FACT CHECK: Roma hakutekwa, alijiteka kwa maslahi binafsi ya kiMuziki

FACT CHECK: Roma hakutekwa, alijiteka kwa maslahi binafsi ya kiMuziki

Mmeshaitoa ile picha ya muasisi wa taifa kwenye ile nanihii yenu kama sheria inavyowataka? Itoeni basi!
 
Mtoa uzi unachekesha. Sijasoma yote ila kitendo cha kulazimisha huo ni utekaji tosha.
Kwa akili yako inawezekanaje mtu akuamlishe ukubali?
Wakaingia ndani, wakamlazimisha Roma achukue simu, na wakabeba na Tv.
Hiv kwa akili yako tu mtu aje kwako, akuambie chukua simu,na achukue Tv unamuangalia tu, tena humjui ni kwa mara ya kwanza halafu anakuambia panda kwenye noah twende. Halafu unapanda, wanaondoka na ww, hapo kwenu hawajui wala mke wako. Simu haipatikani halafu unasema hawajateka. Km hivyo ni raha sana
basi mtoa uzi mm nakuja kwako, namchukua mkeo, pamoja na simu ya mkeo na nitamrudisha mkeo siku 5 kupita. Sawa?
 
Mtoa mada inaonekana hauna uelewa wa kutosha kuhusu masuala ya Uhalifu wa Utekaji na other Organised Crimes. Picha uliyonayo kichwani ni ya "UJAMBAZI" ambao kwa bahati mbaya sana una ilinganisha na "UTEKAJI", kwa kukusaidia tu Watekaji usidhani labda walikua na shida ya kuharibu studio au mali nyingine au kuua mtu, watekaji hawana tamaa ya hizo mali ila wanaangalia ni kitu gani wameagizwa na ni "VALUABLE" cause ya utekaji wao. Mfano wamechukua Kompyuta inayotumiwa kutengenezea nyimbo hiyo ni valuable asset kwao kwa sababu aliyetekwa ni msanii/wasanii na mtayarishaji wa muziki hivyo basi kazi zao huifadhiwa humo kwenye kompyuta. Hata wangekuta Bilioni 100 mezani wasingezigusa unless kama wao wangekua ni Majambazi.

Pia unazungumzia kuhusu roma kubadilisha nguo. Hii ni hoja dhaifu sana, umejiuliza Roma kabla ya kufika oysterbay alitokea wapi?

Pia unashaka juu ya waliotekeleza tukio la utekaji kutokumfahamu Roma eti kisa ni Vijana na Roma ni Msanii. Je una uhakika gani kama waliomteka ni Watanzania? Kila kijana usidhani yuko busy na wasanii.

Kwa kuhitimisha nimeona umejikita sana kwenye hoja ya watekaji kua WASTAARABU, hii ni hoja ya ajabu sana inaonekana wewe ulitarajia waanze kufyatua risasi hewani. HIZI KAZI HAZIFANYIKAGI HIVYO.

Bonafsi nongependa kukushauri ujikite zaidi kwenye kujiuliza kwanini Ndugu Daudi Bashite awe na uhakika juu ya watekwaji watapatikana Lini?, kwanini ahadi yake itimie? Je anakipi anachokijua nyuma ya pazia?.

Hili suala la Daudi Bashite kusema hawa watu watapatikana kabla ya siku fulani na kweli ikatokea sio dogo hata kidogo, ila kwa sababu hii ni Tanzania hakuna atakaye muhoji lakini nakuapia hili suala angelizungumza kwenye nchi za dunia ya kwanza basi yeye ndio angekuwa suspect namba MOJA.

Mwisho kabisa Elewa kilichofanyika ni Utekaji sio UJAMBAZI. Vyote ni UHALIFU katika mizania tofauti.
 
Siku chache zilizopita mwanamuziki maarufu wa miondoko yakufokafoka almaarufu Roma mkatoliki aliripotiwa kutekwa na watu wasiojulikana katika studio za Tongwe record zinazomilikiwa na kijana jina maarufu (J mada),inasemekana ilikuwa ni majira ya usiku wavamisi walipowasili katika viunga vya ilipo studio hizo.

