watu ni wapumbavu sana nchi hii!

Fikiria mtu anajisifu kabisa eti siku 19 kweli?

Ina maana ikitokea chochote mipaka ya nchi ikafungwa tunajifia kama nzi
 
Ni hatari sana nchi kuwa na akiba ya siku 19.

Nchi jirani yaani Rwanda wao sera ni akiba ya miezi minne ndiyo wanaona nchi ipo salama.

Sera ya mafuta ya petroli ambayo ilipitishwa mwaka 2012 nchini Rwanda ililenga kuongeza mara tano hifadhi ya mafuta ya Rwanda kutoka lita milioni 30 hadi lita milioni 150 mwaka 2017. Ilikadiriwa kuwa hifadhi hii ingetosha kuchochea shughuli za kiuchumi za nchi, hasa katika sekta ya usafiri. kwa angalau miezi minne kuweza kubabiliana na changamoto ikitokea ya, uhaba wa usambazaji au usumbufu.

Lakini, ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za mwaka wa fedha 2019/2020 Rwanda iligundua kuwa lengo lilifikiwa kwa karibu asilimia 50.

Rwanda inategemea mafuta ya petroli kutoka bandari za Dar es Salaam, Tanzania na Mombasa, Kenya.
 
Kazi ipo huku Tz.
Kazi tunayo.
Kazi iliyopo ni moja tu, mama kumtumbua Majaliwa au ajiudhuru; huyo ndio credible candidate serikalini aliebaki inayofanya baadhi ya wananchi wawe na imani na serikali ya huyu mama.

Nakuhakikishia Majaliwa akitoka hapo CCM moto watauona.

Mimi namwambia ‘bi Tozo’ kama ana amini anakubalika amtoe Majaliwa kwenye hiyo nafasi; halafu tuone.

Political leadership is about trust na Majaliwa ndio mtu pekee aliebaki hapo wananchi wanamwamini.

I dare raisi Samia, J.K, Kinana na washauri wengine wa ‘bi tozo’ wamtoe Majaliwa kwenye nafasi yake tuone huu mziki. Itakuwa kazi rahisi sana kwa CDM.

Ndio wataelewa meaning of trust in leadership; Samia, baraza lake la mawaziri na uongozi wa CCM hawana. Majaliwa ndio anawabeba.

Hawaamini hilo wamtoe hapo au ajiudhuru kuliko kuletewa dharau za kupewa naibu kama vile kashindwa kazi wakati yeye ndio anawabeba.
 
Ufanyike uchunguzi, wote wanaofanya market manipulation wafungiwe maisha!!!
Tatizo ni kuagiza kwa pamoja (PBPA) na kukokotoa bei kila mwezi (EWURA).

Soko liachwe liamue bei, serikali iingilie pale inapoona imezidi sana.

Hizi taasisi zinaongeza nini kwenye mnyororo wa thamani? Zipo kisiasa zaidi.
 
Sijasikia vizuri amesema siku 19 au miezi 19 maana ukiwa chini ya miezi 4 mpaka sita Tayari unakuwa na shortage sasa unapokuja hadharani na kusema kuhusu siku dah inafikirisha sana
Kama tulivyokuwa na ghala la taifa nadhani ni wakati pia tuwe na hifadhi ya taifa ya nishati ya mafuta na dawa za binadamu za kutuendesha hata mwaka basi kwa uchache miezi 6 bila kuagiza nje ili wakati wa shortage la sivyo kuna siku our existence itakuwa mashakani kama yakitokea kama ya covid kwa kiwango kikubwa na pia tuwajengee uwezo sekta binafsi uwezo tupunguze hizi importation, uganda wana crude oil ni wakati wa kutumia fursa ya kujenga au kupata investor kwa ajili ya oil refinery halafu tukawauzie hao hao wanaozalisha crude.
 
