Mindyou
JF-Expert Member
- Sep 2, 2024
- 1,869
- 4,877
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA) hivi karibuni imetoa taarifa kwa umma kuhusu maombi ya vibali vya ujenzi wa miundombinu ya mafuta na leseni kwa ajili ya biashara na shughuli mbalimbali katika sekta ya mafuta ya petroli.
Taarifa hiyo ya EWURA imewataja waliiomba vibali vya ujenzi wa miundombinu ya mafuta katika maeneo ya mkondo wa kati na chini wa usambazaji wa Petroli nchini.
Mamlaka hiyo imesema kuwa mtu yeyote au kikundi cha watu wenye pingamizi dhidi ya maombi hayo, ambaye anaona kuwa mwombaji asipewe leseni au kibali cha ujenzi, anapaswa kuwasilisha pingamizi hilo kwa EWURA.
Pingamizi hizo zinatakiwa kufikishwa ndani ya siku kumi na nne (14) kuanzia tarehe ya kutolewa kwa tangazo hili.
Soma pia: EWURA yaagiza Mamlaka za Maji kuacha kupika takwimu za huduma zake
Taarifa hiyo inawataka wananchi wote ambao wana mapingamizi kwa watu waliopata tenda hiyo kuwasilisha malalamiko yao kwa EWURA kwa mujibu wa sheria.
Taarifa hiyo ya EWURA imewataja waliiomba vibali vya ujenzi wa miundombinu ya mafuta katika maeneo ya mkondo wa kati na chini wa usambazaji wa Petroli nchini.
Mamlaka hiyo imesema kuwa mtu yeyote au kikundi cha watu wenye pingamizi dhidi ya maombi hayo, ambaye anaona kuwa mwombaji asipewe leseni au kibali cha ujenzi, anapaswa kuwasilisha pingamizi hilo kwa EWURA.
Pingamizi hizo zinatakiwa kufikishwa ndani ya siku kumi na nne (14) kuanzia tarehe ya kutolewa kwa tangazo hili.
Soma pia: EWURA yaagiza Mamlaka za Maji kuacha kupika takwimu za huduma zake
Taarifa hiyo inawataka wananchi wote ambao wana mapingamizi kwa watu waliopata tenda hiyo kuwasilisha malalamiko yao kwa EWURA kwa mujibu wa sheria.