Kulingana na maelezo yaushaidi uliotolewa na shuhuda (the city) mwanadada aliyefika muda mchache kabla gari lawatekaji kuondoka alisema "ilikuja Noah nyeupe na wakashuka watu watatu,baada ya hapo wakatuamrisha mimi,bin Laden na wageni kutoka morogoro tuingie ndani ya geti,tulipoingia ndani ya geti walituuliza kwamba tumemkuta junior au tumemkuta Roma,tukasema junior hayupo ila Roma yupo ndani,wakatuamrisha Tukamuite Roma,tukamuita Roma,Roma akatoka akaulizwa wewe ndio ROMA na ilivyoonekana hawakumjua na pia walimuambia simu yake ipo wapi atokenayo Roma alitokanao sikuweza kujua nini kiliendelea kwa sababu waliongelea nnje ya gari,walirudi ndani wakamlazimisha binladen aingie studio akiwa amesindikizwa na mmoja wao na Wakarudi tena wakachukua TV zilizopo pale,wakatoka na imma walikuwepo wote ndani ya studio,studio ikabaki tupu,walivyotoka hapo wakaniambia mimi na wageni wengine waliotoka morogoro tusiende popote na nilichosikia baada ya hapo ni mshindo wa gari na gari kuondoka "

Fact:katika ushahidi wa shuhuda (Rozaree) umejidadavua watekaji hawakuwa na haiba yautekaji kwani kiwango Chao cha ustaarabu kilikuwa juu sana ukilinganisha na watekaji wengine tunaowasikia na hata kuwashuhudia.
Hoja ya kwanza (1):watekaji waliuliza tumemkuta Roma na wakatuambia tukamuite?? Niajabu kwa mtekaji kuwa na nidhamu ya namna hii, mara nyingi hutumia nguvu kuhakikisha wanatimiza lengo Lao,mtekaji gani huyu anaogopa kuingia ndani anawaambia mashuhuda nendeni mkamuite Roma ??
Hoja ya pili (2):watekaji wakamuuliza Roma,wewe ndio Roma.sikawaida kwa msanii maarufu kama Roma ashindwe kujulikana tena na hawa watekaji ambao kwa asilimia kubwa huenda wakawa ni vijana,tena vijana hawa ndio wapenzi namba moja wa mziki huu wakufokafoka unaoimbwa na Roma ni wazi na sio rahisi kutokumfahamu Roma.
Hoja ya Tatu (3):watekaji wakaingia ndani na binladen,picha tunayoipata hapa bado watekaji walikuwa na ustaarabu napo hawakutaka kuingia studio wenyewe bado waliitaji mtu mwenyeji waingie nae ndani, wavamizi wengi hutumia nguvu na wakati mwingine huwa hawajali Mali ya waliodhamiria kumteka hawa waliomteka Roma watofauti sana.viashiria hivi vya ushahidi wa rosare unatuonyesha wazi kunamaslahi binafsi yakisanà na wala siutekaji kama unavyoripotiwa..

Hoja ya 4.watekaji wakatuambia tusiondoke
.watekaji baada yakuwachukua wahusika wakuu waliwaamuru the city na wenzake wasiondoke hii inamaana bado walitaka kuhakikisha usalama wa studio unakuwa salama hivyo walionyesha kujali na kudhamini Mali na vifaa vinginee vya studio. hali isiyo ya kawaida mtekaji kuhakikisha ulizi wa Mali za mtekwaji.

Upande wa mmiliki wa Tongwe record :nae mmiliki wa Tongwe record aliskika akiongea akisema "usiku wa jana likitokea tukio lakutisha sana,walikuja watu ambao hawakufaamika wametoka wapi au wametumwa na nani,bahati nzuri mimi si kuwepo studio,wakamuhoji ROMA baada ya kumuhoji Roma wakamuhoji na monie ambaye ni msanii wangu pia kutoka Tongwe record baada yakumaliza mahojiano yao wakaingia ndani studio wakachukua TV, computer pamoja na kamera"

Maelezo ya mmiliki wa studio na shuhuda namba moja hayatofautiani sana bado yote yanaukakasi wa kiwango cha ustaarabu wa hawa watekaji.

Hoja watekaji walimuhoji ROMA.ni tanzania pekee watekaji hupata muda wakuhoji mtekwaji,sidhani kama inaingia akilini kuskia mtekaji anaweza kufanya interview na mtekwaji,nguvu na ubabe huwa hawana muda wa kuwa wakarimu na kuchukua maelezo mara zote watekaji hawana huo muda,ili lililotokea kwa Roma ni maigizo yenye maslahi binafsi.

