Exclusive: Haya Ndiyo Matukio Makubwa Yaliyopelekea Mauaji Ya Bosi Wa Iebc Musando Huko Kenya

Exclusive: Haya Ndiyo Matukio Makubwa Yaliyopelekea Mauaji Ya Bosi Wa Iebc Musando Huko Kenya

Jawani, jamani, ...majirani zetu wanahitaji kuombwewa maana wanakoelekea sasa ni mashaka matupu!
Haya hapa mengine...

dn.jpg
 
Lakini Msando sikuona sababu ya yeye kusema wazi kwenye media kuwa hakuna atakaye ingilia mfumo wa matokeo labda akatwe kiganja....Kwangu mimi niliona kama alikuwa amewapa mbinu wauwaji kabisa na zile zilikuwa tambo zisizo na msingi na hapa kusema kweli kabisa ndipo niliamini hakuna kitu kinaitwa Tume huru...
Kama mtu alipata wasaha kutazama mahojiano ya Msando atagundua kabisa kuwa alikuwa na upande wake na ndio maana alikuwa anaweka tambo na katika maongezi yake alionesha wazi kabisa uchaguzi uliopita uliingiliwa na wazi alikuwa ana watuhumu Jubilee...
Kwa hiyo Msando angeliweza kuhakikisha hakuna anaye ingilia mfumo wa matokeo kwa kuonesha vitendo na sio lazima kuweka tambo na kuonesha jinsi ambavyo wanaweza kuingilia matokeo...hilo ni kosa alilo lifanya pale kwenye usaili wake.

Halafu Kifo chake kina utata sana maana upande wa pili ule unaweza kuwa umetekeleza hii mission ili kuonesha kuwa wahusika ni watu fulani na kuhalalisha kuwa kura zimeibiwa na kabla ya kifo chake NASA walisema wamegundua kuna mpango wa wizi wa kura sasa najiuliza kwanini wasiwe NASA wame usika kwenye hili jambo ili kuthibitisha madai yao kuwa kuna mpango wa wizi wa Kura?
Halafu ni jana tuu NASA wamehoji usalama wa Kura zao baada Msando kuuwawa...
Bado naamini kuna mengi sana nyuma ya kifo cha Msando.

Kwa nini uwaze NASA wakati JUBILEE ndio walitakiwa watoe uLINZI KWAKE NA HAWAKUFANYA hivyo

kwangu mimi hii soo ni ya bwana RUTTO na U.K
 
Ni kweli alikuwa na upande ambao ni upande wa haki kitu kinachoendana na kiapo chake. Mawazo yako yanafikirisha lakini yamekaa 'kikwenu' zaidi. Nadhani upumbavu wetu waafrika na madikteta wengine duniani katika ujasiri wa kuiba kura ungeelekezwa katika ujasiri wa kuwatangazia wananchi kuwa "hatuna haja ya uchaguzi" ingelikuwa na maana zaidi kuliko kupoteza muda na watu muhimu!
Maelezo yako mbona yana hitimisha kuwa kuwa Jubilee ndio wamehusika? Kwanini si NASA kwa kutafuta public sympathy kupitia mgongo wa Kura kuibiwa na kuingiza nchi kwenye machafuko? NASA hata kabla ya kupotea kwa msando walileta story za kuibiwa kura na hata baada ya Msando kupatikana ndio wameonesha wazi kuwa hawana imani na mfumo wa matokeo ,,,,Kwanini sio kwamba hili jambo limepangwa ili kuonesha ulimwengu kuwa Kura zinaibiwa?
Mimi bado nina wasi wasi kabisa na pande zote kuhusika........maana mazingira ya kifo cha Msando bado kina waweka kwenye mashaka pande zote mbili kuhusika...
 
Habari ya wauaji kukata kiganjia siyo kweli. Mwili umepatikana na mikono yote miwili ila inayo majeraha ya kisu.Picha Zipo mtandaoni ,kwa sababu za kimaadili siwezi kuzirusha hapa.
 
Tunaweza tusiwe na uhakika lakini haina shaka kifo cha huyu bwana kilipangwa. Wakenya wakitafuta uongozi UTU huwaondoka kabisaaa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Dah, nakikumbuka kitabu nilisoma zamaani kinaitwa "The River Between ". Mhusika mmoja alikuwa akiitwa Waiyaki na mwingine kama sikosei ni Gikuyu Mumbi! Ah basi acha nisiendelee!
 
Kwa nini uwaze NASA wakati JUBILEE ndio walitakiwa watoe uLINZI KWAKE NA HAWAKUFANYA hivyo

kwangu mimi hii soo ni ya bwana RUTTO na U.K
Kimsingi kutopewa Ulinzi haraka hakufanyi hitimisho kuwa Jubilee ndio wahausika maana wengine tunaweza kusema kuwa NASA wametumia huu mwanya kummaliza ili kuonesha na kuthibitisha kuna wizi wa kura....
 
Habari ya wauaji kukata kiganjia siyo kweli. Mwili umepatikana na mikono yote miwili ila inayo majeraha ya kisu.
Ndio maana nasema hivi kwenye mauaji yake kuna maswali wengi.... Halafu hivi kama kiganja kikikatwa finger print itafanya kazi? Hivi finger print haitegemei mzunguzo wa damu?
 
Movie za James Bond We Strong Antibiotic nakuiubali sana kwa kufikiri krb na ukweli we si wa Africa
 
Africa ni bara la ajabu mno mno maana always tunaangalia tulipoangukia sio kujikwaa,ni huzuni mno maisha ya binadamu wenzetu yanapotea hivi bila ya sababu maalum,why kura zikishapigwa kituoni ,kuhesabiwa pale na kuingizwa moja kwa moja katika mfumo mkuu wa matokeo kuwa tatizo ?mbona wenzetu hapa hapa SADC wanafanya hili kwa hiyo aliyeko nyumbani,au kwenye ktuo kikuu cha makusanyio ya kura unapata matokeo moja kwa moja,wote mnaangalia kwenye big screen kura zikiingia na mshindi kuanza kuonekana mapema ?
 
Back
Top Bottom