Facts: 16 most powerful militaries in Africa

Tanzania ina watu wanauelewa mdogo sana yeriko yeye kaleta utafiti uliofanywa na wewe leta was kwako. Miaka 5 ijayo Tanzania itakuwa na wajinga wengi sana, mungu wasaidie
Umeona ee..badala ya watu kujadili na kuainisha mapungufu ya ripoti wao wanadhani Yericko ndiye aliyeiandaa ripoti, Mungu tusaidie angalau utupandishie IQ.
 
tuwekee ukweli mkuu , tumzodoe mleta uzi .

Mkuu hapana aisee, sitaki kuamini kabisa..
Jeshi la Somalia, na South Sudan kama yako imara kwa kiwango cha kuzidi hili la Mwamunyange pamoja ya kuwa ni la Kiboya lakini bado sijalishusha chini ya hizo nchi hapo jju
 
Hao waliofanya huu utafiti wanafikiri kwa kusema hvyo ndo Tanzania itatetemeka kwenda kununua silaha zao.

Silaha zimewadodea ndo wanakuja utafiti wao uchwara. Hakuna sababu yoyote ya msingi ya kuingia gharama kununua silaha zisizo na kazi wakati technologia inakuwa kila siku na silaha za kisasa zinavumbuliwa kila uchao. Ni kupoteza hela tu.

Wakitaka kufahamu waite mechi ya kirafiki.
 
Kwani we unalipimaje Jeshi la Tanzania na la Nigeria?


Mpaka Mataifa Yapigane? Haya basi, sisi tuliposhambuliwa na Amin tulimuondoa kwa uwezo mkubwa

Nigeria Kampiga nani?
Mkuu kujua uwezo wa nchi kijeshi sio lazima uione inapigana, SA hajapigana lakini hatuwezi kuizidi kijeshi.
 
Mkuu kujua uwezo wa nchi kijeshi sio lazima uione inapigana, SA hajapigana lakini hatuwezi kuizidi kijeshi.

Mi nasema Jeshi letu ni bora kuliko la Nigeria, kwa nini unanivutia kwa hao wazungu wa south?
 
Kama wanazani jeshi letu ni legelege wajalibu kuvamia halafu waone hizo takwim sio sahihi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 


Ha ha ha tafiti zingine hazina mashiko. DRC, Nigeria, Somalia, South Sudani ziko juu ya Tz. Tuamini ipi?? Kati ya tafiti hii na ile iliyoweka Jwtz kuwa ni moja ya majeshi bora duniani? Hizo ni propaganda za Rwanda na Malawi.
 
Hii listi imepangwa na wanyarwanda nini??
Mbona nafsi inakataabkukubaliana na takwimu hizo!

Mpuuzi yeyote anaweza kuandaa ripoti yake ya utafiti wa kipuuzi kisha akaiandika kwa kiingereza akijua atawatisha wabongo.
Hiyo ni ripoti ya kipuuzi kama za wapuuzi wengine tu, huwezi kuniambia Somalia, Congo DRC ziko juu wakati hazina hata jeshi la kueleweka.
 
Mimi ni muumini wa wa fikra machipuko, huamini kuwa, hakuna upuuzi ulio upuuzi mtuputu, Vijana turuhusu akili zetu zizunguke nyuzi 360, tusijifungie kwenye matawa ya akili zetu, tusidumae katika muono huo huo,

Utafiti hupingwa kwa utafiti, kamwe haupingwi na matakwa ya mbongo zetu, niseme wazi, mimi nilipoona taarifa hii nilistuka, kwakuwa akili yangù iliamini kuwa Tz ni ya kwanza Afrika kwakuwa na jeshi imara hasa nikirejea historia ya ukombozi wa kusini mwa jangwa la Sahara na vita vya Uganda,

Ninawashangaa kweli tena ninawashangaa kwelikweli wale wote wanaopinga utafiti huu bila kupinga kwa utafiti mbadala, tangu watu waanze kuchangia hapa sijaona mtu akija na utafiti mbadala ili atushawishi kuupinga utafiti huu,

Nani anajua ripoti ya JWTZ ya uimara wa jeshi letu? Nani anajua ripoti ya Wizara ya Ulinzi juu ya uimara wa jeshi letu? Nani anayo na atuletee hapa ripoti yoyote mbadala ya uimara wa majeshi ya Afrika? Turuhusu mbongo zetu zitamalaki kwa mapana yote, tusifungwe na mawazo yetu mgando, tujenge tabia ya udadi yakinifu kwa falsafa ya sura tenge!

Hivi sisi tunaopinga huu utafiti tunatumia utafiti ama takwimu zipi zinazotambuliwa kitaifa na kimataifa?
 
Tanzania kipindi cha nyuma tulikuwa tunapambanishwa na nchi kama Ethiopia, Algeria, Misri nk, sio Kenya, Uganda, eti na Rwanda jamani!!!. Na hii inatokana na kuzidi kwa utawala mbovu ambapo ni chanzo cha kuingiza siasa Jeshini. Mafisadi yanapo tafuta kukubalika Jeshini kwa ajili ya usalama wao, nidhamu lazima ishuke kwa maofisa wa kuu wa Jeshi. Na hiyo inachangia kuharibu mfumo kwa masuala ya kiulinzi ambayo ni muhimu . Kiukweli tumeshuka japo sio katika kiwango hicho. Nafasi yetu bila shaka imechukuliwa na Angola.
 
Aliyeandika upuuzi huu ajaribu kutia mguu nchini ndipo atajua TZ ni ya mwishoni au la. Nchi ambazo masuala ya kijehsi yako surrounded na secrecy, huwezi kusema umefanya utafiti, chanzo cha data zako ni kipi.

somalia ina jeshi imara, bila serikali??
 
Kaka ukana mimi nipo pamoja na wewe,Yericko ni mmoja wale watu ambao uchambuzi wao unaongozwa na itikadi zao.mimi nimeangalia hii web siku nyingi tuuinaitwa www.africaranking.com vigezo walivyotumia ni wingi wa vifaru,ndege,idadi ya askari na defence budget, sasa wewe unajeshi kubwa kama kenya alafu unashindwa kuwashika watu watano ambao wapo kwenye closed space kwa siku tatu hii ni sawa na mtu anayejisifu ana mtoto mkubwa kuliko mwenzie wakati mtoto mwenyewe taahira na mwenzie mdogo lakini IQ yake ni kubwa balaa.tuache kudharau vyetu akuna tulichojaribu kijeshi tukashindwa.
Lakini kaka kitu kingine yericko ni mwandishi mzuri tuu wa essay ambazo zina mpangilio mzuri lakini hazina uzito wowte katika uhalisia wowote
 

Mkuu hivi huu ni uchambuzi wa Yericko au ni ripoti ya CIA??
 
Mkuu yeriko siwezi kukuunga mkono kwa ulichokiandika maana nikichekesho Somalia, Congo, Kenya ambayo inapeleka vifaru west gate itushinde?uongooo
 
Mkuu yeriko siwezi kukuunga mkono kwa ulichokiandika maana nikichekesho Somalia, Congo, Kenya ambayo inapeleka vifaru west gate itushinde?uongooo

Mkuu wangu nisamehe sana, sijaandika mimi haya,

Hiyo link inaeleza vizuri walioandika hayo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…