Kauli ya mkuu wa mkoa mh.Paul makonda.mkuu wa mkoa ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa mkoa ni haki na wajibu wake kuhakikisha mkoa unakuwa salama pamoja na Raia wake,ni haki na sahihi mkuu wa mkoa kuingilia kati upotevu wa watu wake.

Mh.Makonda aliskika akisema
"bado tunayomamlaka yakudhibiti kila aina ya utekaji na kuhakikisha wanannchi wetu wanaendelea kuwa salama,sambamba na hilo nawapa imani tu haitafika jumapili tutakuwa tumeshawapata ndugu zetu wote wanne na mimi naomba kwa dini zetu kwa imani zetu kila mmoja kokote kule alipo aombe ili tuhakikishe ndugu zetu tunawarejesha wakiwa salama.

Kutokana na kauli ya mh Paul makonda imepelekea watanzania kijuiliza maswali kadhaa.

Hoja ya kwanza (1).
kauli ya haitafika jumapili Roma na wenzake watakuwa wamepatikana.Niwazi kauli hii ni Tata na ilikuwa na viashiria vya huenda kuna Jambo muheshimiwa alikuwa analifahamu zaid, tena ukizingatia huwa anaukaribu na vijana hawa wanaofanya sanaa,nikweli jumapili hajafika na vijana wamepatikana,mh ni kijana anajua mbinu nyingi za vijana wenzake wanazotumia kujipatia umaarufu nadhani alishashtukia na akatoa kauli iliyojipambanua kuna kitu anafahamu.

Hoja ya pili (2).kauli yakuwarejesha Roma na wenzake wakiwa salama nayo ni moja ya kauli iliyotolewa na mh mkuu wa mkoa tutawarejesha wakiwa salama kauli hii nayo iliashiria mchezo mzima huenda mkuu wa mkoa alikuwa anajua mahali alipo mkatoliki.

Uchambuzi wa kauli ya mhusika mkuu (Roma)
.Roma mara baada yakupatikana alipelekwa kituo cha Polisi ambapo naamini aliacha maelezo yakutosha.

Roma aliskika akisema " kutokana na mazingira na situation nzima hatutakuwa na muda mrefu wakuzungumza, kwakifupi tu niwaakikishie mimi ni mzima mpaka Sa hivi kiafya na kiakili hata monie,bin LadenI wote tuwazima wa afya,niwaakikishie sisi wote ni wazima tunaendelea vizuri"


Hoja ya kwanza (1)
.nifuraha kuskia wapo salama ila yapo maswali ya kujiuliza nini hasa lengo la watekaji je ni kweli watu hawa walitekwa? ni kweli mtekaji anaweza kuwateka wasipigwe hata vibao kimoja kiasi cha kuachiwa wakiwa 100% sawa bila jeraha na hata mkwaruzo wowote?

Hoja namba mbili (2).mavazi ya Roma siku anatekwa na siku anaonekana,siku anatekwa Roma aliripotiwa kuwa alikuwa amevaa t shirt nyeupe suruali ya blue aina ya Jinsi, ila siku anapatikana alionekana akiwa na mavazi meusi .Niwazi uko alikokuwepo alipata fursa ya kupata huduma muhimu kama kuoga na hata kubadilisha nguo bado kuna ulakini wa aina hii ya utekaji,sio rahisi kwa watekaji kuwa na moyo wa namna hii vijana wasanaa inaonekana walikuwa bado katika mwendelezo wa sanaa yao,haingii akilini aina hii yautekwaji kwakweli.

My take.tusishangae na kuskia nyimbo mpya ya Roma katika kipindi cha mwezi mmoja kutoka sasa,attention aliyokusudia kuipata amefanikiwa kwa 100% otherwise kesho siku ya jumatatu atuambie wa Tanzania hoja nzito kutuakikishia ni kweli alitekwa na sio kutafuta umaarufu kisanaa.
huyu mtu kesho kwanza aanze kutupa identity yake kama roma mkatoliki ni nani..ni elibariki..au ibrahim mussa. tusipoangalia kama taifa tutachezewa na wakora wa mtaani.
 