Unamjua Lakini?😂🌟
Kuna haja gani ya kumjua MTU Kama huyu.
Watu wanashinda kwenye foleni ya mafuta hapa Handeni, Tanga halafu MTU mwenye PhD anakutambia mafuta yapo ya kutosheleza zaidi ya nusumwezi.
Sasa Kuna umuhimu gani wa kua na PhD. Kama watoto wadogo hata shule hawajaanza wanaona LIVE hakuna mafuta. Mwenye PhD anakutambia mafuta yapo.
Hivi niulize tu kwa Nia njema,
Kariakoo Kuna duka linauza PhD? Au mpaka uende India?
 
Halafu DP World wakiwa na monopoly ya bandari na hifadhi ya mafuta ni hatari kwa usalama wa nchi.

Toka maktaba :
Aprili 5, 2022


Akizungumza katika mdahalo wa mafuta jijini Dar es Salaam, leo Jumamosi, Aprili 2, 2022 amesema hadi kufikia leo, nchi ilikuwa na hifadhi ya mafuta ya Petrol ya siku 27.

"Sheria inatutaka tuwe na hifadhi ya mafuta ya kuanzia siku 15. Ina maana hatuko katika hatari japo tunapaswa kuongeza uwezo wetu wa kuhifadhi zaidi," – alisema.

Mhandisi Chibulunje alisema kwa upande wa mafuta ya dizeli yapo ya kutosheleza siku 19, ya taa siku 108 na ya ndege yapo ya siku 35.

Mhandisi Chibulunje alisema kuwa matumizi ya mafuta kwa sasae ni mwezi mmoja na tayari mengine yameshaagizwa huku meli nyingine zikishusha shehena yake.

Aidha, amesema Aprili 24, 2022, kuna meli zitaingiza mafuta nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara na nyingine ikitarajiwa kuingizwa nchini mwezi ujao kupitia Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa wote PBPA.

Mhandisi Chibulunje alisema kwa sasa Tanzania ina maghala makubwa matatu yenye uwezo wa kuhifadhi mafuta kwa siku 122 katika mikoa ya Dar es Salaam, Tanga na Mtwara.

Chanzo: TEF
 
View attachment 2739153
Mkurugenzi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati (EWURA) Dkt. James Andilile amesema hayo na kufafanua kuwa Petrol iliyopo inatosheleza matumizi ya siku 19 na Dizeli ipo ya kutumika kwa siku 18.

Aidha, EWURA imevifungia kwa miezi 6 Vituo 2 vya Mafuta ambavyo ni Camel Oil na Mtemba vilivyopo Msamvu na Turiani Morogoro huku Kituo GBP cha Ipuli Tabora kikifungiwa kwa muda usiojulikana baada ya kutuhumiwa kuficha Mafuta.

Takwimu za Mahitaji ya Mafuta Nchini zinaonesha Tanzania inatumia Lita Milioni 4.5 za Petroli kwa siku na Dizeli Lita Milioni 6.6 kwa siku.
Hakuna sababu ya kutangaza takwimu kama hizi kiusalama.
Kama adui anazitumia ni hatari sana, anaweza kuzishambulia meli au kuzuia kuingia bandarini/ nchini, halafu anaanzisha vita ili mshindwe kupambana.
Changamoto inatokakana na kukokotoa bei kila mwezi ambapo wafanyabiashara wataacha kuuza wakisubiri bei mpya wakati wa kupanda na kinyume chake inaposhuka.
 
Kazi iliyopo ni moja tu, mama kumtumbua Majaliwa au ajiudhuru; huyo ndio credible candidate serikalini aliebaki inayofanya baadhi ya wananchi wawe na imani na serikali ya huyu mama.

Nakuhakikishia Majaliwa akitoka hapo CCM moto watauona.

Mimi namwambia ‘bi Tozo’ kama ana amini anakubalika amtoe Majaliwa kwenye hiyo nafasi; halafu tuone.

Political leadership is about trust na Majaliwa ndio mtu pekee aliebaki hapo wananchi wanamwamini.

