Fact: Prince Dully Sykes ndio muanzilishi wa muziki wa bongofleva

Yote kwa yote huyu dully anastahili heshima kwenye huu mziki wa bongo wazee. Apewe maua yake

Wote tunastahili heshima kwasababu Bongo fleva ilikataliwa na jamii lakini sisi wengine tukatoa support yetu mpaka leo tuko hapa
 
Wape heshima wakina Mike mhagama
Na taji liundi hao ndiyo walipush na kuja na idea ya bongo flavour

Ova
Una upeo mdogo sana na huwezi elewa kila napokwambia sababu upeo ni gift toka kwa Mungu
 
Uko sahihi atakayebisha n mchawi
 
Wote tunastahili heshima kwasababu Bongo fleva ilikataliwa na jamii lakini sisi wengine tukatoa support yetu mpaka leo tuko hapa
Hata bolingo ilipoanza, jamii walikua wagumu kuelewa mana walizoea ngoma za asili mkuu....all in all kila muziki lazma ulipata changamoto mwanzoni mbka kuja kueleweka na jamii
 
NENO BONGO ALILIANZISHA MTANGAZAJI WAKUITWA SUNDAY SHOMARI, KTK KIPINDI CHA DJ SHOW. SUNDAY SHOMARI NA SEBASTIAN MAGANGA WALIANZISHA UTARATIBU WA KUPIGA WENYE MAHADHI FULANI KWA DKK 30, ILIPOFIKA ZAMU YA MUZIKI WA KIBONGO, BAADA YA KUMALIZA KUPIGA R&B ZA MAREKANI, WAKAPIGA MUZIKI WA BONGO WA KUNDI LA 4KREW, HALAFU WAKAPIGA MUZIKI WA UNIQUE SISTERS, ZOTE NI R&B.


NDIPO KWA MARA YA KWAN ZA SANDE, ALIPOUITA HUU MUZIKI NI BONGO FLEVA, INGAWA JINA LAKE AU NENO LAKE HILI HALIKUVUMA SANA, LILIKUJA KUFAHAMIKA SANA BAADA YA DULLY SYKES KUUTAMBULISHA MUZIKI WAKE KWA JINA LA BONGO FLEVA,
LAKINI KIASILI KABISA ALIYEANZISHA BONGO FLEVA NI JABIRI SWALEHE, MIAKA YA 91-92 ALIPOTOA ALBUM YAKE YA KWANZA ILIYOITWA SWAHILI RAP
 
Sasa Swahili rap inakuaje bongofleva mbona unakuwa hauna akili?
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana kumtaja Mak Muga.

Alikuwa na rap lake moja kila mara anajitaja "Mak Mugaa, Mak Mugaa".

Shuleni anakuja na kikapu anaweka madaftari.
 
Walianzisha wakina Mike mhagama na taji liundi
Huo usemi wa jina bongofleva,
Kweli mwanzilishi wa mziki wa rap ya kiswahili alikuwa saleh jabri
Na mziki harakati mapinduzi ulianzaga wakati wa tamasha lile la yo rap bonanza nakumbuka lilifanyika new africa floor ya 7
Na mm wakat huo nlikuw3po
Ila naona humu kuna watoto wadogo wa 2000 tunabishqna nao wao bila kuelewa
Dully hajaanzisha bongo fleva labda kus3ma alileta manjonjo kwenyw mziki na yeye kujipenda kuliko msanii yoyote

Ova
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana kumtaja Mak Muga.

Alikuwa na rap lake moja kila mara anajitaja "Mak Mugaa, Mak Mugaa".

Shuleni anakuja na kikapu anaweka madaftari.
Mac muga alisoma tambaza kitu kama hicho,harakati za mziki pia nyingi zilianzia donbosco nakumbuka wakat wa maevent kusaga na bony walikuwa wanakuja sana kupiga
Alafu alikuwepo dogo mmj wakat huo smbdy Paul beda alikuwa anasoma mzizima agakhan naye alikuwa na harakati sana za mziki

Ova
 
Mac Muga alikuwa mwana sana, ukimuona kama kadata hivi lakini mtu poa saaana. Mnyamwezi fulani hivii kitambo.
 
Sasa Swahili rap inakuaje bongofleva mbona unakuwa hauna akili?
Ahsante kwa kunitoa akili, kwanza naomba kuufahamu tafadhari. Naomba nikukumbushe ewe kizazi cha manifongo. Huo muziki wenu hapo kabla uliitwa "kigodoro" baadae ukaitwa "kiduku" na sasa hivi mnauita singeli. Mnanda hapo kabla uliitwa mchiriku. Aliyeunzisha huu muziki wa kibongo bongo "bongo fleva" ni SALEHE JABIRI, jina la kwanza kabisa alilolianzisha ni SWAHILI RAP, hiyo ni miaka ya 88, 89, 90, 91 mpk 92,
 
Mimi nazungumzia muziki wa bongofleva sizungumzii hip-hop wala rap. Bongofleva sio muziki wa rap.
 
Watoto wa 2000 mna matatizo sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…