NGOJA TUONE JUMATATU ATASEMA NINI.
BUT SIWEZI KURUHUSU AKILI YANGU IKUBALI NI KWELI ULIKUWEPO UTEKAJI.

UMETEKWA ALAFU UNASEMA NIATASEMA JTATU!!!?
DR ULIMBOKA ALIPOONEKANA TU ALIANZA KUSEMA ILIVYOKUWA AKIWA KWENYE GARI ANAPELEKWA HOSPITALI.

UMETEKWA UNASEMA NITASEMA JTATU!!?
UNATAKA UKAANDAE HOTUBA!?
ALAFU WATU WANAAMINI KWELI.
HAPA KUNA KITU KATI YA HAWA WASANII NA RC MAKONDA, SISI TUNACHEZA NGOMA ZAO.
 
Wabadilike vipi sasa wapinzani, yaani huoni ninyi ndo mnapaswa kubadilika? Nyie watu sijui huwa mnalishwa nini!!!
Umenukuu sehemu tu ya hoja zangu, ukaacha yenye jibu la swali lako. Rejea bandiko langu.
 
Mleta mada kwanini usisubili mtendewa akasema nini kilitokea? Ukalinganisha na kutoa maoni yako subili mtekwaji atoe yaliyo moyon
 
Watekaji waliotumwa na serikali hawaitaji kuogopa maana wanakuwa wanatekeleza kazi waliotumwa.kwahyo hamna kizuizi cha kuwatisha.lakini watekaji ambao awajatumwa na serikali wao wanafanya fasta fasta wakiogopa kukamatwa na serikali.


Nimekujibu kipumbavu kama ulivyotoa hoja zakipumbavu.
 
Siku chache zilizopita mwanamuziki maarufu wa miondoko yakufokafoka almaarufu Roma mkatoliki aliripotiwa kutekwa na watu wasiojulikana katika studio za Tongwe record zinazomilikiwa na kijana jina maarufu (J mada),inasemekana ilikuwa ni majira ya usiku wavamisi walipowasili katika viunga vya ilipo studio hizo.

Kulingana na maelezo yaushaidi uliotolewa na shuhuda (the city) mwanadada aliyefika muda mchache kabla gari lawatekaji kuondoka alisema "ilikuja Noah nyeupe na wakashuka watu watatu,baada ya hapo wakatuamrisha mimi,bin Laden na wageni kutoka morogoro tuingie ndani ya geti,tulipoingia ndani ya geti walituuliza kwamba tumemkuta junior au tumemkuta Roma,tukasema junior hayupo ila Roma yupo ndani,wakatuamrisha Tukamuite Roma,tukamuita Roma,Roma akatoka akaulizwa wewe ndio ROMA na ilivyoonekana hawakumjua na pia walimuambia simu yake ipo wapi atokenayo Roma alitokanao sikuweza kujua nini kiliendelea kwa sababu waliongelea nnje ya gari,walirudi ndani wakamlazimisha binladen aingie studio akiwa amesindikizwa na mmoja wao na Wakarudi tena wakachukua TV zilizopo pale,wakatoka na imma walikuwepo wote ndani ya studio,studio ikabaki tupu,walivyotoka hapo wakaniambia mimi na wageni wengine waliotoka morogoro tusiende popote na nilichosikia baada ya hapo ni mshindo wa gari na gari kuondoka "

Fact:katika ushahidi wa shuhuda (Rozaree) umejidadavua watekaji hawakuwa na haiba yautekaji kwani kiwango Chao cha ustaarabu kilikuwa juu sana ukilinganisha na watekaji wengine tunaowasikia na hata kuwashuhudia.
Hoja ya kwanza (1):watekaji waliuliza tumemkuta Roma na wakatuambia tukamuite?? Niajabu kwa mtekaji kuwa na nidhamu ya namna hii, mara nyingi hutumia nguvu kuhakikisha wanatimiza lengo Lao,mtekaji gani huyu anaogopa kuingia ndani anawaambia mashuhuda nendeni mkamuite Roma ??
Hoja ya pili (2):watekaji wakamuuliza Roma,wewe ndio Roma.sikawaida kwa msanii maarufu kama Roma ashindwe kujulikana tena na hawa watekaji ambao kwa asilimia kubwa huenda wakawa ni vijana,tena vijana hawa ndio wapenzi namba moja wa mziki huu wakufokafoka unaoimbwa na Roma ni wazi na sio rahisi kutokumfahamu Roma.
Hoja ya Tatu (3):watekaji wakaingia ndani na binladen,picha tunayoipata hapa bado watekaji walikuwa na ustaarabu napo hawakutaka kuingia studio wenyewe bado waliitaji mtu mwenyeji waingie nae ndani, wavamizi wengi hutumia nguvu na wakati mwingine huwa hawajali Mali ya waliodhamiria kumteka hawa waliomteka Roma watofauti sana.viashiria hivi vya ushahidi wa rosare unatuonyesha wazi kunamaslahi binafsi yakisanà na wala siutekaji kama unavyoripotiwa..