I dare raisi Samia, J.K, Kinana na washauri wengine wa ‘bi tozo’ wamtoe Majaliwa kwenye nafasi yake tuone huu mziki. Itakuwa kazi rahisi sana kwa CDM.

Ndio wataelewa meaning of trust in leadership; Samia, baraza lake la mawaziri na uongozi wa CCM hawana. Majaliwa ndio anawabeba.

Hawaamini hilo wamtoe hapo au ajiudhuru kuliko kuletewa dharau za kupewa naibu kama vile kashindwa kazi wakati yeye ndio anawabeba.
Halafu kwa nini viongozi wengi anaowateua ni kama hawajali chochote, Imani kwa serikali inazidi kushuka, ila hawarekebishi chochote na yeye bado anawaamini sana.
 
1 September 2023
Tabora, Tanzania

UHABA WA MAFUTA TABORA, POLISI WAITWA KUSAIDIA FOLENI


View: https://m.youtube.com/watch?v=2bkJ_cXkF2M
Baadhi ya watumiaji wa vyombo vya moto vya usafiri mkoani Tabora wamelalamikia hali ya upatikanaji wa mafuta ya petroli kwenye vituo vinavyouza nishati hiyo ambapo katika kituo kimoja cha MOUNT MERU cha mjini Tabora kilionekana kuwa na msongamano mkubwa wa watu waliopanga foleni wakihitaji huduma hiyo ya mafuta.
 
Kama tulivyokuwa na ghala la taifa nadhani ni wakati pia tuwe na hifadhi ya taifa ya nishati ya mafuta na dawa za binadamu za kutuendesha hata mwaka basi kwa uchache miezi 6 bila kuagiza nje ili wakati wa shortage la sivyo kuna siku our existence itakuwa mashakani kama yakitokea kama ya covid kwa kiwango kikubwa na pia tuwajengee uwezo sekta binafsi uwezo tupunguze hizi importation, uganda wana crude oil ni wakati wa kutumia fursa ya kujenga au kupata investor kwa ajili ya oil refinery halafu tukawauzie hao hao wanaozalisha crude.
January Makamba pamoja na mapungufu yake ya ufisadi ana quality za leadership (particularly listening skills).

Ukimtwanga kwa hoja zenye mashiko za uwezo wake wa kuelewa he is reasonable kuona merit ya hoja (mind you his reasoning ability is very limited).

Ukweli ni kwamba J.M katika muda wake kwenye hiyo wizara he understood the importance of having three months of oil reserve. Na alichukua hatua kadhaa za supply security security kujaribu kutafuta wawekazaji wa kuongeza storage capacity kila alipoenda; kuanzia Morroco na mikutano mingine ya kimataifa kila opportunity aliyopata alijaribu kuuza huo uwekezaji wa kukuza reserve capacity kwa kuelewa madhara yake ya hifadhi ndogo ya mafuta.

Kwa hivyo kumlaumu kwenye hili sio sahihi pamoja na upoyoyo wake (mainly Issue za investment na biashara ni kiazi anasifiaga ujinga asioelewa hesabu zake).

Shida ya mafuta msingi wake ni usimamizi wa currency trade; ambapo mshauri wa hayo mambo kwa raisi ni Jakaya Kikwete na uwezo wake mdogo wa maswala ya uchumi. Jumlisha na timu ya iliyopo wizara ya fedha ku counter argue ushauri ambao raisi anapewa na J.K hili maza aamue tofauti.

Ila kwenye hili la mafuta January is ‘taking one for the team’; yeye kama waziri alijaribu kufanya yake but he has no control for the bigger economic policy picture. Na tatizo haluudu la huko ni raisi Samia ndiyo aliyelitengeneza kw kuanza kurudisha irresponsible foreign currency exchange market.
 
Halafu kwa nini viongozi wengi anaowateua ni kama hawajali chochote, Imani kwa serikali inazidi kushuka, ila hawarekebishi chochote na yeye bado anawaamini sana.
Ndio maana nikasema amtoe Majaliwa hapo hii ngoma inogole.
 
Back
Top Bottom