Hoja ya 4.watekaji wakatuambia tusiondoke
.watekaji baada yakuwachukua wahusika wakuu waliwaamuru the city na wenzake wasiondoke hii inamaana bado walitaka kuhakikisha usalama wa studio unakuwa salama hivyo walionyesha kujali na kudhamini Mali na vifaa vinginee vya studio. hali isiyo ya kawaida mtekaji kuhakikisha ulizi wa Mali za mtekwaji.

Upande wa mmiliki wa Tongwe record :nae mmiliki wa Tongwe record aliskika akiongea akisema "usiku wa jana likitokea tukio lakutisha sana,walikuja watu ambao hawakufaamika wametoka wapi au wametumwa na nani,bahati nzuri mimi si kuwepo studio,wakamuhoji ROMA baada ya kumuhoji Roma wakamuhoji na monie ambaye ni msanii wangu pia kutoka Tongwe record baada yakumaliza mahojiano yao wakaingia ndani studio wakachukua TV, computer pamoja na kamera"

Maelezo ya mmiliki wa studio na shuhuda namba moja hayatofautiani sana bado yote yanaukakasi wa kiwango cha ustaarabu wa hawa watekaji.

Hoja watekaji walimuhoji ROMA.ni tanzania pekee watekaji hupata muda wakuhoji mtekwaji,sidhani kama inaingia akilini kuskia mtekaji anaweza kufanya interview na mtekwaji,nguvu na ubabe huwa hawana muda wa kuwa wakarimu na kuchukua maelezo mara zote watekaji hawana huo muda,ili lililotokea kwa Roma ni maigizo yenye maslahi binafsi.

Kauli ya mkuu wa mkoa mh.Paul makonda.mkuu wa mkoa ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa mkoa ni haki na wajibu wake kuhakikisha mkoa unakuwa salama pamoja na Raia wake,ni haki na sahihi mkuu wa mkoa kuingilia kati upotevu wa watu wake.

Mh.Makonda aliskika akisema
"bado tunayomamlaka yakudhibiti kila aina ya utekaji na kuhakikisha wanannchi wetu wanaendelea kuwa salama,sambamba na hilo nawapa imani tu haitafika jumapili tutakuwa tumeshawapata ndugu zetu wote wanne na mimi naomba kwa dini zetu kwa imani zetu kila mmoja kokote kule alipo aombe ili tuhakikishe ndugu zetu tunawarejesha wakiwa salama.

Kutokana na kauli ya mh Paul makonda imepelekea watanzania kijuiliza maswali kadhaa.

Hoja ya kwanza (1).
kauli ya haitafika jumapili Roma na wenzake watakuwa wamepatikana.Niwazi kauli hii ni Tata na ilikuwa na viashiria vya huenda kuna Jambo muheshimiwa alikuwa analifahamu zaid, tena ukizingatia huwa anaukaribu na vijana hawa wanaofanya sanaa,nikweli jumapili hajafika na vijana wamepatikana,mh ni kijana anajua mbinu nyingi za vijana wenzake wanazotumia kujipatia umaarufu nadhani alishashtukia na akatoa kauli iliyojipambanua kuna kitu anafahamu.

Hoja ya pili (2).kauli yakuwarejesha Roma na wenzake wakiwa salama nayo ni moja ya kauli iliyotolewa na mh mkuu wa mkoa tutawarejesha wakiwa salama kauli hii nayo iliashiria mchezo mzima huenda mkuu wa mkoa alikuwa anajua mahali alipo mkatoliki.

Uchambuzi wa kauli ya mhusika mkuu (Roma)
.Roma mara baada yakupatikana alipelekwa kituo cha Polisi ambapo naamini aliacha maelezo yakutosha.

Roma aliskika akisema " kutokana na mazingira na situation nzima hatutakuwa na muda mrefu wakuzungumza, kwakifupi tu niwaakikishie mimi ni mzima mpaka Sa hivi kiafya na kiakili hata monie,bin LadenI wote tuwazima wa afya,niwaakikishie sisi wote ni wazima tunaendelea vizuri"


Hoja ya kwanza (1)
.nifuraha kuskia wapo salama ila yapo maswali ya kujiuliza nini hasa lengo la watekaji je ni kweli watu hawa walitekwa? ni kweli mtekaji anaweza kuwateka wasipigwe hata vibao kimoja kiasi cha kuachiwa wakiwa 100% sawa bila jeraha na hata mkwaruzo wowote?

Hoja namba mbili (2).mavazi ya Roma siku anatekwa na siku anaonekana,siku anatekwa Roma aliripotiwa kuwa alikuwa amevaa t shirt nyeupe suruali ya blue aina ya Jinsi, ila siku anapatikana alionekana akiwa na mavazi meusi .Niwazi uko alikokuwepo alipata fursa ya kupata huduma muhimu kama kuoga na hata kubadilisha nguo bado kuna ulakini wa aina hii ya utekaji,sio rahisi kwa watekaji kuwa na moyo wa namna hii vijana wasanaa inaonekana walikuwa bado katika mwendelezo wa sanaa yao,haingii akilini aina hii yautekwaji kwakweli.

My take.tusishangae na kuskia nyimbo mpya ya Roma katika kipindi cha mwezi mmoja kutoka sasa,attention aliyokusudia kuipata amefanikiwa kwa 100% otherwise kesho siku ya jumatatu atuambie wa Tanzania hoja nzito kutuakikishia ni kweli alitekwa na sio kutafuta umaarufu kisanaa.

Cheki mtanzania ambae hafati mkumbo wa kukurupuka alivyo tumia akili kufikiri na kuja na hoja zinazo jaribu kutuonyesha sura ya pili ya hili tukio,hongera kwa kuumiza kichwa kufikiri kiasi hiki.
 
Kajiteka haf kuna mtu anatabiri kabla ya jumapili atapatikana
 
Kila mtu siku hizi amekuwa mchambuzi wa masuala ya usalama

Yaani Tanzania kila mtu ni TISS
 
Hivi huko Lumumba huwa hamruhusiwi hata kutafakari na kuchanganua mambo japo kidogo sana!!!?

Lumumba ndio wapi, inakuuma nini wewe kie kumsoma na kujilia popcorn?

Wewe wa kutafakari andika yako, muache aliyeamua amejitahidi.


Mengine siongezi, nimeamua kumpa support na kulike juu... tu ha ha haaaaa jipige vibao vya usoni.
 
Nimeamini wewe ni bashite!!! Unawaza kibashite bashite tu watekaji walikuwa na akili timamu sio akili
kama zako!!

Huenda mazingira aliyokuwa roma kulikuwa na ulinzi kwaiyo wale walijua hilo hawawezi tu kipiga piga risasi na kuamrisha amrisha tu kila mtu ajue nini kinaendelea
Wasingefanikisha zoezi lao gari lingefuatiliwa na taarfa zingesambaa haraka sana wangekamatwa tu au wasinge toka nae pale

lakini huenda wakati wanaongea na roma walimueleza hali halisi kwamba ukifanya akajua hata mtu mmoja hapa kinachoendelea tutakuua hapahapa fanya kama hamna kinachoendelea fanya kama tulivyokuagiza tuondoke kwa hiyo mtu wapembeni kama uyo dada aliyetoa ushaidi ataona nimaongezi ya kawaida tu yalikuwa yanaendelea pale

Unasema roma amerudi akiwa mzima kabisa??? Sio kweli!! Roma kutembea mwenyewe hawezi anasaidiwa kutembea ila amesema ni mzima kabisa kwa sababu ya usalama wake ndio kama nilivyokwambia vitisho alivyopata sio vya kawaida
 
Back
Top Bottom